Je, mikutano miwili ya China ina maana gani kwa Afrika?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111484185917.jpg


"Wakati Mikutano Miwili" inafanyika wiki hii, dunia nzima sasa inaangazia tena China.

Mikutano Miwili yaani Bunge la Umma na Baraza la Mashauriano ya Kisiasa ya kila mwaka ni dirisha muhimu kwa dunia kutazama na kuifahamu China. Hivi karibuni, mkutano wa pamoja wa wataalam wenye kaulimbiu ya "Nchi za Afrika Zinanufaika na Maendeleo ya China" ulifanyika Nairobi, Kenya, ambapo washiriki wa sekta mbalimbali walieleza matumaini yao kuwa Mikutano Miwili itakuza zaidi uhusiano kati ya China na Afrika.

Kutokana na udhaifu wa kufufuka kwa uchumi wa dunia na kuongezeka kwa sintofahamu, nchi za Afrika zinafuatilia kwa karibu jinsi uchumi wa China utakavyoimarishwa zaidi ili kuleta manufaa zaidi kwa Afrika.

Mwaka 2023, licha ya kukabiliwa na changamoto na taabu mbalimbali, uchumi wa China ulipata ukuaji wa asilimia 5.2, kasi ambayo inaongoza kati ya nchi zenye uchumi mkubwa duniani na China imeendelea kuwa chachu kubwa zaidi ya ukuaji wa dunia.

Kiwango cha biashara kati ya China na Afrika pia kiliweka rekodi mpya na kufikia dola za kimarekani bilioni 282.1. Miongoni mwao, mauzo ya "bidhaa mpya" kama magari ya umeme barani Afrika imeongezeka kwa kiasi kikubwa, jambo ambalo limesaidia sana maendeleo endelevu ya Afrika.

Mhariri Mtendaji wa Shirika la Magazeti Zanzibar Ali Haji Mwadini alisema kuwa maendeleo ya China katika nyanja ya teknolojia ya hali ya juu katika miaka ya hivi karibuni yamekuza ipasavyo ukuaji wa viwanda vya aina mpya.

Anatazamia zaidi kusikia kuhusu "mpango wa China" wa kuboresha tija mpya za uzalishaji katika Mikutano Miwili ya mwaka huu, na anatumai kuwa China inaweza kutoa msaada kwa nchi za Afrika katika nyanja hii katika siku zijazo.

Tangu ufanyike Mkutano mkuu wa 20 wa Chama cha Kikomunisti cha China, jinsi ya kugeuza maono mazuri ya "maendeleo ya kisasa kwa mtindo wa kichina" kuwa uhalisia imekuwa moja ya mambo ambayo nchi za Afrika zimetilia maanani maendeleo ya China.

Sio tu kwamba imetoa mfano mzuri kwa Afrika kuchunguza usasa na maendeleo, lakini pia inakuwa kichocheo cha uboreshaji wa mtindo wa Kiafrika.

Mwanahabari wa Gazeti la Mwananchi, Tanzania Ephrahim Edward Bahemu ambaye mwaka jana alikuja kushuhudia vikao hivi vikipitisha ajenda zake mbalimbali, anasema kuwa mtindo wa kisasa wa Kichina sio tu unakuza maendeleo ya China, lakini pia nchi zinazoendelea zinaweza kujifunza uzoefu wake katika kujiendeleza na kuboresha ustawi wa nchi.

Mbali na mipango ya kiuchumi na maendeleo, sera ya mambo ya nje ya China pia inafuatiliwa sana na nchi za Afrika katika mikutano miwili. Mwaka 2023, hali ya amani na usalama barani Afrika ilikabiliwa na changamoto mpya.

Kwa mfano, matatizo ya usalama wa chakula yanayosababishwa na mzozo unaoendelea katika ukanda wa Gaza yanazidisha hali ambayo tayari si shwari katika eneo la Pembe ya Afrika. Katika ripoti ya kazi ya serikali ya mwaka huu, Waziri Mkuu wa China Li Qiang alisema kuwa China itatetea kujenga utaratibu wa kimataifa wenye usawa na ncha nyingi.

Msomi wa masuala ya kimataifa wa Kenya Adhere Cavins amesema kuwa, nchi za Afrika zinatumai kuwa Mikutano Miwili ya China itatoa taarifa zaidi zinazofaa kwa maendeleo na utulivu wa dunia, na wanatarajia China itaendelea kuchukua nafasi muhimu katika kukabiliana na masuala na changamoto za kimataifa.
 
Back
Top Bottom