Timu ya kampeni ya Dr. Magufuli yasambaratika

wamesambaratika mr pushup kageuka pusher and push watu outside his circle kwa mbwembwe zake za kijinga
 
Mtoa mada una bahati sana kwamba habari yako itakuwa ni ya kuwafurahisha wengi hapa jamvini hasa wale wanaopenda

kutukana. Kwa mfano ungeandika Lowassa njiapanda timu ya kampeni imesambaratika ungetukanwa ungeitwa mnafiki,

Magamba, msaliti, Yuda yaani kila jina. Ila angalau ubunifu wako mzuri hapa utapewa hongera na kuonekana mpenda

mabadiliko.
Na hii ndio picha kwamba wananchi wamechoshwa na watawala.
wanakula nchi wanabakiza mtaji wa kutumia kulaghai wananchi pindi uchaguzi ukikaribia.
safari hii,hizo fedha wale watafiti,sisi msimamo wetu ni mmoja tu LOWASA for presidency.
 
Hahaha Angela kairuki simuoni kwenye campaign kabaki anaambatana na lukuvi kwenye mambo ya viwanja😂😂😂😅😅
 
Nimeambiwa kuwa ile ya kampeni ya CCM iliyoundwa kwa kumsaidia Dr. Magufuli na Mama Samia imesambaratika jana usiku baada ya kikao cha kimkakati. Nimearifiwa na mmoja wa wajumbe wa timu hiyo kuwa kusambaratika kwa timu hiyo kunatokana na sababu mbalimbali. Wapo wajumbe waliosusa baada ya kuona wananchi hawaelewi somo la CCM na kuielewa Ilani. Wananchi wamekuwa hawaelewi wanachoambiwa na sasa wajumbe wanaishiwa cha kusema.

Wapo wajumbe waliosusa kwakuwa wanatuhumiana, na hata na Dr. Magufuli mwenyewe, kuwa ni popo wa kisiasa. Wanaunga mkono harakati za wapinzani kwa kificho na kumharibia Dr. Magufuli majukwaani kwa kutamka maneno ya kukwaza na kukera yanayochochea hasira za wananchi dhidi ya wagombea wa CCM wa ngazi za Urais, Ubunge na Udiwani.

Wapo wajumbe waliosusa kutokana na kutotimiziwa matakwa yao hasa ya malipo kwa kila siku wanayoifanyia kazi. Wajumbe hao wamesema kuwa hawana muda wa kusubiri kulipwa baadaye kwakuwa uchaguzi ni bahati nasibu na lolote laweza kutokea. Wanasisitiza kulipwa marupurupu yao sasa kwa mujibu wa makubaliano ya kichama na kutoahidiwa kulipwa baada ya uchaguzi.

Wapo wajumbe waliosusa kwakuwa hawapewi uzito na umaarufu kama ilivyotarajiwa. Wanamlaumu Dr. Magufuli na viongozi waandamizi chamani, kwa mfano, kumuamini sana Abdallah Bulembo ambaye hana hadhi kichama, kisera na kihela kupewa nafasi ya kutawala majukwaa kama afanyavyo sasa. Wanalalama kuwa watu maarufu wamewekwa kando na sasa wanaanza kuota utando.

Sasa timu imesambaratika. Dr. Magufuli yuko njiapanda kikampeni. Itambidi kupambana kiume ili kuendelea kujieleza mbele ya wananchi. Apambane kivyake sasa na watakaobaki naye!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Kweli mnamtumia vzur tambwe hiza
Msisahau ya kuwa tunataka mdahalo wa wagombea before Oct
 
Ni hatari sana mtu kuwa maarufu na nguvu zaidi ya chama. Sina hakika ume-type ukiwa na mihemko au ndiyo ukweli wenyewe. Ila sishangai as kwenye kampeni, JPM anajinadi yeye mwenyewe badala ya chama, hata mabango yake say all.
huo ndio ukweli,
kwanini tunaichagua ccm pamoja na hayo ni kuwa chama hiki mkutano wake mkuu ni imara kuliko mtu maarufu yeyote hata mwalimu nyerere alikuwa na kura moja tu. na hakuwa na nafasi ya kumtengeneza raisi nyumbani kwake!
rejea! chama chako cha chadema kinawatu wawili tu wenye nguvu kuliko wote, mtei na mkwewe. walimfukuza zitto, slaa na wakamuweka lowasa. bahati mbaya elimu zao na uwezo wao kisiasa ni mdogo na wapo ktk chama kisichojua na kisichoweza kusimamia misingi ya usawa na demokrasia!
nadhani jifikirie upya, kama unayowaza ni sahihi na yanatoka moyoni, fanyia utafiti mpya chama chako labda kuna kitu utaona. ila hili ni kwa wale wote wenye mioyo safi, kama ndio mabadiliko kwa maslahi ya mtu mmoja poa!
 
