Black Jesus
JF-Expert Member
- Mar 7, 2008
- 256
- 10
Mkandara Mkuu, mimi nakubaliana na wewe sana hasa kwenye issue ya imani. Naamini kwa ufahamu mzuri ulionao, unaoanisha imani ya sera za chama tawala na mafanikio ama kushindwa kwa malengo ya Taifa letu. Mimi naamini kama wewe, nishichokiamini ni kuwa CCM haina sera nzuri. Hili si la kweli. CCM ina sera nzuri sana tu na pia ina imani na malengo mazuri. Kama umefuatilia kwa makini nilichokisema kwenye post iliyotangulia, niliweka pia kushindwa kutekelezwa sera nzuri za CCM.
Mkuu, mafundisho ya imani ya dini, au itikadi yoyote yanategemea sana na kiongozi/mfundishaji/msimamizi wa mafundisho hayo n.k. CCM imeshaweka sera zake ambazo kwa kweli ndizo zilizotufanya tusisite kukichagua kwa mara nyingine mwaka 2005. Sera hizo nzuri zilisambazwa vizuri, zikaeleweka. Ambacho hakikufanyika ni utekelezaji wa sera zenyewe. Hili ndilo linalotufanya tuamini kuwa tulilaghaiwa na sasa inatosha. Sioni sababu ya kuendelea kuamini kuwa itafika siku mtu yule yule alieshindwa akaweza kutekeleza vyema yote aliyoahidi. Sioni mwelekeo huo.
Kufananisha walioshindwa na kudhani kuwa wote ni watakaoshindwa nalo ni kosa kubwa. Bondia akianguka kwenye pambano, halafu akaanza kufikiria waliowahi kuanguka katika mashindano ya nyuma, ni wazi kuwa ataishia kushindwa kwa knock-out. Tunachotakiwa kama Taifa ni kuangalia tulipoanguka na kuchukua hatua za kutuhakikishia kutoanguka tena siku za mbele. Kwa maneno mengine ni kwamba, inatakiwa kujua kuwa, tulianguka wapi, kivipi na jinsi gani ya kukwepa kufikia kuanguka kama huko.
Mkandara ndugu yangu, mimi naweza kutaja watu wengi tu ndani ya CCM wenye uwezo mkubwa wa kuleta unafuu kiuchumi, kisheria, kijamii, n.k., kuliko tunavyoendelea hivi sasa. Ila nitakuwa siwatendei haki watu hao kama nitawataja na wao wasiwe na nia ya kutaka kuongoza Taifa hili. Ndio maana nikasema (hapo juu), kuwa hata mimi ninaamini kuwa ningeweza vizuri zaidi.
Ninachoweza kukiomba chama changu CCM ni kutoa ruhusa kwa wenye uwezo kugombea nafasi hiyo kwa usawa na haki. Baada ya wote kuchukua form na kuzirudisha, ndipo tutakapoweza kuona options tulizonazo.
Mkuu Bubu hebu kuwa na msimamo unaoeleweka. Namna unavyoelezea mfumo mbaya ulioko CCM na baadae kufikiria kuwa huyo mwanachama alieko Manzese tawini ataweza kupata nafasi ya kuteuliwa nafasi ya urais Duh! nafikiri hii ndio aninacha sio hiyo unayoiona wewe.
Be realistic nani kwenye CCM alitokea tawini tu akawa mjumbe wa halmashauri kuu sembuse kamati kuu na nafasi ya kugombea urais.
Mfano wako wa Obama does nt hold water na hali hii tunayoizungumza.
Obama alipitia nafasi zote na ilikuwa stahiki yake kupanda hapo alipo na kwa mfano huohuo wa Obama na sisi tunawapima wana CCM walikokuwa tayari kufikia kiwango hicho cha kugombea urais na tunashindwa kumuona na hasa kwa kigezo chako mwenyewe kuwa wote si safi kwa vile wamebebwa na Chama kilichokuwa si safi.
Kama unakubali kuwa CCM ina mizizi katika ufisadi utawezaje kutegemea mmoja wa wajumbe wa mafisadi kupigana na ufisadi. Ni miaka minne sasa tangu CCM iingie madarakani kwa pesa za EPA ni nani katika CCM,awe mbunge, Waziri,Mwenyekiti wa Mkoa au mjumbe aliekikana Chama kwa ufisadi wake?
Mapambano tunayoyaona si mapambano ya kukisafisha chama bali ni kulipizana kisasi kwa wanachama binafsi. ingekuwa vita hivyo ni dhidi ya shina hasa CCM basi tungesema kuwa anaweza akatokea mtu alietofauti na wenzake ndani ya CCM na kwa hivyo huyo alieko mwache amalize muda wake, kwani si hatuna Chama chengine cha kushika Madaraka.?
