lakini kaka wewe ni mnafiki haueleweki moto ama baridi!
Waende Mahakamani,Ushahidi hautolewi Mitaani!!
Waende kama wana Ubavu huo!!
Sasa TRA wamembana vipi Dr Slaa?........au sioni vizuri labda
wapenda anasa wametajwa kinawauma sana,matanuzi mtaani hatunywi maji,watu hawana amani na ndoa zao kisa wafanyakazi wa TRA,maana hawa jamaa kamamke wa mtu ni mzuri wanakunyang'anya,dhambi ilioje
Basi watoe 'press release' ya kupinga kauli ya Dr. Slaa kama wana ubavu huo.
TRA kupitia taarifa yake iliyotolewa na Idara ya Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi, imekanusha madai hayo na kuyaita kuwa uzushi tu wa Dk Slaa na kumtaka atoe uthibitisho wa madai yake hadharani.
"Huu ni uzushi unaopaswa kulaaniwa vikali kwa sababu unapotosha wananchi na hasa wasomaji wa magazeti. Dk. Slaa atoe nakala ya hukumu hiyo ili wananchi wamwamini. Bila kufanya hivyo kutaonyesha kuwa ametoa habari za uongo kwa kusingizia mahakama," ilisema taarifa.
Taarifa hiyo ilimtaka Dk. Slaa kutoa vielelezo vya maelezo yake hadharani na kwenye mkutano ili awathibitishie wananchi kuwa alichosema ni cha kweli.
TRA ilisema kama Dk. Slaa atashindwa kufanya hivyo, ni dhahiri kuwa yeye si mtu makini na ni mtu mwenye nia ya kupotosha umma wa Watanzania na kuchafua heshima ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.
"Kudanganya watu kwa siri au hadharani ni aina mojawapo ya aina nyingi za kutokuwajibika. Kutokuwajibika kuna sura nyingi na uongo ni mojawapo. Dk. Slaa lazima ajisafishe na hili," ilisisitiza taarifa ya TRA. Taarifa hiyo ya TRA ilisema Luoga hajawahi kuzuia wala kukamata magari yanayodaiwa na Dk. Slaa.
.
Kwa kusema kuwa maelezo aliyoyatoa ni ya UONGO, TRA kama taasisi ya umma haiwezi ikaenda mahakamani kumshitaki mwanasiasa kwa anayoyaongea jukwaani, walichofanya ni kuweka record sawa na kutoa alert kwa wananchi kuwa jamani eh mnalishwa kasa.
Kama wameshatoa basi tutamsubiri Dk. Slaa atoe uthibitisho wake.
lakini kaka wewe ni mnafiki haueleweki moto ama baridi!
Silaa alipotaja wezi hajapindisha maneno, Alitaja watu kwa majina. Sioni kwa nini TRA wanazungukazunguka. Wanachotakiwa kufanya ni kwenda mahakamani vinginevyo wanatafuta pa kuzuga tu
Usijidharirishe kwa kwenda kwenye level za watoto ambao hawajakomaa, you can do better than this!!
Basi watoe 'press release' ya kupinga kauli ya Dr. Slaa kama wana ubavu huo.