TRA yakusanya kwa mwezi trilioni 1.7

TRA yakusanya kwa mwezi trilioni 1.7

Magufulu is strategically re-aligning resources! Indeed, kuna kilanja mpya Magogoni!
 
Ni hatua nzuri sana hii kwa usawa huu tutafika mbali sana pongezi kwa Rais magufuli na serikali yake kwa ujumla kazeni kamba tupo nanyi.
 
Safi sana.. Naona serikali imewekeza zaidi ktk elimu
 
MBONA HUO UTARATIBU HAUNA EFFECT KWENYE MATUMBO YETU NI KWENYE TAKWIMU TU
Wewe kaa ndani subiri uletewe kiroba cha mchele nyumbani kwako lakini serikali inafanya kwa nafasi yake wewe unayetaka mpaka uletewe vitumbua shauri yako.
 
Umequote post nyingi sana hapa... Karibia kila mtu umemjibu... Ila mbona swali la chige hujalijibu???

Billion 200 zimeenda wapi??
Bwah! bwah! bwah! Huyu MsemajiUkweli mbaguzi sana huyu jamaa-- yaani wengine anawajibu lakini sie ambao tumeuliza mapema zaidi hataki kutujibu! Au labda hajaona swali langu, ngoja nirudie:
Alphayo Kidata alisema makusanyo yameongeza kutoka Sh trilioni 1.2 Desemba hadi Sh trilioni 1.79 Januari.Kwa hisani ya Habarileo
Jumla ya shilingi trilioni 1.4 imekusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kipindi cha mwezi Desemba mwaka uliopita wa 2015. Takwimu hizo zimetolewa na leo jijini Dar es salaam na Kaimu Kamishna Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata..... From Michuzi
Billion 200 yetu wameipeleka wapi?
 
Umequote post nyingi sana hapa... Karibia kila mtu umemjibu... Ila mbona swali la chige hujalijibu???

Billion 200 zimeenda wapi??
Kwani ni lazima nimjibu?

Kama umedhani sijamjibu, unaweza kumjibu!

By the way, kwani hufahamu hata kukaa kimya ni jibu.

Siyo lazima nimquote ndio ionekane nimemjibu.
 
Pamoja na yote hayo bado nchi yetu hatuzalishi tunafanya uchuuzi! Afufue viwanda na kuimarisha teknolojia vinginevyo tutaendelea kuwa watumwa wa Wachina na Mataifa ya Ng'ambo


Hauna Akili!
 
Mwanzo mzuri. Kama trend ikiwa hivi basi kwa miez 12 tutapata 12.48tn/-.

Jambo moja sijalielewa kwamba mbona zote zinatumika sasa, bajeti ijayo itatoka wapi?!

Yote kwa yote VIVA Hon Magufuli
 
Bwah! bwah! bwah! Huyu MsemajiUkweli mbaguzi sana huyu jamaa-- yaani wengine anawajibu lakini sie ambao tumeuliza mapema zaidi hataki kutujibu! Au labda hajaona swali langu, ngoja nirudie:
Billion 200 yetu wameipeleka wapi?
please!
Piga hii namba ya simu ya ofisi ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango uwaulize!
+255 22 2111174
 
SERIKALI imeendelea kupaa katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya hadi Sh trilioni 1.79, ambazo imezipeleka katika huduma za jamii, ikiwamo elimu, maji, miundombinu na miradi ya maendeleo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Servacius Likwelile alisema hayo jana wakati akitoa taarifa ya hali ya mapato kwa kipindi cha Februari mwaka huu. Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata alisema makusanyo yameongeza kutoka Sh trilioni 1.2 Desemba hadi Sh trilioni 1.79 Januari.

Kabla ya Oktoba mwaka jana, makusanyo hayo hayakuzidi Sh bilioni 900 kwa mwezi. Dk Likwelile alitaja maeneo ambayo fedha hizo zimeelekezwa ni kwa Mamlaka ya Elimu (TEA) iliyopewa Sh bilioni 23.078; Sh bilioni 18.7 zinatekeleza utoaji wa elimu bure kwa wanafunzi wa shule za awali, msingi hadi kidato cha nne kwa ajili ya ada, chakula na ruzuku.

Aidha, Sh bilioni 13 zimeelekezwa kwenye mikopo ya elimu ya juu na Sh bilioni moja zitatumika kujengea uwezo walimu walio masomoni na wakufunzi wao. Pia Sh bilioni mbili zimeelekezwa kupanua udahili katika mkoa wa Dar es Salaam kama Rais John Magufuli alivyoahidi katika mkutano wake na wazee wa mkoa huo.

Dk Likwelile alitaja maeneo mengine yaliyonufaika na fedha hizo na shilingi kwenye mabano ni Mpango wa Maji Vijijini (bilioni 17.1), maendeleo ya ujenzi wa barabara (bilioni 58.8), miradi ya umeme vijijini (bilioni 20.2), reli (bilioni 2.034) Serikali za Mitaa (bilioni 4.5), na Mahakama zimepatiwa Sh bilioni 12.3.

Wakati huo huo imeelezwa kuwa makusanyo yameongeza kutoka Sh trilioni 1.2 Desemba hadi Sh trilioni 1.79 Januari. Kabla ya Oktoba mwaka jana, makusanyo hayo hayakuzidi Sh bilioni 900 kwa mwezi. Aidha, Dk Likwelile alisema ili kuwajengea uwezo walimu walio masomoni na wakufunzi wao, Wizara imetoa Sh bilioni 1.65 kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo.

