Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Mfumo wa uchumi ulikua free sana mpaka pesa yetu ikashuka thamani.Chamaana anatakiwa apandishe mishahara kwa watumishi wa chini ili ireflect kwenye maendeleo ya mtu wa chini.Elimu bure si sahihi sana maana uendeshaji wa shule umekua mgumu sana.Arudishe michango ya mitihani na taaluma,mambo yataenda vizuri tu.
 
Mfumo wa uchumi ulikua free sana mpaka pesa yetu ikashuka thamani.Chamaana anatakiwa apandishe mishahara kwa watumishi wa chini ili ireflect kwenye maendeleo ya mtu wa chini.Elimu bure si sahihi sana maana uendeshaji wa shule umekua mgumu sana.Arudishe michango ya mitihani na taaluma,mambo yataenda vizuri tu.

Well said
Tunahitaji watu kama nyie wenye ushauri wa maana

Kiukweli hali ni mbaya akipandisha mishara kwa watumishi wa hali ya chini pesa itarudi kwenye mzunguko
 
01.Mkoa wa Ruvuma wilaya ya Namtumbo raia wanatozwa sh elfu saba ya bili ya maji kila mwezi wakati maji hayatoki.
Raia wasio na maji kwenye mabomba yao wanapata huduma ya maji kwa majirani ambapo pia hutakiwa kulipia sh 100 kwa ndoo.Hili ni jipu maana idara ya maji inatunyang'anya elfu saba kila mwezi kwa kila kaya na huenda wamekula dili na wenye mabomba wachache wanao endelea kutuuzia maji japo tunalipia hiyo elfu saba kwa mwezi.

02.Wadau wa elimu wafatilie shule ya sekondari Rwinga iliyopo hapo Namtumbo walimu wake kwa sasa hawafundishi.
Ikifika saa nne asubuhi wengi huondoka eneo la kazi.
 
Ufisadi Ni Mbaya Kwa Nchi, Lakini jambo Baya zaidi ya Ufisadi, ambalo Limeleta Vita, Kusababisha Wakimbizi na Aibu Kubwa sana Mataifa ya Afrika ni Udictator, Kama Mafisadi na Wazembe wanatakiwa "Kutumbuliwa" Mimi Nasema Kadhalika Madictator wanatakiwa "KUTUNGULIWA" Maana sasa hakuna Jinsi Nyingine Kusema Ukweli
 
Wizi wa pikipiki umekithiri ndani ya gereza la Segerea.
Wageni wanaolitembelea gereza hilo siku za jmosi na jpili ili kuwaona ndugu na jamaa zao waliofungwa,wanalalamikia kukosekana kwa usalama wa vyombo vyao vya moto,hasa pikipiki.
Cha ajabu parking ipo ndani ya eneo la gereza ambapo mtu hukaguliwa anapoingia,lakini hakuna utaratibu unaoeleweka wakati wa kutoka na hivyo wajanja wameamua kutumia fursa hiyo,unaingia unapaki pikipiki lako,ukitoka halipo,na karibia kila weekend kuna pikipiki zinaibiwa kwa jinsi hiyo.
Hii ni aibu kwa jeshi la Magereza,eneo linalopaswa kuwa na ulinzi wa hali ya juu na itifaki za kiusalama zinazoeleweka,linakosa ulinzi kwa kiasi hiki hadi wajanja wanaligeuza shamba la kuvunia bodaboda!
Jeshi la Magereza lishughulikie tatizo hilo.
 
Ndugu wana JamiiForums,

Nchi yetu imetafunwa mno na ni wakati sasa tuseme imetosha. Tumsaidie Rais Magufuli na Serikali yake kuweza kuzifahamu kero zetu za yanayotusumbua kama watanzania ambayo tungependa yafanyiwe kazi.

Karibuni sana.

MWONGOZO:
Elezea jipu/kero yako na kama ina ufafanuzi wa kutosha (nani, wapi, lini, kivipi n.k) ukiambatana na nyaraka itapendeza zaidi.

Kero hizi zitachapwa na kupelekwa kwa mamlaka husika ili zifanyiwe ufuatiliaji.
Nyumba za serikali zilizouzwa nchi nzima kila mtu shahidi,Lugumi mkataba wake umeisha vipi.
 
