TRA someni hapa: EFD zenu WIZI MTUPU

TRA someni hapa: EFD zenu WIZI MTUPU

Subirini mfumuko wa bei utakapo anza mwisho wa siku anaumia mwananchi wa mwisho mlaji

Mara nyingi mfumuko wa bei tulikuwa tunaupata baada ya uchaguzi...mkuu...lakini kwa hali iliyopo....nadhani muda si mrefu hata kabla ya uchaguzi mkuu mfumuko utalipuka kwa kishindo cha kutisha sana.
 
mkuu
mbali ya hiyo mashine leseni sasa ni.kuanzia tsh 200,000 hadi 800,000 wanaangalia uwezo wa duka kila mwaka.
_fire kila mwaka 100,000.
~taka sh 24,000kila mwezi.
na hizi zote wamemlenga mwenye duka.
sasa tumechoka kuwa chuma ulete,kesho mgomo unaendelea

Mimi hawa jamaa wa taka walikuja kwangu nikawatimua nikawaambia tukutane mahakamani. Hawajanisumbua tena. EFD nayo niligoma. Wazush hawa.
 
Setuba Noel Mfanyakazi hana gharama? Au mnazo nyinyi tu?
Acheni kulialia mlipe kodi

Nyie si mnapiga mabao ya visigino humo maofisini mwenu! Sisi kila senti tano tunaitolea jasho sio kama akina home shopping center bana! We unazungumza hivyo wakati hata bei ya kisado cha viazi hujui, unakula KFC au Mary Brown na familia yako kila siku? Acha ungese bana!
 
Last edited by a moderator:
Acheni visingizio, tulipe kodi. Tumeshavuna sana kwenye biashara pasipo kulipa kodi halali ya serikali. Tuache visingizio na vijihesabu vya uongo.

kwani unadhani hatulipi kodi mkuu , MPAKA HAPA TUNALIPA ! tunachokataa ni huo mradi wa watu unaoitwa EFD ' S
 
Naona Mku wangu unakazana kujikita na revenue floor iliyotolewa na TRA kama ndio bas yako! Kimahesabu upo sawa lakini practically hao wanaouza sh. 38,000/- wala bado hawajaguswa! Wanaofanya biashara ya mapato ghafi ya sh. 38,000/= kwa siku wengi wao kama sio wote ni wale wenye viduka vidogovidogo huku uswahilini tena mitaa ya ndani! Hao wa sh.38,000/ kwa siku ni wale wanaouza mafuta ya taa na ya kula kwa vipimo vya shilingi mia mia....hawa ni wale wanaouza majani ya chai ya shilingi 50/-, hawa ni wale wanaouza sukari au bidhaa zingine hata kwa robo kilo...hawa ni wale mtu unafika dukani, unalazimika kutoa mia mfukoni kugonga nondo ili mwenyewe aliyekaa sebuleni akusikie na kuja kukupa huduma!! In short, ni wale ambao viduka vyake ni vile ambavyo mteja anasimama dirishani na ni MARUFUKU kuingia ndani!!!! Hawa ndio hao wanaofanya mauzo ya sh.38,000/-na wala sio wale wanaogoma! And in fact, hata hawa nao wanauza zaidi ya hiyo....waht does it take? Maharage 10kg@2000+Unga 15kg@1000+Mchele 10kg@1500=50,000/- per day....hatujataja sigara, viberiti, mafuta ya taa, mafuta ya kula ya mia mia, majani ya chai ya hamsini hamsini and so much more!


Nazdaz katika hili napenda kupishana na wewe... Nakiri wapo wafanyabiashara wasio waaminifu ambao wanakwepa kodi.Lakini mfumo mzima wa Kodi una mapungufu makubwa yanayostahili serikali kuunda tume maalumu ya kuyachunguza na kuyapatia ufumbuzi..

