TRA, wafanyabiashara wana temper na EFD machines

TRA, wafanyabiashara wana temper na EFD machines

Puuzi jingine hili..kwani nikidai receipt ninanufaika na nini...or wewe ndo bashite mnaokula kodi zetu na lile jiziii linalojifanya limetumwa na mungu
Kwa hiyo usipodai receipt utanufaika na nini? haujui hiyo yote inaenda kwenye tumbo la huyo ambapo ingeenda kuboresha huduma za jamii.

Akili zingine bora ifike tu mahali muwe mnaazimishwa akili maana naona kuna watu wamewashikia akili zenu. Kwenye ujenzi wa uchumi wa nchi akili kama hizi tunaziita ni za kishenzi kabisa na za kipumbavu. Right ungekuwa unaishi nchi za ulimwengu wa kwanza unakula kifungo cha miezi kadhaa gerezani ukitoka akili imepunguza makengeza.
 
Mtaani hakishindikani kitu kuna EFD fake zinatoa risiti kama za TRA lkn hazina connection Na TRA.Hapana chezea Bongo Dar es salaam
 
Pole mfanyabiashara, kimekunukia tayari.
Hiyo mashine haijachezewa chochote, ipo sahihi kabisa katika hizo calculation. Huyu jamaa ana mtihani wa kudhibitisha kwamba alitoa 210,000/= na si 178,000/= kama risiti (mkataba) inavyoonyesha, otherwise anaweza kufunguliwa kesi ya 'defamation' na huyo mwenye duka, na akipata wakili mzuri, anaweza hata kumfilisi mtoa mada.
 
Ni kweli mkuu wengine huenda mbali na kutoa discount kwa wateja ambao hawachukui risiti, Hii haikubaliki na ni ukwepaji wa kodi ambapo kodi hizo hutusaidia sisi wenyewe mimi huwa nakemea mno mno mfanyabiashara akitaka kufanya ujanja
 
Ikiwa mfanyakazi analipa kodi kwenye mshahara kwa shuruti vivyohivyo mfanyabishara anapaswa kulipa kodi. Hakuna nchi inaendelea bila kodi labda arabuni kwenye mafuta na gesi. Ukinunua dai risiti, ukiuza toa risiti.
 
Shida ni kuthibitisha umempa hiyo amount
Ndio hilo nililolisema, hivi anataka TRA waamini maneno yake tu bila ushahidi wowote? Alichopaswa kufanya ni kuigomea ile risiti(mkataba) maana haukuwa sahihi, na kama angeendelea kunyimwa ilibidi adai arudishiwe pesa yake!
 
Du mkuu unajionyesha jinsi ulivyopitwa sana na nahesabu ukiwa shule!!!
210,000 ni jumpla ya bei na VAT yake, sasa hapo bei halisi ni
210,000/1.18 = 177,966.10 (round up 178,000)

Kwa hiyo, bei ni 178,000 , VAT inay0takiwa kulipwa ni 18% ya 178,000!!!
Tafakari, penda hesabu!!!!
Mkuu 18% sio 1. 18 ni 0.18!
We ndiye hujui hesabu!
Na kama 210, 000 ni VAT inclusive maana yake thamani ya vitu ni 210, 000-18% ambayo ni 210, 000-37, 800 =172, 200 na sio 178, 000.
 
Na hawa ndio waTanzania....
Unajisikia raha kodi zetu zinavyonunuliwa ndege bila ruhusa ya bunge then zinalipwa in full kabla ya delivery then zinashikiliwa bondi huko Canada? Au wanavyojenga viwanja vya ndege na hospitali za rufaa vijijini bila ruhusa ya bunge?
 
Du mkuu unajionyesha jinsi ulivyopitwa sana na nahesabu ukiwa shule!!!
210,000 ni jumpla ya bei na VAT yake, sasa hapo bei halisi ni
210,000/1.18 = 177,966.10 (round up 178,000)

Kwa hiyo, bei ni 178,000 , VAT inay0takiwa kulipwa ni 18% ya 178,000!!!
Tafakari, penda hesabu!!!!
Hata kama ingekuwa km unavyosema kuwa VAT ni 18% ya 178, 000/ bado 18% ya 178, 000 ni elfu 32 na ushee sasa angalia risiti! Usikosoe kwa kejeli kabla hujahakiki!
 
