TICTS yamuondoa Dr. Mwakyembe uchukuzi!

TICTS yamuondoa Dr. Mwakyembe uchukuzi!

BONGOLALA

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2009
Posts
16,511
Reaction score
11,913
Kitendo cha Mwakyembe kumtishia mkurugenzi wa TICTS juu ya utozaji exchange rate tofauti na ya BOT,inaonekana ameingilia maslahi ya kigogo kwani mnakumbuka TICTS iliongezewa mkataba wa miaka 25 kimya kimya.Karamagi pale ni boya tu.
 
Sitta kapelekwa pale kukusanya za uchaguzi. Si unajua kwa sasa bandari ndo ng'ombe wa maziwa ameshalishwa vema na Mwakyembe. CCM wanaogopa wakimwacha Mwakyembe atakataa kukamua bandari kwa ajili ya uchaguzi. Chama hakina pesa jamani kwa sasa. Kingine ndo hicho cha kigogo wetu baba mwenye house alosema Bongolala
 
Tehe....tehe...tehe...! Nnji hii bwana! Kumbe kuna dili za vigogo huko? Kwahiyo Sita ni nduhu taabu watu watakula kwa raha mustarehe.!
 
...sisiem wakikupa uongozi, kwanza unatakiwa kujua kwamba unatakiwa kulinda njia zao wanazotumia vigogo kujiingizia kipato kisicho halali; uwe tayari kulinda ufisadi wao; husiguse njia za kupitisha magendo, kama vile madawa ya kulevya, nk!
 
Mwakye amefanya kaz kubwa kwenye wizara hiyo Ikitokea chama chake kikishinda uchaguzi rais ajaye ampe uwaziri mkuu kabisa asimamie wizara zote.

...ni kweli mkuu'
Mwakyemba ni mchapakazi, pamoja na Magufuli' ndiyo mawaziri waliofanya vizuri zaidi kwenye awamu ya JK.
 
Kweli Ccm imechoka yaani sura zile zile toka enzi za Mwinyi na awajawahi kufanya wonders et bado wanateuliwa.ebu anayejua Wassira amewahi fanya nini aniambie.Mama Nagu jamani Viwanda na biashara ni wa China kwa kwenda mbele TIC mna hongwa tu.
 
Jamaa alikuwa vizuri sana kiutendaji kwani ni muda usiozidi wiki mbili tu zilizopita aliweza kuzuia dili za watu TRL kwa wale wanao husika na ukaguzi wa tiketi ndani ya treni. Hili ni mara baada ya jamaa kuwa na mtandao wa tiketi feki waliokuwa wanawakatia watu waliopanda bila ya kuwa na tiketi.
 
Mmmh TZ ni zaidi ya tuijuavyo, si dhani kama washauri wa raisi wanamsaidia kwa dhati, sijui ilifaa vipi kwa kipindi hichi kifupi kufikia ukomo wa bunge na baraza la mawaziri kuwabadili Mwakyembe na Sitta, je, kuna tija gani? Hapana, haisaidii kabisa, kilichotakiwa.ni kuziba mapengo yalowazi bila kuwagusa wengine, labda tuu kuwapandisha manaibu na kuwapa wengine nafasi hizo, ila tunapiga marktime sana, siasa zinapotosha utendaji halisi wa watu
 
Hiki kilichofanyika ndo kilichoyauwa mashirika ya uma tz,
 
Vigogo wote wa bandari watakuwa wamefurahi sana kuwa mnoko wao hayupo sasa...naona sasa hivi ni zamu ya wanyamwezi kufurika hapo bandari au siyo?
 
Bandari,TRL navyo kuvifuata ATC kufa kama TTCL walivyofilisika.Sitta hajafanya chochote EAC
 
Mpaka sasa waziri bora bado ni mwakyembe!! Magufuli hagusi kwa mwakyembe
 
Mmmh TZ ni zaidi ya tuijuavyo, si dhani kama washauri wa raisi wanamsaidia kwa dhati, sijui ilifaa vipi kwa kipindi hichi kifupi kufikia ukomo wa bunge na baraza la mawaziri kuwabadili Mwakyembe na Sitta, je, kuna tija gani? Hapana, haisaidii kabisa, kilichotakiwa.ni kuziba mapengo yalowazi bila kuwagusa wengine, labda tuu kuwapandisha manaibu na kuwapa wengine nafasi hizo, ila tunapiga marktime sana, siasa zinapotosha utendaji halisi wa watu
Kwani nchi inaongozwa na rais au inaongozwa na washauri!?
Basi tubadilishe mfumo wa uchaguzi na badala yake tuchague washauri then wao wajichagulie rais badala ya mfumo wa sasa ambapo tunamchagua rais alafu naye anajichagulia washauri!
Hii itatupunguzia muda na gharama tunazopoteza/tulizopoteza kufanya tuliyoyafanya!

 
Ni kama wakati ule alipomtoa magufuli miundo na kumpeleka uvuvi!jamaa akawasha moto akamrudisha!sasa hii ya jana ni mshangao mwingine...kumtoa mwakyembe uchukuzi??!!!
 
Back
Top Bottom