Kati ya fedha hizo, wakufunzi wamepatiwa Sh milioni 431.6, walimu walio masomoni wametengewa Sh milioni 249.2 kwa ajili ya vifaa vya kufundishia, posho na nauli. Alisema kuwa fedha nyingine kati ya hizo, kiasi cha Sh bilioni 573.7 zimetolewa kwa ajili ya ishahara ya watumishi wa umma na ulipaji wa deni la taifa kwa mwezi huu zimetolewa Sh bilioni 842.1 na mifuko ya hifadhi za jamii Sh bilioni 81.13.

Aidha kiasi kilichotolewa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo ni Sh bilioni 166.2 huku Chuo kipya cha Sayansi ya Tiba kilicho katika hatua ya ujenzi cha Mloganzila huko Kibamba, nje ya Jiji la Dar es Salaam, kimepatiwa Sh bilioni 18 .
Kwa hisani ya Habarileo

JE HUKO WANAKOZIKUSANYA WAMEPABORESHA ? ? AU WANANYAKUA NA KUUA KABISA UZALISHAJI ?
JE HAYO NI MATOKEO YA MAPATO HALISI ? AU NI MALIMBIKIZO YA UZEMBE WA SERIKALI ILIOPITA ?
JE KUNA MBINU YEYOTE YA KUONGEZA KODI MPYA/KIPATO ? ? AU MBINU NI VITISHO VYA NYAU TU ? ?
HONGERA SANA LAKINI MSIPOKUWA MAKINI MTAUWA/KUFILISI WAJASIRIAMALI SME's HASA WAZAWA WOTE.
 
Wakati serikali ikijipanga kujenga viwanda hii ni hatua nzuri sana ya ukusanyaji mapato, ndani ya miezi 3 ukusanyaji wa kodi umeenda hadi karibu mara mbili ya makusanyo ya awali..Kazi nzuri sana tutakapo anza kuzalisha kwa viwanda vyetu mapato haya yaneweza kufikia hadi mara nne kwa mwezi na hapo ndipo tunapozungumzia taifa lenye uchumi wa kati..Viva JPM
 
JE HUKO WANAKOZIKUSANYA WAMEPABORESHA ? ? AU WANANYAKUA NA KUUA KABISA UZALISHAJI ?
JE HAYO NI MATOKEO YA MAPATO HALISI ? AU NI MALIMBIKIZO YA UZEMBE WA SERIKALI ILIOPITA ?
JE KUNA MBINU YEYOTE YA KUONGEZA KODI MPYA/KIPATO ? ? AU MBINU NI VITISHO VYA NYAU TU ? ?
HONGERA SANA LAKINI MSIPOKUWA MAKINI MTAUWA/KUFILISI WAJASIRIAMALI SME's HASA WAZAWA WOTE.
Hata kama ni malimbikizo vp ulitaka yasikusanywe? Kwa miezi zaidi ya mitatu sasa makusanyo yamekuwa yakipanda na biashara zinaendelea kama kawaida,,hatuwez kuacha kukusanya kodi halali ya serikali kwakuhofia wajasiriamali wazawa kufilisika..mimi ni mtumishi na ninalipa kodi kila mwezi na sitegemei kufilisika..[HASHTAG]#Tujengenchi[/HASHTAG]
 
Tuliambiwa November 1.4 Trilioni
December 1.6 Trillioni
January 1 Trillion

Leo wanatwambia 1.7 Trillion, mbona basi Figure hazitally?

Je Huyo ng'ombe mnayemkamua mnampa majani? au mnaenjoy kukamua tu.

Sera ya Serikali inabidi iwe kuwakuza wajasiriamali na siyo kuwakamua tu
 
Jitihada nzuri sana. Tuome tu Mungu awape nguvu na uwezo wa akili kung'amua mianya mingi ya ukwepaji kodi. Waangalieni sana WAHINDI maana wanaikosesh sana nchi mapato kwa ujinga ujinga wao wa "UNATAKA YENYE RISITI" ama "ISIYO NA RISITI" mara utasikia Machine imeharibika na TRA wanajua. WEZI sana hawa jamaa hasa maeneo ya Posta na Kariakoo.

Viva Rais na watendaji wa taasisi zinazohusika.
 
Bwah! bwah! bwah! Huyu MsemajiUkweli mbaguzi sana huyu jamaa-- yaani wengine anawajibu lakini sie ambao tumeuliza mapema zaidi hataki kutujibu! Au labda hajaona swali langu, ngoja nirudie:
Billion 200 yetu wameipeleka wapi?
teh teh teh teh teh teh.... Anasema hivi

Kwani ni lazima nimjibu?

Kama umedhani sijamjibu, unaweza kumjibu!

By the way, kwani hufahamu hata kukaa kimya ni jibu.

Siyo lazima nimquote ndio ionekane nimemjibu.

 
JE HUKO WANAKOZIKUSANYA WAMEPABORESHA ? ? AU WANANYAKUA NA KUUA KABISA UZALISHAJI ?
JE HAYO NI MATOKEO YA MAPATO HALISI ? AU NI MALIMBIKIZO YA UZEMBE WA SERIKALI ILIOPITA ?
JE KUNA MBINU YEYOTE YA KUONGEZA KODI MPYA/KIPATO ? ? AU MBINU NI VITISHO VYA NYAU TU ? ?
HONGERA SANA LAKINI MSIPOKUWA MAKINI MTAUWA/KUFILISI WAJASIRIAMALI SME's HASA WAZAWA WOTE.
Huko wanapokusanya wanaua kila kitu.. Kuna baadhinya maduka yamefungwa na wawekezaji wameondoka zao.. Watanzania wapo mtaani hawana kazi... Sijajua kwa stlye hii tunajijengea guture gani.. Ingetakiwa wakae chini na walipa kodi na sio kutumia nguvu na vitisho
 
Back
Top Bottom