YOU KNOW YOUR TRULY EXISTENCE AND ITS TIME TO FOCUS YOUR REAL DESTINY,NA KIFIKRA UNAKUWA HURU NA HUWEZI KUWA MANIPULATED KWA KUWA UNAUJUA UKWELI.
Sent using
Jamii Forums mobile app
Uhuru gani unazungumzia kwenye mambo ya tafiti za kisayansi? Tafiti zinafanywa ili kutatua matatizo ya binadamu si vinginevyo,
wanasayansi wanaangalia uwezekano wa kutoka nje ya dunia ili kutatua tatizo la kuchakaa kwa hii sayari au kukitokea tatizo kuwe na alternative ya maisha,
Sioni kama binadamu unaozungumza nao wanakosa uhuru kwa kuamini dunia ni flat au duara.
Mmasai au mkuria huko kijijini au hata mimi raia wa kawaida nakosa vipi uhuru kwa kutokujali kuhusu umbile la dunia au kuamini ni flat au duara?
Umuhimu wako wewe mtafiti utakuja pale ambapo kukitokea hatari wewe mwanasayansi na mtafiti ukaja na suluhisho.
Raia hata ukimwambia dunia ni chungu au bakuli atakwambia sawa na ataendelea kuwa huru kabisa akifurahia zawadi ya maisha mpaka pale kutakapotokea shida ndipo wataalam, wagunduzi na wanasayansi watafuatwa kwa ajili ya utatuzi
Utlist yule aliyesema NASA hawataki watu waamini biblia juu ya uwepo wa MUNGU, maana atakaporudi kila jicho litamwona so NASA ni mpango wa shetani watu wasiamini.
Utlist huyu anasababu za kwanini asiamini dunia ni duara. Na ukimuuliza what is next labda atakuambia tufanye mahuburi watu wamrudie MUNGU waachane na wanasayansi, but hii itaingizwa kwenye imani si sayansi.
Tukirudi kwenye sayansi sioni sababu ya kwann tuamini kuwa wanasayansi ni waongo, kwanini wanasayansi watumie nguvu kukuza technology ili wakudanganye?
Si wangekunyima tu hiyo technology, Maana hao hao waliotuambia dunia ni duara, ndio hao hao waliogundua mpaka sasa tuna simu n. K.
Kama kuna siri kubwa sana ya kuficha dunia, kwanini akupe nyenzo za wewe kugundua kuwa ni waongo?
Mwisho swali la msingi linabaki pale pale, tukishaamini dunia ni flat nn kinafuata?
Tutegemee nini kutoka kwako ww mtafiti unayesema dunia ni flat?
Hata kama mategemeo ni ya chini kabisa tuambie, Maana kwa wanasayansi wanaosema ni duara, tunategemea mengi sana katika tafiti zao ikiwepo uwezekano wa miaka ya mbele kufanya utalii kwenye anga za juu au uwezekano wa kuendeleza maisha nje ya dunia itakapokuwa kwenye hatari ya kutoweka.
Kama ni waongo dunia itawahukumu tu maana wameshatupa na technology za kutunza kumbukumbu yaani internet.