TRA wana jambo lao, Sio kwa watu maarufu tu, ndugu yangu alieanza biashara 2015 kwa mara ya kwanza kapigwa faini nzito ya kukwepa kodi,

Niwaambie TU wanajf
Hamna mfanyabiashara anapenda kukwepa Kodi kwa maendeleo ya nchi yake

Tatizo Ni

1. mfumo wetu wa Kodi umekaa kinyonyaji sana, anaetunga sheria na kanuni za Kodi ni mwanasiasa bill kumhusisha mfanyabiashara na hayajui mazingira halisi ya biashara.

Ukiifuata sheria ya Kodi inavotaka unafilisika mchana kweupe na hakuna anaekuonea huruma, kiukweli Kodi zetu sio rafiki kwa mfanyabiashara yeyote mzalendo.

2. Matumizi ya Kodi,
Inaumiza Sana unalipa Kodi kizalendo afu unaskia Kodi yako uliolipa Kuna wahuni wanafuja fuja TU kwa maslahi Yao binafsi Tena kwa majigambo lukuki wakiitana majina wanayojua wao kana kwamba sisi wengine hatuna akili wametupa limbwata.Inaumiza sana na kuvunja Moyo.
Na hapa umezungumzia Compliance za TRA pekee.

Bado mfanya biashara huyo huyo anadaiwa Leseni, Fire, Afya, Ulinzi Shirikishi, Wakala wa Vipimo, TBS, Usafi, Parking n.k n.k..

Na wote hao kila mmoja anakuja au unamfata kwa wakati wake.

Hii nchi mfanyabiashara ili Ufanikiwe ni lazima utaonekana haramia tu..

Wakati huo huo Ripoti za CAG kila mwaka zinataja matumizi mabaya ya Pesa za Umma miongoni mwa Watendaji wa Umma. Na hakuna hatua zinachukuliwa kudhibiti hili
 
Hivi unajisikiaje unajikaba kulipa kodi halafu unakuja kuambiwa serikali imekopa pesa Trillion 4 kwa ajili ya kuboresha uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma, just imagine, ndio kitua gani hicho? Halfu riba tilllion 2, hivi hata ingekuwa wewe utajisikiaje?
Sasa serikali inajiweza kifedha!!?..makusanyo kiasi gani na bajeti kiasi gani!?
 
Umenunua bidhaa ya elf 20,.... Kwenye risiti inaonesha umelipia vat asilimia 18% sawa na 3,050

Unaenda kuiuza kwa shilingi elf 25,000, ukitoa risiti kwa bei hio ni kwamba umechukua chako shilingi 21,186 na kwenye vat itayohesabiwa ya shilingi 3,814 utajilipa mwenyewe ile vat ya mwanzo ya 3,050, Tra wanachotaka ni hio iliyozidi ambayo haikuhusu (3,814 - 3,050 = 764)

unakusanya pesa yote na kufidia vat uliyolipa... Tatizo lipo wapi ???
Mkuu,
Achana na uchumi wa makaratasi,
Twende kwenye vitu vyenye uhalisia.

Ndo maana nmekuuliza hivi unajua

1. cement mfuko mmoja unauzwaje nawe unapaswa ukauzeje?

2. Soda/bia kreti moja Inauzwa sh. Ngapi na Ina faida sh ngapi?

3. Sukari kiroba kimoja kinauzwa sh. Ngap,unatakiwa kuuza sh. Ngap na faida itakua Kias gani.

4. Mchele kiroba kimoja kg100 kinanunuliwa sh ngapi, unatakiwa kuuza sh ngapi na faida Kia's gani?

Hivi unadhan wafanyabiashara wakiamua kuuza kwa kutaka faida unazosema wewe kwenye makaratasi, unadhan Kuna mwananchi atalimika uko mtaani?

Au Ndo mtakuja mitandaoni kulalamika makali ya maisha, serikali itangaze Bei elekezi na iweke taski force kukamata na kuonea wafanyabiashara.
 
Tatizo umesoma tu kichwa cha habari hujasoma post, soma kila neno kwenye post uniambie ni wapi nomefurahia
Hapa unaemlaumu kwa uzembe Ni Nani?

Hiki Umeandika wewe au mwingine?

