JULIASI KAMBARAGE NYERERE.
Wewe ndio raisi wa kwanza wa taifa hili la Tanganyika na baadae Tanzania. Umeondoka duniani miaka kumi na nne iliyopita sikumbuki walisema kwa shinikizo la nini vile. Ninakukumbuka sana na ninayakumbuka maneno yako matamu uyatoayo ukiwa mbele za watu. Umekua ukikemea UDINI, UKABILA, UMASIKINI,RUSHWA, UFISADI N.K. Mheshimiwa ningependa sana kile ulichokuwa ukikizungumza majukwaani kingekuwa ndio matendo yako halisi ila hali ilikuwa tofauti. Nakupongeza kwakuwa ulikuwa sikiongozi unaependa kujilimbikizia mali lakini karibu mateso yote tupatayo watanzania baada ya miaka 51 ya uhuru wewe ndio chanzo cha matatizo hayo. Ngoja nikukumbushe mheshimiwa miaka ile ya sabini uliwalazimisha watanzania kwenda kuishi vijiji vya ujamaa na waliogoma kama babu yangu ulimchomea nyumba yake na kuifanya familia yake ikalala nje. Wewe ndie uliyekuwa ukilazimisha watanzania wanunue betri za NATIONAL zilizotengenezwa kwenye kiwanda chako binafsi pamoja na kwamba haukuwa ruhusu watanzania kuwa na radio, uliifikisha nchi sehemu mbaya mpaka watu wakafikia kula nyasi. Ulikuwa haudhamini ELIMU na uliwaruhusu wachache kusoma tena kwa maagizo ya kuja kuendeleza fikra zako. Wewe ndie uliyetaifisha mali za watu na taasisi na kuwarudishia wengine na kuwanyima wengine. Wewe ulikuwa dikteta mbaya sana uliyewaua kila uliowaona wanamawazo kinyume na yakwako. Ulikuwa unapenda kusikika wewe tu na kutajwa pekeyako na viongozi wengine waliokuwa nawe hukutamani wasikike. Tanzania mpaka leo inasheria kandamizi katika katiba uliyotengeneza wewe mwenyewe pasi kuwashirikisha watanzania. Leo magazeti yanafungiwa kwa sheria zilezile kandamizi ulizoziweka dikteta wewe. Najisikia uchungu kuendelea kuandika kwani sijui niandike lipi niache lipi.