Hussein Massanza
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 1,016
- 2,195
"Tunapenda kuujulisha umma kuwa TLS inatoa mitazamo, matamko au elimu juu ya sheria kupitia account zake rasmi za kijamii na si account za wanachama wake binafsi. Hivyo chochote anachokipost mwanachama au kiongozi kupitia account binafsi hakifungamani na mtazamo wa @TanganyikaLaw"
Hiyo ni taarifa ambayo imetolewa muda mfupi na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kupitia mtandao wa Twitter.
Ifahamike kuwa taarifa hii inakuja muda mfupi baada ya uwepo wa vuguvugu la mijadala tata inayoendelea nchini ambapo Rais wa chama hicho amekuwa akitoa maoni yanayoibua maswali na wadau kuhusisha mitazamo hiyo kama ndio mtazamo wa chama anachokiongoza.
Huenda ikawa ni clarification nzuri. Lakini kwa jicho lingine, hii inatoa taswira kwamba pengine TLS haifurahii misimamo yake kadha wa kadha kiasi kwamba inaamua kujiepusha nazo.
Mjadala unaoendelea kushika kwa kasi hivi sasa ni kuhusu suala la Ushoga ambapo Rais wa TLS, Fatma Karume ameonekana kulitetea kwa nguvu zote na hata kushauri yafanyike mabadiliko ya kisheria ili ikibidi wapenzi wa jinsia moja watambuliwe.
Kwa maoni yangu: Hii ni good move ambayo TLS wameifanya. Itasaidia kuepusha mikanganyiko iliyoanza kujitokeza baina ya wasiokubaliana na mitazamo ya Rais huyo na ya wanachama wengine.
Hiyo ni taarifa ambayo imetolewa muda mfupi na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kupitia mtandao wa Twitter.
Ifahamike kuwa taarifa hii inakuja muda mfupi baada ya uwepo wa vuguvugu la mijadala tata inayoendelea nchini ambapo Rais wa chama hicho amekuwa akitoa maoni yanayoibua maswali na wadau kuhusisha mitazamo hiyo kama ndio mtazamo wa chama anachokiongoza.
Huenda ikawa ni clarification nzuri. Lakini kwa jicho lingine, hii inatoa taswira kwamba pengine TLS haifurahii misimamo yake kadha wa kadha kiasi kwamba inaamua kujiepusha nazo.
Mjadala unaoendelea kushika kwa kasi hivi sasa ni kuhusu suala la Ushoga ambapo Rais wa TLS, Fatma Karume ameonekana kulitetea kwa nguvu zote na hata kushauri yafanyike mabadiliko ya kisheria ili ikibidi wapenzi wa jinsia moja watambuliwe.
Kwa maoni yangu: Hii ni good move ambayo TLS wameifanya. Itasaidia kuepusha mikanganyiko iliyoanza kujitokeza baina ya wasiokubaliana na mitazamo ya Rais huyo na ya wanachama wengine.