Bado unamtihani wa kudhibitisha kwamba siku hiyo hukufanya manunuzi mara 2 kwenye duka lake, mara ya kwanza ulifanya manunuzi ya 178,000/=, mara ya pili ukafanya manunuzi ya 210,000/=, au akitaka kukupa za uso kwa style nyingine, anaweza akakwambia hiyo risiti ya mkono si yake bali umeichapisha kwenye kastationery huko vichochoroni, au hujui risiti za mkono ni batili ba hazitambuliki kokote na mtu yeyote? Hata TRA hawazitambui, kiufupi hiyo ya mkono sio risiti, ni karatasi tu. Kwahiyo bado unakesi ya kujibu kama akitaka kukushtaki for defamation. Ila pia elewa kwamba, kwa kukubali kuchukua risti ya 178,000/= huku umelipa 210,000/= maana yake ni kwamba umeshiriki wizi wa kodi kwa kuuziwa kitu cha 220,000/= kwa 210,000/=, ambapo hilo punguzo la 10,000/= ulilopewa ni limetoka kwenye kodi iliyotakiwa kulipwa, hivyo in reality wewe ndio mwizi wa kodi na hata TRA nao wakitaka kukushtaki wanaweza pia! Kua makini, unaposhiriki kwenye wizi, usiende kuripoti polisi, kula kimya kimya nenda zako, roho mbaya haijengi. Wenzako wanajenga viwanja vya ndege na mahospitali ya rufaa vijijini kwao we unapayuka tu hapa kama umekula mafuta ya nguruwe!