TRA wanavyofunga biashara za wazalendo

TRA wanavyofunga biashara za wazalendo

Hawa jamaa kuanzia kamishina ni ndumi la kuwili sana. Wanapoongea katika vyombo vya habari juu ya taasisi hii na majukumu yake utasema hawa wafanyabiashara ni wakorofi sana na sio waelewa. Ila ukipewa rekodi ya madudu yao wanayofanya ndipo unajua kuwa haujui......

Tazama tu hata makadirio ya kodi ya bidhaa zinazopita bandarini. Yaani magharama yapo juu kweli kweli kuliko hata bei ya bidhaa. Unanunua gari Us dola 2,500, kodi inakuja milioni saba..... Sasa unajiuliza imekuwaje kodi ni zaidi ya 100% ya original price ya bidhaa?!

Tunahitaji kiwakazia wale misukule pale bungeni kujadili upya hizi kanuni za TRA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu pale Bungeni ni wabunge siyo misukule kama unavyosema.
Na Wabunge wana kazi kubwa ya kubadili sheria ya Kodi ili indane na uhalisia.
Sasa ndio wakati wa wabunge wa chama tawala kuonyesha kuwa wanaweza kwenda sambamba na serikali ili kubaoresha sekta ya biashara ambayo sasa hivi inadidimia kutokana na kodi zisizoelewela.

Nimefurahia msimamo wa Rais Hussein Mwinyi katika hili.
Yeye amesema wazi hapendelei kodi za kuumiza mfanya biashara , bali kodi ndogo ili zilipike kirahisi na kwa wingi.
 
Sasa hii ni State Robbery.
Na haya yanafanyika kila leo.
Pole sana mkuu, kama nawe umefikiwa.

However, I should remind you; you need to be consistent.

IfahamikesSitetei upande wowote hapo. Kwa upande mmoja umesema "makosa ya kiuhasibu", na huo wapili unaoulalamikia, kazi yao ni kukusanya kodi ili serikali iweze kuendesha mambo yake. Kama wanagundua "makosa ya kiuhasibu" yaliyofanyika na kuikosesha serikali mapato, hapo sasa wafanyeje?
Ninalokubaliana nalo ni makosa ya kufunga biashara.
 
Bank sasa siyo mahala salama kwa pesa za wafanyabiashara kwani TRA huenda kufunga A/C kienyeji na kupora pesa za wafanyabiashara kwa njia haramu za kishetani
Hii ni changamoto kubwa sana ...hii kitu ni mbaya sana unafika bank unakutana na statement ya maagizo
 
Una matatizo ya kimsingi, na pengine hata uwezo wa kudadavua kwako ni duni kiasi.
Kwamba nashabikia chama tawala haina maana kubariki madudu ya watendaji.
Na unajaribu kuingiza siasa uchwara mahali pa kutumia akili ya kiutendaji.
Kama umesoma Mzumbe tukupe pole tu.
Kwa hiyo unamlilia nani sasa? Fafanua mana madudu haya yapo toka kitambo shida ni kwamba wewe uliishia kama malaika sasa kuwa shetani hutaki...
 
Hao Tra mnawalaumu bure kabisa, baada ya uwekezaji kupungua na mataifa wafadhili kusita kutoa misaada/mikopo basi hayo ndio matokeo yake na bado huku tunakoelekea hali itakuwa balaa.

Wafadhili wanahofia hatua kali zisipochukuliwa dhidi ya serikali hii basi hakutakuwa tena na uchaguzi ktk nchi hii.
Wewe ndio uliongea na wafadhili hao? Hii mbona kali
 
Bank sasa siyo mahala salama kwa pesa za wafanyabiashara kwani TRA huenda kufunga A/C kienyeji na kupora pesa za wafanyabiashara kwa njia haramu za kishetani
Hahahahahaaa, na wasipoweka bank wataanza kuja kusachi majumbani mwenu
 
Kwa hiyo unamlilia nani sasa? Fafanua mana madudu haya yapo toka kitambo shida ni kwamba wewe uliishia kama malaika sasa kuwa shetani hutaki...

