Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
asante kutukumbusha; nadhani kuna mambo mazuri ambayo wenye akili timamu watayakumbuka!
Imechukua zaidi ya wiki tatu kuwasha mtambo mmoja tu wa megawati 10 wa IPTL na kwa usumbufu na gharama kubwa. Sasa kama haya yanayosemwa ni kweli, ndani ya dakika tano tu, megawati 100 za Dowans zingekuwa zimeingia kwenye grid ya taifa, kwa gharama nafuu na mgawao ungetoweka kabisa.
Hivi kweli nchi hii inaviongozi thabiti?
Kwani tatizo ni mitambo? Tatizo ni kuwa tukiwalipa hata senti moja tutakuwa tumehalalisha biashara na kampuni ya kitapeli. Wanachodaiana JK, RA na Brigedia watafute njia nyingine ya kulipana. Kama serikali inajali wananchi basi iitaifishe mitambo hiyo mara moja.
Imechukua zaidi ya wiki tatu kuwasha mtambo mmoja tu wa megawati 10 wa IPTL na kwa usumbufu na gharama kubwa. Sasa kama haya yanayosemwa ni kweli, ndani ya dakika tano tu, megawati 100 za Dowans zingekuwa zimeingia kwenye grid ya taifa, kwa gharama nafuu na mgawao ungetoweka kabisa.
Hivi kweli nchi hii inaviongozi thabiti?
Teh teh teh teh teh zao la ufisadi wewe!
Hatudanganyiki ng'o!!Mitambo yetu bado ni mizima na ikiwashwa tu ndani ya dakika tano inazalisha umeme wa MW 100," alitamba Munai.
Ifike kipindi mjadala kuhusu Dowans ufungwe na tusonge mbele.Tunashindwa kufikiria other viable options,huku tukiendelea kuililia Dowans.Its jus another nu brand day,but old same bulsh!T.Damn.
Teh teh teh teh teh zao la ufisadi wewe!
Nadhani mna miss the point. Mjadala huu hauwezi kufungwa kwa sababu kila siku yanajitokeza mambo mapya ambayo hapo awali tulikuwa hatuyajui. Mimi binafsi, kwa mfano, kwanza sikujua kuwa itachukuwa wiki tatu kuwasha mtambo wa megawati 10 wa IPTL. All along I thought that it will take not more than a week kuwasha mitambo yote ya megawati 100. Pili nilikuwa sikujua kuwa kuiwasha mitambo ya Dowans itachukua si zaidi ya siku moja au mbili kupata megawati zote 100. Sasa jambo kama hili lenye maslahi makubwa kwa nchi haliwezi kupita hivi hivi kimya kimya bila kuliweka jamvini. Sasa kosa langu hapa liko wapi?
Tataizo nililonalo mimi si kwamba nasukumwa na ufisadi bali mimi ndie hasa napingana na ufisadi kwa kuonea uchungu ufujaji wa mali za umma.
Kwa kweli mimi nashindwa kuwaelewa. Inakuwaje viongozi wa nchi wanaamua kutekeleza maamuzi ambayo yanaigharimu nchi zaidi ya mara kumi wakati suluhisho la wepesi na gharama nafuu lipo? Ikiwa mimi ninayetetea maslahi ya nchi naitwa fisadi jee ninyi mnao tetea ubadhirifu mtaitwaje?
Ulijua lini na wapi kuwa kuiwasha mitambo ya dowans kutakuchukua dk 5 tu?
Ukweli ni kuwa nimejua leo hii baada ya kusoma habari hizo kwenye Tanzania Daima.
Huwezi kupingana ufisadi A kwa kutetea ufisadi B. Yaani unataka kureplace ufisadi A (IPTL) na ufisadi B (Dowans)
Sawa. IPTL yenyewe ina ufisadi ndani yake. Kwa hiyo ukichukuwa Dowans au IPTL bado umo humo humo kwenye ufisadi. Similarly mikataba mingi iliyoingiwa nchini ni ya kifisadi. Huwezi kukwepa hilo. Sasa tuchukue fisadi mwenye gharama kubwa au mwenye gharama ndogo?
Maslahi ya nchi hujayaonyesha bado...
Tuache hayo mengine yote ya running costs, fast availability etc. tuchukue slahi moja tu kuwa mpaka sasa nchi bado imo katika mgao wa umeme na athari zake kwa uchumi bado zinaendelea kwa ajili ya uzembe huu tu.
Imechukua zaidi ya wiki tatu kuwasha mtambo mmoja tu wa megawati 10 wa IPTL na kwa usumbufu na gharama kubwa. Sasa kama haya yanayosemwa ni kweli, ndani ya dakika tano tu, megawati 100 za Dowans zingekuwa zimeingia kwenye grid ya taifa, kwa gharama nafuu na mgawao ungetoweka kabisa.
Hivi kweli nchi hii inaviongozi thabiti?