Tofauti ya rangi za binadamu: Ni nini siri yake ?

Tofauti ya rangi za binadamu: Ni nini siri yake ?

Nmeandika hii makala kujaribu kugusia aliyoyahoji Equation x katika uzi wake aliouliza swali


Vishu Mtata
mshana
Shukrani kwa tag kali.

Mkuu hilo la mazingira ya kua binadamu alianzia maeneo yetu haya naona bado kuna utata juu ya hali ya hewa ya wakati huo.

Hii East Africa ni maeneo gani yenye joto kali kiasi cha binadamu kushindwa kuhimili hadi awe mweusi tii?
Mfano hii mikoa ya pwani inayosifika kwa joto kali, zamani kidogo tu hapo miaka ya 80 unaambiwa kuna maeneo yalikua pori lenye msitu mnene lenye wanyama wa mwituni kabisa.

Vipi kwa kipindi hicho ambacho hata binadamu hana shughuli nyingi, hakati miti hovyo, hajengi, hana viwanda, si ajabu hata moto hakua anaujua, haharibu vyanzo vya maji yaani nature imetamalaki, kweli kunaweza kua na joto kali kama la sasa??

Au E.A ya Pangaea??
 
Kulingana na kitabu The Journey of man. Ancestor wa binadamu aliishi misitu ya Afrika ya kati. Alikuwa kama sokwe(akiwa mweupe na mwenye manyoya mengi kama tu sokwe wa leo. Akiishi mitini na kutembea kwa miguu minne). Msituni ni baridi hivyo alihitaji manyonya mengi ya kumkinga. Pia hakuna jua la kutosha hivyo alikuwa mweupe ili kutengeneza vitamin D za kutosha. Watu wa kale zaidi wanaaoonyesha kuwa binadamu alitoka msituni akiwa mweupe ni Wabushmen(Jamii ya kale zaidi duniani). Hawa, tofauti na Waafrika wengi wao ni weupe.

Kama miaka 200K iliyopita akatoka msituni na kuingia nyika za Afrika Mashariki(Kenya,Tz). Huko sababu ya jua kali akatengeneza melanin ili kujilinda dhidi ya hilo jua. Na sababu hakuna miti na alihitaji kuwinda nyikani akaanza kutembea kwa miguu miwili.

Baadae alipoongezeka akaanza kuhama. Njia aliyotumia kuhama ni kuambaa na pwani ya bahari. Pwani ya Tz, Kenya, Somalia, Yemen, Arabia, India, wengine wakavuka kuingia visiwa vya SEA hadi Australia. Hawa walihama zamani na ndiyo unakuta kuanzia India hadi Australia kuna watu weusi. Baadaye wengine wakapita kuelekea Ulaya na Siberia na kutengeneza rangi nyeupe(yaani polepole wenye rangi nyeusi wanakufa sababu kwenye mazingira ya baridi hawawezi tengeneza vitamin D na wale wenye weupe kidogo wanasurvive hadi mwisho wanabaki weupe watupu.) Baadaye kutoka Siberia wakashuka Tena kuingia China, Asia ya kati hadi Japan. Sababu ya kupigwa na mwanga unaoakisiwa kwenye barafu huko wakatokeza macho ya kujifinya. Ndiyo maana Wachina na Waeskimo(Inuits) wana macho ya kujifinya. Wote asili yao ni huko kaskazini kwenye barafu.

Jamii hii hii baadaye ikavuka mlango bahari wa Bering na kuingia bara la Amerika(wakati wa baridi bahari huganda mtu huweza kuvuka kwa kutembea). Huko walisambaa kutoka Amerika kaskazini hadi kusini. Ndiyo wahindi wekundu. Study za DNA zinaonyesha kuna uhusiano wa karibu sana kati ya wahindi wekundu na watu wa Asia Mashariki kama Wachina na Wajapan, ni watu wale wale walioamua kuvuka bahari kwenda Amerika.

Afrika kuna watu wa kila aina sababu ndiyo asili ya binadamu, hivyo waafrika wana vinasaba vya kutoa watu wa aina mbalimbali. Watu wenye vinasaba vichache zaidi ni wale wa asili ya Amerika.
Linaleta mashiko, story imepangika.

Kwahiyo, mabadiriko yanakadiriwa kuchukua miaka mingapi?
 
Moja vitu vigumu kuujua ukweli wake basi ni kujua asili ya dunia hii
Hakuna namna tuweza kurudi nyuma kujua nini kilitokea na kufanya haya yote

Angalau sayansi inaweza kutengeneza theories mbalimbali
Tofauti na sayansi na historia ya kale na dini kwa Ujumla hatuna majibu ya moja kwa moja ya asili ya dunia yetu
 
Kulingana na kitabu The Journey of man. Ancestor wa binadamu aliishi misitu ya Afrika ya kati. Alikuwa kama sokwe(akiwa mweupe na mwenye manyoya mengi kama tu sokwe wa leo. Akiishi mitini na kutembea kwa miguu minne). Msituni ni baridi hivyo alihitaji manyonya mengi ya kumkinga. Pia hakuna jua la kutosha hivyo alikuwa mweupe ili kutengeneza vitamin D za kutosha. Watu wa kale zaidi wanaaoonyesha kuwa binadamu alitoka msituni akiwa mweupe ni Wabushmen(Jamii ya kale zaidi duniani). Hawa, tofauti na Waafrika wengi wao ni weupe.

Kama miaka 200K iliyopita akatoka msituni na kuingia nyika za Afrika Mashariki(Kenya,Tz). Huko sababu ya jua kali akatengeneza melanin ili kujilinda dhidi ya hilo jua. Na sababu hakuna miti na alihitaji kuwinda nyikani akaanza kutembea kwa miguu miwili.

Baadae alipoongezeka akaanza kuhama. Njia aliyotumia kuhama ni kuambaa na pwani ya bahari. Pwani ya Tz, Kenya, Somalia, Yemen, Arabia, India, wengine wakavuka kuingia visiwa vya SEA hadi Australia. Hawa walihama zamani na ndiyo unakuta kuanzia India hadi Australia kuna watu weusi. Baadaye wengine wakapita kuelekea Ulaya na Siberia na kutengeneza rangi nyeupe(yaani polepole wenye rangi nyeusi wanakufa sababu kwenye mazingira ya baridi hawawezi tengeneza vitamin D na wale wenye weupe kidogo wanasurvive hadi mwisho wanabaki weupe watupu.) Baadaye kutoka Siberia wakashuka Tena kuingia China, Asia ya kati hadi Japan. Sababu ya kupigwa na mwanga unaoakisiwa kwenye barafu huko wakatokeza macho ya kujifinya. Ndiyo maana Wachina na Waeskimo(Inuits) wana macho ya kujifinya. Wote asili yao ni huko kaskazini kwenye barafu.

Jamii hii hii baadaye ikavuka mlango bahari wa Bering na kuingia bara la Amerika(wakati wa baridi bahari huganda mtu huweza kuvuka kwa kutembea). Huko walisambaa kutoka Amerika kaskazini hadi kusini. Ndiyo wahindi wekundu. Study za DNA zinaonyesha kuna uhusiano wa karibu sana kati ya wahindi wekundu na watu wa Asia Mashariki kama Wachina na Wajapan, ni watu wale wale walioamua kuvuka bahari kwenda Amerika.

Afrika kuna watu wa kila aina sababu ndiyo asili ya binadamu, hivyo waafrika wana vinasaba vya kutoa watu wa aina mbalimbali. Watu wenye vinasaba vichache zaidi ni wale wa asili ya Amerika.
naam nadhanu umekimega kwa urefu kidogo japo nayo ni dhana kama wakina sarah tishkof na kina spancer walivyojaribu kuidadavua lakini mfano kwenye mrengo wa dini hakuna anaeamini hilo
 
Back
Top Bottom