Toka mtandaoni

Toka mtandaoni

Hata bongo ni hivyo hivyo tu ..serikali lini imewaangalia wananchi wa kipato cha chini ..

Halafu mimi nilikuwa nazungumzia hali ya umoja waliyo nayo wananchi achana na hizo habari za serikali za africa .... ina fahamika na iko wazi kwamba serikali zote za Africa huwa zinawageuza wananchi wake kuwa chuma ulete /ng'ombe wa maziwa
Ndugu yangu hakuna la kujifunza Kenya ukiwa Kenya ndio unaona utofauti wa maisha ebu fikilia huyo mtoto yupo chini ya miaka 5 ingepaswa atibiwe bure lakini hakuna sheria hiyo pili Jana bunge limejadiri hali imezidi kuwa mbaya maiti zimerundikana mortuary familia hazina uwezo wa kuzikomboa zika zikwe sheria inasema huwezi kuzika mpaka maiti ifanyiwe uchunguzi na gharama ni kubwa zinabebwa na familia na wana shindwa kupata ela wasalia wema ujitokeza kila siku kulipia gharama ukiwa na bahati unalipiwa..Kenya kuna umasikini mbaya kila kitu ni ela aiangali wa kipato cha chini..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani " watanzania tuna mengi sana ya kujifunza toka kwa wakenya

Imagine watu hawa walipitia machafuko makubwa ya kisiasa mnamo mwaka 2007 lakini hiyo kwao haijawa sababu ya msingi ya kuwagawa pindi yanapo kuja masuala ya kitaifa huwa wana simama pamoja na kushirikiana kwa moyo wote na wadhati ...

Katika yale machafuko yao kuna ambao waliopoteza wazazi .ndugu na jamaa " lakini hiyo kwao haijawa sababu ya wao kuendeleza chuki baina ya wao kwa wao

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio wanafki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pia kitendo Afisa wa Polisi kuamua kutoa mshahara wake kumpa Murage ni ishara kwamba utu ni tunu muhimu kwa wakenya. Polisi haohao waliomkamata na kumpandisha kizimbani ndio wanatoa hela wanampa. That means walimkamata tu ili kukidhi matakwa ya kisheria. Wakaiacha sheria ichukue mkondo wake, lakini haikuwaondolea ubinadamu wa kumsaidia

Jr
Bongo tunapolice wenye moyo wa aina hiyo?
 
Kisa cha Boniface Murage


Anaandika Goliath Goliath Mfalamagoha
_
Boniface Murage, mkazi wa Embakasi, Nairobi nchini Kenya, amekuwa gumzo katika vyombo vya habari Afrika Mashariki baada ya kukamatwa akijaribu kumtorosha mwanae Hospitali kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

Murage alishindwa kulipa Shilingi 56,000/= za Kenya (sawa na 1.3 milioni za Tanzania), ambazo ni bill ya mtoto wake aliyepatiwa matibabu hospitali ya Kenyatta.

Gharama hizi ni kubwa sana kutokana na uhalisia wa hali yake ya kiuchumi na hivyo akaamua kumtorosha mtoto wake kwa kumficha kwenye Begi.

Askari walipofungua begi walimuona mtoto. Murage akakamatwa na kufunguliwa mashtaka. Jumanne February 19 mahakama ilimkuta na hatia na kumhukumu kifungo cha nje cha miezi mitatu na kutakiwa kulipa gharama hizo.

Tukio hili limegusa hisia za watu wengi nchini Kenya, na baadhi walijitokeza kumuwekea dhamana, na wengine kumlipia gharama za mawakili.

Gavana wa Nairobi Mike Sonko amelipia gharama zote za hospitali na amemfanyia shopping mtoto huyo ya mahitaji yake muhimu ikiwemo nguo, chakula na vifaa vya kuchezea. Pia amempa Murage offer ya kazi ili aweze kutunza familia yake.

Mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino amempatia Murage KSH 200,000/= (sawa na 4.5Milion za Tanzania) kama alivyoahidi siku Murage anakamatwa.

Mkuu wa Polisi Embakasi SSP Tamo Sanaiet alifika mahakamani juzi wakati hukumu ikisomwa na kumkabidhi KSH 56,000/= akidai ameamua kutoa mshahara wake kumsaidia Murage kutokana na kuguswa na kisa chake.

