Hahahaha wameondoa hiyo ili watu wakiquestion waseme ni typo... 1.79 trilion ni pesa mingi mnoo.
Hiyo December walifanikiwa kukusanya ile 1.2 trillion kwa sababu ya yale majipu yaliyotumbuliwa sana kwenye kodi na kupewa two weeks kulipia, pia Desember ni mwisho wa mwaka na kodi nyingi ie provissional tax zinatakiwa kulipwa.
Hii 1.79 trillion ni jipu pia... Huenda hata bwana mkubwa hajui watendaji wake wanamdanganya ili tu wapate sifa machoni pa watanzania, lakini in the long run hii ishu itakuja kuback fire.
Habari za ndani zinasema makusanyo ya January, 2016 ni 1.06 trillion. Na hij pia imechangiwa na walipakodi majipu walioshindwa kulipa within the given two weeks.
Kwa tax base yetu ni ngumu mnoo kumaintain collection ya a trillion per month.
Wamekomaa sana na wafanyabiashara wakubwa na kusahau kuna baba mwenye nyumba anakula kodi million na nusu hapo nyuma ya ofisi za TRA mwenge.. Ukimkomalia na huyu akalipa 10% rental (W/T), wako wangapi Tanzania?