Timu ya kampeni ya Dr. Magufuli yasambaratika

Timu ya kampeni ya Dr. Magufuli yasambaratika

Bado nawashauri wana UKAWA kuna haja ya kuihoji tume watadhibiti vip upigaji kura zaidi ya mara moja kwenye vituo viwili tofauti hasa ukizingatia kura ya Uraisi inapigwa kwenye kituo chochote na matokeo kutangazwa hapo hapo kituoni. Muda wa ku reconcile waliopiga mara mbili am sure hautakuwepo
 
Halafu kesho mtu ajipendekeze kwake , ndio atamtambua.
 

Kuna habari kuwa Kamati ya Wajumbe 32 ya Kampeni ya CCM wamevurugana. Na ndiyo maana "updates" kuhusu Kampeni inavyoendelea zinatolewa na January Makamba, badala ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. Ndiyo maana pia kuwa Kinana, haionekani sana na Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Magufuli. Inonekana Mwenyekiti wa CCM, JK, amemuelekeza Makamba afanye hivyo! Baadhi ya Wajumbe wamezila. Wengine wamekemewa kwa kurusha matusi ya nguoni badala ya kujieleza kwa nini Serikali ya CCM imeshindwa hili na lile ili angalau kurejesha imani ya Wapigakura!

Kama kamati ya kampeni ya ccm inawategemea Abdalah Bulembo na January Makamba ndio wawavushe ...its shame ...

Wanasema mwigulu kakemewa au kasimamishwa baada ya pesa kuliwa ......huo utakuwa uonevu kwa kuwa kila mtu anajuwa Nani anayekula pesa ..za kampeni ya ccm
Kila mtu anajuwa Nani anapokea michango haifikishi kwenye Chama ...
 
Ni yeye mwenyewe mgombea Magufuri kaisambaratisha team yake baada ya kuwakataa baadhi yao kama Rais Makapa na Makongoro Nyerere kwa kudai wanamfukuzia au kumpunguzia wapiga kura kwa matusi yao. Wao wawili kura zao haziwezi kumpa urais
 
Ni yeye mwenyewe mgombea Magufuri kaisambaratisha team yake baada ya kuwakataa baadhi yao kama Rais Makapa na Makongoro Nyerere kwa kudai wanamfukuzia au kumpunguzia wapiga kura kwa matusi yao. Wao wawili kura zao haziwezi kumpa urais

Makongoro yupo kwenye kampeni muda huu,usijitekenye na kucheka mwenyewe
 
Uzushi mwingine bana, kama imesambaratika vipi haya mafuriko?


Umati ukiwa umefurika kumsikiliza mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli kwenye uwanja wa Karangalala,Geita mjini.
Mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Geita mjini kwenye uwanja wa Karangalala ambapo aliwaeleza wakazi wa mji huo kuwa atahakikisha viwanda vinajengwa , wacimbaji wadogo wadogo wanapata maeneo ya kuchimba, ataboresha maslahi ya wafanyakazi , kuhakikisha madawa na huduma za afya zinakuwa bora zaidi na elimu bure kuanzia shule za msingi mpaka kidato cha nne.
sasa we naye umekurupuka mtu anaongelea kamati ya watu 32,we una leta habari za hayo unayoita mafuriko!! hayo yameletwa na ile kamati nyingine ya BURUDANI LA FIESTA.
 
Bado nawashauri wana UKAWA kuna haja ya kuihoji tume watadhibiti vip upigaji kura zaidi ya mara moja kwenye vituo viwili tofauti hasa ukizingatia kura ya Uraisi inapigwa kwenye kituo chochote na matokeo kutangazwa hapo hapo kituoni. Muda wa ku reconcile waliopiga mara mbili am sure hautakuwepo

mkuu kupiga kura ni lazima jina lako liwemo kwenye orodha ya majina aliyonayo msimamiz wa uchaguz.........sasa km mtu atapiga kura mara 2 ina maana huyo atakua alijiandikisha mara 2 vinginevyo huwez kupiga kura mara 2!!
 
Uzushi mwingine bana, kama imesambaratika vipi haya mafuriko?


Umati ukiwa umefurika kumsikiliza mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli kwenye uwanja wa Karangalala,Geita mjini.
Mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Geita mjini kwenye uwanja wa Karangalala ambapo aliwaeleza wakazi wa mji huo kuwa atahakikisha viwanda vinajengwa , wacimbaji wadogo wadogo wanapata maeneo ya kuchimba, ataboresha maslahi ya wafanyakazi , kuhakikisha madawa na huduma za afya zinakuwa bora zaidi na elimu bure kuanzia shule za msingi mpaka kidato cha nne.


we wa wapi wewe?si tunaendaga kwenye fiesta. kufuli likimaliza tu kufurama na kupiga pushapu tunawekewa fiesta.
 
naweza kuliamini bandiko lako mkuu maana kama mtu anaamua kupiga push-up jukwaani ni kutafuta njia ya kujinasua!
 