Nchi hii ni ya watanzania. Tusipojua kutengenisha siasa zetu za vyama na maisha yetu ya kawaida, tutaendelea kuwa maskini wa mwisho.
Issue za TRA sio za leo wala jana. Zipo miaka mingi. Umefika muda sasa ziangaliwe. Kukwepa kodi, sehemu kubwa walikuwa wanachangia wao. Risiti feki nani aliyekuwa anatengeneza na wao bila kujua?
Sasa wamehamia kukamua kodi ambazo wala hazipo. Hawa jamaa wanajijari wao tu. Rushwa tupu. Sasa hilo nalo ni tatizo la nani?
 
Kwa hiyo unamlilia nani sasa? Fafanua mana madudu haya yapo toka kitambo shida ni kwamba wewe uliishia kama malaika sasa kuwa shetani hutaki...
Kama hayakuhusu kukaa kimya unaona mzigo?
Pilipili hii ya shamba wewe haikuhusu bro..........!
Kaa kimya tu ule mkate wako!
 
Pole sana mkuu, kama nawe umefikiwa.

However, I should remind you; you need to be consistent.

IfahamikesSitetei upande wowote hapo. Kwa upande mmoja umesema "makosa ya kiuhasibu", na huo wapili unaoulalamikia, kazi yao ni kukusanya kodi ili serikali iweze kuendesha mambo yake. Kama wanagundua "makosa ya kiuhasibu" yaliyofanyika na kuikosesha serikali mapato, hapo sasa wafanyeje?
Ninalokubaliana nalo ni makosa ya kufunga biashara.
Ni kweli mkuu.
Ideally , kodi hutokana na mapato.
Sasa kodi ikigeuka kuwa fine kama za traffic wa barabarani kuwa ndio msingi wa mapato, hapo maana ya kodi, kwa msingi wa kuyapiga kodi mapato ya kibiashara tena hakuna.

Kwa misingi hiyo kama vitabu havijakaa vizuri unalipishwa mamilioni.
Ndiyo, serikali inapata mapato lakini si kwa maana ya kodi ya mapato ya kibiashara kama tunavyofahamu.
 
Tunalazimika kueleza jinsi TRA wanavyofunga biashara za wafanyabiashara.

TRA wamepangiwa malengo ya ukusanyaji fedha, kinyume cha hivyo mtu anafukuzwa kazi na ajira inakoma.

TRA kama ilivyo ada kwao, hawafuati weledi wa kibiashara au kuona jinsi ya kupata mapato endelevu, wao ni kutimiza amri ya mkubwa wao, iwe isiwe.

Mfano:
Wafanyakazi wawili wawili au watatu wanapewa kampuni mbili au tatu na wanatakiwa watazame makosa ya kiuhasibu ndani ya returns za mfanyabiashara zilizowasilishwa TRA hata miaka 10 iliyopita.

Haijalishi kama kuna wenzao walipita mwaka jana na mwaka juzi. Ni kama mtu anaamrishwa kuvuna shamba lililokwisha kuvunwa.

UKWELI hapo ni kwamba hakuna kodi ya mapato inayotafutwa, ni hela tu, basi. Uwe nazo usiwe nazo unalijua Jiji.

Hivyo makosa ya kiuhasibu yanatafutwa kwa nguvu. Tunajua fika level ya wahasibu wetu, ambao hata serikalini wapo, na makosa yanayoweza kufanywa.

Hiyo timu ya wakaguzi wa TRA wanapata makosa ya kulazimisha kama kumi hivi, na huo ndio mtaji wa “kodi”, na si kutokana na mapato.

Kwanza, makosa hayo yajengewa uhalali wa kupigwa kodi
Pili, yanapigwa fine
Tatu, yanapigwa interest-riba

Yakijumlishwa ndiyo eti unaletewa assessment ya kodi unayodaiwa-wizi mtupu, maana hizi ni kodi za kupikwa.

Ukiwa na Tax Consultant ataweza kupangua baadhi ya hizo “kodi”, kama huna TRA wanakimbilia akaunti yako benki na kukomba chochote kilichomo.

Sasa hii ni State Robbery.
Na haya yanafanyika kila leo.

