This man is either a sadist or alimuua kibaka, akanywa bia kusherehekea?

Hawa ni watu ambao watakapoondolewa madarakani na kutupwa nje.. wataanza kuelezea kuwa "walipotea tu". Labda anafikiri kwa vile ni Mkuu wa Mkoa basi yuko juu ya sheria. Sasa polisi na mahakama zina kazi gani? Lengo zima la kuwa na sheria na vyombo vya dola ni kwa sababu jamii imeendelea na haitaki kila mtu kuwa mshtaki, jaji na mnyongaji! Huyu ni kiongozi mbovu. Ila asipoangalia anaweza kuishia kama Ditopile.


Acha kuzuga brother. Aliyemteua huyu mkuu wa mkoa wa Mbeya ndiyo yuleyule anayemuacha mkuu wa mkoa wa Dar kuendelea kupeta ilhali akiwa na tuhuma nyingi za ufisadi. Bandiko lako linakosa kuaminika unapokuwa unatoa matamko kama haya kwa baadhi ya viongozi wa serikali huku ukifumbia macho matendo ya viongozi wengine wa serikali.
 
Nchi za wenzetu huyu asingekua uraiani sasa hivi. Katoa ma ushahidi dhidi yake mwenyewe!

Kiukweli huyu si kiongozi ni mtawala anaona kuua ni sifa. Kuua ni sifa ya wanaotawala kiimla.

Kiongozi angetumia nafasi hiyo kujua nini kinafanya watu au vijana wawe vibaka. Tatizo ni nini na litatuliwe vipi na hiyo hadhira ingetoa mawazo na iwataje vibaka, akutane nao ajadiliane nao na kuwapa mawazo mbadala ili waache kuwa vibaka.

Kama hii nchi inatawaliwa na sheria, basi sheria ifuate mkondo wake.

Akijitetea alikua akichangamsha genge, basi avuliwe madaraka kwa sababu si mkweli, anatunga mambo na
kuyawasilisha mbele ya hadhara.
 
Ogopa katibu wako wa chama anongea kuhusu ukichaa wako hata masaa 24 hayajaisha unatoa kauli tata ujasiri unatoka wapi?

Huo sio ujasiri bali ni ujinga, mjinga ni yule anaefanya jambo bila kujua kama ni zuri au baya. Mjinga anafanya au kusema chochote, popote, muda wowote bila kufikiria au kujali athari ya matendo au maneno yake.
 
Wanabodi,
Siamini ninachokisikia hapa kwa kiongozi huyu!.



Japo wote tunamasikio inawezekana sio wote tunaweza kusikiliza kitu tukasikia, hivyo kwa faida ya wengine naomba kusema kwa kifupi tuu mimi nilichosikia na kilicho nifanya nipandishe bandiko hili.

Kiongozi huyu anasema kibaka akiingia kwako hata kama ni kuiba chumvi, anakuwa ameomba mambo matatu.
1. Ameamua kuiba
2. Ameamua kuua
3. Ameamua kuuwawa

Amewaambia polisi wa mkoa wake kuwa kufuatia magereza kufurika, wayajibu maombi ya vibaka wote mkoani kwake kwa kuwapatia ombi lao la tatu yaani wauwawe!.

Kubwa kuliko ni akajitolea mfano yeye mwenyewe jinsi alivyomuua kibaka aliyevamia nyumbani kwake kwa kumpiga risasi mbili na kufa papo hapo, na yeye ili kukamilisha furaha yake kwa kufungua bia moja kunywa kwa kujipongeza!.

Kwa watu wanaojua kitu kinachoitwa psychoanalysis ya binaadamu, unaweza kumbaini a person of unsound mind kwa jinsi anavyoongea.

Kwa jinsi mtu huyu alivyoongelea hili tukio la kumuua kibaka na Kusherehekea kwa kunywa bia, I seriously doubt the soundness of his mind, this is a sadist!.

Naombeni sana msi question mamlaka yake ya uteuzi huwa inawaokota wapi watu kama hawa, kwa sababu huwa hakuna kipimo cha soundness of state of mind kabla ya uteuzi hi nina amini kabisa alipoteuliwa, mteua hakujua state of mind ya mteuliwa huyu!.

Kwa vile state of mind is not static, ni dynamic, inawezekana kabisa wakati anateuliwa he was OK, akaja kubadilika mbele ya safari, kama hata baada ya kuyasema haya ataachwa aendelee, huu utakuwa ndio uthibitisho kuwa hali hii inafahamika vyema, hivyo mwacheni apige kazi.

Kitu nitakachowaomba wana jf wenzangu mfuatilie, ni kitu kinachoitwa Karma kinavyoshughulikia watu kama hawa, hivyo bandiko hili liwekeni pending kwenye kumbukumbu zenu, ili siku karma itakapo anza ku hit back, tutakumbushana.

P
P, fanya mambo yako mengine achana na hayo. Utaulizwa maana ya Mayala law Kisukuma. Ccm wote wapo juu ya sheria, iko wazi. Kuna mtu alimpiga mtu risasi kanisani. Maisha yanaendelea.
 