Kuna mengi ya kujifunza katika kisa hiki cha Murage. Lakini kwa uchache nitakueleza machache.

Kwanza ni namna kina baba wanavyohangaika ili kutunza familia zao. Hujui anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa salama. Anapitia mangapi kuhakikisha mnapata chakula. Anapitia mangapi kuhakikisha bili zinalipwa. Anapitia mangapi kuhakikisha mnasoma. Anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa na afya bora.

Pili, haijalishi unapitia magumu mangapi, usikate tamaa. Hali yako ya sasa ni ya muda tu. Ipo siku itatoweka, na hutabaki kama ulivyo. Pengine jaribu lako ndio njia ya kukufikia mafanikio yako. Murage hakujua kama kitendo cha kumtorosha mwanae kingebadili kabisa maisha yake. Amelipiwa bill zote na kupatiwa kazi.

Tatu; ni suala la umoja wa kitaifa. Ukiona namna jamii ya wakenya walivyoguswa na tukio hili utaamini katika umoja ninaousemea. Ukianza na wanasiasa waliomsaidia ambao wanatoka vyama hasimu, Babu Owino (NASA) na Sonko (Jubilee) lakini waliweka tofauti zao pembeni. Hapa kwetu kuna Waziri alitamka hadharani kuwa hawezi kumsaidia binti mmoja mgonjwa kwa sababu anayekusanya michango hiyo ni kiongozi wa Chadema. Kenya siasa ni diversion za maendeleo, but kwetu siasa ni uadui.

Pia kitendo Afisa wa Polisi kuamua kutoa mshahara wake kumpa Murage ni ishara kwamba utu ni tunu muhimu kwa wakenya. Polisi haohao waliomkamata na kumpandisha kizimbani ndio wanatoa hela wanampa. That means walimkamata tu ili kukidhi matakwa ya kisheria. Wakaiacha sheria ichukue mkondo wake, lakini haikuwaondolea ubinadamu wa kumsaidia.!

Jr
So touchy na inaelimisha, kwa Tanzania ya leo chuki iliyopo kati ya serikali na opposition parties na chuki kati ya polisi na raia hicho kilichotokea huko Kenya hakiwezekani.
 
Mshana hii Mada Ina mafunzo muhimu. Lakini, sidhani kama wa Tanzania watayaona. Fikiria, mtu anamiminiwa risasi 30,watu wanajawa na simanzi na kuandaa ibada ya kumuombea, waziri anayeongoza jeshi la polisi anazuia maombi hayo kufanyika. Naamini maombi hayo yangeambatana na kuchanga fedha ya matibabu. Kwanini? Kwa sababu aliyeumizwa si mwenzetu, yeye ni chadema, si ccm.
Tumepofushwa mno na siasa za majitaka kiasi kwamba hata uwezo wetu wa kuona logic umeisha. Kila kitu Sasa kinatafasiriwa kisiasa. Kwa hatua tuliyofikia, hakuna jinsi tunaweza kurudisha upendo tena mpaka tuuane kwanza kama wakenya walivyofanya, ndipo tutaiona thamani ya kupendana.
Ni bahati mbaya kwetu kwa Sasa uongozi uliopo ndio unachochea migawanyiko ya kisiasa. Ona, baada ya kupata ajali, aliyezuia watu wasimwombee aliyepigwa risasi a naomba watanzania wamwombee! Ona mijadala ya humu ilivyojaa migawanyiko. Ukisoma comment ya mtu, unajua yuko upande gani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kisa kimenipa kitu na kuniongezea ujazo flani ktk kuingia na kutoka.kwangu..

ubarikiwe sana mzee mshana...

i like you mzee wa busara..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
siasa za hapa kwetu bi uadui..