"Ila nikowa muwazi bila kupepesa macho, kapigwa faini kwa uzembe wake maana haiingii nimeshangaa inakuwaje anunue mzigo wenye kodi ya vat alafu asitoe risiti"
 
Umenunua bidhaa ya elf 20,.... Kwenye risiti inaonesha umelipia vat asilimia 18% sawa na 3,050

Unaenda kuiuza kwa shilingi elf 25,000, ukitoa risiti kwa bei hio ni kwamba umechukua chako shilingi 21,186 na kwenye vat itayohesabiwa ya shilingi 3,814 utajilipa mwenyewe ile vat ya mwanzo ya 3,050, Tra wanachotaka ni hio iliyozidi ambayo haikuhusu (3,814 - 3,050 = 764)

unakusanya pesa yote na kufidia vat uliyolipa... Tatizo lipo wapi ???
Umepiga mahesabu yako kitoto Sana

Haya mahesabu yako wanapiga sn watoto wa pale IFM kila siku, ila ukiingia mtaani Hali Ni tofauti kabisa.

Bado mfanya biashara huyo huyo anadaiwa BIMA, Leseni, Fire, Afya, Ulinzi Shirikishi, Wakala wa Vipimo, TBS, Usafi, Parking n.k n.k..
 
Nimejiridhisha kwamba kwa sasa TRA wana jambo lao kwa wakwepa kodi maana si kwa kelele hizi, wakiona unakwepa wanapita na wewe.

Mwezi uliopitwa nilipatwa na simanzi baada ya kuona ndugu yangu kapatwa na pigo zito la kulipa faini ya TRA, masikitiko yake yamenigusa na mwanzoni nilidhani kaonewa lakini hali ni tofauti.



Hawa kina diamond na huyo pck wanaolalamika ni kwasababu ni maarufu ndio maana wanasikika lakini wakae wakijua sio wao tu, hii ni operation kubwa sana iliyonasa wengi tena kihalali bila uonevu wala mabavu.



Binafsi nina ndugu yangu alianza biashara kwenye mwaka 2015 hivi, Enzi hizo Magu kaingia na msisitizo watu watoe risiti kwa mashine, hapa waliokuwa hawana mashine ndio walikiona cha mtemakuni, kukwepa huu mhaho wengi ilibidi wanunue hizo mashine ila wakawa wanatoa risiti chache za kuzugia, kwa sasa hali ni tofauti kabisa, hio style ya kutoa risiti za kuzugia utapigwa pini tu, yaani kwa sasa wanafatilia mfano biashara za kuuza bidhaa inabidi mzigo ulionunua uwe na risiti yake ya mashine ya tra na pia uwe unauza kwa kutoa risiti kwa mashine, huyu ndugu yangu alipodakwa ni kwamba alikuwa ananunua bidhaa na alikuwa anapewa risiti lakini yeye anatoa tu risiti chache za kuzugia kwa bidhaa alizouza, Tra wakastuka wakaenda dukani kwake kukagua mzigo wakamwambia wameona kwenye system yao anauziwa bidhaa nyingi na watu wanaomuuzia kwa risiti lakini yeye vitu anavyouza kwa risiti ni vichache, mzigo uliobaki uko wapi ? Akaanza kupiga kiswahili pale lakini haikusaidia, TRA wakahitimisha kihalali kwamba anauza bila kutoa risiti a.k.a anasaidia ukwepaji wa kodi.

Wakati anasubiri hatma ya kitachomkuta alitumia connections zake na kwenda kuwabembeleza Tra kwenye ofisi zao lakini wapi... Kwanza hata huko akagundua wapo wengi.

mwezi uliopita kapigwa faini ya takribani milioni 160 kwa kosa la kuuza bidhaa bila kutoa risiti.



Cha kushukuru ni kwamba hawakufunga akaunti zake ama kumpeleka mahakamani, hadi hapa alipo imebidi aanze kurejesha mdogo mdogo kwa maumivu makali sana, yaani kwa sasa yupo makini sana kuuza bidhaa kwa kutoa risiti za vat.

Ila nikowa muwazi bila kupepesa macho, kapigwa faini kwa uzembe wake maana haiingii nimeshangaa inakuwaje anunue mzigo wenye kodi ya vat alafu asitoe risiti jli kuikomboa vat, nimeumia sana hapa maana hili lilikuwa linakwepeka.

Kimbembe kipo kwa wanaonunua mizigo isiyo na risiti za tra, hii mara nyingi ni kwa wale wanaouza magendo yaliyoingizwa nchini bila vibali, Yani hapa utayaita maji Mma!!
Watu walipe Kodi ,TRA inadekeza Sana wafanyabiashara na Wananchi ambao hawadai Risiti.
 
