Toka mtandaoni

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,791
Kisa cha Boniface Murage


Anaandika Goliath Goliath Mfalamagoha
_
Boniface Murage, mkazi wa Embakasi, Nairobi nchini Kenya, amekuwa gumzo katika vyombo vya habari Afrika Mashariki baada ya kukamatwa akijaribu kumtorosha mwanae Hospitali kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

Murage alishindwa kulipa Shilingi 56,000/= za Kenya (sawa na 1.3 milioni za Tanzania), ambazo ni bill ya mtoto wake aliyepatiwa matibabu hospitali ya Kenyatta.

Gharama hizi ni kubwa sana kutokana na uhalisia wa hali yake ya kiuchumi na hivyo akaamua kumtorosha mtoto wake kwa kumficha kwenye Begi.

Askari walipofungua begi walimuona mtoto. Murage akakamatwa na kufunguliwa mashtaka. Jumanne February 19 mahakama ilimkuta na hatia na kumhukumu kifungo cha nje cha miezi mitatu na kutakiwa kulipa gharama hizo.

Tukio hili limegusa hisia za watu wengi nchini Kenya, na baadhi walijitokeza kumuwekea dhamana, na wengine kumlipia gharama za mawakili.

Gavana wa Nairobi Mike Sonko amelipia gharama zote za hospitali na amemfanyia shopping mtoto huyo ya mahitaji yake muhimu ikiwemo nguo, chakula na vifaa vya kuchezea. Pia amempa Murage offer ya kazi ili aweze kutunza familia yake.

Mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino amempatia Murage KSH 200,000/= (sawa na 4.5Milion za Tanzania) kama alivyoahidi siku Murage anakamatwa.

Mkuu wa Polisi Embakasi SSP Tamo Sanaiet alifika mahakamani juzi wakati hukumu ikisomwa na kumkabidhi KSH 56,000/= akidai ameamua kutoa mshahara wake kumsaidia Murage kutokana na kuguswa na kisa chake.

Kuna mengi ya kujifunza katika kisa hiki cha Murage. Lakini kwa uchache nitakueleza machache.

Kwanza ni namna kina baba wanavyohangaika ili kutunza familia zao. Hujui anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa salama. Anapitia mangapi kuhakikisha mnapata chakula. Anapitia mangapi kuhakikisha bili zinalipwa. Anapitia mangapi kuhakikisha mnasoma. Anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa na afya bora.

Pili, haijalishi unapitia magumu mangapi, usikate tamaa. Hali yako ya sasa ni ya muda tu. Ipo siku itatoweka, na hutabaki kama ulivyo. Pengine jaribu lako ndio njia ya kukufikia mafanikio yako. Murage hakujua kama kitendo cha kumtorosha mwanae kingebadili kabisa maisha yake. Amelipiwa bill zote na kupatiwa kazi.

Tatu; ni suala la umoja wa kitaifa. Ukiona namna jamii ya wakenya walivyoguswa na tukio hili utaamini katika umoja ninaousemea. Ukianza na wanasiasa waliomsaidia ambao wanatoka vyama hasimu, Babu Owino (NASA) na Sonko (Jubilee) lakini waliweka tofauti zao pembeni. Hapa kwetu kuna Waziri alitamka hadharani kuwa hawezi kumsaidia binti mmoja mgonjwa kwa sababu anayekusanya michango hiyo ni kiongozi wa Chadema. Kenya siasa ni diversion za maendeleo, but kwetu siasa ni uadui.

Pia kitendo Afisa wa Polisi kuamua kutoa mshahara wake kumpa Murage ni ishara kwamba utu ni tunu muhimu kwa wakenya. Polisi haohao waliomkamata na kumpandisha kizimbani ndio wanatoa hela wanampa. That means walimkamata tu ili kukidhi matakwa ya kisheria. Wakaiacha sheria ichukue mkondo wake, lakini haikuwaondolea ubinadamu wa kumsaidia.!

