This is too much! Unyanyasaji huu wa kituo cha Polisi Murieti

Ntu

JF-Expert Member
Sep 9, 2011
951
552
Ndugu wanajamvi, naomba niende moja kwa moja kwenye mada.

Mida ya saa 10 jioni hii katika eneo la Uswahilini hapa Arusha (Mjini), maaskari wa kituo cha Murieti wamemkamata mke wangu nakumpeleka kituoni kisa nyumba tunayoishi haina matundu yakutosha ya vyoo.

Ukweli uliopo:
1. Nyumba hii huyu mmiliki mpya ameinunua kama miezi 2 iliyopita na katika muda huu mchache katuunganishia maji safi na kafanya utaratibu wote na hivi sasa tunasuburi kuunganishwa kwenye bomba la maji taka. Nyumba hii tayari AUWSA wameshaweka alama kwamba wakati wowote wataiunganisha kwenye mfumo wa maji taka.

2. Mke wangu kakabidhiwa kukusanya kodi ya mwenye nyumba hapa tunayoishi, na siye mmiliki. Mmiliki haishi na sisi. Na hatujui anapoishi. Mke wangu kampigia simu kasema yupo safarini.

3.Kuna matundu 2, ila moja mmiliki mpya kaambiwa asubiri mpaka idara ya maji wakianza kuunganisha mfumo wa maji taka basi watampa maelekezo jinsi yakuiunganisha na mfumo wao.

4. Tangu niishi kwenye hii nyumba, ambapo ni takribani mwaka wa 4 huu, hatujawahi kufwatwa kwa jambo kama hili, ukizingatia kwamba huyu mmiliki mpya huwa ananyonya mara kwa mara choo kikijaa katika nyumba hii. Na leo walivyokuja hawakukuta uharibifu wowote wakimazingira.

Naombeni msaada wenu ndugu zanguni. Nifanyeje???
 
Kwan kwenye Hiyo nyumba mpo wangap hapo had muwe na matundu zaid ya moja ya chooo pia police s jukumu lao la kukagua nyumba zna matundu mangap ya vyoo kwa Tanzania yetu hiii nakushaur toa pesa dhamin mke wako
 
Inaonekana polisi wana shida na mwenye nyumba na nyinyi mmeshindwa kuthibitisha kuwa sio wenye nyumba kwa kuleta taarifa za mwenye nyumba mnayemkusanyia kodi.

Tafuta namna upate dhamana. Gharama unazoingia mhamishie mwenye nyumba wakati unamkusanyia kodi.
 
Inaonekana polisi wana shida na mwenye nyumba na nyinyi mmeshindwa kuthibitisha kuwa sio wenye nyumba kwa kuleta taarifa za mwenye nyumba mnayemkusanyia kodi.

Tafuta namna upate dhamana. Gharama unazoingia mhamishie mwenye nyumba wakati unamkusanyia kodi.
Hajui kuwa sikukuu imekaribia
 
Imekuwaje polisi waingilie suala la maji taka mbona kama Kuna kilichojificha?

Hiyo ni kazi ya afisa mtendaji wa mtaa au kata na watakupa muda wa kurekebisha tatizo na kama Kuna maji yanatiririka basi watakupigia faini.

Ila kama imeshindikana utapelekwa baraza la kata na ukishindikana kabisa ni mahakamani moja kwa moja
 
Inaonekana polisi wana shida na mwenye nyumba na nyinyi mmeshindwa kuthibitisha kuwa sio wenye nyumba kwa kuleta taarifa za mwenye nyumba mnayemkusanyia kodi.

Tafuta namna upate dhamana. Gharama unazoingia mhamishie mwenye nyumba wakati unamkusanyia kodi.
Umenishawishi, naweza kusimama na wewe
 
Imekuwaje polisi waingilie suala la maji taka mbona kama Kuna kilichojificha?
Hiyo ni kazi ya afisa mtendaji wa mtaa au kata na watakupa muda wa kurekebisha tatizo na kama Kuna maji yanatiririka basi watakupigia faini.Ila kama imeshindikana utapelekwa baraza la kata na ukishindikana kabisa ni mahakamani moja kwa moja
Asante Kwa PM Mkuu.

Mimi mwenyewe sielewi sababu ni nini mkuu wangu. Hakuna maji yaliyotiririka wala choo hakijajaa mkuu. Isitoshe huyu mmiliki mpya katuunganisha kwenye maji taka kalipia kila kitu sisi tunasubiri idara ya maji watuunganishie lakini chakushangaza mke wangu kaja kachukuliwa na kupelekwa polisi jioni hii!

Hapa nimechanganyikiwa sijui chakufanya mkuu....
 
AUYZ3t.jpg
 
Pole sana, kamwekee dhamana shemeji atoke, akishatoka mambo mengine yatajipa.
 
Inaonekana polisi wana shida na mwenye nyumba na nyinyi mmeshindwa kuthibitisha kuwa sio wenye nyumba kwa kuleta taarifa za mwenye nyumba mnayemkusanyia kodi.

Tafuta namna upate dhamana. Gharama unazoingia mhamishie mwenye nyumba wakati unamkusanyia kodi.
Sawa mkuu....
 
Kwan kwenye Hiyo nyumba mpo wangap hapo had muwe na matundu zaid ya moja ya chooo pia police s jukumu lao la kukagua nyumba zna matundu mangap ya vyoo kwa Tanzania yetu hiii nakushaur toa pesa dhamin mke wako
Nimekupata mkuu lakini huu ni unyanyasaji kwa wanyonge kama mimi mkuu.....
 
Huo ndio unyanyasaji!!! Dhamana kwa ajili ya kosa gani mkuu???

CC @RC Mongela
Mkuu wa Wilaya Arusha
Meya wa Arusha
GEORGE BONIFACE SIMBACHAWENE
Wewe toa hela tu yaishe....tena siku nyingine wakianza kuleta zao usikubali muende kituoni....mimi nilishafanya kiburi mambo ya haki zangu nilipigwa na kukaa ndani siku 5 na bado ndugu na jamaa wa karibu walitoa hela ili nitoke...hao jamaa ni wanyama wanaovaa sare na kutembea kwa miguu miwili
 
Wewe toa hela tu yaishe....tena siku nyingine wakianza kuleta zao usikubali muende kituoni....mimi nilishafanya kiburi mambo ya haki zangu nilipigwa na kukaa ndani siku 5 na bado ndugu na jamaa wa karibu walitoa hela ili nitoke...hao jamaa ni wanyama wanaovaa sare na kutembea kwa miguu miwili
Pesa ntatoa mkuu ila NTAWASHTAKIA KWA MUNGU......
 
Back
Top Bottom