Wizara ya elimu hebu fuatilieni haraka kinachoendelea shule ya sekondari ya kata ya Matosa iliyoko manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam wakati huu wa mitihani ya form iv.
Kuna wanafunzi takriban 17 ambao wamezuiwa na academic master wa shule hiyo kufanya mitihani yote ya form iv kwa sababu zisizokubalika kisheria.
Sababu alizotoa ni kwamba wanafunzi hao hawajiwezi kitaaluma na hivyo hataki wafanye mtihani wa form iv.
Sijawahi kusikia kitu kama hiki,labda wana jf wenzangu mnisaidie.
Vijana hao wamesoma pale kuanzia form one,form two mtihani wa taifa walifanya na kupita,wamesoma hadi form four na mock walifanya,cha ajabu jtatu siku ya kuanza mitihani wakati wa kupangwa na kupewa namba mwalimu huyo aliwaita na kuwaeleza kuwa wao hawataruhusiwa kufanya mitihani kwa sababu nilizokwishaeleza hapo juu.
Kwa kawaida katika chumba cha mtihani wa taifa kama kuna mtahiniwa ambaye hayupo huwa namba yake inabandikwa kwenye dawati lake na kubaki wazi na wakaguzi wanapokutana na nafasi iliyo wazi ni lazima waite mwalimu mkuu kupata maelekezo.
Kwa hili la Matosa,madawati ya wanafunzi hao yameondolewa lakini katika karatasi zile za kusaini kila wakati wa kufanya mtihani fulani,wenzao huona majina ya wanafunzi hao na namba zao za mtihani zikiwa kwenye orodha ya watahiniwa.
Nimejaribu kuchunguza na kuuliza huku na kule kuona kama kuna mabadiliko yoyote katika taratibu za kufanya mitihani ya taifa siku hizi lakini sijaona,na hivyo kuhitimisha kuwa hili la Matosa ni la kipekee.
Kwingineko hata wale wanafunzi watoro wazazi wao waliandikiwa barua kuhimiza mtoto aende akafanye mtihani kwa vile ni haki yake na serikali imeingia gharama kuhakikisha kila mwanafunzi anaexercise haki yake hiyo,sasa hili la Matosa limeanzia wapi na lini na kwanini dk za mwisho kabisa tena kwa wanafunzi wenye mahudhurio darasani?
Kwanini hawakupewa namba zao za mtihani wafanye mitihani wakati namba hizo zinaonekana kwenye list toka wizarani?
Nakuwa suspicious hapo kwa kweli.
Naomba wizara itume wakaguzi kwenda Matosa kujiridhisha na kilichotokea kabla mitihani hii haijaisha.
Jf ifikisheni hii taarifa panapohusika haraka kama mlivyoahidi kwenye bandiko hapo juu.
Invisible
 
Na pia naomba serikali ifuatilie kwa umakini namna zoezi zima la usimamizi wa mitihani ya mwaka huu lilivyofanyika,na hasa kuhakikisha kuwa waliofanya mitihani hiyo kweli ni wale waliosajiliwa kuifanya,katika vituo walivyopangiwa.
Hii habari ya uhakiki wa vyeti katika awamu hii inalazimisha pia serikali kuwa makini katika usimamizi wa mitihani ya taifa hasa ya form iv maana sote tunajua figisu nyingi za wale wapenda njia za mkato hufanyika hapo.
 
Ili rais Magufuli awe mtendahaki wa ukweli inampasa afukue makaburi yote. Kwa mwelekeo inaoonekana vita dhidi ya ufisadi inayoendeshwa na rais Magufuli ni kwa watumishi wa umma, wapinzani na wafanyabiashara. Huo ndio mwelekeo wa vita ya Magufuli. Zaidi ya hapo mengine yote ( wizi uliofanya na wanasiasa wakubwa wa chama chake) ndiyo makaburi yasiyopaswa kufukuliwa.

Tumekuwa tukiona kelele zote za kunyang'anywa mashamba zinawahusu wakina Sumaye, Lowassa na wengine niliowataja hapo awali. Rais wangu Magufuli naomba utambue kwamba Mungu ni mtenda haki na mwenye kuipenda sana hiyo haki na anapenda kuiona ikitendekeka.

Kama Lowassa mwizi ashughulikiwe, kama Kinana shughulikia kama Kikwete nyang'anya mali za wizi mwache na kinga yake akiwa mtupu.

Naomba nikukumbushe tena kuwa Mungu ni mtenda haki. Mimi binafsi yangu nimekuwa nikikuombea lakini kama hutendi haki siamini kama maombi yetu yatafika kokote.

Rais usimuonee mtu kwa chama chake, kabila yake wala dini yake. Simama katika mkono wa haki ukatende haki. Kitendo cha kudili na wezi na kuacha mijizi kama wale wa kiwanda hewa cha Lindi unafikiri ni kutenda haki? Je unafikiri jambo hili ni jema machoni pa Mungu?

Ni bora uongoze miaka 5 ya haki kuliko miaka 10 ya dhuluma. Ukitenda haki ndipo utakapokuwa kwenye ulinzi wa Mungu hata bila kuombewa. Mungu atakuona kwani Mungu huangalia watenda haki kutoka Mbinguni tena bila kuangalia dini zao.
 