Jr
 
Asante sana " .... mafundisho mazuri kwaajili ya chakula cha ubongo

Naona ile nahau ya UKIMPIGA CHURA TEKE NDIO UNAMUONGEZEA MWENDO
imechukua nafasi yake ipaswavyo katika kisa hiki cha Murage

Sent using Jamii Forums mobile app
Pia kitendo Afisa wa Polisi kuamua kutoa mshahara wake kumpa Murage ni ishara kwamba utu ni tunu muhimu kwa wakenya. Polisi haohao waliomkamata na kumpandisha kizimbani ndio wanatoa hela wanampa. That means walimkamata tu ili kukidhi matakwa ya kisheria. Wakaiacha sheria ichukue mkondo wake, lakini haikuwaondolea ubinadamu wa kumsaidia

Jr
 
Kisa cha Boniface Murage


Anaandika Goliath Goliath Mfalamagoha
_
Boniface Murage, mkazi wa Embakasi, Nairobi nchini Kenya, amekuwa gumzo katika vyombo vya habari Afrika Mashariki baada ya kukamatwa akijaribu kumtorosha mwanae Hospitali kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

Murage alishindwa kulipa Shilingi 56,000/= za Kenya (sawa na 1.3 milioni za Tanzania), ambazo ni bill ya mtoto wake aliyepatiwa matibabu hospitali ya Kenyatta.

Gharama hizi ni kubwa sana kutokana na uhalisia wa hali yake ya kiuchumi na hivyo akaamua kumtorosha mtoto wake kwa kumficha kwenye Begi.

Askari walipofungua begi walimuona mtoto. Murage akakamatwa na kufunguliwa mashtaka. Jumanne February 19 mahakama ilimkuta na hatia na kumhukumu kifungo cha nje cha miezi mitatu na kutakiwa kulipa gharama hizo.

Tukio hili limegusa hisia za watu wengi nchini Kenya, na baadhi walijitokeza kumuwekea dhamana, na wengine kumlipia gharama za mawakili.

Gavana wa Nairobi Mike Sonko amelipia gharama zote za hospitali na amemfanyia shopping mtoto huyo ya mahitaji yake muhimu ikiwemo nguo, chakula na vifaa vya kuchezea. Pia amempa Murage offer ya kazi ili aweze kutunza familia yake.

Mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino amempatia Murage KSH 200,000/= (sawa na 4.5Milion za Tanzania) kama alivyoahidi siku Murage anakamatwa.

Mkuu wa Polisi Embakasi SSP Tamo Sanaiet alifika mahakamani juzi wakati hukumu ikisomwa na kumkabidhi KSH 56,000/= akidai ameamua kutoa mshahara wake kumsaidia Murage kutokana na kuguswa na kisa chake.

Kuna mengi ya kujifunza katika kisa hiki cha Murage. Lakini kwa uchache nitakueleza machache.

Kwanza ni namna kina baba wanavyohangaika ili kutunza familia zao. Hujui anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa salama. Anapitia mangapi kuhakikisha mnapata chakula. Anapitia mangapi kuhakikisha bili zinalipwa. Anapitia mangapi kuhakikisha mnasoma. Anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa na afya bora.

Pili, haijalishi unapitia magumu mangapi, usikate tamaa. Hali yako ya sasa ni ya muda tu. Ipo siku itatoweka, na hutabaki kama ulivyo. Pengine jaribu lako ndio njia ya kukufikia mafanikio yako. Murage hakujua kama kitendo cha kumtorosha mwanae kingebadili kabisa maisha yake. Amelipiwa bill zote na kupatiwa kazi.

Tatu; ni suala la umoja wa kitaifa. Ukiona namna jamii ya wakenya walivyoguswa na tukio hili utaamini katika umoja ninaousemea. Ukianza na wanasiasa waliomsaidia ambao wanatoka vyama hasimu, Babu Owino (NASA) na Sonko (Jubilee) lakini waliweka tofauti zao pembeni. Hapa kwetu kuna Waziri alitamka hadharani kuwa hawezi kumsaidia binti mmoja mgonjwa kwa sababu anayekusanya michango hiyo ni kiongozi wa Chadema. Kenya siasa ni diversion za maendeleo, but kwetu siasa ni uadui.

Pia kitendo Afisa wa Polisi kuamua kutoa mshahara wake kumpa Murage ni ishara kwamba utu ni tunu muhimu kwa wakenya. Polisi haohao waliomkamata na kumpandisha kizimbani ndio wanatoa hela wanampa. That means walimkamata tu ili kukidhi matakwa ya kisheria. Wakaiacha sheria ichukue mkondo wake, lakini haikuwaondolea ubinadamu wa kumsaidia.!