..Inaumiza mnoo

hatujali utu tena,
Mshana hii Mada Ina mafunzo muhimu. Lakini, sidhani kama wa Tanzania watayaona. Fikiria, mtu anamiminiwa risasi 30,watu wanajawa na simanzi na kuandaa ibada ya kumuombea, waziri anayeongoza jeshi la polisi anazuia maombi hayo kufanyika. Naamini maombi hayo yangeambatana na kuchanga fedha ya matibabu. Kwanini? Kwa sababu aliyeumizwa si mwenzetu, yeye ni chadema, si ccm.
Tumepofushwa mno na siasa za majitaka kiasi kwamba hata uwezo wetu wa kuona logic umeisha. Kila kitu Sasa kinatafasiriwa kisiasa. Kwa hatua tuliyofikia, hakuna jinsi tunaweza kurudisha upendo tena mpaka tuuane kwanza kama wakenya walivyofanya, ndipo tutaiona thamani ya kupendana.
Ni bahati mbaya kwetu kwa Sasa uongozi uliopo ndio unachochea migawanyiko ya kisiasa. Ona, baada ya kupata ajali, aliyezuia watu wasimwombee aliyepigwa risasi a naomba watanzania wamwombee! Ona mijadala ya humu ilivyojaa migawanyiko. Ukisoma comment ya mtu, unajua yuko upande gani.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kisa cha Boniface Murage


Anaandika Goliath Goliath Mfalamagoha
_
Boniface Murage, mkazi wa Embakasi, Nairobi nchini Kenya, amekuwa gumzo katika vyombo vya habari Afrika Mashariki baada ya kukamatwa akijaribu kumtorosha mwanae Hospitali kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

Murage alishindwa kulipa Shilingi 56,000/= za Kenya (sawa na 1.3 milioni za Tanzania), ambazo ni bill ya mtoto wake aliyepatiwa matibabu hospitali ya Kenyatta.

Gharama hizi ni kubwa sana kutokana na uhalisia wa hali yake ya kiuchumi na hivyo akaamua kumtorosha mtoto wake kwa kumficha kwenye Begi.

Askari walipofungua begi walimuona mtoto. Murage akakamatwa na kufunguliwa mashtaka. Jumanne February 19 mahakama ilimkuta na hatia na kumhukumu kifungo cha nje cha miezi mitatu na kutakiwa kulipa gharama hizo.

Tukio hili limegusa hisia za watu wengi nchini Kenya, na baadhi walijitokeza kumuwekea dhamana, na wengine kumlipia gharama za mawakili.

Gavana wa Nairobi Mike Sonko amelipia gharama zote za hospitali na amemfanyia shopping mtoto huyo ya mahitaji yake muhimu ikiwemo nguo, chakula na vifaa vya kuchezea. Pia amempa Murage offer ya kazi ili aweze kutunza familia yake.

Mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino amempatia Murage KSH 200,000/= (sawa na 4.5Milion za Tanzania) kama alivyoahidi siku Murage anakamatwa.

Mkuu wa Polisi Embakasi SSP Tamo Sanaiet alifika mahakamani juzi wakati hukumu ikisomwa na kumkabidhi KSH 56,000/= akidai ameamua kutoa mshahara wake kumsaidia Murage kutokana na kuguswa na kisa chake.

Kuna mengi ya kujifunza katika kisa hiki cha Murage. Lakini kwa uchache nitakueleza machache.

Kwanza ni namna kina baba wanavyohangaika ili kutunza familia zao. Hujui anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa salama. Anapitia mangapi kuhakikisha mnapata chakula. Anapitia mangapi kuhakikisha bili zinalipwa. Anapitia mangapi kuhakikisha mnasoma. Anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa na afya bora.

Pili, haijalishi unapitia magumu mangapi, usikate tamaa. Hali yako ya sasa ni ya muda tu. Ipo siku itatoweka, na hutabaki kama ulivyo. Pengine jaribu lako ndio njia ya kukufikia mafanikio yako. Murage hakujua kama kitendo cha kumtorosha mwanae kingebadili kabisa maisha yake. Amelipiwa bill zote na kupatiwa kazi.

Tatu; ni suala la umoja wa kitaifa. Ukiona namna jamii ya wakenya walivyoguswa na tukio hili utaamini katika umoja ninaousemea. Ukianza na wanasiasa waliomsaidia ambao wanatoka vyama hasimu, Babu Owino (NASA) na Sonko (Jubilee) lakini waliweka tofauti zao pembeni. Hapa kwetu kuna Waziri alitamka hadharani kuwa hawezi kumsaidia binti mmoja mgonjwa kwa sababu anayekusanya michango hiyo ni kiongozi wa Chadema. Kenya siasa ni diversion za maendeleo, but kwetu siasa ni uadui.