Ni kwa nini mtu anafanya kosa, anashikwa na polisi. Kwa vipindi tofauti tofauti mtu huyo, kwa kinywa chake kile kile anarudia tena makosa yale yale? Je, polisi hawana njia mbadala ya kumfanya mtu mwenye kiburi asithubutu kurudia tena ujinga wake wa siku zote? Kama polisi hawana uwezo huo, basi tuwaombe JWTZ wawe wanatusaidia kuwanyoosha watu wenye usugu wa namna hiyo.
 
Tatizo kubwa idara nyingi nchii hii hazina na haziwathamini wabunifu wa mambo mbali mbali sisi tunafata fata tuu
 
Aende amfatilie mkuu wa wilaya ya sumbawanga. Alikuwa mkurugenzi manispaa ya musoma, alikuwa fisadi ile kinoma. ana kesi zaidi ya tatu huko takukuru, sjui alichomoka chomoka vipi.
 
Wizara ya elimu hebu fuatilieni haraka kinachoendelea shule ya sekondari ya kata ya Matosa iliyoko manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam wakati huu wa mitihani ya form iv.
Kuna wanafunzi takriban 17 ambao wamezuiwa na academic master wa shule hiyo kufanya mitihani yote ya form iv kwa sababu zisizokubalika kisheria.
Sababu alizotoa ni kwamba wanafunzi hao hawajiwezi kitaaluma na hivyo hataki wafanye mtihani wa form iv.
Sijawahi kusikia kitu kama hiki,labda wana jf wenzangu mnisaidie.
Vijana hao wamesoma pale kuanzia form one,form two mtihani wa taifa walifanya na kupita,wamesoma hadi form four na mock walifanya,cha ajabu jtatu siku ya kuanza mitihani wakati wa kupangwa na kupewa namba mwalimu huyo aliwaita na kuwaeleza kuwa wao hawataruhusiwa kufanya mitihani kwa sababu nilizokwishaeleza hapo juu.
Kwa kawaida katika chumba cha mtihani wa taifa kama kuna mtahiniwa ambaye hayupo huwa namba yake inabandikwa kwenye dawati lake na kubaki wazi na wakaguzi wanapokutana na nafasi iliyo wazi ni lazima waite mwalimu mkuu kupata maelekezo.
Kwa hili la Matosa,madawati ya wanafunzi hao yameondolewa lakini katika karatasi zile za kusaini kila wakati wa kufanya mtihani fulani,wenzao huona majina ya wanafunzi hao na namba zao za mtihani zikiwa kwenye orodha ya watahiniwa.
Nimejaribu kuchunguza na kuuliza huku na kule kuona kama kuna mabadiliko yoyote katika taratibu za kufanya mitihani ya taifa siku hizi lakini sijaona,na hivyo kuhitimisha kuwa hili la Matosa ni la kipekee.
Kwingineko hata wale wanafunzi watoro wazazi wao waliandikiwa barua kuhimiza mtoto aende akafanye mtihani kwa vile ni haki yake na serikali imeingia gharama kuhakikisha kila mwanafunzi anaexercise haki yake hiyo,sasa hili la Matosa limeanzia wapi na lini na kwanini dk za mwisho kabisa tena kwa wanafunzi wenye mahudhurio darasani?
Kwanini hawakupewa namba zao za mtihani wafanye mitihani wakati namba hizo zinaonekana kwenye list toka wizarani?
Nakuwa suspicious hapo kwa kweli.
Naomba wizara itume wakaguzi kwenda Matosa kujiridhisha na kilichotokea kabla mitihani hii haijaisha.
Jf ifikisheni hii taarifa panapohusika haraka kama mlivyoahidi kwenye bandiko hapo juu.
Invisible
C wamerudishwa form3 wakakuze taaluma zao
 
Hao jamaa wanaowapa rushwa hao jamaa usiku ktk giza wana roho ngumu.Wanajuaje ni askari na si majambazi?Hawa askari watauwawa kipuuzi ktk dili za kijinga.Raia mwenye mshaka atawatungua.
 
Utaratibu wa kugawa hela zilizochangwa kwa ajili ya tetemeko la kagera uchunguzwe , sasa je serikali inaweza kujiumbua yenyewe ?
 
Mimi namuomba mh RC Makonda siku moja afiche sura yake aende Gerezani Mida ya jioni siku za kazi akate tiketi asafiri na mwendokasi toka kkoo hadi Kimara.Akifika salama ntajua RC wetu ana afya njema sana maana...
 
Back
Top Bottom