SIMULIZI: Sumaya Fate of Love

Janie_Kelvin

Member
Jun 5, 2022
33
51
SUMAYA FATE OF LOVE

SEHEMU YA PILI



Lakini alijitahidi asioneshe hilo kwa Mama yake lakini damu ni nzito kuliko maji Zuleya aliitambua vema hali aliyonayo Sumaya nae alificha hilo mpaka atakapo pata nafasi ya kuzungumza nae kwa uzuri zaidi na hata hivyo tabia za Sumaya hazikuwa tofauti sana kama marehemu mama yake na hiyo ilikuwa rahisi sana Zuleya kutambua kwa haraka tatizo lolote alilonalo Sumaya………..


ENDELEA…………..



Ni jumapili tulivu wakiwa katika mandhari yaliyovutia sana katika fukwe ya bahari Zuleya na Sumaya huku wakiwa wameshikana mikono kila aliyewaona hakusita kusema kuwa walikuwa ni mama na mtoto kutokana na kufanana kwao mikononi walishika ice cream.Walitembea kwa hatua kadhaa ndipo walipopata sehemu nzuri na kuketi, baada ya kumaliza ice cream zao ndipo Zuleya alipoanzisha mazungumzo.

“It’s been a long time since we came here for refreshment my dearest daughter Sumaya”

(Ni kipindi kitefu tokea tuje hapa kwa kujiliwaza binti yangu mpenzi Sumaya)

Alitabasamu Zuleya huku akimtizama Sumaya kwa upendezi wa hali ya juu na kumfanya Sumaya aone aibu za kitoto kwa mama yake huyo

“Mama I have…….” (Mama nina….)

Kabla hajamaliza kuongea Zuleya alimziba mdomo na kumkumbatia

“Najua kama haupo okay Sumaya, tell me what’s your problem?”

“Mom…..why don’t I look familiar with my mom and dad?? But I look familiar with you? It’s true that you are my biological mother? And if not who are you what do you mean to me?.Why me and you are Islamic and others are Christian? Tell me why mom Zuleya” (Mama.. kwanini sifanani na mama na baba yangu?? Lakini nafanana na wewe? Ni kweli kwamba wewe ni mama yangu mzazi? Na kama sio wewe una maana gani kwangu?.Kwanini mimi na wewe ni waislamu na wengine ni wakristo? Niambie Kwanini mama Zuleya)

Swali hilo lilimshitua sana Zuleya hakutegemea kuulizwa swali kama hilo kutoka kwa mtoto huyo

“Oooh well Sumaya Mr Hernad and Mrs Hernad are your biological parents.I’m not your biological mother Sumaya but I’m your aunt as you calling me”
(Ooh vizuri Sumaya Mr Hernad na Mrs Hernad ni wazazi wako.Mimi sio mama yako mzazi Sumaya lakini ni mama yako mdogo kama unavyoniita)

“But mom Zuleya……” (Lakini mama Zuleya…..)

“Shiii!!!!!! Sumaya wachana na hayo mawazo”Alimkumbatia kwa upendo.

Baada ya kukaa kwa muda waliona ni wakati mzuri wa kurejea nyumbani, walielekea kwenye gari na kuondoka.Lakini kitu cha kushangaza baada ya kufika nyumbani walikuta mgeni nje na wote walimfahamu vizuri sana mgeni huyo, baada tu ya kushuka kwenye gari yule mgeni alimfuata Zuleya kwa hasira na kumshika mkono huku akitaka kumfokea lakini Zuleya alimtuliza na kumwambia asubiri afungue mlango waende chumbani kuliongea hilo hata hivyo kulikuwa na mtoto, ilimbidi awe mvumilivu na ndipo walipoingia chumbani lakini haukupita muda mrefu zilisikika kelele za Zuleya akilia na baada ya Sumaya kusogea jirani na mlango wa mama yake mdogo alisikia pia kelele za mtu akifoka kumfokea Zuleya.

“Where have you been Zuleya? And you didn’t pick up my phone, you just think am I crazy Zuleya?”

(ulikuwa wapi Zuleya? Na hautaki kupokea simu zangu, unadhani mimi ni kichaa Zuleya?)

“But Dajuan I didn’t do anything bad….”

(lakini Dajuan sijafanya kitu chochote kibaya..)