Jr
Ni kweli kabisa kuna mambo kadhaa ya msingi sana ya kujifunza kutoka kisa hiki ambacho kiukweli kimeaanza kwa uchungu na kuisha kwa faraja na matumaini makubwa.

Kwa muktadha wa hapa kwetu Bongo hivyo visa vya namna hiyo vipo,sema tu huwa haviripotiwi kutokana na labda waandishi wetu kutovutiwa na habari hizo.

Kwenye suala la kusaidia kwa sasa kwa maoni yangu tumeshaharibiwa kifikra na siasa zetu za kisenge-lema. Tumeshavuka msitari mwekundu na kamwe hatuwezi kurudi nyuma...!! Mathalani wee angalia tu kwenye harusi,misiba,sherehe na hata kwenye michezo nako kumekuwa na CCM na UKAWA, kama unabisha angalia hili linaloendelea na boss Ruge,soon litachagua mkondo...!!

Just wait & see....!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii inanikumbusha jamaa aliyejitolea kumuokoa yule mtoto aliyekuwa ananin'ginia kwenye ghorofa Ufaransa, hakuna aijuaye kesho yake jamaa kuugua kwa mtoto wake ametoka kimaisha.
 
Wanaume tumeumbiwa mateso by msondo ngoma baba ya muziki..Mshana Kenya Sekta ya afya imekuwa chungu kwa masikini jana Wabunge wamelazimika kujadiri hoja ya kuondoa gharama za uhifadhi na uchunguzi wa maiti.Sheria yao ina sema popote utako fia hiwe nyumbani au popote pale maiti lazima ifanyiwe uchunguzi na gharama ina beba familia imepelekea watu kushindwa kuzika wapendwa wao mpaka miezi minne wabunge na wasalia wema utoa fedha kusaidia kukomboa maiti..Kama maiti ina zuiliwa kwa Mgonjwa ni hali mbaya..Angalau waweke sheria watoto chini ya miaka 5 na wazee hiwe bure..
 
KAMA YAPI? UNAOA UKIWA NA HELA BAADAE UNAPOTEZA KAZI AMA BIASHARA UNAANZA KUTAABIKA, SO ULITAKA AMKIMBIE MTOTO??
MTU ana miaka 22 lini aliwahi kuwa na fedha? Huyo alikurupuka tu kuanzisha family...
 
Kabisa, mimi nimependa huyo askari alivyojitolea mshahara wake, sidhani kama bongo kuna askari wakufanya hivyo kwamuharifu zaidi ndio kwanza angekazia msumari asurubiwe huyooo

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani " watanzania tuna mengi sana ya kujifunza toka kwa wakenya

Imagine watu hawa walipitia machafuko makubwa ya kisiasa mnamo mwaka 2007 lakini hiyo kwao haijawa sababu ya msingi ya kuwagawa pindi yanapo kuja masuala ya kitaifa huwa wana simama pamoja na kushirikiana kwa moyo wote na wadhati ...

Katika yale machafuko yao kuna ambao waliopoteza wazazi .ndugu na jamaa " lakini hiyo kwao haijawa sababu ya wao kuendeleza chuki baina ya wao kwa wao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kisa cha Boniface Murage


Anaandika Goliath Goliath Mfalamagoha
_
Boniface Murage, mkazi wa Embakasi, Nairobi nchini Kenya, amekuwa gumzo katika vyombo vya habari Afrika Mashariki baada ya kukamatwa akijaribu kumtorosha mwanae Hospitali kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

Murage alishindwa kulipa Shilingi 56,000/= za Kenya (sawa na 1.3 milioni za Tanzania), ambazo ni bill ya mtoto wake aliyepatiwa matibabu hospitali ya Kenyatta.

Gharama hizi ni kubwa sana kutokana na uhalisia wa hali yake ya kiuchumi na hivyo akaamua kumtorosha mtoto wake kwa kumficha kwenye Begi.

Askari walipofungua begi walimuona mtoto. Murage akakamatwa na kufunguliwa mashtaka. Jumanne February 19 mahakama ilimkuta na hatia na kumhukumu kifungo cha nje cha miezi mitatu na kutakiwa kulipa gharama hizo.

Tukio hili limegusa hisia za watu wengi nchini Kenya, na baadhi walijitokeza kumuwekea dhamana, na wengine kumlipia gharama za mawakili.

