Things We Do For Love & Things we demand in name of Love

sun wu

JF-Expert Member
Apr 1, 2012
2,020
1,419
Wote tunajua kwamba hakuna kitu mtu hawezi kufanya “in the name of love”.., iwe kuiba, kusema uongo, kufuja pesa, kutapeli… n.k.

Hivyo basi badala ya kumwona anayetenda (kufuja mali, kuingia majaribuni, kulala njaa n.k.) ni mzembe / mpuuzi / wakuja / hana akili.., Inabidi kumuona yule anayependwa ndio anakosea kwa kutokumkataza yule anayetenda hivi vitu, (kuliko kumwambia nataka hiki ni busara kumwambia usifanye hiki, kitakufikisha pabaya)

Mfano kama unaona mwenza wako kipato hakitoshi kataa hizo zawadi na kila siku kujirusha.., badala yake mshauri mjenge au ku-invest for future.

Ukisema ahaa mimi siwezi kutapeliwa au kuwa buzi (labda hayajakukuta, ni vigumu kufahamu utafanya nini kwenye situation fulani bila kuwa kwenye hio situation). Na wewe uliyendwa usitumie mapenzi unayopewa kumkomoa anayekupenda

Kumbuka hakuna jambo mtu ambalo hawezi / hatafanya kwa anayempenda…

Hivyo basi kama unajua someone will die for you, jaribu kuepuka kutokujiweka / au ku-demand mambo ambayo yatapelekea anayekupenda kuishia pabaya
 
unaweza kuwa umejipanga wewe kama wewe kujenga mahusiano hata kwa kulala njaa
kumbuka mahusiano ni watu wawili
kumbe wewe ukiwaza kulia mwenzia anawaza kushoto
sijui kama kuna mapenzi ya kweli
 
unaweza kuwa umejipanga wewe kama wewe kujenga mahusiano hata kwa kulala njaa
kumbuka mahusiano ni watu wawili
kumbe wewe ukiwaza kulia mwenzia anawaza kushoto
sijui kama kuna mapenzi ya kweli

Wewe tokaga hapa wewe...
 
Sun tunarudi pale pale ambapo mimi na wewe twapishana….lol. The rigid of the thot itself....:embarrassed1:

Mie ninachoelewa wale ambao wanabahati ya kupendana kweli pande zote mbili (which is rare) mara nyingi hua hawafanyi vitu nje ya uwezo wao kupita mpaka kwa wapenzi wao…. WHY? Kama mtu ampenda kweli Mpenzi wake (ume mwanamke AMA mwanaume) mara nyingi wanajuana vema, in terms of kipato, uwezo, capability na the like. Na if both of them wanajua hilo then automatically kila mmoja atajaribu kumridhisha mpenzi wake kadri ya uwezo wake…. Kwa kujua fika hio kadri yake itakua appreciated na mpenziwe for tayari ajua ni to which length ameenda. Hivo basi…


Tatizo huja kama kati ya wapenzi kuna mmoja ambae deliberately anamtumia mwenzie (hasa bada ya kumchota akili ama kushika masikio in the name of love). Kwa mwanadamu kawaida… If you are capable to lead on a person kua wampenda sababu tu akupa kitu Fulani, at the end of the day it means hujali his/her welfare…. Hujali uwezo wake… Hujali kama anaweza kutwa na majanga ama matatizo. Ambacho wajali ni kua LAZIMA a deliver… atatumia njia gani? Atatoa wapi? Nani anaumia in the Process? You don’t give a damn.

Ingawa kwa kweli mtu ambae anapenda ni mpofu like no other….
 
Kusaidiana kwenye maisha ni lazima na ukiwa unapenda kweli huwezi kumshuku mwenzio kama huenda atabadilika au laa.
 
Haya mambo yapo sana tu. Na kwanza hata haijalishi kama

mkosaji ndie aliependa, sabb hata kama ukimwambia yule hafai anakuona

kama adui badala ya kwamba unamjenga. Tena basi wale ambao

hawana mapenzi ya kweli wana bahati ya kupendwa kweli.
 
Tatizo huja kama kati ya wapenzi kuna mmoja ambae deliberately anamtumia mwenzie (hasa bada ya kumchota akili ama kushika masikio in the name of love). Kwa mwanadamu kawaida… If you are capable to lead on a person kua wampenda sababu tu akupa kitu Fulani, at the end of the day it means hujali his/her welfare…. Hujali uwezo wake… Hujali kama anaweza kutwa na majanga ama matatizo. Ambacho wajali ni kua LAZIMA a deliver… atatumia njia gani? Atatoa wapi? Nani anaumia in the Process? You don't give a damn.

Ingawa kwa kweli mtu ambae anapenda ni mpofu like no other….

Ni kweli usemayo ila sometimes watu tuna-demand vitu sio sababu hatumpendi mtu (ila tamaa zinatuziba macho).., mfano ukiletewa gauni unanungunika au zawadi ya birthday unaona kama haitoshi (wakati ndio ni kweli unajua kwamba mtu anaweza ku-deliver ila kwa kutumia njia gani (kuchukua rushwa..?), na kama ana kazi nzuri je hii kazi itadumu milele au ni wakati wa kuangalia kesho vilevile.