“Shut up Zuleya, you didn’t care about it now a days you just doing at your own……you cared much your own things”

(kelele Zuleya siku hizi haujali kuhusu hiki unafanya vitu upande wako tu….unajali sana vya vitu vyako)

“Dajuan I didn’t mean that….. I just want to spend a day with my daughter because most of the time I didn’t get a chance to be with her like today”

(Dajuan sijamaanisha hivyo…. Nilitaka kutumia siku hii na binti yangu kwa sababu mara nyingi sipati nafasi ya ya kuwa na yeye kama leo)

“Liar!!!!!!!!”(Muongo!!!!)

Alianza kumpiga Zuleya, Zuleya alilia kilio cha maumivu hata Sumaya alisikia uvumilivu ulimshinda Sumaya alianza kugonga mlango kwa hasira na hatimaye ulifunguliwa na Dajuan ndiye alitoka ndani kwa hasira Na kuelekea sebuleni kwa nia ya kutaka kuondoka lakini Sumaya alimuita kwa nyuma.

“Yow bro!!!…..” Dajuan aligeuka nyuma na kumtizama Sumaya

“How dare are you”(unathubutu vipi?)

“Simama hapo hapo.Mwanaume huna haya wewe huwa nakuangalia tu kila siku ukija hapa na unampiga na kumfokea Mama kila siku unakuja kwa shari.Sikupendi nakuchukia, nampenda sana mama Zuleya na namthamini sana kama wewe hujui thamani yake naomba umuache.Upo kwaajili ya pesa tu unachukua pesa zake na bado una mpiga”Aliongea Kipatois huku akiwa anamaanisha kile ambacho alikuwa akikisema.Hata Zuleya chumbani alisikia na kujiuliza Sumaya amepata wapi ujasiri wa kuzungumza na Dajuan hivyo wakati yeye hakuthubutu hata kutia neno alitoka chumbani na kumfuata Sumaya

“Wah gwaan Sumaya?” “Nini kinaendelea Sumaya” “please stop…….Enough!!!!”

(Tafadhali acha….. inatosha!!!!)Aliongea Zuleya akionekana mwenye wasiwasi sana kutokana na hali aliyoikuta sebuleni

“Mom please leave me, I hate this guy mom i wish i could be stronger and fight him but I don’t have such power”

(mama tafadhali niache, namchukia huyu mtu natamani ningekuwa mwenye nguvu nipigane nae lakini sina hizo nguvu)

“But he is your da….”(lakini ni ba..)

“He is not mom…. Never he can’t be my dad”

(sio mama…… kamwe hawezi kuwa baba yangu)Aliongea kwa ujasiri mpaka kila mtu alishangaa ujasiri wa Sumaya kuongea hivyo na bado alimgeukia tena Dajuan

“Dajuan siwezi kuwa na baba ambaye kila siku ana mnyanyasa mama yangu ondoka nyumbani kwetu”

“Zuleya hivi ndo umeamua si ndio Kwahiyo umemtuma mwanao anidhalilishe tena mbele yako ukishuhudia”Aliongea kwa lugha ya Patois

“Mama mwambie ukweli kuwa humtaki huyu mwanaume hakupendi anatumia pesa zako tu mwambie”naye Sumaya alimgeukia mama yake na kuongea kipatois

“Enough Sumaya!!!!!!!!! Dajuan leave my house please, right now”

( Inatosha Sumaya!!!!!! Dajuan ondoka nyumbani kwangu tafadhali, sasa hivi)

“Zuleya…..”

“I said leave Dajuan..!!”

(nimesema ondoka Dajuan)

Sumaya alielekea mlangoni na kumfungulia mlango Dajuan ambaye alitoka huku akiwaangalia kwa hasira wawili hao.