Kwenye tamko la TRA wanaostahili kuanza kutumia machine za EFD ni wneye kipato cha wastani wa Milioni 14 Mpaka 40( ikumbukwe wa milioni 40 na kuendelea walianza zamani). Sasa kwa mtu wa kipato cha 14M ni sawa na kipato cha 44,000 kwa siku( assume 26 days per week 12 month per year). Kwa rule of thumbs!!! mfanya baishara huyu ( au nimwite mmachinga) anapata faida baada ya kutoa manunuzi ya TSHS 4,400 Kwa siku ... ukitoa gharama za uendeshaji mmachinga huyu ana faida ya chini ya tshs 1,100 kwa siku...amabayo ndio inayostahili kukatwa kodi...

Leo serikali/ TRA inataka mtu huyu aikopeshe serikali bila liba kwa kununua machine ya tshs 800,000... Kumbuka kwamba ili kuweza kufanya hivyo mmachnga huyu inabidi asubiri siku 72(Miezi 3) ili aweze kununua kifaa hicho bila kutumia chcchote kwenye faida yake... Akiamua kutumia 25% ya faida yake itambidi asubiri siku 2909(MIEZI 111) Miaka 9.3 kuweza kupatafedha za kununulia machine hiyo... ILI ASIWEZE KUHARIBU MTAJI WAKE WA TSHS 500,000/

ILI KUKIDHI MATAKWA YA SHERIA.. MMACHINGA huyu ataenda kukopa kwenye taasisi za fedha saccos, bank au popote awezavyo ili apate 800,000 ya Kununulia kifaa cha EFD... Na riba ya 24% mtu huyu atalazimika kulipa si chini ya TSHS 1000,000 ILI TU KUFUATA SHERIA BILA SHURUTI.... Na kwa kuwa kifaa hichi hakiongezi tija kwenye biashara yake zaidi ya kuongeza gharama za uwendeshaji.. mmachinga huyu atatakiwa kulipa deni kwa tshs 166,000 Kwa mwezi { 6,400} KWA SIKU... AMBAYO NI ZAIDI YA PATO LAKE KWA SIKU....

HICHI NDICHO CHANZO CHA MGOMO!!!!!!


  1. Kwa nini serikali ikope toka kwa mmachinga tshs 800,000 bila riba na kumlazimisha mmachinga kwenda kukopa hiyo laki 8 tena kwa riba ambayo hata biashara yake haiwezi kulipa?
  2. Kwa nini serikali isikitoe hichi kifaa bure na kumpatia mmachinga huyu ili aweze kufanya biashara yake kwa faida.
  3. ikumbukwe kelele hizi hazikuwepo kwa wafanyabiashara wakubwa kwani waliweza kumudu sio tu kununua hata kuzimaintaini na gharama zake za karatasi..
  4. gharama za karatasi za EFD ni wastani wa tshs 12,000-20,000 kwa mwezi na mainatenance ni mpaka 200,000
  5. Machine zina usumbufu mwingi ambao utaleta gharama zisizo rasmi za kuwapigia simu na kwenda kuripoti TRA kila mara zinapoharibika.
  6. Ni rahisi sana kuweza kujuwa kipato cha wafanyabiashara hawa wa kati... Kwa nini serikali iwaongezee mizigo wafanyabiashara hawa usiwo na lazima?



kwenye mfumo mzima wa kodi kuna mapungufu mengi ambayo yamekuwa kilio cha wafanyabiashara wengi kama nilivyoainisha kwenye post zangu za awali.. serikali, TRA na wadau wa wafanyabiashara wanatakiwa kuunda task force ya kuona naman aya kuyatatua matatizo haya..