Hivi unajisikiaje unajikaba kulipa kodi halafu unakuja kuambiwa serikali imekopa pesa Trillion 4 kwa ajili ya kuboresha uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma, just imagine, ndio kitua gani hicho? Halfu riba tilllion 2, hivi hata ingekuwa wewe utajisikiaje?
Nikukwepa tu hakuna namna
 
Umenunua bidhaa ya elf 20,.... Kwenye risiti inaonesha umelipia vat asilimia 18% sawa na 3,050

Unaenda kuiuza kwa shilingi elf 25,000, ukitoa risiti kwa bei hio ni kwamba umechukua chako shilingi 21,186 na kwenye vat itayohesabiwa ya shilingi 3,814 utajilipa mwenyewe ile vat ya mwanzo ya 3,050, Tra wanachotaka ni hio iliyozidi ambayo haikuhusu (3,814 - 3,050 = 764)

unakusanya pesa yote na kufidia vat uliyolipa... Tatizo lipo wapi ???
Nilitaka kuandika hivi ila nimepita kimya. Kuna thread ingine huko nimefafanua hivi nimeshambuliwa sijui kitu ni mwajiriwa tu.
 
Nimejiridhisha kwamba kwa sasa TRA wana jambo lao kwa wakwepa kodi maana si kwa kelele hizi, wakiona unakwepa wanapita na wewe.

Mwezi uliopitwa nilipatwa na simanzi baada ya kuona ndugu yangu kapatwa na pigo zito la kulipa faini ya TRA, masikitiko yake yamenigusa na mwanzoni nilidhani kaonewa lakini hali ni tofauti.



Hawa kina diamond na huyo pck wanaolalamika ni kwasababu ni maarufu ndio maana wanasikika lakini wakae wakijua sio wao tu, hii ni operation kubwa sana iliyonasa wengi tena kihalali bila uonevu wala mabavu.



Binafsi nina ndugu yangu alianza biashara kwenye mwaka 2015 hivi, Enzi hizo Magu kaingia na msisitizo watu watoe risiti kwa mashine, hapa waliokuwa hawana mashine ndio walikiona cha mtemakuni, kukwepa huu mhaho wengi ilibidi wanunue hizo mashine ila wakawa wanatoa risiti chache za kuzugia, kwa sasa hali ni tofauti kabisa, hio style ya kutoa risiti za kuzugia utapigwa pini tu, yaani kwa sasa wanafatilia mfano biashara za kuuza bidhaa inabidi mzigo ulionunua uwe na risiti yake ya mashine ya tra na pia uwe unauza kwa kutoa risiti kwa mashine, huyu ndugu yangu alipodakwa ni kwamba alikuwa ananunua bidhaa na alikuwa anapewa risiti lakini yeye anatoa tu risiti chache za kuzugia kwa bidhaa alizouza, Tra wakastuka wakaenda dukani kwake kukagua mzigo wakamwambia wameona kwenye system yao anauziwa bidhaa nyingi na watu wanaomuuzia kwa risiti lakini yeye vitu anavyouza kwa risiti ni vichache, mzigo uliobaki uko wapi ? Akaanza kupiga kiswahili pale lakini haikusaidia, TRA wakahitimisha kihalali kwamba anauza bila kutoa risiti a.k.a anasaidia ukwepaji wa kodi.

Wakati anasubiri hatma ya kitachomkuta alitumia connections zake na kwenda kuwabembeleza Tra kwenye ofisi zao lakini wapi... Kwanza hata huko akagundua wapo wengi.

mwezi uliopita kapigwa faini ya takribani milioni 160 kwa kosa la kuuza bidhaa bila kutoa risiti.



Cha kushukuru ni kwamba hawakufunga akaunti zake ama kumpeleka mahakamani, hadi hapa alipo imebidi aanze kurejesha mdogo mdogo kwa maumivu makali sana, yaani kwa sasa yupo makini sana kuuza bidhaa kwa kutoa risiti za vat.

Ila nikowa muwazi bila kupepesa macho, kapigwa faini kwa uzembe wake maana haiingii nimeshangaa inakuwaje anunue mzigo wenye kodi ya vat alafu asitoe risiti jli kuikomboa vat, nimeumia sana hapa maana hili lilikuwa linakwepeka.

Kimbembe kipo kwa wanaonunua mizigo isiyo na risiti za tra, hii mara nyingi ni kwa wale wanaouza magendo yaliyoingizwa nchini bila vibali, Yani hapa utayaita maji Mma!!
We jamaa ulishawahi kufanya biashara kweli au unategemea dirishani mwisho wa mwez
 
Umepiga mahesabu yako kitoto Sana

Haya mahesabu yako wanapiga sn watoto wa pale IFM kila siku, ila ukiingia mtaani Hali Ni tofauti kabisa.

Bado mfanya biashara huyo huyo anadaiwa BIMA, Leseni, Fire, Afya, Ulinzi Shirikishi, Wakala wa Vipimo, TBS, Usafi, Parking n.k n.k..
Wewe ndie unaeleta utoto, umeona nimekuja na facts na mifano halisi ya hesabu za vat umekosa cha kujibu umeanza umeanza kuzungumzia bima, leseni, fire, ulinzi, n.k.
 
Back
Top Bottom