Dajuan alikuwa ni mpenzi wa muda mrefu sana wa Zuleya kwa karibia miaka minne tokea wafike nchini Jamaica ni mzawa wa Jamaica lakini alikuwa akimnyanyasa sana Zuleya kwa kumpiga na kumfokea kila alipoenda nyumbani kwa Zuleya, hakuwa na kazi ya kueleweka hivyo muda mwingi aliutumia kuvuta bangi na kunywa pombe wakati huo pesa alizokuwa akizitumia alizichukua kutoka kwa Zuleya mara nyingi alikuwa akimlazimisha ampe pesa hata nusu yote ya mshahara wa Zuleya alichukua na kwenda kufanyia starehe zake.Lakini Zuleya alimpenda sana mwanaume huyo licha ya kuchoka na manyanyasiko aliyokuwa akiyapata japo kadri muda ulivyozidi kwenda upendo kwa Dajuan ulipungua lakini bado alimpenda kwa kiasi hiko hiko ila shida ilikuwa upande wa Sumaya aliyekuwa akishuhudia manyanyaso aliyokuwa akipewa mama yake na kuamua kufanya jambo ili kumsaidia mama yake na hiyo ndio aliona njia ya pekee ya kumsaidia kwani hakuwa na nguvu za kupambana na Dajuan hata hivyo alimjengea mama yake wakati mgumu sana juu ya alichokifanya mbele yake na yeye akidhani ana saidia.

“Sumaya what have you done??”

(Sumaya umefanya nini)

“I’m tired…. Mom I’m tired and I’m not scared about him anymore.He is bullying you mama every day”(nimechoka… mama nimechoka na simuogopi tena.Anakuonea mama kila siku”

“But he didn’t deserve it Sumaya, you are young and can’t understand it just leave it as it is”( lakini hakustahili hiki Sumaya, wewe ni mdogo na huwezi kulewa hiki kiache kama kilivyo)

“He deserve it mom…. Weh yuh ah deal wid?” (Anastahili hiki mama…. Utafanya nini na hili?)

Aliongea kwa hasira na kumuacha mama yake hapo kisha naye akaenda chumbani kwake na kujitupa kitandani huku akilia.Zuleya alitambua ni kiasi gani Sumaya aliumia kutokana na jambo lililotokea muda mfupi uliopita alijifikiria na kumfuata chumbani kwake japo aongee naye labda wanaweza kuelewana.Alipofika mlangoni alikuta mlango upo wazi hivyo alichungulia na kumuona Sumaya akiwa amelala huku akilia alitaka kuingia lakini alisita kutokana na hali aliyokuwa nayo Sumaya kwa wakati huo, aliona amuache kwanza mpaka atakapo tulia na kupata chakula cha jioni ndipo waongee jambo hilo.

Hata Zuleya alipoandaa chakula Sumaya hakuthubutu kushuka chini kwaajili ya kwenda kula hata kwa upande wa Zuleya hakuweza kula bila ya kujumuika na mtoto wake hamu ya chakula iliisha kabisa na ndipo akapanda juu kuelekea chumbani kwa Sumaya na sasa alimkuta ametulia kidogo hata kuongea anaweza alisogea taratibu mpaka kitandani na kuketi pembeni ya Sumaya, aliishia kumtizama tu asipate ujasiri wa kuongea neno lolote.

“Mom…”Aliita Sumaya “I’m so……”

“Shii!!!…. Sumaya I know what have you been through, hata mimi nina huzuni sana my dear”

“Nilikuwa na hasira sana.. it’s just a temper, kutokana na kilichotokea na vyote ambavyo vinatokea.Nakupenda mama siwezi vumilia kwa yote unayopitia mama aah najua…..”

“Inatosha Sumaya najua umeumia sana mwanangu nakuahidi haitatokea tena, sipendi kukuweka katika situation kama hii”Alimkumbatia na kumfuta machozi yaliyokuwa yakitiririka katika mashavu yake.

“Pramise … mom?”

( unaniahidi mama?)

“Mi pramise yuh my daughter”

( nakuahidi binti yangu)

Walishuka chini na kujumuika pamoja kupata chakula huku Sumaya akikisifia chakula kilichopikwa na mama yake kuwa kilikuwa kitamu sana pia utani wa kawaida uliendelea wakati wakipata chakula ilikuwa ni nyumba yenye watu wawili tu lakini kulikuwa na furaha muda mwingi.

