TRA 'wambana' Dk Slaa

TRA 'wambana' Dk Slaa

Code:
Hata hivyo  jana TRA kupitia taarifa yake iliyotolewa na Idara ya Elimu na Huduma  kwa Mlipa Kodi, imekanusha madai hayo na kuyaita kuwa uzushi tu wa Dk  Slaa na kumtaka atoe uthibitisho wa madai yake hadharani.
Tatizo kwa TRA ni kuwa unapodai madai ya Dr. Slaa ni uzushi inabidi na wewe utoe uthibitisho wa tuhuma ya kuwa ni uzushi kwa kuthibitishakama kweli TRA iliwahi kushitakiwa mahakamani au la na mtajwa na mwenendo wa kesi ukoje.........majibu ya kiujumla yanatoacha na mashaka ya kuwa huenda tuhuma hizo ni za kweli...................
 
Sawa Mkuu-
Huyu Luoga ni fisadi kwelikweli. Amehusika pia katika ukwapuaji wa Bilioni 15 za mradi wa ASYCUDA. Hizi pesa hakulipwa Contractor halali. Luoga na wenzake walimwekea ZENGWE Contractor na kwa muda mrefu walikataa kumlipa hela zake hadi pale walipojilainishia kwa kuunda NECO yao wenyewe ilosajiliwa Tanzania. NECO ya Tanzania ndio iliyolipwa hayo mabilioni. Contractor ni kampuni ya NECO ya Zambia. Mlipaji mkuu anajulikana kwa jina la Happiness na ana ubini wa Nkya. Habari ndiyo hiyo pia.
 
Tatizo mamlaka zetu na Serikali kurusiana mpira, kwanini wao hawatoi vithibitisho kujenga confidence kwa wananchi?
 
Ukifika Arusha maeneo ya Friend corner njia ya kwenda Unga LTD utaona hayo mascrepa ya magari ya Tango Transport Ltd, kweli TRA ni wauwaji, yaani malori yamekaa hadi yameozea pale! Inasikitisha kuona TRA huwa hata hawajisumbui kutafuta njia mbadala na walipa kodi inapotokea kutoelewana, badala yake wanatumia njia chafu za kuwakomoa walipa kodi na madhira yake ndo haya sasa, sasa wanatapatapa!
 
Ukifika Arusha maeneo ya Friend corner njia ya kwenda Unga LTD utaona hayo mascrepa ya magari ya Tango Transport Ltd, kweli TRA ni wauwaji, yaani malori yamekaa hadi yameozea pale! Inasikitisha kuona TRA huwa hata hawajisumbui kutafuta njia mbadala na walipa kodi inapotokea kutoelewana, badala yake wanatumia njia chafu za kuwakomoa walipa kodi na madhira yake ndo haya sasa, sasa wanatapatapa!

Yale magari chakavu, Mkurugenzi wa Tango Transport, Verani anadai kadi zipo TRA. TRA wanapopinga ukweli aliosema Dr. Slaa wanajaribu kughilibu wananchi kana kwamba hatukumbuki kwani kesi hiyo iliendeshwa Arusha na hukumu ya kwamba Tango alipwe fidia ilitangazwa hata na magazeti.
 
Leo Dr.Slaa amewajibu TRA na kaweka sehemu ya ushahidi hadharani, subirini media kesho.
 
Nakumbuka hata siku alipokuwa bungeni alipotoa taarifa za wizi wa EPA spika alimwambia hawatakaa wakubaliane na ushahidi wa kwenye internet lakini mwishoni ni nani alikuwa mkweli, watanzania wote wanajua hadi vijijini. Subilini tuone mwisho utasikia wameanza kupekelekana mahakamani wenyewe
 
TRA Ni waongo na wazushi wakubwa tena kutumia kodi za watanzania kuandika uongo ni ufisadi mwingine.

N a wana JF hebu tujenge utamaduni wa kusoma ripoti mbalimbali zinazowekwa hapa , kuhusu ufisadi wa Luoga na TRA CAG ALISEMA HIVI;

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA
HESABU ZA SERIKALI KUHUSU TAARIFA ZA
FEDHA ZA SERIKALI KUU KWA MWAKA​
ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI, 2010

•​
Malipo ya fidia isiyostahili kwa kampuni ya TANGO
Limited Sh.554,464,133

Kiasi cha Shs.554,464,133.60 kililipwa kwa M/S Tango
Transport Limited (Verani Tango) kama fidia kwa
mujibu wa hati za Magari yake zilizodaiwa
kuchukuliwa na maafisa wa TRA mwaka 1997 kwa
muda wa siku tisini (90). Hata hivyo, mapungufu
yafuatayo yalibainishwa:
i. Mrejesho ya Shs.53,650,151 yaliambatanishwa na
hati ya kukiri mapokezi ambayo uhalisi wake
haukuthibitishwa. Aidha, kiasi hiki kililipwa mara
mbili, wakati awamu ya kwanza malipo yalifanywa
kwa amri ya mahakama.
ii. Malipo ya Sh.6,788,840 hayakuhusiana na madai ya
msingi
iii. Malipo ya riba ya Shs.554,464,133.60 yalifanyika​
kwa ‘compound interest” badala “simple interest”.

SASA WANAPOSEMA HAWAJAWAHI KULIPA KIASI HICHO NA HAWANA KUMBUKUMBU KAMA KUNA KESI YA TANGO TRANSPOTERS WANAMAANISHA NINI?

NTAREJEA.

Asante Mkuu Namuamini Dr. Slaa huwa Hakurupuki sema siku Hizi kuna Haters wengi sana
 
hiyo habari Dk. aliitoa kwenye ripoti ya mkaguzi mkuu! si wangeanza na huyo kama wanao ubavu???? TRA shughulikieni matatizo yanayowakabili na kujibu tuhuma si kuwa deffensive... hilo halitawasaidia.
 
Back
Top Bottom