Walianza na matusi watamaliza kwa kutukana na kuzomewa , ukawa walianza na mungu watamaliza kwa neema na mafanikio, pimbi wao kawatia mikosi wamesambaratika
 
Kuandika habari sio kuandika tu. Lazima ujue unaandika kuhusu jambo gani na kwa wakati gani. Unatukanwa kutokana na kuandika udaku, uzushi, kashfa zisizo na ukweli na mambo kama hayo sehemu ya siasa ambayo watu wanatumia akili nyingi, muda na mali zao kujadili mambo ya maendeleo. Ni mbaya sana kufikiria kwamba wenye kupenda mageuzi ya kimaendeleo hapa Jamii Forum kazi yao ni kutukana. Kumbuka JF wengi ni Great thinkers na nina amini hivyo nikijua hata wewe ni mmoja wapo, Sasa unapoleta habari za mzaha mzaha na habari zisizo na tija yoyote katika kulisukuma kurudumu hili na maendeleo sioni ni kwanini usitukanwe. Tujifunze kukubaliana na hali tuliyo nayo japo wakati mwingine itikadi zetu zina tofautiana.
Mheshimiwa umeandika kitu cha maana sana, lakini kumbuka siyo wewe tu ambaye unayetaka mabadiliko na maendeleo

kwa ujumla, hii ni kila mtu analitaka. Lakini hapa jamvini sawa inawezekana mwenzetu hauoni hayo matusi kutokana na

upo una unashabikia upande fulani. Kuna habari nyingi tu ambazo watu wanaandika ukweli kabisa kuhusu madudu let's

say ya Chadema baada ya sekunde chache huyo mtoa mada atatukanwa sana na kudhalauliwa na kuonekana hiyo habari

ya uzushi, ila ukumbuke sasa hivi watu wengi wanatumia mitandao kuandika uzushi either kwa upande wa CCM au wa

Chadema kwa manufaa yao binafsi au manufaa ya wanasiasa wanaowapenda, kwa hiyo tujitahidi kuchuja na siyo

kushabikia upande mmoja kwani mwisho wake siyo mzuri. Tanzania ni yetu sote na mabadiliko chanja ni ambayo

tunayataka.
 
Na hii ndio picha kwamba wananchi wamechoshwa na watawala.
wanakula nchi wanabakiza mtaji wa kutumia kulaghai wananchi pindi uchaguzi ukikaribia.
safari hii,hizo fedha wale watafiti,sisi msimamo wetu ni mmoja tu LOWASA for presidency.

Wananchi ningewaelewa sana kama wangekuwa wanataka mabadiliko chanya, na siyo haya tunayoyashabikia sasa.

Kulikuwa na watu ambao walianzisha UKAWA na walikuwa wana movements za ukweli na zenye maana na siyo hivi vituko

tunavyoviona sasa.
 
Kauli mbiu yenu Hapa ni kazi tu, kweli mwaka huu kazi mnayo.
Ndio sababu kutwa kucha CCM inajaribu kufanya kampeni kwa kutumia lugha chafu, na hata kupika matokeo kwa kutumia TWAWEZA na REDET.
Ukweli ni kwamba Magufuli na CCM haiuziki, watu tumewachoka, na siyo siri.
Na hizo njama zinazotumiwa kutaka kulazimisha kukubalika ndizo zinazokwenda kuwamaliza!
endeleeni kula upepo. Kuna kila dalili mmeshindwa na ukawa yenu, mikutano inajieleza
 
Wananchi ningewaelewa sana kama wangekuwa wanataka mabadiliko chanya, na siyo haya tunayoyashabikia sasa.

Kulikuwa na watu ambao walianzisha UKAWA na walikuwa wana movements za ukweli na zenye maana na siyo hivi vituko

tunavyoviona sasa.

Wanauziwa mbuzi kwenye gunia
 
Wala siyo ubunifu, ni taarifa zilizothibitishwa toka ndani ya "kamati" Na ni kweli kamati imebomoka jana usiku. Na ajabu kuna ya ghafla imeundwa ikiongozwa na naibu waziri fulani Kijana kuliko wengine.

Kuna taarifa pia huwa zinamuhusu Lowassa ambazo ni za kweli kabisa, mara nyinyi mashabiki wa Lowassa wakiona hizo

taarifa huwa wanasema si za kweli na mwisho wa siku uishia kutoa matusi na kejeli kwa mtoa mada.
 
VUTA-NKUVUTE

Umeamua kuwapunguza nguvu wapinzani wa CCM kisayansi zaidi kuliko hata Twaweza walivyofanya.

Twaweza walikatiwa fungu la kutakata. Zipo tweets za Nchemba na Makamba wakipanga mipango hiyo ili kurudisha imani ya wananchi na hata chama chao kitakapotekeleza uharamia wao wa kuiba kura ionyeshe hata watafiti walishaona hivyo. Sasa watafiti walichukua maoni hata kabla ya wagombea wa vyama hawajaanza kampeni na bado unauita utafiti. Kesho redet nao watawasilisha ngonjera zao ambazo hazitakuwa na tofauti na za hawa twaweza.
 
Back
Top Bottom