Nchi ya Jamaica ilisifika sana kwa uzuri wake wa mandhari ya kijiogragfia kama bahari na fukwe zinazovutia, milima, misitu ya kiasili, maporomoko ya maji na sehemu mbalimbali zinazovutia kwa starehe na kufurahi hivyo kuifanya Jamaica kupendeza zaidi na kujulikana kama taifa la kisiwa cha Caribbean(Caribbean island nation) kutokana na kuzungukwa na bahari ya Caribbean,Ni nchi inayojitegemea iliyopo bara la America, America ya kaskazini huku ikiwa imezungukwa na bahari ya Caribbean.Kitu kingine kikubwa kinachotambulisha Jamaica ni nchi ambayo muziki maarufu wa rege ulizaliwa na msanii maarufu aliyejulikana dunia nzima kwa kuimba muziki huo wa rege, Bob Marley alizaliwa hapo.Na pia hata mavazi ya asili ya Jamaica yalikuwa ni ya kuvutia sana hasa kwa wanawake hata hivyo walikuwa na tamaduni zao husika kama ilivyo kwa kila nchi kuwa na tamaduni kama ilivyo nchini Tanzania Kwahiyo ni kawaida kwa kila nchi kuwa na tamaduni, mila na desturi pamoja na miiko.


* * *
Nchini Tanzania ni kipindi ambacho Mr Hernad alishastafu na alikuwa na nguvu angalau za kuendesha biashara zake bila shida, ni muda ambao alikaa kwenye bustani yake ya maua akisoma kitabu cha siasa ya dunia ambacho kiliandikwa kwa lugha ya Kiingereza taratibu akishushia na kahawa yake aliyoipenda hasa Sumaya alipokuwa hai alikuwa akimtengenezea kila siku, alipenda sana maua na pia kuna kumbukumbu fulani za maisha ya nyuma kila akaapo kwenye hiyo bustani kubwa zaidi ni binti mrembo Sumaya aliyemuheshimisha na hatimaye kuitwa baba, mwanzoni wakati anaijenga nyumba yake bustani yake ilikuwa ya kawaida sana na maua machache kwani hakuwa mtu wa kupenda sana maua lakini alipomuoa Sumaya bustani ilianza kupendeza kwa kuongezwa maua mbalimbali yaliyovutia zaidi na ndipo Mr Hernad alianza kupenda maua na kuanza kuitunza bustani hiyo.

“Ni miaka kumi imepita tokea uniache Sumaya wangu, still Nakupenda sana siwezi kukusahau, siwezi kusahau huba lako Sumaya ulinifanya nijivunie kuwa mwanaume na nikaitwa baba, baba Sumaya……”Wakati akiendelea kutafakari hayo alimuona mtu akija kwake alionesha tabasamu baada ya kumuona mtu huyo na kusimama kwaajili ya kumkaribisha.

“Mr Hernad I’m so happy to meet you”

(Mr Hernad nina furaha sana kukutana na wewe)

“Aah Mr Khaleed Karibu sana” Akimkaribisha kiti ili akae

“Asante sana” Akiketi “Habari za siku rafiki yangu”

“Salama tu za hapa nyumbani, Vipi wote wazima lakini”

“Tunashukuru Mungu anasaidia Khaleed”

Mr Hernad alimuagiza mtu alete kinywaji kwaajili ya mgeni huyo wa muhimu sana, na baada ya muda mfupi kinywaji kililetwa huku kikiambatana na biskuti.Mr Khaleed alikaribishwa na kisha mjadala uliomleta ulianza.

“Kuna kitu muhimu sana Mr Hernad cha kuzungumza mimi na wewe tu na ni lazima kiwe siri”

“Mmmh kitu gani tena?”

“Hivi Gedione unaweza kuamini kuwa kuna mtu anakufuatilia na pia anataka kufuatilia nyaraka zako za muhimu sana?”

“Khaleed inawezekana vipi hiko kitu?”

“Amini usiamini ila ukweli ndio huo na inaonekana anayekufuatilia hatoki mbali na ni moja ya familia yako na pia sidhani kama yupo pekeyake kuna mtu nyuma yake”

“Hili ni jipya kabisa kwangu”

“Unajua una biashara nyingi sana na pia nyumba magari na mali nyingine za thamani, kuna yeyote umemdokeza kuhusu kuandikisha mali zote kwa mtoto wako?”