Ndio hilo nililolisema, hivi anataka TRA waamini maneno yake tu bila ushahidi wowote? Alichopaswa kufanya ni kuigomea ile risiti(mkataba) maana haukuwa sahihi, na kama angeendelea kunyimwa ilibidi adai arudishiwe pesa yake!
Alinipa na risiti ya mkono inayosoma 210, 000!/=
 
Nataka kuanzisha uzi wa wachawi kama uyu Jamaa... Huu ni uchawi uliopitiliza... Endelea raisi anaweza kukukumbuka
Mkuu, wewe nafikiri unahitaji kuelimishwa kuhusu umuhimu wa kulipa kodi, na kama una elimu hiyo basi we ndiyo nchawi kuliko hata mtoa post. Kodi kimantiki ndiyo chanzo cha Huduma za msingi Kama Maji, Huduma za afya, Barbara tunakopita, Elimu na mambo mengine mengi tu. Kwa nchi za wenzetu mtu anapeleka mwenyewe kodi bila shuruti, ifike Mahala tuwe wazakendo, tulips kodi kwa kupenda.
 
Nimenunua bidhaa za ujenzi za Tsh 210, 000 lakini RISITI YA EFD inasoma total cash Tsh 178, 000 na VAT Tsh 27, 152. Nilipomuuliza mbona mashine yake haitoi risiti sahihi maana 18% ya 210, 000/= ni 37, 800 na risiti yake ilipaswa kusomeka:
cash ni 172, 200
VAT 18% ni 37, 800
Hivyo Total cash isomeke 210, 000 akawa hana majibu.
Kama mtanzania mlipa kodi sikuridhika. Wito wangu kwa mamlaka ya Mapato nchini kukagua mashine hizi, nimegundua maduka mengi ya vifaa vya ujenzi hayana kabisa hizi mashine hivyo kuwepo na mwanya wa ukwepaji kodi kwa kutolipa kodi sahihi.

Unaelewa maana ya TAX INCLUSIVE ama TAX EXCLUSIVE? kwenye hiyo bei aliyokupa ungemwambia aongeze asilimia 18 then akutolee risiti halali.
 
Nimenunua bidhaa za ujenzi za Tsh 210, 000 lakini RISITI YA EFD inasoma total cash Tsh 178, 000 na VAT Tsh 27, 152. Nilipomuuliza mbona mashine yake haitoi risiti sahihi maana 18% ya 210, 000/= ni 37, 800 na risiti yake ilipaswa kusomeka:
cash ni 172, 200
VAT 18% ni 37, 800
Hivyo Total cash isomeke 210, 000 akawa hana majibu.
Kama mtanzania mlipa kodi sikuridhika. Wito wangu kwa mamlaka ya Mapato nchini kukagua mashine hizi, nimegundua maduka mengi ya vifaa vya ujenzi hayana kabisa hizi mashine hivyo kuwepo na mwanya wa ukwepaji kodi kwa kutolipa kodi sahihi.
Machine haina kosa; Garbage in = Garbage out
 
Alinipa na risiti ya mkono inayosoma 210, 000!/=
Bado unamtihani wa kudhibitisha kwamba siku hiyo hukufanya manunuzi mara 2 kwenye duka lake, mara ya kwanza ulifanya manunuzi ya 178,000/=, mara ya pili ukafanya manunuzi ya 210,000/=, au akitaka kukupa za uso kwa style nyingine, anaweza akakwambia hiyo risiti ya mkono si yake bali umeichapisha kwenye kastationery huko vichochoroni, au hujui risiti za mkono ni batili ba hazitambuliki kokote na mtu yeyote? Hata TRA hawazitambui, kiufupi hiyo ya mkono sio risiti, ni karatasi tu. Kwahiyo bado unakesi ya kujibu kama akitaka kukushtaki for defamation. Ila pia elewa kwamba, kwa kukubali kuchukua risti ya 178,000/= huku umelipa 210,000/= maana yake ni kwamba umeshiriki wizi wa kodi kwa kuuziwa kitu cha 220,000/= kwa 210,000/=, ambapo hilo punguzo la 10,000/= ulilopewa ni limetoka kwenye kodi iliyotakiwa kulipwa, hivyo in reality wewe ndio mwizi wa kodi na hata TRA nao wakitaka kukushtaki wanaweza pia! Kua makini, unaposhiriki kwenye wizi, usiende kuripoti polisi, kula kimya kimya nenda zako, roho mbaya haijengi. Wenzako wanajenga viwanja vya ndege na mahospitali ya rufaa vijijini kwao we unapayuka tu hapa kama umekula mafuta ya nguruwe!
 
Safi sana wahusika wameona TIN hiyo. Haiwezekani wengine tukamuliwe hadi mwisho wengine wateleze na ganda la ndizi tu.
 
Back
Top Bottom