The sinicization of religion (vita ya China dhidi ya dini)

Mto Songwe

JF-Expert Member
Jul 17, 2023
6,015
12,294
The Sinicization Of Religions In China

Huu ni utaratibu maalumu unaofanywa na nchi ya China kuzifanya dini zote za ng'ambo ziendane na utamaduni na mfumo mzima wa maisha wa jamii ya kichina.

Utaratibu huu umeanza karne na karne na umekuwa ukipitia maboresho kadhaa mpaka sasa chini ya China ya ukomunisti.

Utaratibu huu unafanyika maalumu kwa ajili ya kulinda tamaduni na mfumo mzima wa maisha ya wachina dhidi ya muingiliano wa tamaduni na taratibu za jamii za nje.

Utendaji kazi wa sera au utaratibu huu katika karne hii na miaka hii ya karibuni umeshuhudiwa ukitenda dhidi ya dini za ng'ambo kama Uislam na Ukristo.

Mtindo na tamaduni nyingi za waislam wa sehemu mbalimbali duniani ni nadra kutendeka China bali waislam wa China wameweza kujitofautisha kwa kiasi kikubwa na waislam wa sehemu kubwa duniani katika mambo mbalimbali.

Serikali ya ukomunisti iliyopo China mara kwa mara imekuwa ikisisitiza ni muhimu waislam wa China kufuata na kutii sheria na maagizo ya serikali katika utimizaji wa imani yao kwa kuendana na kuheshimu misingi na tamaduni za China ya usoshalisti.

Pia katika dini ya Ukristo utaratibu huu wa sanicization umeshuhudiwa dhidi ya madhehebu ya kiprotestanti na ukatoliki.

Kwa pamoja waumini, viongozi na wafuasi wa imani ya kikristo wamekuwa wakisisitizwa kufuata na kuheshimu taratibu na sheria za China zinazo wataka viongozi wakuu wa madhehebu kuteuliwa na serikali ya kikomunisti katika uongozi wa makanisa yao.

Mara nyingi kanisa katoliki limekuwa likiingia migogoro kadha wa kadha na serikali ya China kuhusu huu utaratibu unaoipa mamlaka serikali ya China kuteua na kuchagua makasisi viongozi wa ngazi mbalimbali za kanisa kinyume na taratibu za kanisa katoliki linalomtaka papa kufanya hivyo.

Pia serikali ya China imekuwa ikisisitiza umuhimu wa ukristo kwa madhehebu yote kuishi na kuheshimu taratibu na tamaduni za jamii ya kichina katika kujenga umoja wa kitaifa.

Sinicization ilianzishwa kale kwa misingi ya kulinda taratibu na tamaduni za China, kadiri muda unavyozidi songa utaratibu huu katika dini unazidi kutiliwa mkazo ili kuepusha na kupunguza ushawishi wa dini za ng'ambo kitamaduni ndani ya jamii za wachina.
 
Huko wavaa kobaz wa takbirrr wanachapika saana.
Hili suala halihusu waislam pekee na Sinicization haihusishi matumizi ya nguvu bali muingiliano mkubwa wa kitamaduni za kichina ndani ya imani na kuathiri tamaduni za nje zilizopo kwenye hizo dini.
 
Bila china kufanya hivyo itaingiliwa na tamaduni za watu wengine na kuharibu tamaduni zao.

Kwa mfano, Waislamu ama utamaduni wa kiislamu ukiingia mahala unataka wenyewe ndio uwe dorminant, tamaduni nyingine zote ziheshimu na kutii na kufuata utamaduni wa kiislamu. Ndio maana waislamu sio rahisi kua compatible na jamii nyingine kwa urahisi.

Wakija watakwambia hiki sio halal, sijui wachinje wao, sijui mnatakiwa kuishi hivi mara vile nk.

China wana haki ya kupambana na kulinda utamaduni wao dhidi ya tamaduni nyingine za ajabu ajabu.
 
Ukomunisti wa China umetegemea mno kuendelea kwa tamaduni zao ili kusalia mamlakani.
 
Bila china kufanya hivyo itaingiliwa na tamaduni za watu wengine na kuharibu tamaduni zao.

Kwa mfano, Waislamu ama utamaduni wa kiislamu ukiingia mahala unataka wenyewe ndio uwe dorminant, tamaduni nyingine zote ziheshimu na kutii na kufuata utamaduni wa kiislamu. Ndio maana waislamu sio rahisi kua compatible na jamii nyingine kwa urahisi.

Wakija watakwambia hiki sio halal, sijui wachinje wao, sijui mnatakiwa kuishi hivi mara vile nk.

China wana haki ya kupambana na kulinda utamaduni wao dhidi ya tamaduni nyingine za ajabu ajabu.
Yaah upo sahihi na China ilitambua hili toka karne karne za nyuma kabisa na kuanza kutumia mbinu hii kwa kila tamaduni au imani itakayo vamia eneo lao.

Vitu vingi vilivyo ingia kwenye eneo lao vili badilishwa na kuendana na tamaduni za kichina hakika wamefanikiwa katika hili.

Sisi waafrika tuliangamizwa na tamaduni za nje mpaka sasa utamaduni wetu kwa asilimia kubwa umekufa
 
Ukomunisti wa China umetegemea mno kuendelea kwa tamaduni zao ili kusalia mamlakani.
Nafikiri suala la wakomunisti kuwepo madarakani lina sababu nyingi kuu ni maendeleo ambayo hata kabla wananchi hawajaomba jambo fulani tayari wao wamekwisha fanya.

Ukifuatilia vizuri kuhusu nchi yao ni kwamba wapo mbele ya muda au wapo mbele ya wananchi hawana tofauti sana na chama cha Singapore PAP ambacho toka uhuru 1959 mpaka leo kipo madarakani na wao sababu kuu ni hiyo hiyo maendeleo.

Hata CCM ingekuwa inaleta maendeleo kama hao wakomunisti wa China na hao PAP wa Singapore hakuna ambaye angejali kuhusu uwepo wao madarakani.

Nakubaliana nawe pia kuwa tamaduni za China wananchi wake kwa fuata historia hupenda kuongozwa na watu strong hivyo chama cha kikomunisti ni kama ufalme mwingine wa kichina katika modern era baada ya Qing dynasty
 
Kwahili china nawasifu sana wakazie hapo hapo,wavaa kobazi watalazimisha wanawake wavae majuba hata watoto wakike darasani upuuzi mtupu,watataka wao ndio wawe wachinjaji machinjioni na nguruew wataita haramu wakati ndio nyama pendwa uchina na ulimwenguni kote.

Bila kusahau maspika yao kelele tupu.
 
Back
Top Bottom