Sasa Mimi Dini yangu naiachaje..yaani tuanze kiamini jua au mwezi. Hapana.. NATAKA imani yangu kwa Mungu ikue Sana...Ni jambo naloliomba..naona kuwa naye..itafifisha imani yangu.
Pole sana Dada..ni wachache sana wanaojitambua kiimani na wakawa tayari kufanya maamuzi kwaajili ya ya imani na sio mapenzi.
Ukikuta mtu kaingia kwenye mapenzi na mtu tofauti na imani yake halafu baadaye anasema kwani Mungu si yuleyule jua huyo ni mtu hatari sana...ingawa anaweza badirika wakati fulani..probably..
Lakini endapo umempata mwenzi tofauti na imani yako na ukatumia muda kwa siri kunifunza na kujua juu ya imani yake na ukaielewa vizuri not hear say (sio perception uliyopandikizwa juu ya hiyo imani noo..but yale uliyojifunza kwa kina na kwa unyenyekevu)..utafanya2 maamuzi sahihi ..ukiamua kumfuata Unamfuata kwa kuwa una hakika bila ya shaka kuwa naenda au nimepata njia sahihi au mwanga fulani kuliko awali.
Na kwa vyovyote vile Utakuja kuipenda mno hiyo imani na kuwa muumini mzuri na mwaminifu zaidi ya uliowakuta sababu tuu umeijua hiyo imani vyema.
Ukitazama hata baadhi ya mabishano ya kiimani katika jamii zetu simply ni kwa sababu wengi hawazijui vizuri imani zao wanazoamini ingawa wao wanaamini kuwa wazijua...na pia hawajui kabisa juu ya imani ya wanayebishana naye zaidi ya kusikia kusikia na kuambiwa negativity ya hiyo imani..na vifungu au viushahidi viwili vitatu vya kuokoteza ili kuhalalisha anachokipinga dhidi ya imani nyingine.
Kama watu wengi wangekuwa na tamaduni za kujifunza imani za wengine kama njia ya kuongeza Elimu tuu...religious knowledge..Duniani tungeishi kwa upendo na kuheshimiana sana sana.
Hata kama baada ya kujifunza hizo imani kwa kina za wenzetu na kuona kuna mapungufu basi namna ya kusaidiana na kuelimishana Ingekuwa ni ya upendo mno mno wala dharau..kiburi..jeuri..majigambo visingekuwepo bali hekima na akili ingetawala na busara kuamua kwa adili kila tuzungumziapo mambo ya imani na wale tunaotofautiana nao.
Kwa sababu wengi wetu mbali ya kwamba tumejifunza sana labda mpaka tukakielewa tunachokiamini na kuwa ndio sahihi kuliko anachoamini mwingine...
Lakini ukweli unabaki pale pale..unaamini katika Dini yako kwa sababu za kijiografia tuu..ungezaliwa kule lazima ungejikuwa wewe ni muislam..au ungezaliwa kule automatically ungekuwa mkristo no matter what au umejifunza dini yako kiasi gani.
So why malumbano ya Din I????
Nakushauri uamue juu ya imani yako au yake kwa kuwa umejifunza zote mbili..nyingine kwa kuzaliwa automatically ukaijua kupitia malezi na nyingine kupitia incidence ya mahusiano au ulishaijua vyema kabla.sio kwa kusikia kupitia dini yako ilivyokufunza hapana bali uliijua wewe mwenyewe kwa kunifunza juu yake.
Muoane au msioane bado mtaheshimiana..kuliko kikwazo cha dini kikamfanya mmojawapo adharau hata imani nyingine zote kupitia malumbano yenu yaliyosababishwa na mapenzi.
Wote wawili mlikua hamzijui kabisa kabisa hizo imani zenu mnazoziamini ndio maana mliamua mkiwa na akili timamu kuwa uzinzi ndio jambo la kwanza kwenu...halafu unasema kupitia uzinzi ndipo mapenzi yakachanua mpaka kuanza kuhisi au kuamua juu ya nia ya kuishi kama wanandoa..ni ajabu sana sana.
Huu msimamo wa kiimani mlio nao ungeanza kabla hata hamjaanza mahusiano yeyote..mmeshatiana mihuri isiyofutika mioyoni na rohoni mwenu eti ndio mnashtuka leo.
Kama tunazo imani na tunaziamini kweli na tupo tayari hata kufa kwaajili4 hiyo ziwe zinatufanya tuamue mapema na kwa wakati sio baada ya dhambi..
Best wish katika safari yako ya kumpata mwenzi wa maisha...
Samahani samahani mniwie radhi kwa lecture ndefu tena isiyo na maana..
Nawaombeni radhi nyote mliokwazwa nami...