TRA wanavyofunga biashara za wazalendo

TRA wanavyofunga biashara za wazalendo

TAX BURDEN PRINCIPLE (KANUNI YA MIZANIA/MZIGO WA KODI)

Jambo kubwa nililojifunza kutoka kwa wachangiaji wa huu uzi ni kuwa ufahamu wa kodi ni tatizo kubwa kuliko kodi yenyewe. The problem is not "tax" but "understanding of tax".

Jambo muhimu kwa kila mfanyabiashara si tu kujua aina za kodi bali kujua MIZANIA YA KODI (TAX BURDEN) ktk aina hizo za kodi.

Laiti wafanyabiashara weng wangejua kanuni (principle) hii ya TAX BURDEN watafahamu kuwa kodi nyingi hazilipwi na wafanyabiashara bali wao ni wakusanyaji (Witholding tax agent) na watoa taarifa ktk mamlaka husika (file returns).

TAX BURDEN ni kanuni inayoonyesha ni nani haswa (Halisi) anawajibika kuilipia kodi fulani. Kwa dhana hii kuna tofauti kati ya mkusanyaji kodi na mlipaji wa kodi. Unaweza kuwa mkusanyaji kodi fulani lakini si wewe mlipaji wa kodi husika. Na hapa ndio wafanyabiashara wengi wameshindwa kuelewa kanuni hii na kuhisi wanaonewa au kulipa kodi kupita kiasi. Si sahihi

Kwanza, Mfano ni kodi ktk mishahara ya wafanyakazi inayoitwa PAYE anayelipa(kukatwa) ni mfanyakazi husika ila mwajiri anaiwakilisha tu ofisi za mapato

Pili, Kodi ya zuio (Withholding tax) ktk kodi ya pango (rent) na huduma (outsourced services) anayelipa/kukatwa ni Land Lord au anayepokea pango na sio mfanyabiashara anayelipa pango. Jukumu la mfanyabiashara ni kuikata na kuipeleka ofisi ya mamlaka.

Vivyo hivo ktk kodi ya ongezeko la thamani (Value added tax - VAT) pamoja na Capital gain tax ni kodi ambazo wafanyabiashara hawalipi wao direct ila wanakusanya kwa watu wengine na kuikabidhi kwa mamlaka husika.

Changamoto inakuja pale ambapo aliyepewa jukumu la kukusanya kodi kisheria hafanyi jukumu lake (failure to collect and remit tax to authority), hapo ndipo TAX BURDEN huhama kutoka kwa MLIPAJI halisi wa kodi husika kwenda kwa MKUSANYAJI., na wafanyabiashara wengi huishia kuumia kwa kubeba msalaba usio wao.

Kutokana na principle hii ya TAX BURDEN tayari tunaona kodi nyingi kimsingi hazilipwi na wafanyabiashara bali wao ni wakusanyaji tu (Collect and file returns). Ukielewa principle hii kama mfanyabiashara utafanikiwa sana katika biashara yako na utapunguza Tax liabilities zisizo na ulazima.

ITAENDELEA..
Mkuu asante kwa ushauri.
Lakini nafikiri unajua fika kuwa kodi kama With Holding Tax na Provisional Tax huwa ni sehemu tu ya Annual Corprate Tax.
Na unajua madudu ambayo yanafanyika katika hili.
Kodi hizi zinakatwa (hasa WHT) kupita na kuzidi makadirio ya Corporate Tax,
Na ikishakatwa hairudishwi.
Nataka neno lako katika hili.

Halafu kwenye Invoicing.
Wafanyabiashara wengi hawalipwi in time, lakini wanapaswa kuwasilisha VAT at source and in time.
Yaani ukimpelekea Invoice na risiti ya EFD mteja wako(mara nyingi Serikali) unatakiwa ulipe a kodi uliyotakiwa kukusanywa ndani ya mwezi mmoja.
Uzoefu unaonyesha kuwa kuna wafanyabiashara hawalipwi hata ndani ya mwaka hivyo kufilisi kampuni.