Pia kitendo Afisa wa Polisi kuamua kutoa mshahara wake kumpa Murage ni ishara kwamba utu ni tunu muhimu kwa wakenya. Polisi haohao waliomkamata na kumpandisha kizimbani ndio wanatoa hela wanampa. That means walimkamata tu ili kukidhi matakwa ya kisheria. Wakaiacha sheria ichukue mkondo wake, lakini haikuwaondolea ubinadamu wa kumsaidia.!

Jr

Umeandika vyema mwenyekiti na kuwasilisha mawazo yako vilivyo. Ubarikiwe.
 
Kisa cha Boniface Murage


Anaandika Goliath Goliath Mfalamagoha
_
Boniface Murage, mkazi wa Embakasi, Nairobi nchini Kenya, amekuwa gumzo katika vyombo vya habari Afrika Mashariki baada ya kukamatwa akijaribu kumtorosha mwanae Hospitali kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

Murage alishindwa kulipa Shilingi 56,000/= za Kenya (sawa na 1.3 milioni za Tanzania), ambazo ni bill ya mtoto wake aliyepatiwa matibabu hospitali ya Kenyatta.

Gharama hizi ni kubwa sana kutokana na uhalisia wa hali yake ya kiuchumi na hivyo akaamua kumtorosha mtoto wake kwa kumficha kwenye Begi.

Askari walipofungua begi walimuona mtoto. Murage akakamatwa na kufunguliwa mashtaka. Jumanne February 19 mahakama ilimkuta na hatia na kumhukumu kifungo cha nje cha miezi mitatu na kutakiwa kulipa gharama hizo.

Tukio hili limegusa hisia za watu wengi nchini Kenya, na baadhi walijitokeza kumuwekea dhamana, na wengine kumlipia gharama za mawakili.

Gavana wa Nairobi Mike Sonko amelipia gharama zote za hospitali na amemfanyia shopping mtoto huyo ya mahitaji yake muhimu ikiwemo nguo, chakula na vifaa vya kuchezea. Pia amempa Murage offer ya kazi ili aweze kutunza familia yake.

Mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino amempatia Murage KSH 200,000/= (sawa na 4.5Milion za Tanzania) kama alivyoahidi siku Murage anakamatwa.

Mkuu wa Polisi Embakasi SSP Tamo Sanaiet alifika mahakamani juzi wakati hukumu ikisomwa na kumkabidhi KSH 56,000/= akidai ameamua kutoa mshahara wake kumsaidia Murage kutokana na kuguswa na kisa chake.

Kuna mengi ya kujifunza katika kisa hiki cha Murage. Lakini kwa uchache nitakueleza machache.

Kwanza ni namna kina baba wanavyohangaika ili kutunza familia zao. Hujui anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa salama. Anapitia mangapi kuhakikisha mnapata chakula. Anapitia mangapi kuhakikisha bili zinalipwa. Anapitia mangapi kuhakikisha mnasoma. Anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa na afya bora.

Pili, haijalishi unapitia magumu mangapi, usikate tamaa. Hali yako ya sasa ni ya muda tu. Ipo siku itatoweka, na hutabaki kama ulivyo. Pengine jaribu lako ndio njia ya kukufikia mafanikio yako. Murage hakujua kama kitendo cha kumtorosha mwanae kingebadili kabisa maisha yake. Amelipiwa bill zote na kupatiwa kazi.

Tatu; ni suala la umoja wa kitaifa. Ukiona namna jamii ya wakenya walivyoguswa na tukio hili utaamini katika umoja ninaousemea. Ukianza na wanasiasa waliomsaidia ambao wanatoka vyama hasimu, Babu Owino (NASA) na Sonko (Jubilee) lakini waliweka tofauti zao pembeni. Hapa kwetu kuna Waziri alitamka hadharani kuwa hawezi kumsaidia binti mmoja mgonjwa kwa sababu anayekusanya michango hiyo ni kiongozi wa Chadema. Kenya siasa ni diversion za maendeleo, but kwetu siasa ni uadui.

Pia kitendo Afisa wa Polisi kuamua kutoa mshahara wake kumpa Murage ni ishara kwamba utu ni tunu muhimu kwa wakenya. Polisi haohao waliomkamata na kumpandisha kizimbani ndio wanatoa hela wanampa. That means walimkamata tu ili kukidhi matakwa ya kisheria. Wakaiacha sheria ichukue mkondo wake, lakini haikuwaondolea ubinadamu wa kumsaidia.!

Jr
Nimepata kitu cha kujifunza hapa!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom