Trafiki apigwa Ubungo mataa

Trafiki apigwa Ubungo mataa

mpwa awa jamaa dili ni.kofia

ukiona anapigwa wahi kofia pesa za dili zote.zinawekwa ndani ya.kofia.sikuyake.inageuka.manyoya

Hahahahahaha

Mpwa kofia naona ilishatangulia mbele ya haki kama sijakosea

Hapo ni Receipt na notification book peke yake ndivyo vilivyobakia.
 
Hao jamaa wakikukamata katika 18 zao hawana msalie mtume tena kwa nyodo sana wanakwambia ulipe 30000 ambazo hata haziingii kwenye mfuko wa serikali na bado wanakunyanyasa utafikiri ni kosa kuwa na chombo cha usafiri, mbaya zaidi wanakupa notifications ambazo zimepitwa na wakati,FAKE, ukigoma unapewa choice au uache chombo chako cha usafiri mpaka utakapo pata hiyo chenji.
Wewe jamaa mpotoshaji sana
 
Mavuno ndio hayo

Hii ni kwamba wananchi wamechoka na uonevu unaofanywa na askari

Huko tunakoelea hakuvutii kabisa

Ila sijui kama wanaona kuwa hizi ni dalili za wananchi waliochoka
Lakini kweli mnao ushahidi IGP anawaka trafiki wampelekee sh 150,00 kila mmoja kila siku? IGP Mangu ninayemfahamu hana tabia hii, na huenda akadai ushahidi wa tuhuma hizi nzito!
 
Vurugu za Ubungo zimesababishwa na Serikali kushindwa kujenga barabara za kutosha,kushindwa kupanga mipango ya maendeleo ambako kumesababisha foleni ya magari na watu kugeuza barabara maduka! Asilimia 70 ya wakazi wanao ishi Dar walitakiwa kuwa mashambani vijijini!
 
bado pale TAZARA wanakera kweli magari yanayotoka vetenari yanakaa sana
 
Lakini kweli mnao ushahidi IGP anawaka trafiki wampelekee sh 150,00 kila mmoja kila siku? IGP Mangu ninayemfahamu hana tabia hii, na huenda akadai ushahidi wa tuhuma hizi nzito!


Hizo hela kamwe haziendi mfukoni kwa Mangu kwani faini zimewekwa kisheria na zinapaswa zilipwa kwa wahasibu na sio askari.Mangu alichofanya ni kuwaweka trafiki bize kwa kuandikia makosa 3 kila siku, yaani 30000x5= 150,000/= , bunge liliridhia kuwa 75% ya faini hizo zitumiwe na Jeshi la polisi na 25% zipelekwe hazina.
Kwa hiyo Ernest Mangu anapaswa kupongezwa kwa kusimamia makusanyo ya faini za barabarani.
Kwa hiyo sio kweli kwamba anapewa hizo hela mkinoni yeye kama yeye bali zinakusanywa kisheria . Labda tatizo lipo kwenye matumizi ya hizo hela kule wizarani.
 
Sijui mnakiona nikionacho?
Trafiki kusababisha ajali ni kosa ambalo kwa tabia za watz zilivyokuwa zamani hata yeye wangempa pole ya kusababisha ajali,lakini leo wamempiga,je,katika akili yako unadhani ni hii ajali tu iliyowafanya kufika mbali hivyo kimaamuzi?
Mie naona kufikia hatua ya wananchi kumpiga askari huyu na uniform yake haijatokana na ajali tu,bali tayari kuna kitu cha ziada akilini mwao kinachojijenga gradually kama reaction kutokana na mazingira wanayoishi hivi sasa kilichowaendesha kufanya hivyo na hicho kitu nakiogopa sana,hakina macho,kuna siku kitawapeleka kwenye kambi za jeshi na magogoni.

Kinajaa taratibu mioyoni mwao,angalia hata comments za wachangiaji wengi wa mjadala huu,utaona jambo jipya mioyoni mwa watz, na kama mnafikiri watz wanamalizia hasira zao mitandaoni tu,basi haya matukio ni ujumbe maridhawa,kwamba wanaweza kutekeleza wanachotamani,hizi ni dalili tu,binadamu ni yule yule Misri,Ulaya,Somalia,Syria and so Tanzania!na ipo siku atadhihirisha hilo duniani kote,endeleeni kuwaonea,stay tuned!
 
Tabia za trafiki kukamata magari na kudai pesa katika siku za karibuni zimekithiri,tena Dar wamejazwa kila kona ni wengi,si ajabu wananchi nao wanaanza kuja juu,hiyo ni reaction!mengi yatafuatia as long as kuna action,reaction itaendelea kuwepo.Tujiulize,ni kwa nini vyombo vya sheria vikose ushawishi katika kuwaongoza wananchi kusimamia sheria?Hivi raia wameamua kuwa "toto tundu" ghafla tu,bila sababu?
Msichokiona watawala ni kuwa wananchi wakichoshwa na sehemu ya mfumo,wanauona mfumo wote mbaya!
Jk and co,hili jeshi lenu la Polisi litawaponza sana msipokuwa makini.Nawaangalieni tu,haya!
 
dah ..mzazi wa mtu huyo....

Aisee, mbona kazi ya Utrafic inaanza kuwa chungu!!! Kufukuzwa wao, kudamka alfajiri wao, kugongwa na magari wao, kufukuzwa kazi wao, na sasa kupigwa na wananchi wao!!! Daaa, hii inabidi trafic waandae mgomo/maandamano na wao sasa.
 
Duh!

Kunahitajika uongozi mpya wa kulijenga upya jeshi la polisi!Maana inapofikia watu bila aibu wanamkwida `msimamizi` wa usalama,basi ujue kuna tatizo kwenye mfumo wa usalama wa nchi!

Leo askari atapigwa ,kesho watu wataunda jeshi kulinda makazi yao,misikiti yao,makanisa yao,mikoa yao na mwisho NCHI YAO!

GOD FORBID!!!

Hapa inatia shaka usalama wa raia na mali zao. Unajua huwa inafika kipindi nawahurumia sana hawa jamaa
1.mishahara kidocho
2.wanashinda juani
3.vumbi linawaathiri
4.hawafaudu mambo ya kifamilia
5.hawaheshimiwi hata na wake zao na watoto
6.huonekana kutokuwa na msaada kwenye mambo ya kuchangia maendeleo ya ukoo (pesa hawana), na mbaya zaidi 7.wanapigwa........
 
Back
Top Bottom