Matokeo yake:
Sasa hivi kuna misururu ya wafanyabiashara kule matawi ya TRA, wanafunga biashara.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba kodi iliyokokotolewa haitokani na mapato, bali makosa ya kiuhasibu.
Kodi iliyokokotolewa na TRA hao haiwezi kulipika kutokana na mapato ya kibiashara, hivyo mtu kulazimika kufunga biashara.

Makampuni tunayoyaona mitaani yametembelewa mara tatu au nne kwa mwaka, TRA wanataka kodi za kupikwa.

USHAURI
TRA inatakiwa ifanye kazi kwa madhumuni iliyo anzishwa, yaani kukokotoa kodi kutokana na MAPATO YA BIASHARA na si vinginevyo.
Sasa hivi kodi zinachukiliwa kutokana na punitive measures na si mapato, hivyo kula mtaji wa biashara.
Kiuchumi hili kosa linaua biashara nchini.
mitano tena.jpg

Wameshafika mpaka kwa wakulima. Hii niliifungulia post naona mod wameifuta
 
Tunalazimika kueleza jinsi TRA wanavyofunga biashara za wafanyabiashara.

TRA wamepangiwa malengo ya ukusanyaji fedha, kinyume cha hivyo mtu anafukuzwa kazi na ajira inakoma.

TRA kama ilivyo ada kwao, hawafuati weledi wa kibiashara au kuona jinsi ya kupata mapato endelevu, wao ni kutimiza amri ya mkubwa wao, iwe isiwe.

Mfano:
Wafanyakazi wawili wawili au watatu wanapewa kampuni mbili au tatu na wanatakiwa watazame makosa ya kiuhasibu ndani ya returns za mfanyabiashara zilizowasilishwa TRA hata miaka 10 iliyopita.

Haijalishi kama kuna wenzao walipita mwaka jana na mwaka juzi. Ni kama mtu anaamrishwa kuvuna shamba lililokwisha kuvunwa.

UKWELI hapo ni kwamba hakuna kodi ya mapato inayotafutwa, ni hela tu, basi. Uwe nazo usiwe nazo unalijua Jiji.

Hivyo makosa ya kiuhasibu yanatafutwa kwa nguvu. Tunajua fika level ya wahasibu wetu, ambao hata serikalini wapo, na makosa yanayoweza kufanywa.

Hiyo timu ya wakaguzi wa TRA wanapata makosa ya kulazimisha kama kumi hivi, na huo ndio mtaji wa “kodi”, na si kutokana na mapato.

Kwanza, makosa hayo yajengewa uhalali wa kupigwa kodi
Pili, yanapigwa fine
Tatu, yanapigwa interest-riba

Yakijumlishwa ndiyo eti unaletewa assessment ya kodi unayodaiwa-wizi mtupu, maana hizi ni kodi za kupikwa.

Ukiwa na Tax Consultant ataweza kupangua baadhi ya hizo “kodi”, kama huna TRA wanakimbilia akaunti yako benki na kukomba chochote kilichomo.

Sasa hii ni State Robbery.
Na haya yanafanyika kila leo.

Matokeo yake:
Sasa hivi kuna misururu ya wafanyabiashara kule matawi ya TRA, wanafunga biashara.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba kodi iliyokokotolewa haitokani na mapato, bali makosa ya kiuhasibu.
Kodi iliyokokotolewa na TRA hao haiwezi kulipika kutokana na mapato ya kibiashara, hivyo mtu kulazimika kufunga biashara.

Makampuni tunayoyaona mitaani yametembelewa mara tatu au nne kwa mwaka, TRA wanataka kodi za kupikwa.

USHAURI
TRA inatakiwa ifanye kazi kwa madhumuni iliyo anzishwa, yaani kukokotoa kodi kutokana na MAPATO YA BIASHARA na si vinginevyo.
Sasa hivi kodi zinachukiliwa kutokana na punitive measures na si mapato, hivyo kula mtaji wa biashara.
Kiuchumi hili kosa linaua biashara nchini.
Jiwe alianza kuwawinda akina massawe, mushi, mosha, mbowe, muro nk amewamaliza sasa yuko na hao waliokuwa washangiliaji!! hadi mkome kuvaa chupi za kijani yenye picha ya dubwana baya lenye vichwa viwili! kikwetu tunasema kura waya/saga chupa/kunyweni sumu tu mlipoambiwa ni muovu mlitoa mimeno kama ngiri hadi mtakoma!! poleni eeh ndugu
 
Jiwe alianza kuwawinda akina massawe, mushi, mosha, mbowe, muro nk amewamaliza sasa yuko na hao waliokuwa washangiliaji!! hadi mkome kuvaa chupi za kijani yenye picha ya dubwana baya lenye vichwa viwili! kikwetu tunasema kura waya/saga chupa/kunyweni sumu tu mlipoambiwa ni muovu mlitoa mimeno kama ngiri hadi mtakoma!! poleni eeh ndugu
Asante ndugu.....!
 
