Nikushauri tu Mkuu, wake za watu wanakupotezea muda wako wa kuwa na mkeo, sijui kama una hata mchumba, hapo ulipofika kwa umri ndiyo haswaa unatakiwa kuwa namke na kuanza kujenga familia yako.
Inaonekana baraka yako iko kwenye ndoa hivyo, unavyochelewa kuoa ndivyo unavyopoteza, unachezewa boya na uovu ili uendele kushughurika na wake za watu wakati kibarua cha ndoa yako kinaharibika, nakuomba jitenge nao najua haitakuwa rahisi kwa sababu ndoa ni eneo lako la baraka shetani atakuletea ugumu mwingi kutoka, na inawezekana hata kupata mkee ikawangumu.
Kama ni kweli itakuwa hivyo, basi huo utakuwa uthibitisho kuwa ndoa ni eneo lako la baraka, hivyo itakuhitaji kutumia ujuzi wako wote kupata mke sahihi kwa maisha yako. kwa maana nyingine utahitaji sana kumshirikisha Mungu kuvuka hapo.
Usiogope yote yanawezekana kwake aaminye, piga chini hao waovu haraka kwa kuwaambia sio kwa siri, na waambie unaoa na hautaki kuchanganya mambo. Ukipata ugumu kuacha omba toba kwa Mungu kisha omba mara kwa mara na utatoka.