Msimamo wangu unaeleweka kamwe usitake kupindisha hilo. Wapi nimefikiria kwani mwanachama wa tawi la Manzese kama anatimiza taratibu zote zilizowekwa ndani ya CCM kwanini asistahili kuteuliwa kama Rais wa Tanzania!!!? Au kuna matawi maalum yanayoruhusiwa kutoa wagombea wa Urais na mengine ni marufuku kutoa wagombea wa Urais!!? 😕
Kama CCM ingekuwa inaenda hivyo unavyofikiri wewe tusingekuwa na viongozi walewale. Nasema huna msimamo kwa kukisema kuwa chama kimeoza na huku ukitegemea mkubwa mmoja atakuwa safi. Basi waliosafi na wajitokeze na kujikosha na tuhuma za kuingia madarakani kwa fedha za EPA na hilo lifanyike sasa ingawa wameshachelewa kwani wamekuwa wakila fedha zetu kipindi cha miaka minne.
Wewe ndiye unahitaji kuwa realistic na mfano wa Obama unalingana kabisa na yanayoendelea nchini maana wakongwe ndani ya chama chake asilimia kubwa sana walimuunga mkono Hillary, hivyo wangejkuja na vitisho kama Wazee njaa wa CCM kwamba atakayempinga Hillary atakiona basi, Obama asingekuwa Rais wa Marekani lakini wakaacha katiba ya chama chao ichukue mkondo wake na yaliyotokea wote tunajua.
Obama alijitokeza kwasababu alikuwa msafi na ili uwe mfano umekamilika jee tayari huyo mtu kutoka CCM ameshajitokeza?
Obama katika wale waliokuwa wanampinga walidai kwamba hakuwa na experience yoyote katika mambo mbali mbali na alikuwa senator kwa kipindi kifupi mno cha miaka minne na pia walidai kama Senator hakuiniate policies zozote nzito hivyo kutokuwa na uzoefu ilitumika dhidi yake. Wacha katiba ya chama ifanye kazi yake!!!!! Na hapo ndiyo mtajua kama kuna mtu mwingine zaidi ya Kikwete anayestahili kuwa Rais au la, na siyo kutaka kuikana na kuikimbia katiba iliyotungwa na kupitishwa na wanaCCM wenyewe.
Sisi hatupingi experience ya mtu. Sisi tunapinga usafi wa watu wa CCM. Na wala hatukatazi kuwa katiba isifuatwe. Tatizo letu ni kuwa katiba ifuatwe kwa wote ikiwa pamoja na Kikwete kupewa nafasi ya kugombea tena URAIS NA KWA MUJIBU WA KATIBA HIYOHIYO SI VIBAYA KUSEMA KUWA NITAMTETEA MTU FULANI.Wazee hawajasema kuwa mtu asigombee lakini ajuwe tu kuwa wao watamtetea Kiwete. Mimi na wewe tunashindania uwezo wa kugombea urais na tuna haki ya kutofautiana. Hoja ndizo zitakazoamuwa.
Wako wengi tu ndani ya CCM waliojaribu kupambana na ufisadi na juhudi zao wakapigiwa simu za kutukanwa matusi ya nguoni au hata kutishiwa maisha yao. Hili siyo siri.
Mkuu bubu hili la kusema kuwa kitu kipo bila ushahidi si jambo muafaka. Hata mimi nitakwambia kuwa JK amefanikiwa kwa kila jambo lakini utaniouliza mambo gani? Nawe nakuuliza kina nani waliofichuwa siri ya CCM kuingia madarakani ambao tutasema kuwa wanastahiki kuwa Marais?
Kwanini kiongozi dhaifu aendelee kumaliza muda wake wakati kazi imemshinda!? Miaka mitano kuwa na kiongozi dhaifu ambaye maslahi ya Taifa hayana umuhimu wowote kwake ni muda mrefu sana kwa nchi yoyote ile duniani. Kwa hiyo wakati umefika wa kumwambia ukweli mpishe mwingine maana wewe kazi imekushinda
Sijaona udhaifu wa kiasi cha kuwa tusimuamini tena kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Unajuwa kwanini? Sioni tofauti kubwa kati ya utawala huu na tawala zilizopita.
Utawala huu angalau unatowa uhuru kwa akina sie kuwakejeli na kuwaumbua viongozi wetu whether ni mafisadi kweli au shutuma tu huku dola kuwa si tishio kwa mwananchi. Yaliobakia ni yale yale kama tawala nyengine, manufaa kwa wakubwa na kutembeza bakuli. Kwa mtaji huo kama walivyomaliza wengine bado akiletwa na CCM naaendelee.
...mimi naamini kuwashinda CCM lazima kuanzie kwenye viti vya ubunge la sivyo kuwaondoa hawa jamaa itakuwa ndoto na wataendelea kutufisadi na kututia umaskini wa milele,siamini chama chenye wabunge wasiozidi 20 kati ya 400 kinaweza kushinda uraisi,battle zote zipo bungeni na kule ndio kelele zinaweza make sense sio za kina Mrema kule manzese wanaonekana wendawazimu tuu!