Gavana wa Nairobi Mike Sonko amelipia gharama zote za hospitali na amemfanyia shopping mtoto huyo ya mahitaji yake muhimu ikiwemo nguo, chakula na vifaa vya kuchezea. Pia amempa Murage offer ya kazi ili aweze kutunza familia yake.

Mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino amempatia Murage KSH 200,000/= (sawa na 4.5Milion za Tanzania) kama alivyoahidi siku Murage anakamatwa.

Mkuu wa Polisi Embakasi SSP Tamo Sanaiet alifika mahakamani juzi wakati hukumu ikisomwa na kumkabidhi KSH 56,000/= akidai ameamua kutoa mshahara wake kumsaidia Murage kutokana na kuguswa na kisa chake.

Kuna mengi ya kujifunza katika kisa hiki cha Murage. Lakini kwa uchache nitakueleza machache.

Kwanza ni namna kina baba wanavyohangaika ili kutunza familia zao. Hujui anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa salama. Anapitia mangapi kuhakikisha mnapata chakula. Anapitia mangapi kuhakikisha bili zinalipwa. Anapitia mangapi kuhakikisha mnasoma. Anapitia mangapi kuhakikisha mnakuwa na afya bora.

Pili, haijalishi unapitia magumu mangapi, usikate tamaa. Hali yako ya sasa ni ya muda tu. Ipo siku itatoweka, na hutabaki kama ulivyo. Pengine jaribu lako ndio njia ya kukufikia mafanikio yako. Murage hakujua kama kitendo cha kumtorosha mwanae kingebadili kabisa maisha yake. Amelipiwa bill zote na kupatiwa kazi.

Tatu; ni suala la umoja wa kitaifa. Ukiona namna jamii ya wakenya walivyoguswa na tukio hili utaamini katika umoja ninaousemea. Ukianza na wanasiasa waliomsaidia ambao wanatoka vyama hasimu, Babu Owino (NASA) na Sonko (Jubilee) lakini waliweka tofauti zao pembeni. Hapa kwetu kuna Waziri alitamka hadharani kuwa hawezi kumsaidia binti mmoja mgonjwa kwa sababu anayekusanya michango hiyo ni kiongozi wa Chadema. Kenya siasa ni diversion za maendeleo, but kwetu siasa ni uadui.

Pia kitendo Afisa wa Polisi kuamua kutoa mshahara wake kumpa Murage ni ishara kwamba utu ni tunu muhimu kwa wakenya. Polisi haohao waliomkamata na kumpandisha kizimbani ndio wanatoa hela wanampa. That means walimkamata tu ili kukidhi matakwa ya kisheria. Wakaiacha sheria ichukue mkondo wake, lakini haikuwaondolea ubinadamu wa kumsaidia.!

Jr
Huku wanaiba hadi rambirambi za marehem, kuna kiongozi na kingozi,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani " watanzania tuna mengi sana ya kujifunza toka kwa wakenya

Imagine watu hawa walipitia machafuko makubwa ya kisiasa mnamo mwaka 2007 lakini hiyo kwao haijawa sababu ya msingi ya kuwagawa pindi yanapo kuja masuala ya kitaifa huwa wana simama pamoja na kushirikiana kwa moyo wote na wadhati ...

Katika yale machafuko yao kuna ambao waliopoteza wazazi .ndugu na jamaa " lakini hiyo kwao haijawa sababu ya wao kuendeleza chuki baina ya wao kwa wao

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yangu hakuna la kujifunza Kenya ukiwa Kenya ndio unaona utofauti wa maisha ebu fikilia huyo mtoto yupo chini ya miaka 5 ingepaswa atibiwe bure lakini hakuna sheria hiyo pili Jana bunge limejadiri hali imezidi kuwa mbaya maiti zimerundikana mortuary familia hazina uwezo wa kuzikomboa zika zikwe sheria inasema huwezi kuzika mpaka maiti ifanyiwe uchunguzi na gharama ni kubwa zinabebwa na familia na wana shindwa kupata ela wasalia wema ujitokeza kila siku kulipia gharama ukiwa na bahati unalipiwa..Kenya kuna umasikini mbaya kila kitu ni ela aiangali wa kipato cha chini..
 
Back
Top Bottom