Nadhani hapa kinachotakiwa ni kuwa wavumilivu na kufikiria kuhusu kesho, (yaani kuchumia juani ili tuweze kula kivulini), kuliko kungangania lile gari kama la jirani wakati bado mnapanga nyumba.., je gari la kawaida halitoshi kwanza mpaka mjenge ndio mnunue kama la jirani (kwahio naona hapa busara pia inatakiwa, na anayependwa ndio wa kumuongeza apendaye sababu anayependa huwa ni kipofu tayari).., :)

Kwahio nadhani kama partner anapokwenda extravagant (hata kama anao uwezo at that time) ni vizuri kumwambia Baba nanihii au mama nanihii kwanza tumalizie kabanda ketu :)
 
Haya mambo yapo sana tu. Na kwanza hata haijalishi kama

mkosaji ndie aliependa, sabb hata kama ukimwambia yule hafai anakuona

kama adui badala ya kwamba unamjenga
. Tena basi wale ambao

hawana mapenzi ya kweli wana bahati ya kupendwa kweli.

Tena usijaribu kuingilia mapenzi ya watu hata kama ni rafiki yako ukimwambia atakwenda kumwambia mpenzi wake na kesho watakuja wote wawili kukushambulia na kukuona mchawi.
 
Ni kweli usemayo ila sometimes watu tuna-demand vitu sio sababu hatumpendi mtu (ila tamaa zinatuziba macho).., mfano ukiletewa gauni unanungunika au zawadi ya birthday unaona kama haitoshi (wakati ndio ni kweli unajua kwamba mtu anaweza ku-deliver ila kwa kutumia njia gani (kuchukua rushwa..?), na kama ana kazi nzuri je hii kazi itadumu milele au ni wakati wa kuangalia kesho vilevile.


Sun take note hapa naongelea wale walopendana kweli.... Hivi wewe kama kweli mpenzi wako akupenda nawewe wampenda kwa dhati si ina maana mwajuana? Na mkijuana it means lazima utajua ni nini mpenzi wako anatamani (in the sense zawadi ambayo ni appropriate kwake iwe ya gharama kubwa ama ndogo); na hapo it means wewe kitendo cha kumpelekea zawadi tayari hio ni furaha ya kwanza (kwa mwenye shukrani na mapenzi ya kweli). Na kitendo cha kupeleka hio zawadi yeye tayari ana furaha na Amani kua mpenziwe kapeleka zawadi....

Ile tu ya kusema atanung'unika kwa kupeleka zawadi ambayo anaona ndogo kuna kua na mawili....



  1. S/He does not love you or appreciate you... Aweza akawa na feelings juu yako of need but not of Love.
  2. Mpenzi ambae ni mnunua zawadi ni bahili.... As much as you love her/him, spending money on him is another matter.


BUT Genuinely siamaini kua kama anampenda kweli na ajua uwezo wa mwenzie upo vipi, kua atalalama why zawadi ni ndogo.... Sijui labda unipe maelezo yake.
 
Nimesikia harufu ya Happuch.... Habari yako dearest? (Sun sorry huyu mdada lazima nimsalimu lol)
 
Ile tu ya kusema atanung'unika kwa kupeleka zawadi ambayo anaona ndogo kuna kua na mawili....

  1. S/He does not love you or appreciate you... Aweza akawa na feelings juu yako of need but not of Love.
  2. Mpenzi ambae ni mnunua zawadi ni bahili.... As much as you love her/him, spending money on him is another matter.


BUT Genuinely siamaini kua kama anampenda kweli na ajua uwezo wa mwenzie upo vipi, kua atalalama why zawadi ni ndogo.... Sijui labda unipe maelezo yake.

Hapo umeweka sababu mbili ila kunaweza kukawa kuna sababu nyingine:-

3. Anakupenda sana ila ni materialistic na hatosheki... yupo radhi mlale njaa lakini apate anachotaka (mchoyo)
4. Hajui ugumu wa maisha kila ukimwambia issue zimekuwa ngumu hakuamini (yupo radhi mkope ili apate atakacho) She does not think about tommorrow
5. Sababu kuna wengine / marafiki zake wanamkoga kwa vitu (wengine hata kazi zao za kawaida ni ndogo kuliko zako) anashangaa kwamba kwanini kama wale wanafanya na wanapata wewe hupati (hapa kumbuka sio kwamba anataka mpige deals ili mjenge nyumba / bali mpige deals ili aende shopping Dubai

Kwahio tutaona kwamba sometimes sio kwamba mtu hakupendi bali tamaa na umimi na kuishi kwa leo bila kuwaza kesho kunampofusha.., hajui kwamba siku ukianguka mtaanguka wote. Ukweli ni kwamba hakuna mtu ambae hapendi mazuri (ila mazuri at what cost is what is important..)
 
Nirahisi sanaa kumpenda anayekupenda, kuliko kusubiri kupendwa na unayempenda
 
Nirahisi sanaa kumpenda anayekupenda, kuliko kusubiri kupendwa na unayempenda
Kama unaweza kujifunza kupenda (ni wachache tunaoweza :) ), ni vema kutafuta anayekupenda ukajifunza kumpenda.., lakini bi bora zaidi kupata mnayependana..


Swali linakuja ..., Smile can you learn to love someone
 
Back
Top Bottom