Asante ndugu.....!
For some reason, I am with 'him' (vichwa viwili) on this!

Sio kila jambo lifanywalo ni baya. Utekelezaji kwa baadhi ya watumishi unaweza kuchangia sana mwonekano huo.

Kule kwingine ulikowahi kuandika kuwa umewahi kuishi huko, sijui mtu utakwepaje kulipa kodi stahiki!
Hapa kwetu hata kutoa tu 'receipt' ya mauzo ni kazi, na ukiidai unatazamwa kwa jicho kali sana. Huko kwingine hawahangaishwi tena na hivi vi-risiti vya mauzo. Bidhaa inapo'scanniwa' wakati wa mauzo, tayari na kodi imeshaingia mahala stahili. Sijui TRA watatufikisha huko lini?

Baadhi ya kelele na vilio vingi hivi vinaweza kuwa vinasababishwa na mafanikio ya kuzuia mbinu za kukwepa kodi wanazozifanya TRA.
 
Hii habari ya kutaka kujenga nchi kwa hela za ndani itatugharimu kama taifa.

Tutabanwa hadi tubanike, saivi naona Leseni ya Udereva imepanda toka 40,000 hadi 70,000 halafu kimya kimya, hatutangazi sasaivi ili msije kupiga kelele. Yaani unaongeza kodi kwenye leseni ya udereva kwa 75% serious?
 
Tunalazimika kueleza jinsi TRA wanavyofunga biashara za wafanyabiashara.

TRA wamepangiwa malengo ya ukusanyaji fedha, kinyume cha hivyo mtu anafukuzwa kazi na ajira inakoma.

TRA kama ilivyo ada kwao, hawafuati weledi wa kibiashara au kuona jinsi ya kupata mapato endelevu, wao ni kutimiza amri ya mkubwa wao, iwe isiwe.

Mfano:
Wafanyakazi wawili wawili au watatu wanapewa kampuni mbili au tatu na wanatakiwa watazame makosa ya kiuhasibu ndani ya returns za mfanyabiashara zilizowasilishwa TRA hata miaka 10 iliyopita.

Haijalishi kama kuna wenzao walipita mwaka jana na mwaka juzi. Ni kama mtu anaamrishwa kuvuna shamba lililokwisha kuvunwa.

UKWELI hapo ni kwamba hakuna kodi ya mapato inayotafutwa, ni hela tu, basi. Uwe nazo usiwe nazo unalijua Jiji.

Hivyo makosa ya kiuhasibu yanatafutwa kwa nguvu. Tunajua fika level ya wahasibu wetu, ambao hata serikalini wapo, na makosa yanayoweza kufanywa.

Hiyo timu ya wakaguzi wa TRA wanapata makosa ya kulazimisha kama kumi hivi, na huo ndio mtaji wa “kodi”, na si kutokana na mapato.

Kwanza, makosa hayo yajengewa uhalali wa kupigwa kodi
Pili, yanapigwa fine
Tatu, yanapigwa interest-riba

Yakijumlishwa ndiyo eti unaletewa assessment ya kodi unayodaiwa-wizi mtupu, maana hizi ni kodi za kupikwa.

Ukiwa na Tax Consultant ataweza kupangua baadhi ya hizo “kodi”, kama huna TRA wanakimbilia akaunti yako benki na kukomba chochote kilichomo.

Sasa hii ni State Robbery.
Na haya yanafanyika kila leo.

