Trafiki apigwa Ubungo mataa

Trafiki apigwa Ubungo mataa

Yote ya nini mpaka umkwide traffic! au umpige? kasababisha ajali basi ita askari mwingine apime ajali then mkatoe maelezo tumegongana sababu hii na hii.! na yeye ni binadamu ana mapungufu yake sio mnakurupuka wengine hapo ni ushabiki wa kijinga..!!
 
Na kumpiga raia asiye na kosa? Au kumpiga mwandishi wa habari akiwa kazini? Mfano wa majitu ya aina yako wkiwa wengi ktk nchi ndivyo nchi inavyozidi kuwa hovyo. Hao watu wajinga sana sijawahi kuona. Mi ningekuwa Dar pindipo wangenisimamisha, ningekuwa nampiga busa la mchubuko tu.
Ndg kosa moja haliahalishi kosa lingine kams askari wanaonea raia katika mazingira fulani raia nao wana haki ya kujitetea lakni kwa mazingira haya ya barabarani raia hawatakiwi kuwa chanzo kwa kuwashambulia walinzi wa amani/askari.
Bado wana umuhimu mkubwa na ukitaka kujua umuhimu wao vituo vyote vifungwe japo kwa siku mbili uone kitachotokea
 
Naskia huyu mkuu wa jeshi wa sasa hawapendi traffic kabisa. Labda ndio maana raia wanawadharau.
 
Mkuu, hukuchukua hata no yake ile ya kwenye uniform? Au kama vipi mtaje tu ni wa sehemu gani!

Hata sikuchukua... ni wa pale ubungo alikua mwanaume na mwanamke huyo mwanamke ndio akawa anasema hayo ya kutubambikia kosa jingine tusipompa hela.
 
Nami nasema wapigwe tu, maana tumechoka sasa. Ee wapigwe sana.
 
Ahaa wanajifikiria wao tu na maslahi yao

Wanajiona wao ndo nchi wakati matumbo yao yanajazwa na kodi zetu plus vihela vya mboga wanavyotupora njiani kwa gia ya makosa ya magari kumbe majizi makubwa. Yapigwe tu.
 
Naskia huyu mkuu wa jeshi wa sasa hawapendi traffic kabisa. Labda ndio maana raia wanawadharau.


Sio Mkuu wa Jeshi hilo peke yake anayewachukia trafiki bali ni watu wengi wenye kutumia barabara, naye akiwa mmoja wapo.
Kuna kero sana barabarani.Yani mtu akiwaona trafiki mbele yake anaona janga la kuchomoa hela zake.Yani ukisimamishw lazima hela itoke bila hata kosa.Ukiuliza kosa lako nini nini mbona unacheleweshwa basi inakuwa tabu kabisa.

Wakubwa wao wamefanya makusudi kuweka viwango vikubwa vya makusanyo kwa siku kwa kila trafiki ili wananchi wapige kelele na kitengo hiki cha kula rushwa rushwa kiondolewe kuepusha lawama zinazolichafua jeshi.

Nasikia kuna askari mmoja aliwahi kununua utrafiki kwa sh. 2,500,000/= kwa kukopa benki kabisa.Sasa sijui atazirudishaje.Wanawake wanaingia kwa rushwa ya ngono.
Hapo usitegemee mtu mwadilifu kama Mangu kukipenda kitengo cha namna hii.

Cha msingi ni kurudisha suala la barabara na matumizi yake kwenye wizara ya miundo mbinu yenye chuo cha usafirishaji.Polisi wabaki na misafara na road block kuzuia magendo.

Mwakyembe aunde chombo maalum kikichojaa wasomi wa vyuo mbalimbali hata kama atawachukua huko polisi lakini kisiwe na hulka za kijeshi na vitisho.
Mbona huko baharini na angani hawahusiki polisi kwenye kutoaadhabu zaidi ya kuimarisha ulinzi tu?
 
...sema tulipofika,we watu wanachakachua hadharani kura za kupitisha rasimu kwa maslai binafsi na rais anachekelea unaona hii nchi inajitambua kweli...?

Tena anachekelea kwa dharau, kejeli na kiburi juu. Tamaa za ngono kila mahali nazo ni shida.
 
Back
Top Bottom