Leo taifa liko katika kumbukumbu za tangu alipotutoka kiongozi shupavu,kipenzi cha watanzania na mwanafalsafa nguli kuwahi kuzaliwa nchini,"Baba wa taifa Mwl. JK NYERERE".Ni kiongozi huyu makini aliyelijenga taifa letu katika misingi ya umoja,amani,upendo na mshikamano..Nyerere enzi za uhai wake alilaani na kupinga vikali ubaguzi wa rangi,jinsi,dini na kabila kutamalaki nchini,pia alishiriki kwa vitendo kupinga na kupiga vita aliowaita maadui wakuu wa mtanzania yaani,UJINGA,UMASKINI na MARADHI na kuwataka wananchi wakupiga vita pale wawaonapo.Ni kiongozi huyu alipenda elimu kwa lengo la kuhakikisha watanzania wanapata mwanga wa ukweli ili kukabiliana na changamoto za ujenzi wa taifa.Alichukia kwa viwango vyote ubinafsi,ufisadi,ulimbikizaji wa mali,ulaghai na wizi katika sekta na taasisi za serikali.Ndugu zangu ni kosa kuu kutomuenzi mpiganiaji mahiri huyu wa haki za mtanzania na wengine wa style yake,katika mchango wao wa kulea na kutengeneza mazingira ya amani na upendo tunaojivunia leo.(R.I.P JK NYERERE).