“Hapana hata Rahel sijamwambia mtu pekee ambaye nilimwambia ni mama na tayari ameshafariki lakini Rahel nimeshampa umiliki wa hii nyumba pamoja na magari mawili ila nyumba zote tatu zilizobaki na magari yote pamoja na biashara ni kwaajili ya binti yangu”

“Vizuri hilo Ndio msaada kwako usimwambie yeyote mpaka wakati sahihi utakapowadia.Unajua mimi ni mwanasheria wako na nimekuhudumu kwa muda sasa naelewa vingi Gedione”

“Lakini ni lazima tuanze kufuatilia mapema ili tujue ni nani”

“Ni kweli lakini halihitaji papara jambo hili, hata hivyo sio rahisi kufanikisha hili na hata hivyo tumeshashtukia mchezo ila hata baadhi ya mienendo na safari zako hawatakiwi kujua sana maana italeta matatizo”

“Sawa tutazidi kuwasiliana”

“Lakini Mr Hernad why Jamaica? Na sio nchi nyingine? Mbona kuna nchi ambazo wanatoa elimu kwa kiwango cha juu sana kama Marekani, Australia, Ufaransa na nchi nyingi tu”

“Aaah Khaleed unajua nimeona ni kawaida tu halafu naipenda sana Jamaica mandhari, tamaduni zao and all about that Country I don’t know why?”

“But it’s good sio mbaya kama umepapenda”

Waliagana na Mr Khaleed aliondoka lakini alimuachia mawazo sana Mr Hernad juu ya jambo hilo zito alilomueleza hata hamu ya kuendelea kukaa bustanini iliisha alichukua vitu vyako vya muhimu na kuelekea chumbani huko alimkuta mke wake ambaye alionekana akimdadisi sana na kumuuliza

“Upo Sawa kweli mume wangu? Halafu ni kama nimemuona Mr Khaleed?”

“Nipo Sawa mke wangu, ni kweli nilikuwa na Mr Khaleed kule bustanini ila ameondoka”

“Mmh mlikuwa mnaongea nini bustanini na ukashindwa hata kumkaribisha ndani mgeni mume wangu?” Aliongea huku akionekana kutopendezwa na hilo, alifikiria kwa muda na kukumbuka onyo alilopewa na Khaleed kuwa iwe siri yao na asimwambie mtu yeyote

“Aah Hakutaka kuingia ndani hata hivyo alihitaji fresh air, usiwe na wasiwasi tulikuwa tunaongea kuhusu biashara”

Alimsogelea mke wake na kumbusu kisha akajitupa kitandani mke wake alimuangalia kwa muda na kuendelea na mambo yake.

Zilipita siku chache na Mr Hernad hakuonesha wasiwasi wowote huku akiwasiliana na Mr Khaleed na kupanga mipango yao kimya kimya.Ni siku ambayo hakuweza kwenda kwenye biashara zake na kupumzika nyumbani kama kawaida akiwa kwenye bustani yake aliyoipenda sana ghafla simu yake ilianza kuita na kuangalia mpigaji kisha akaipokea na kuweka vyema sikioni.

“Hamna shida nakuja sasa hivi nipe dakika 30”

Simu ilikata na aliinuka na kuelekea chumbani ili ajiandae, mke wake alishangaa kwa sababu asubuhi alimwambia kuwa haendi kazini lakini muda huo anajiandaa ili aondoke lakini alimjibu tu kifupi kuwa kulikuwa na dharura na alihitajika haraka.

Kama alivyoomba baada ya dakika 30 alikuwa ameshawasili eneo husika ni katika Hospitali ya Aga Khan moja kwa moja alielekea katika ofisi ya Dokta Luis, baada ya salamu maongezi rasmi yalianza huku Dokta Luis akianza na samahani kwa Mr Hernad kwa kumuharibia muda wake na pia kwa atakachomwambia kwa wakati huo naye Mr Hernad aliipokea kwa moyo wote asijue ni kipi Dokta Luis alikuwa akimaanisha.

“Unajua wewe ni kaka yangu tokea tupo Australia ile siku tuliyokutana kwenye mashindano nilipopoteza wallet yangu yenye nauli na wewe pekee ukanijali na kunipatia nauli, uliacha alama kubwa sana moyoni mwangu Mr Hernad najuta kwa kushindwa kurejesha fadhila hizo”

“Unazungumzia nini Dokta Luis hayo mambo yameshapita wewe ni ndugu yangu tumeshare vitu vingi sana”

“Ni kweli Mr Hernad ila lazima nikuambie hili, miaka kumi imepita nilishindwa kumsaidia shemeji yangu wakati akiwa anajifungua na kupelekea kupoteza maisha na wakati nilikuwa nikitambua ni kiasi gani ulimpenda ni kiasi kikubwa sana kisichokuwa na mfano”