Haya mambo ya vitabuni wee yaache tu, uhalisia na TRA ni kitu kingine.
 
Ndio elimu hii , na mnakubali kabisa kufundishwa huu ujinga

1. Kama mfanyabiashara sii mlipa kodi, kwann watu wa kodi wanamfuata, kwann wasimfute mhusika moja kwa moja?

2. Kama yeye si mlipa kodi, kwann kodi hizo zinaondoka hadi na mtaji wake na kuua biashara na kumwacha na madeni?

3. Kama yeye sii mlipa kodi hiyo, kwann hiyo pesa ikiondoka anai feel kwenye mzunguko wake wa pesa kwamba kuna kitu kimepungua??

Acheni kujificha kwenye vichaka vya ajabu ajabu, wekeni mfumo sahihi wa ukusanyaji kodi, kateni kodi za halali sehem halali
Wewe ndiyo umejificha kwenye kicha cha ajabu ajabu hujui kuwa baadhi ya maofisa wa TRA huwabambikia kodi kubwa wafanyabiashara kwa makusudi kutengeneza mazingira ya Rushwa, umejitoa fahamu zote na kuwaona maofisa wa TRA ni mungu na malaika hawakosei wapo sahihi kwa kila jambo
 
Mkuu asante kwa ushauri.
Lakini nafikiri unajua fika kuwa kodi kama With Holding Tax na Provisional Tax huwa ni sehemu tu ya Annual Corprate Tax.
Na unajua madudu ambayo yanafanyika katika hili.
Kodi hizi zinakatwa (hasa WHT) kupita na kuzidi makadirio ya Corporate Tax,
Na ikishakatwa hairudishwi.
Nataka neno lako katika hili.

Halafu kwenye Invoicing.
Wafanyabiashara wengi hawalipwi in time, lakini wanapaswa kuwasilisha VAT at source and in time.
Yaani ukimpelekea Invoice na risiti ya EFD mteja wako(mara nyingi Serikali) unatakiwa ulipe a kodi uliyotakiwa kukusanywa ndani ya mwezi mmoja.
Uzoefu unaonyesha kuwa kuna wafanyabiashara hawalipwi hata ndani ya mwaka hivyo kufilisi kampuni.

Haya mambo ya vitabuni wee yaache tu, uhalisia na TRA ni kitu kingine.
TRA yafaa ifumuliwe isukwe upya na wale maofisa vinara wa kuwabambikia kodi kubwa wafanyabiashara kuwafungia account kuwafungia biashara watu wachunguzwe na Takukuru juu ya uhalali wa mali zao binafsi
 
Ndani ya miaka 3 nchi itakua hoi sana
Wafanyabiashara wakubwa wamehamishia pesa zao Nchi Jiran kukwepa A/C zao kufungwa na TRA kienyeji kishamba kwa njia haramu za kishetani
 
Ndio elimu hii , na mnakubali kabisa kufundishwa huu ujinga

1. Kama mfanyabiashara sii mlipa kodi, kwann watu wa kodi wanamfuata, kwann wasimfute mhusika moja kwa moja?

2. Kama yeye si mlipa kodi, kwann kodi hizo zinaondoka hadi na mtaji wake na kuua biashara na kumwacha na madeni?

3. Kama yeye sii mlipa kodi hiyo, kwann hiyo pesa ikiondoka anai feel kwenye mzunguko wake wa pesa kwamba kuna kitu kimepungua??

Acheni kujificha kwenye vichaka vya ajabu ajabu, wekeni mfumo sahihi wa ukusanyaji kodi, kateni kodi za halali sehem halali
Nimesoma andiko lake nikabaki kushangaa naona analeta elimu ya darasani ambayo ni tofauti kabisa na uhalisia..Mwambie afungue biashara yake afu a apply hizo theory zake tuone atafika wapi...wasomi wetu ni shida sana
 
Ndio maana hata mabenki sasa hivi wanashindwa kutoaa mikopo sasbabu hamna. Mfanyabiashara mjiinga ataacha pesa yake benki huku akijua kwamba T.R.A wanamnyemelea.kwahio mwisho wa siku ni Tanzania inaingia kwenye great depression.
 