Muoanamambo

A town
 
kodi kubwa ipi??kinachogomba hapa ni kuwa wafanyabiashara hawataki mauzo yao ghafi yajulikane,ili walipe kodi stahiki.kwani kuna wafanya biashara kama 16,000 hivi wanazitumia mashine hizi toka mwaka 2010!hii awamu ya pili inayo walazimisha wengine 200,000 watumie machine ndio inakuwa nongwa???hapa serikali lazima ishinde tu na ndio maana wamesema ambaye hataki arudishe leseni ya biadhara afanye shughuri nyingine.Hata wakati VAT inaanza ilikuwa hivi hivi.Na kwa taarifa yako wafanya biadhara wengi hususani kariakoo wanalipa kodi ya mapato kwa makadillio ya mauzo yao hawataki kusikia kitu kiitwacho VAT,wanacho fanya ni kipunguza kiasi cha mauzo kwa mwaka.ila kwa mashine ya EFD hawataweza tena kuficha kiasi cha mauzo na moja kwa moja watakuwa na sifa za kusajiliwa kwenye ongezeko la thamani (VAT) ndio mziki hapo.Haka kwa akili ndogo tu pale kariakoo mtu analipia kodi ya pango milioni moja kwa mwezi ila kodi ya mapato analipa laki 5 kwa mwaka!!!!
Tatizo kubwa na la msing hapa ni zaidi ya Machine za EFD ni mfumo mzima wa kodi... Wafanyabiashara wana madai zaidi ya machine za EFD ambazo kwa sababu za makusudi serikali chini ya TRA ndio inachokishililia.. IKUMBUKWE Wafanyabiashara hawa ni walipa kodi wazuri wa kodi zao walizokuwa wanakadiliwa.

Madai ya wafanya biashara ni haya..


  1. Kwanza ni BEI ya machine ulikinganisha na BEI ya soko ya machine husika kwa soko la sehemu nyingine duniani.. kenya tu mashine zinapatikana kwa chininya TZS 350,000. ukienda china na kwingineko ni chini ya $80.
  2. Gharama kubwa na usumbufu unaotokana na machine hizo ukilinganisha na cash flow za mlengwa yaani mfanyabiashara anayeingiza 38,000 Kwa siku... Gharama za karatasi moja ni 6000 na gharama za maintenance ambazo ni zaidi ya laki 3 kwa mwaka na usumbufu wa kuripoti TRA NA KWA WAKALA kila machine inapoaharibika...
  3. Utaratibu wa faini kwa amabaye atashindwa kutumia machine hizo unatoa mwanya kwa wafanayakazi wasio waaminifu wa TRA( ambao ni wengi) na Askari waliozoea Rushwa kuleta taabu kwa wafanyabiashara.
  4. Machine za EFD hazionyeshi gharama za manunuzi na gharama za uwendeshaji ambapo hapo hasa ndio penye tatizo kubwa... Gharama nyingi za manaunuzi ama hazina risiti ama zina risiti ambazo hazilingani na gharama halisi... HILI LITAPELEKEA mfanyabiashara kutozwa kodi kubwa kuliko hanavyostahili kutokana na kukosekana na kumbukumbu za manunuzi.
  5. Mfumo mzima wa biashara ama zimetoka nje ya nchi ambazo ulipiwa kodi custom.. kodi ya import duty and VAT...Au zimenunuliwa kwa wakulima na wavuvi ama wafugaji ambao hawatoi risiti...Kwa zinazopita Customs ukadiliaji umekuwa shida kubwa... mzigo huo huo amabo haupishani hata miezi mitatu unaweza kuwa na kodi tofauti na tena yenye tofauti ya kutisha ... hii imeleta mianya ya rushwa kwa watumishi wa TRA na kupelekea wafanyabiashara kulipa malipo mengi yasiokuwa na risiti... amabayo yatakuja kumfanya alipe malipo mengi ya kodi ya mapato.
  6. Kodi zinazotozwa na TRA Customs hazinlingani na thamani halisi ya bidhaa zinazoingizwa na kushawishi wafanaya biashara kukubali kutoa rushwa ili angalau aweze kuuza bidhaa yake kwa gharama nafuu.
  7. kwa mazao yanaotka kwa wakulima mengi hayana risiti na kwa stahili hii mfanyabiashara atalazimaika kulipa zaidi kodi za mapato.
  8. Kwa ujumla mfumo mzima wa kodi unatakiwa kuangaliwa upwa ili uwe wazi na unaoshawishi wafanyabiashara kulipa kodi stahiki na kupunguza mianya ya Rushwa .... GHARAMA Nyingi za uendeshaji hazina risiti na hili ni tatizo la kuangalia ..
  9. Mfumo hauruhusu uingizaji wa mzigo wa pamoja ( sharing importation) ambapo kila mfanyabiashara aliyeshare container atalipa stahiki yake na mzigo wake kuwa na thamanai ya manaunuzi...
  10. kwa ujumla kufanya baishara Tanzania hasa kwa sekta zisizo rasmi zimekabiliwa na kodi nyingi zisizo na kichwa wa miguu... kodi za pango... kodi ya takataka.. kodi za fire... kodi za mabango... kodi za hamashauri... nk nk...