Pia kwa vile ndani ya chama chake hana cheo chochote na inavyoonyesha kichama hawamtaki basi ili aendelee kujikimu napendekeza apewe cheo cha Mkurugenzi wa Tanroads kwa masharti yafuatayo
1.Aache kuomba 10℅ toka kwa makandarasi kama alivyokuwa anafanya.
2.Ajiheshimu katika ndoa na kumtunza vena Mwalimu mke wa ndoa aachane na michepuko kwani alikuwa amezidisha sana mpaka Mwl akagoma kumsapoti

Hahahahahahah
 
CCM haibeb matajiri kama unadhan pesa ndo kila kitu msubir kumuona Lowasa Ikulu
 
naweza kuliamini bandiko lako mkuu maana kama mtu anaamua kupiga push-up jukwaani ni kutafuta njia ya kujinasua!
Ni kuishiwa cha kudanganya. Mwenzie EL anatoa point kidogo kidogo watu wanamwelewa.
 
👏👏👏👏👏✌✌✌✌✌✌
 
SIRI NZITO ZA KAMPENI CCM ZAFICHUKA.


Hakuna siri ya watu wawili au zaidi, hili limethibitika ndani ya CCM baada ya mambo mazito kuibuka hivi karibuni kwenye kampeni za chama cha mapinduzi CCM.

Mnajua ni kwanini Magufuli na Samia wamebaki wapweke kwenye kampeni?
Mnajua kwanini Janauary Makamba anahangaika kuleta propaganda kwa kasi kubwa kuliko wana CCM wengine?

Najua wengi hatujui ni kwanini? Lakini kupitia mmoja wa wajumbe wa kamati ya kampeni ndani ya CCM ukweli umejulikan, umewekwa wazi.

Mh Mwigulu, Mh Mkapa,na viongozi wengine mashuhuri wa CCM wamemsusia Mgombea urais kupitia CCM Dr John Pombe Magufuli kwasababu nyingi sana, mojawapo ya sababu hizo ni kwamba mgombea huyo hashauriki kabisa, habebeki ,anasema John Pombe magufuli anaona yeye anajua kila kitu zaidi ya wenye chama, pia ameonekana kuwa hakipaishi chama hata kidogo zaidi ameamua kujipaisha yeye peke yake.

Hali hii imewapelekea viongozi hawa kususia kabisa kampeni za mgombea urais huyo, lakinj pia mnyetishaji wetu kasema kuwa Mkapa toka alipozomewa Kagera kutokana na kauli yake ya kuwadharau wa Tz Basi kaamua kukaa mbali kabisa ili kulinga heshima yake kwa mataifa ya nje.

Lakini pia inasemekana kuwa mgombea uraisi huyo kawagomea baadhi ya waliotakiwa kuwa naye kwenye kampeni kwa sababu zake binafsi ambazo hazijawekwa wazi lakini mnyetishaji huyo alisema pia tabia za baadhi yao kutumia lugha chafu kwenye mkutano ni kikwazo kikubwa kwa mgombea huyo.

Lakini pia mnyetishaji wetu katueleza kuwa hadi sasa wapo hovyo kifedha japo inasemekana kuwa walichukua 40% ya bajeti kila wizara ili kusaidia kampeni. Amedai kuwa wameishiwa fedha kutokana na matumizi mabovu ya fedha hizo. Inasemekana kuwa kuna wengine wanaiba fedha za kampeni na kufanyia mambo yao na kumpa wakati mgumu mgombea wa ccm na msaidizi wake katika kufanikisha adhima yao.

Alidai kuwa mmoja wa wana team ya kampeni anayeungwa mkono na katibu wa CCM na Familia ya Jk kwa nguvu zote amekuwa akizitumia pesa nje ya makubaliano ya team hii imetokana na lengo lake la kujiimarisha yeye kisiasa.Na hii ndio sababu kuu za mmoja huyo kutumia nguvu kubwa kwenye kampeni hizi kupitia media na mitandao ya kijamii.

Mnyetishaji huyo alimtaja January Makamba kuwa anatengeneza mazingira ya kuwa waziri Mkuu endapo Magufuli atashinda na pia mazingira ya urais 2025,ametajwa kuwa mmoja wa wanaotengeza genge dogo ndani ya chama hicho.

Anatumia pesa nyingi kwenye wizara yake kwa ajili ya kuhakikisha umma unapotoshwa, kama alivyofanya kupitia kwa watafiti kama vile Taasisi ya Twaweza na nyinginezo na wasanii mbalimbali.

Hali hii mbaya imemfanya mkuu wa kaya kukimbilia nchi za nje.
Katika mazingira haya ya utata ambapo hadi sasa Mgombea urais amekuwa akiongozana na Bulembo ambaye ameonekana pia kuvuruga kampeni kwa kufanya siasa za 1995 kipindi hiki cha watu wenye uelewa, anapelekea kuzomewa kwa mikutano yao.

Mtoa taarifa kasema hali imakua mbaya kila siku, hali inayomkatisha tamaa Magufuli, alisema hali hii ikiendelea kuna uwezekano mkubwa sana Dr. JOHN POMBE MAGUFULI anaweza kujiengua na kusubili huruma ya Lowassa ateuliwe tu kuwa Waziri Mkuu au waziri wa wizara aliyopo hadi sasa.

Nitaendelea kuwapa taarifa kadri nitakavyozipata toka kwa mmoja wa waliopo kwenye team ya kampeni za magufuli.
 
Back
Top Bottom