Nimesoma andiko lake nikabaki kushangaa naona analeta elimu ya darasani ambayo ni tofauti kabisa na uhalisia..Mwambie afungue biashara yake afu a apply hizo theory zake tuone atafika wapi...wasomi wetu ni shida sana
Ha ha ha hao wasomi watetea uonevu uovu Rushwa za baadhi ya maofisa wa TRA ni bora wangesalia na Elimu ya darasa la pili kuliko wakajiita wasomi huku wakitetea mateso manyanyaso uonevu kwa wafanyabiashara, hakunaga msomi wa hivyo
 
Hawa jamaa kuanzia kamishina ni ndumi la kuwili sana. Wanapoongea katika vyombo vya habari juu ya taasisi hii na majukumu yake utasema hawa wafanyabiashara ni wakorofi sana na sio waelewa. Ila ukipewa rekodi ya madudu yao wanayofanya ndipo unajua kuwa haujui......

Tazama tu hata makadirio ya kodi ya bidhaa zinazopita bandarini. Yaani magharama yapo juu kweli kweli kuliko hata bei ya bidhaa. Unanunua gari Us dola 2,500, kodi inakuja milioni saba..... Sasa unajiuliza imekuwaje kodi ni zaidi ya 100% ya original price ya bidhaa?!

Tunahitaji kiwakazia wale misukule pale bungeni kujadili upya hizi kanuni za TRA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wakati Sasa na sisi Tanzania tuwe na Bodi ya Rufaa za Kodi yenye kujielewa
 
Ndio maana hata mabenki sasa hivi wanashindwa kutoaa mikopo sasbabu hamna. Mfanyabiashara mjiinga ataacha pesa yake benki huku akijua kwamba T.R.A wanamnyemelea.kwahio mwisho wa siku ni Tanzania inaingia kwenye great depression.
Wafanyabiashara wengi sasa wanabuni mbinu za kuhifadhi pesa zao Nchi zingine ama hata kuficha ndani mwao, hawana imani na Bank tena, na hii ni hatari kubwa kwa usitawi wa mabenk na mifumo ya mikopo ni vigumu Tanzania kupiga hatua kimaendeleo kwa kuendelea kuwalinda baadhi ya maofisa wa TRA vinara wa kuwabambikia kodi kubwa, kuwafungia Account, kuwafungia biashara wafanyabiashara wengi.
 
Ni wakati Sasa na sisi Tanzania tuwe na Bodi ya Rufaa za Kodi yenye kujielewa
TRA ifumuliwe isukwe upya imejaa wala Rushwa mno akina masamaki wapo wengi sana, Takukuru iwachunguze maofisa wa TRA wale vinara wa kufunga biashara na Account za watu kwa njia haramu za kishetani
 
Njia pekee ya kumaliza Tatizo la usumbufu wa TRA ni kuundwa tume ichunguze mapungufu yote juu ya ukasanyaji kodi na pia wale maofisa wasumbufu wale majanga kwa wafanyabiashara wawajibishwe kwa manufaa ya Taifa
 
Wewe ndiyo umejificha kwenye kicha cha ajabu ajabu hujui kuwa baadhi ya maofisa wa TRA huwabambikia kodi kubwa wafanyabiashara kwa makusudi kutengeneza mazingira ya Rushwa, umejitoa fahamu zote na kuwaona maofisa wa TRA ni mungu na malaika hawakosei wapo sahihi kwa kila jambo
Umeandika nn hapa? Mada inahusiana na nn? Unapinga au unakubali? Unapinga nn unakubali nn?