Wewe mleta mada wewe! Kwahiyo umeshahitimisha kuwa ni kosa la hali ya akili ya mteuliwa na si kosa la aliyemteua. Unafikaje kwenye hitimisho hilo? Je, aliyemteua alitathmini hata kidogo tu kiwango cha uelewa cha aliyemteua? Au ndo ule uandishi wa style ya kung'ata na kupuliza ili angalau na wewe ukumbukwe kwenye teuzi?
 
Wanabodi,
Siamini ninachokisikia hapa kwa kiongozi huyu!.



Japo wote tunamasikio inawezekana sio wote tunaweza kusikiliza kitu tukasikia, hivyo kwa faida ya wengine naomba kusema kwa kifupi tuu mimi nilichosikia na kilicho nifanya nipandishe bandiko hili.

Kiongozi huyu anasema kibaka akiingia kwako hata kama ni kuiba chumvi, anakuwa ameomba mambo matatu.
1. Ameamua kuiba
2. Ameamua kuua
3. Ameamua kuuwawa

Amewaambia polisi wa mkoa wake kuwa kufuatia magereza kufurika, wayajibu maombi ya vibaka wote mkoani kwake kwa kuwapatia ombi lao la tatu yaani wauwawe!.

Kubwa kuliko ni akajitolea mfano yeye mwenyewe jinsi alivyomuua kibaka aliyevamia nyumbani kwake kwa kumpiga risasi mbili na kufa papo hapo, na yeye ili kukamilisha furaha yake kwa kufungua bia moja kunywa kwa kujipongeza!.

Kwa watu wanaojua kitu kinachoitwa psychoanalysis ya binaadamu, unaweza kumbaini a person of unsound mind kwa jinsi anavyoongea.

Kwa jinsi mtu huyu alivyoongelea hili tukio la kumuua kibaka na Kusherehekea kwa kunywa bia, I seriously doubt the soundness of his mind, this is a sadist!.

Naombeni sana msi question mamlaka yake ya uteuzi huwa inawaokota wapi watu kama hawa, kwa sababu huwa hakuna kipimo cha soundness of state of mind kabla ya uteuzi hi nina amini kabisa alipoteuliwa, mteua hakujua state of mind ya mteuliwa huyu!.

Kwa vile state of mind is not static, ni dynamic, inawezekana kabisa wakati anateuliwa he was OK, akaja kubadilika mbele ya safari, kama hata baada ya kuyasema haya ataachwa aendelee, huu utakuwa ndio uthibitisho kuwa hali hii inafahamika vyema, hivyo mwacheni apige kazi.

Kitu nitakachowaomba wana jf wenzangu mfuatilie, ni kitu kinachoitwa Karma kinavyoshughulikia watu kama hawa, hivyo bandiko hili liwekeni pending kwenye kumbukumbu zenu, ili siku karma itakapo anza ku hit back, tutakumbushana.

P

Pascal, my friend, LIKE FATHER LIKE SON! Ile kauli ya "mnajua msaliti huwa anafanywa nini" ya baba yao ina madhara makubwa! Kupotea kwa akina Ben, Azory, sandarusi za maiti ufukweni bila kuchunguzwa na sababu za ajabu ajabu zlizotolewa na polisi wakati ule, they sent a go-ahead msg to those pretending to be "loyal" to the father! and hence such matamshi! Wanasema maovu na kutenda hawakemewi/kuadhibiwa, wonderful enough kinachofuata ni kupandishwa vyeo, what do you expect from others! UKWELI UNAUJUA WA CHANZO CHA MAOVU HAYA!
 
Ukiona umemuoa mwanamke mlevi kupindukia ujue wewe pia ni mlevi. Bila ChengA aliyemteua ndio chanzo cha vichaa kama hawa. Tuseme tu kazi ya punguani lazima upunguani udhirike kwa watu wote.


Na haya ndio matokea ya viongozi ambao hawatokani na sie wenyewe
 
Hawa ni watu ambao watakapoondolewa madarakani na kutupwa nje.. wataanza kuelezea kuwa "walipotea tu". Labda anafikiri kwa vile ni Mkuu wa Mkoa basi yuko juu ya sheria. Sasa polisi na mahakama zina kazi gani? Lengo zima la kuwa na sheria na vyombo vya dola ni kwa sababu jamii imeendelea na haitaki kila mtu kuwa mshtaki, jaji na mnyongaji! Huyu ni kiongozi mbovu. Ila asipoangalia anaweza kuishia kama Ditopile.

Chini ya awamu hii, kiongozi kuwa katili ni sifa ya utendaji madhubuti. Na hii ni sifa toka viongozi wa juu kabisa kushuka chini. Fuatilia vizuri utabaini hilo.
 
Pascali wala usishangae na ukishangaaa zaidi utakuta kawa waziri ttzo lipo ktk ngazi ya uteuzi wew mpka katibu mkuuu kaongea mteuzi kimya muda haujaisha karudia kuharibu hawa si ndo wale hawafati sheria wanatuma watu kuandamana kudai ndege .shame on them hakuna wa afadhali na Paco unakujua sema unaogopa mataja anayewapa kiburi u najua vikao vya ndani huwa anawaaambia nn ? Simlaumu rc
 
Back
Top Bottom