Tubadilike nchi ni yetu sote... sekta hii nayo ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa... iundwe tume maalumu ya kurekebisha mfumo mzima wa ulipaji kodi na kuwaka fair ness kwa pande zote.... na kusitisha zoezi la EFD

Muonamambo

A town
 
FaizaFoxy nishakushtukia...isije na wewe una kaduka pale mitaa ya Kariakoo lakini kutokana na mahaba uliyonayo kwa serikali yako tukufu ndo unataka kusingizia kwamba kuna "rafiki yako hapo unaongea nae!!" Acheni ujanja ujanja...tumieni EFDs tupate kodi yetu! Huo umeme umekatika lini; jana? EFDs si kama Desk Top PC, kwamba ukikatika umeme ndo basi tena...ina maana hiyo ya shoga'ako haitunzi chaji??!! Wengine ukienda dukani huwa hawatoi risiti kwa kusingizia network wakati suala la kutoa risiti wala halina uhusiano na network!

Mimi nna maduka Kariakoo, si moja, lakini yote nimeyakodisha, isipokuwa nna biashara zangu (zisizo za duka) zingine na nnatumia EDF zaidi ya mwaka na nusu sasa. Lakini kwa muijibu wa biashara zangu nnaweza kukaa hata miezi mitatu nikatoa risiti moja au mbili. Ni consultancy firm ambayo sichukuwi kazi zaidi ya moja mpaka inapokaribia kwisha, gap ya malipo ni ndefu na si kama biashara za kawaida, kwa hiyo binafsi umeme si tatizo. Tatizo ni huyo mwenye duka niliyekuwa naongea nae asubuhi hii ya leo.
 
mi ni mfanyakazi lakini nawasapoti wafanyabiashara.hata wakinunua hizo mashine bado mzigo ni kwetu sisi walaji.kama ujuavyo biashara za bongo ni maelewano.hatujafika hatua ya kuwa na fixed price.nguo ya elf 40 utainunua kwa 15000.just imagine wauza mitumba wa karume au mchikichini wawe na efds unategemea walalahoi tutavaa?.suruali ya ekf 10 utainunua kwa elf 25.ile ya dukani ya elf30 utainunua kwa 50.mshahara wenyewe laki 4 utaweza kuishi?usiwe na myopic minded.kabla ya kuropoka uwe unafikiria matokei ya kitu kwa mapana yake.sio tu ushabikie wafanyabiashara kulipa kodi bila kujua position yako itakuwaje kama mlaji katika mzunguko wa kibiashara.
kwa wafanyabiashara kulipa kodi ni sawa kabisa kakini kuwepo na utaratibu ambao hautaleta madhara kwaa end user.bei ya umeme imepanda maji nayo yamepanda kutoka50 kwa ndoo moja hadi 100 tsh.kwa uelewa wako mdogo hapo muathirika ni nani?unadhani ni tanesco au serikali?acha ushabiki usiokuwa na tija kijana

nakuunga mkono hata mimi sio mfanyabiashara lkn hilo nilishaliona
1. Kwanza hata hao wafanyakaz hasa wa TRA wanajua kuwa kuna maisha baada ya
kustaafu na huo ugumu wa maisha wataupata na watamlaumu nan?

2. Wakuu wa nchi hii kweli ni vichwa ngumu wakula kimya wakat hili swala linagusa uchumi wa nchi.

3. Kulipa kodi ni uzalendo 'sawa' kulipa kodi ni sheria 'ndio', TRA wanakusanya mapato af vitendea kazi vinunuliwe na wafanyabiashara kweli? Wajuvi nijuzeni!!
Kuna mtu humu asiyeijua thamani ya friji ya kufanyia biashara (yale makubwa yenye kioo mbele kuonyesha vilivyomo ndan) yana bei kuanzia lak 8-1ml na ushee lkn baadhi ya makampuni ya vinywaji ikiwepo Coca na Pepsi wanatoa
bure kwa kununua kreti 20 za soda ktk duka lako na wanakupa bure ili wao wapate faida na ukishindwa wanachukua friji lao na wakat mwingine nimeshuudia ktk mgahawa furan walileta viti na meza mara kwa mara wanabadilisha kwani wao hawazijui hela?? Tuachane na hayo ya soda
tujiulize nchi za jirani mf. Kenya wamewezaje au hawana hizo mashine za Efds na je kama zipo wameziana shingapi na wafanyabiashara wao?? Kuna nn nyuma ya pazia juu ya hiz mashine?
[COLOR

  1. Kwanza ni BEI ya machine ulikinganisha na BEI ya soko ya machine husika kwa soko la sehemu nyingine duniani.. kenya tu mashine zinapatikana kwa chininya TZS 350,000. ukienda china na kwingineko ni chini ya $80.
    A town
 
Unahimiza watu wagomee risit za serikali
Mtaanza ln kujidai kwamba unalipa kodi vizuri?
 
Mie nadhani huu mpango wa EFD wameugawa kulingana na aina ya biashara na turnover inayokisiwa kwa kipindi cha mwaka,hapa tatizo ni kwamba kwa kila mfanyabiashara aliye katika kundi la kutumia EFD anaagiza mzigo wake toka nje,ingawa kwa kipindi hiki kifupi Wachina ndio waingizaji wakubwa wa mali toka kwao na pia wanauza kwenye vizimba kama wazalendo wengine ,je hapo uwiano wa kodi unakuwaje ? Na je hao wageni wawekezaji wamezidi kuua hata viwanda vidogo vya wamasai waliokuwa wakitengeneza 'sendozi' na hata wakina mama watengenezaji wa batik nao wameathiriwa na hawa wageni ,sasa hawa wazalendo serikali haiwaoni ?na mpango mkakati upi utawasaidia hawa watu? nadhani wakiweza hapo EFD itakuwa inamaana sana kwao na hii migomo itakwisha.

Serikali itoe njia mbadala ya kiubunifu ili viwanda vidogo visife ambavyo vitanufaisha nchi kiuchumi kuliko hao wageni wanaozorotesha pato la ndani
 
Hivi vimashine navichukia kwanza siyo imara network inasumbua ni majanga tu.
 
muonamambo,
kwanza nakubaliana na hoja yako kwa kiasi fulani kwa kuangalia jambo moja; nalo ni bei ya mashine. Hili la bei hata mimi nimepata kulizungumzia hapa siku za nyuma. Tatizo ni kwamba, hadi leo hii ni ngumu kufahamu wanachogomea wafanyabiashara ni nini hasa...am very certain hata leo hii serikali ikitangaza kwamba inatoa hizi mashine bure; bado kuna watu watapinga tu coz' wengine wengine ambao ni wengi tu, msingi wao wa madai yao wala si bei ya mashine bali hawataki tu hizi mashine; hususani wafanyabiashara wa Kariakoo! Pale Kariakoo, bei ya fremu kwa uchache kabisa ni sh.500,000/- kwa mwezi....huku uswahilini ni kama laki 2! So, it doesn't make any sense mtu awe na uwezo wa kulipa laki 5 kwa mwezi kukodi fremu lakini ashindwe kununua mashine ya laki 8 ambayo utaitumia for years.