Comment yako ni kama polo haieleweka inasimama wapi, unapinga nn inaafiki nn
 
Umeandika nn hapa? Mada inahusiana na nn? Unapinga au unakubali? Unapinga nn unakubali nn?

Comment yako ni kama polo haieleweka inasimama wapi, unapinga nn inaafiki nn
Ni vigumu kunielewa kwa sababu wewe ni mnufaika wa Rushwa na uonevu wote wa baadhi ya maofisa wa TRA
 
Ni vigumu kunielewa kwa sababu wewe ni mnufaika wa Rushwa na uonevu wote wa baadhi ya maofisa wa TRA

Ume misquote , rudi nenda ka quote ulie tarajia Ku quote

Wazazi wako bora wangetumia condom tu,
Unakua kama nyumbu, unavamia tu kila kinachokuja mbele yako
 
Tunalazimika kueleza jinsi TRA wanavyofunga biashara za wafanyabiashara.

TRA wamepangiwa malengo ya ukusanyaji fedha, kinyume cha hivyo mtu anafukuzwa kazi na ajira inakoma.

TRA kama ilivyo ada kwao, hawafuati weledi wa kibiashara au kuona jinsi ya kupata mapato endelevu, wao ni kutimiza amri ya mkubwa wao, iwe isiwe.

Mfano:
Wafanyakazi wawili wawili au watatu wanapewa kampuni mbili au tatu na wanatakiwa watazame makosa ya kiuhasibu ndani ya returns za mfanyabiashara zilizowasilishwa TRA hata miaka 10 iliyopita.

Haijalishi kama kuna wenzao walipita mwaka jana na mwaka juzi. Ni kama mtu anaamrishwa kuvuna shamba lililokwisha kuvunwa.

UKWELI hapo ni kwamba hakuna kodi ya mapato inayotafutwa, ni hela tu, basi. Uwe nazo usiwe nazo unalijua Jiji.

Hivyo makosa ya kiuhasibu yanatafutwa kwa nguvu. Tunajua fika level ya wahasibu wetu, ambao hata serikalini wapo, na makosa yanayoweza kufanywa.

Hiyo timu ya wakaguzi wa TRA wanapata makosa ya kulazimisha kama kumi hivi, na huo ndio mtaji wa “kodi”, na si kutokana na mapato.

Kwanza, makosa hayo yajengewa uhalali wa kupigwa kodi
Pili, yanapigwa fine
Tatu, yanapigwa interest-riba

Yakijumlishwa ndiyo eti unaletewa assessment ya kodi unayodaiwa-wizi mtupu, maana hizi ni kodi za kupikwa.

Ukiwa na Tax Consultant ataweza kupangua baadhi ya hizo “kodi”, kama huna TRA wanakimbilia akaunti yako benki na kukomba chochote kilichomo.

Sasa hii ni State Robbery.
Na haya yanafanyika kila leo.

Matokeo yake:
Sasa hivi kuna misururu ya wafanyabiashara kule matawi ya TRA, wanafunga biashara.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba kodi iliyokokotolewa haitokani na mapato, bali makosa ya kiuhasibu.
Kodi iliyokokotolewa na TRA hao haiwezi kulipika kutokana na mapato ya kibiashara, hivyo mtu kulazimika kufunga biashara.

Makampuni tunayoyaona mitaani yametembelewa mara tatu au nne kwa mwaka, TRA wanataka kodi za kupikwa.

USHAURI
TRA inatakiwa ifanye kazi kwa madhumuni iliyo anzishwa, yaani kukokotoa kodi kutokana na MAPATO YA BIASHARA na si vinginevyo.
Sasa hivi kodi zinachukiliwa kutokana na punitive measures na si mapato, hivyo kula mtaji wa biashara.
Kiuchumi hili kosa linaua biashara nchini.
Nilimwona Lissu kwenye kampeni zake akipita kariakoo, mkamwambia mambo yako poa kabisa.

Ni kama vile haya usemayo yanawapata watu wachache sana.
 
Back
Top Bottom