“Luis huu Sio muda wa kujilaumu ulikuwa ni mpango wa Mungu ni kweli nilimpenda sana na nitaendelea kumpenda”

“Kaka, siku ambayo Sumaya alikuja hapa kwaajili ya kujifungua haikuwa nzuri kwa upande wake”

“Una maanisha nini Dokta? Sijakuelewa vizuri”

“Ni dhahiri kuwa mkeo kuna dawa au niseme sumu kwa lugha nyingine alipewa na aliyempa alidhamiria kuwaondoa wote wawili yaani mama na mtoto wakati wa kujifungua na ndio maana aliwahi zaidi kupata uchungu kabla ya muda”

“Whaaaaaat!!!!!!!!” Alishituka

“Yeah! Lakini japo kuwa tulishindwa kuwaokoa wote ila angalau tulifanikiwa kumuokoa mtoto kuliko tungewakosa wote”

“Luis una..una…una uhakika na hili jambo?”

“Kaka I’m professional na naelewa vizuri na mimi ndiye nilishughulika na Sumaya”

“Why Luis?!! Why?!! Kwanini hukuniambia mapema kuhusu hili suala kwanini unajua ni kiasi gani nimeumia kumpoteza Sumaya? na mpaka nilianza kijihukumu mwenyewe”

“Kaka na ndio maana nimeanza na samahani najua kama nilifanya makosa miaka iliyopita lakini nataka kufuta kosa nililofanya na pia nilikuwa naangalia mbali kuhusu usalama wa mtoto unadhani kama mpango ungeenda vibaya si tungempoteza na mtoto Mr Hernad lakini pia wacha nikupongeze kwa kuchukua hatua ya kumpeleka Sumaya nje ni kama umesave maisha yake”

“Una maanisha nini Dokta Luis?”

“Hivi unadhani kama mtu yule aliweza Kufanya jaribio la kuwaondoa mama na mtoto kabla hajajifungua angeshindwa sasa kumuondoa mtoto?”

“Ni kweli kabisa Luis lakini unataka kuniambia kuwa mtu huyo atakuwa ni miongoni mwa familia yangu?”

“Wake up brother unadhani kuwa ni mtu wa nje ndiye afanye huo upuuzi?”

“Lakini mbona hakuna hata mtu aliyekuwa akionekana kuwa na chuki dhidi ya Sumaya? Hata mtoto alipozaliwa hakuna aliyeonesha chuki?”

“Kaka wake up from a nightmare sisi binadamu ni viumbe vya ajabu sana na ni hatari kuliko unavyofikiria, unajua ni kwanini mke wako mkubwa hakuja siku ambayo mke wako alikuwa akijifungua na ilikuwa muhimu afike yeye kama mwanamke?”

“Kwahiyo Unataka kusema kuwa mke wangu anahusika kwa haya yote?”

“Hapana sijamaanisha kuwa mke wako ndo ana husika lakini tumia akili brother, mimi yangu Ndio hayo nadhani sasa naweza kwenda kwenye majukumu yangu”



Mr Hernad alianza safari ya kurejea nyumbani huku akuonekana kuwa mnyonge sana na hapo akapokea taarifa kuwa mmoja Kati ya watumishi wake amefiwa na kaka yake aliyempa taarifa ni mtumishi wake ambaye alimteua kuwa kiongozi wa hiyo biashara yake.Hakuweza kuijibu kwa muda huo kwani alikuwa akiendesha gari hata hivyo hakuwa kwenye hali nzuri kutokana na taarifa alizopewa na Dokta juu ya kifo cha Sumaya kilichotokea miaka kumi iliyopita, moja kwa moja alimuwazia msaidizi wa kazi ambaye alikuwa akimuhudumia Sumaya kipindi chote cha ujauzito na hata kumlea Sumaya baada ya mama yake kufariki alimfikiria sana lakini hakuamini kama msaidizi huyo angeweza kutenda unyama kama huo, lakini hakuacha kumfikiria mkewe lakini napo akili ilikataa kabisa kuwa naye Rahel angeweza kumuua Sumaya.Aliporudi nyumbani baada ya kuulizwa na mke wake hakumwambia chochote walichozungumza na Dokta Luis badala yake alimwambia kuhusu msiba uliotokea.



ITAENDELEA………
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom