NetMaster
JF-Expert Member
- Sep 12, 2022
- 1,454
- 4,853
Nimejiridhisha kwamba kwa sasa TRA wana jambo lao kwa wakwepa kodi maana si kwa kelele hizi, wakiona unakwepa wanapita na wewe.
Mwezi uliopitwa nilipatwa na simanzi baada ya kuona ndugu yangu kapatwa na pigo zito la kulipa faini ya TRA, masikitiko yake yamenigusa na mwanzoni nilidhani kaonewa lakini hali ni tofauti.
Hawa kina diamond na huyo pck wanaolalamika ni kwasababu ni maarufu ndio maana wanasikika lakini wakae wakijua sio wao tu, hii ni operation kubwa sana iliyonasa wengi tena kihalali bila uonevu wala mabavu.
Binafsi nina ndugu yangu alianza biashara kwenye mwaka 2015 hivi, Enzi hizo Magu kaingia na msisitizo watu watoe risiti kwa mashine, hapa waliokuwa hawana mashine ndio walikiona cha mtemakuni, kukwepa huu mhaho wengi ilibidi wanunue hizo mashine ila wakawa wanatoa risiti chache za kuzugia, ila kwa sasa hali ni tofauti kabisa, hio style ya kutoa risiti za kuzugia utapigwa pini tu,
yaani kwa sasa wanafatilia mfano biashara za kuuza bidhaa inabidi mzigo ulionunua uwe na risiti yake ya mashine ya tra na pia uwe unauza kwa kutoa risiti kwa mashine, huyu ndugu yangu alipodakwa ni kwamba alikuwa ananunua bidhaa na alikuwa anapewa risiti lakini yeye anatoa tu risiti chache za kuzugia kwa bidhaa alizouza, Tra wakastuka wakaenda dukani kwake kukagua mzigo wakamwambia wameona kwenye system yao anauziwa bidhaa nyingi na watu wanaomuuzia kwa risiti lakini yeye vitu anavyouza kwa risiti ni vichache, mzigo uliobaki uko wapi ? Akaanza kupiga kiswahili pale lakini haikusaidia, TRA wakahitimisha kihalali kwamba anauza bila kutoa risiti a.k.a anasaidia ukwepaji wa kodi.
Wakati anasubiri hatma ya kitachomkuta alitumia connections zake na kwenda kuwabembeleza Tra kwenye ofisi zao lakini wapi... Kwanza hata huko akagundua wapo wengi.
mwezi uliopita kapigwa faini ya takribani milioni 160, hio faini ni mchanganyiko wa VAT walizokadiria kakwepa + interest + efd penalty, n.k.
Cha kushukuru ni kwamba hawakufunga akaunti zake ama kumpeleka mahakamani, hadi hapa alipo imebidi aanze kurejesha mdogo mdogo kwa maumivu makali sana, yaani kwa sasa yupo makini sana kuuza bidhaa kwa kutoa risiti za vat.
Ila nikowa muwazi bila kupepesa macho, kapigwa faini kwa uzembe wake maana haiingii nimeshangaa inakuwaje anunue mzigo wenye kodi ya vat alafu asitoe risiti jli kuikomboa vat, nimeumia sana hapa maana hili lilikuwa linakwepeka.
Kimbembe kipo kwa wanaonunua mizigo isiyo na risiti za tra, hii mara nyingi ni kwa wale wanaouza magendo yaliyoingizwa nchini bila vibali, Yani hapa utayaita maji Mma!!
Mwezi uliopitwa nilipatwa na simanzi baada ya kuona ndugu yangu kapatwa na pigo zito la kulipa faini ya TRA, masikitiko yake yamenigusa na mwanzoni nilidhani kaonewa lakini hali ni tofauti.
Hawa kina diamond na huyo pck wanaolalamika ni kwasababu ni maarufu ndio maana wanasikika lakini wakae wakijua sio wao tu, hii ni operation kubwa sana iliyonasa wengi tena kihalali bila uonevu wala mabavu.
Binafsi nina ndugu yangu alianza biashara kwenye mwaka 2015 hivi, Enzi hizo Magu kaingia na msisitizo watu watoe risiti kwa mashine, hapa waliokuwa hawana mashine ndio walikiona cha mtemakuni, kukwepa huu mhaho wengi ilibidi wanunue hizo mashine ila wakawa wanatoa risiti chache za kuzugia, ila kwa sasa hali ni tofauti kabisa, hio style ya kutoa risiti za kuzugia utapigwa pini tu,
yaani kwa sasa wanafatilia mfano biashara za kuuza bidhaa inabidi mzigo ulionunua uwe na risiti yake ya mashine ya tra na pia uwe unauza kwa kutoa risiti kwa mashine, huyu ndugu yangu alipodakwa ni kwamba alikuwa ananunua bidhaa na alikuwa anapewa risiti lakini yeye anatoa tu risiti chache za kuzugia kwa bidhaa alizouza, Tra wakastuka wakaenda dukani kwake kukagua mzigo wakamwambia wameona kwenye system yao anauziwa bidhaa nyingi na watu wanaomuuzia kwa risiti lakini yeye vitu anavyouza kwa risiti ni vichache, mzigo uliobaki uko wapi ? Akaanza kupiga kiswahili pale lakini haikusaidia, TRA wakahitimisha kihalali kwamba anauza bila kutoa risiti a.k.a anasaidia ukwepaji wa kodi.
Wakati anasubiri hatma ya kitachomkuta alitumia connections zake na kwenda kuwabembeleza Tra kwenye ofisi zao lakini wapi... Kwanza hata huko akagundua wapo wengi.
mwezi uliopita kapigwa faini ya takribani milioni 160, hio faini ni mchanganyiko wa VAT walizokadiria kakwepa + interest + efd penalty, n.k.
Cha kushukuru ni kwamba hawakufunga akaunti zake ama kumpeleka mahakamani, hadi hapa alipo imebidi aanze kurejesha mdogo mdogo kwa maumivu makali sana, yaani kwa sasa yupo makini sana kuuza bidhaa kwa kutoa risiti za vat.
Ila nikowa muwazi bila kupepesa macho, kapigwa faini kwa uzembe wake maana haiingii nimeshangaa inakuwaje anunue mzigo wenye kodi ya vat alafu asitoe risiti jli kuikomboa vat, nimeumia sana hapa maana hili lilikuwa linakwepeka.
Kimbembe kipo kwa wanaonunua mizigo isiyo na risiti za tra, hii mara nyingi ni kwa wale wanaouza magendo yaliyoingizwa nchini bila vibali, Yani hapa utayaita maji Mma!!