Matokeo yake:
Sasa hivi kuna misururu ya wafanyabiashara kule matawi ya TRA, wanafunga biashara.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba kodi iliyokokotolewa haitokani na mapato, bali makosa ya kiuhasibu.
Kodi iliyokokotolewa na TRA hao haiwezi kulipika kutokana na mapato ya kibiashara, hivyo mtu kulazimika kufunga biashara.

Makampuni tunayoyaona mitaani yametembelewa mara tatu au nne kwa mwaka, TRA wanataka kodi za kupikwa.

USHAURI
TRA inatakiwa ifanye kazi kwa madhumuni iliyo anzishwa, yaani kukokotoa kodi kutokana na MAPATO YA BIASHARA na si vinginevyo.
Sasa hivi kodi zinachukiliwa kutokana na punitive measures na si mapato, hivyo kula mtaji wa biashara.
Kiuchumi hili kosa linaua biashara nchini.
Masuali yangu ni haya mawili tu kwako mleta mada.

1. Kuna biashara gani ambayo si ya mfanya biashara?
2. Mzalendo ni nani?
 
Mkuu sio kila kitu ni siasa.

Ebo kodi ni siasa Mkuu,hivi kura yako una piga kwa kutazama sura ya mtu au rangi ya chama !.

Kuna jirani yangu wakati wa kampeni alikuwa mshabiki mzuri wa mboga mboga juzi kati shule ya mwanae imepigwa pini na TRA (St Jude) kabaki kulia lia tu kamwambia Sisi tumeshazoea kulipa school fees wewe ulikuwa unasaidiwa sasa nenda kaombe msaada ulikoshabikia.

Halafu kuna uhusiano gani kati ya ujinga na kushabikia utawala huu ?.Utafiti wangu unaonyesha wajinga wengi ni wapenzi wa Mboga mboga.
 
Tatizo hata wenyewe wanashinda kutafasiri sheria, wanakimbilia, afisa anaruhusiwa kukadiria kodi anavyoona, Suluhisho ni kubadili sheria na kufanya kila kitu online, bila kukutana na ofisa wa tra kama nchi zilizoendelea.
 
Ebo kodi ni siasa Mkuu,hivi kura yako una piga kwa kutazama sura ya mtu au rangi ya chama !.

Kuna jirani yangu wakati wa kampeni alikuwa mshabiki mzuri wa mboga mboga juzi kati shule ya mwanae imepigwa pini na TRA (St Jude) kabaki kulia lia tu kamwambia Sisi tumeshazoea kulipa school fees wewe ulikuwa unasaidiwa sasa nenda kaombe msaada ulikoshabikia.

Halafu kuna uhusiano gani kati ya ujinga na kushabikia utawala huu ?.Utafiti wangu unaonyesha wajinga wengi ni wapenzi wa Mboga mboga.
Tatizo mtu akifika mwisho wa kufikiri huwa hana hoja ya kuchangia!
Undelea na tafiti zako zisizo na machapisho wala rejea, pengine utapata point za kuchangia.
 
Nchi hii ni ya watanzania. Tusipojua kutengenisha siasa zetu za vyama na maisha yetu ya kawaida, tutaendelea kuwa maskini wa mwisho.
Issue za TRA sio za leo wala jana. Zipo miaka mingi. Umefika muda sasa ziangaliwe. Kukwepa kodi, sehemu kubwa walikuwa wanachangia wao. Risiti feki nani aliyekuwa anatengeneza na wao bila kujua?
Sasa wamehamia kukamua kodi ambazo wala hazipo. Hawa jamaa wanajijari wao tu. Rushwa tupu. Sasa hilo nalo ni tatizo la nani?
Huwezi kutenganisha mfumo mbovu wa utawala na taasisi ambazo ziko chini ya mfumo wa kisiasa. Kwa hiyo dawa ni nini?
 
Kwa hiyo solution ni kulilia mitandaoni ndio watajirekebisha? 😂😂 Kama suluhisho hujui bora hata usingeandika,mana haya malalamiko yashasemwa sana, wafanyabishara, wanasiasa na wawekezaji pia. Unahisi ili TRA ijirekebishe nini kifanyike?
Kama hayakuhusu kukaa kimya unaona mzigo?
Pilipili hii ya shamba wewe haikuhusu bro..........!
Kaa kimya tu ule mkate wako!
 
Back
Top Bottom