Tukija suala la maintenance kwamba ni hadi laki 2, ulitakiwa kufafanua....hadi laki 2 kwa muda gani na ktk mazingira gani coz' hizi mashine zinatolewa kwa 3 years guarantee!

Sasa tuje kwenye hiyo hoja ya kwamba wanaotakiwa kutumia EFDs ni wale wenye annual sales of at least 14m ambazo calculation zako zimekupa daily sales ya sh.44,000/-! Let's be honest here mkuu...hata usipotaka kukiri hapa hadharani basi angalau nafsini mwako! Wanaofanya daily sales ya sh.44,000/- ni wafanyabiashara wadogo sana; tena sana na wala sio wale wanaogoma! Hao wanaofanya daily sales za 44,000/- ni hawa wenye viduka vidogo vidogo vilivyopo mitaani tena mitaa ya ndani ambao biashara zao kubwa ni for daily domestic consumption! Hawa wa daily sales za 44,000/- ni wale wanaotupimia mafuta ya taa ya mia mia, mafuta ya kula ya mia mia; majani ya chai ya hamsini hamsini...and the like...tuwe wakweli hawa ndio wenye daily turnover ya tsh. 44,000/- ambao kwa maelezo yako ni kweli kabisa kwamba hawawezi kununua mashine kwa laki 6. Hata hivyo, wengi wao hawa wala hawajaguswa hata kama sheria inasema wenye annual sales ya 14m ndio wanatakiwa kutumia EFDs. UKichukua mfano wa post yangu uliyo-quote, nimeonesha jinsi sh.50,000 inavypopatikana kwa siku kwa kuuza maharage 10kg, unga 15 kg, mchele 10kg!Narudia, waliogoma sio hao wa sh.50,000/- kwa siku ambao unawaombea public sympathy...
 
Last edited by a moderator:
mi ni mfanyakazi lakini nawasapoti wafanyabiashara.hata wakinunua hizo mashine bado mzigo ni kwetu sisi walaji.kama ujuavyo biashara za bongo ni maelewano.hatujafika hatua ya kuwa na fixed price.nguo ya elf 40 utainunua kwa 15000.just imagine wauza mitumba wa karume au mchikichini wawe na efds unategemea walalahoi tutavaa?.suruali ya ekf 10 utainunua kwa elf 25.ile ya dukani ya elf30 utainunua kwa 50.mshahara wenyewe laki 4 utaweza kuishi?usiwe na myopic minded.kabla ya kuropoka uwe unafikiria matokei ya kitu kwa mapana yake.sio tu ushabikie wafanyabiashara kulipa kodi bila kujua position yako itakuwaje kama mlaji katika mzunguko wa kibiashara.
kwa wafanyabiashara kulipa kodi ni sawa kabisa kakini kuwepo na utaratibu ambao hautaleta madhara kwaa end user.bei ya umeme imepanda maji nayo yamepanda kutoka50 kwa ndoo moja hadi 100 tsh.kwa uelewa wako mdogo hapo muathirika ni nani?unadhani ni tanesco au serikali?acha ushabiki usiokuwa na tija kijana
Ngoja nikuulize...yaani unaamini kweli nguo ya sh. 40,000/- huwa unanunua kwa sh. 15,000/-? Unadhani wafanyabiashara ni wapumbavu kiasi hicho? Hiyo nguo since then anafahamu bei yake ni sh. 10,000/- lakini kv mnapenda kuombea; ndo atakuambia 40,000/- na akikuuzia kwa elf 15 unajiona mjanja kumbe umeliwa elfu 5....so, elfu tano yako amekula na kodi halipi vilevile...mkilipwa mishahara midogo mnalalamika wakati mnatetea watu wasilipe kodi!
 
ahhhhh kodi lazima ilipwe asee hila, Tatizo serikali ya CCM si bunifu na TRA nao mizigo tuu kama mizigo mingine, TRA NA SERIKALI KWA UJUMLA Haijandaa mazingira rafiki ya kulipa kodi kwa wazelendo kama hilivyo kwa wawekezaji wa nje, harafu hakuna direct impact kwa walipa kodi, MAJI TABU UMEME TABU MADAWA HOSPITALINI TABU, BARABARA TABU. kwa maana hiyo basi hakuna anyeona humuimu wa kulipakodi. Hilo ndo tatizo
 
Versity ya wapi umesoma wewe? Hivi siku hizi huko wanapokea hadi division five kumbe? Wewe kwa mawazo yako nikinunua bidhaa kwa 34,000 nikaziuza kwa 38,000 kumbe nimepata 38,000 mapato ghafi? Na mtaji uko wapi? Kama ni kweli wewe umesoma hizo economics unazosema basi kumbe ndio maan nchi hii haiendelei!
Umejaa matusi na kejeli lakini nimegundua jambo moja kuhusu wewe! Unajifanya kujua kumbe ni boya tu hujui lolote!!
Sasa nikufundishe na economics zako za feki. Mapato ghafi ni kile kinachobakia ukishatoa bei ya kununulia bidhaa uliyouza.
rudi shule ukajifunze....sijui unapata wapi mambo ya ajabu kama haya!! Kama kweli unafanya biashara utakuwa unafanya biashara ya sidiria wewe!! Yaani kama mtu amenunua mchele gunia 10 kwa sh. 100,000/- kisha akauza kwa sh. 150,000/-, hapo sh. 50,000/- ndo gross income!!! omg! this's might be one of the monthly joke.
Mapato halisi yanakuja utakapotoa gharama nyingine za biashara.
Kama gharama zipi?
Huyo anayelipwa mshahara wa sh 6,000 kwa siku hiyo ndiyo mapato ghafi
Ndo maana nikasema we kilaza? Kwani mie nimesemaje? Au hufahamu kwamba mapato ghafi na Gross Income ni kitu kile kile?
akitoa gharama za kuihudumia hiyo ajira (usafiri, mlo wa mchana nk) anabaki na mapato halisi. Aliyeuza mali ya 38,000 kutoka manunuzi ya 34,000 mapato yake ghafi ni sh 4,000, nako pia akitoa gharama za kuhudumia biashara yake (nauli, pango, ulinzi, usafi, umeme nk) anabaki na mapato halisi. Yupi mwenye mapato halisi kubwa hapa boss mchumi? Hapa pia unahitaji hesabu za "versity"?
Pamoja na kwamba umejaa matusi na kashifa lakini kila unachoandika kinadhihirisha tu usakala na ukilaza wako! Nimekuambia mfanyakazi ana gross income ya sh.6000 kwa siku (180,000 kwa mwezi)...gross income ni mapato ghafi...hapo hajakatwa PAYE, hajalipa nauli, n.k...na zile cost zinazokuwa associated na kazi yake. Na ndio maana nikakuambia, ukishatoa gharama zote hizo; unakuta anabaki na negative balance na ndio maana wengi wao kama sio wote mshahara unakuwa umeisha tarehe 27 ya mwezi ule ule aliopokea; implying kwamba tayari ana-operate under negative balance...kwahiyo kwa akili yako unadhani huyo anayebaki na negative balance anabaki na pesa nyingi sio?
Kwahiyo mheshimiwa wa hesabu za "versity", mapato ghafi ya sh 4,000 kwa siku na yale ya sh 6,000 kwa siku yapi makubwa boss mchumi? Hesabu zako na economics za "versity" zikasema sh 4,000 ndiyo kubwa (umeichanganya kwenye mtaji ikawa 38,000! kwahiyo unataka huyu ndugu ale mtaji wake kwa kujidanganya ana mapato makubwa kuliko huyo wa 6,000, na kesho atazungusha mtaji upi?)
Wewe hufahamu nini maana ya mapato ghafi....rudi darasani ukajifunze!
Hili janga la division five sikujua kama limeenea hadi "versity"!
Ndo tatizo la vilaza...hawafahamu kwamba ni vilaza! Jielimishe mambo yafuatayo...gross income, net income, gross profit, net profit! Hapa unachanganya mambo
 
Back
Top Bottom