Ndio maana tukasema bora huyo JK. Uko serious kweli na unayoyasema?
Unataka maendeleo yalyokosekana miaka 50 uyapate kwa kipindi cha miaka mitano na huku unakaa kwenye Forum na kuanika pumba ukitaka Jk akuletee maendeleo? Maendeleo huletwa na watu sio mtu binafsi.
Unaijua Ilani ya CCM? Ni kujinufaisha na hilo lilihakikishwa kabla Mkapa hajaondoka Kwa Fedha zetu. JK anatekeleza vizuri na ndio maana wanamgangania
Tangu aingie Kikwete angalau mauwaji ya Polisi yanafanyiwa kazi. Hata hivyo si kazi ya Rais kufatilia Kesi na ukichungua hivi sasa ndio wakati ambao haki mara nyingi zinafuatwa.
Na hizi harakati za wanaojipendekeza nazo umbebeshe yeye? Lini katika hotuba zake ukamsikia kama Rais wetu aliepita akisema kila wakati " Nilpoingia madarakani nchi ilikuwa hivi .............,vile.........?
Tumekuwa tukiomba kupatiwa mbadala wa Kikwete na tutaendeleza kudai hivyo, wewe la!
SixGembe,
Mkuu kwani Uongo?
Nani CCM anaweza kuwa bora kuliko Kikwete naomba sababu au vigezo vya mtu huyo ktk Uongozi bora..
Six
Ameonyesha mabadiliko makubwa katika utendaji wa BUNGE.
Ameonyesha uwazi na kuweka maslahi ya taifa before him.
Mambo yaliyofanyika BUNGENI chini ya uongozi wake ,yameandika historia mpya ya taifa hili.
Mkuu umesahau Six alichemka alitumia ubabe na busara ndogo kumtupa nje Zitto Kabwe bungeni?
Pia amezuia mijadala wa Vitambulisho vya shilingi bilioni 200 na ununuzi wa Kiwira ambao una kila dalili ya ufisadi kwa sababu ambazo haziingii akilini. Pia alisimamisha mjadala kufanyika kwa sababu alikuwa amalikwa dinner Marekani. Mimi sikubaliani kwamba ameleta mabadiliko yoyote bungeni.
- Mkuu wangu tema mate pembeni, kama sio Six ungeona maaajbu kuliko haya ya sasa, tizama mazingara mkuu, muulize Lowassa, nani aliyemtoa kule juu.
FMES
Pia amezuia mijadala wa Vitambulisho vya shilingi bilioni 200 na ununuzi wa Kiwira ambao una kila dalili ya ufisadi kwa sababu ambazo haziingii akilini. Pia alisimamisha mjadala kufanyika kwa sababu alikuwa amalikwa dinner Marekani. Mimi sikubaliani kwamba ameleta mabadiliko yoyote bungeni.
Bubu ataka Kusema,
Mkuu una kila haki ya kusema Kikwete hakuleta maendeleo yoyote.. Wala hauko peke yako.. Ni imani ambayo hata huko Marekani unakozungumzia wapo watu kibao walichukia Bush aliporudia kipindi cha Pili, Clinton aliporudia kipindi cha Pili inategemea na mtazamo wa kila mtu ktk ujenzi wa Taifa..
Sasa ajabu unatuletea mfano wa Obama, kama vile baadhi ya wanachama wa Domokratik walimpendekeza Kelly arudie kusimama na McCain..Licha ya yote hayo Obama kama situation ingekuwa sawa na yetu nina hakika watu wangependekeza majina ikiwa ni pamoja na Obama kusimama against Kelly..hawa watu wote kina Obama, Clinton, Joe wangesimama na kupinga mfumo huo wakisema wao watapenda kugombea Urais na sifa zao watazitaja..
Hii inakwenda vyama vyote, Chadema wanaweza kumsimamisha tena Mbowe, CUF wakamsimamisha Lipumba, TLP na Mrema bila upinzani inategemea na vyama hivyo vimejipanga vipi..Siwezi kutumia sababu za Mbowe kushindwa uchaguzi ama kukiendeleza chama wakati sina mfano mzuri kama vile Dr. Slaa, Zitto na wengineo..
Unapinga kitu ukiwa na mtu mwenye uwezo zaidi ktk matakwa yako, hupingi kwa sababu unapinga wakati gari halina dereva zaidi yake ukisema tu kila mtu anaweza kuendesha.. Cheo ni dhamana ya chama na wananchi.. sasa chama kimechagua nani dereva wao wewe hutaki, tupe jina la dereva mwingine.. hutaki unatumia mfano wa Obama ambaye tunajua kwanza ilikuwa lazima demokratik wawe na ushindani ndani ya chama kumpata mgombea tofauti naa wakati Bush auClinton walipopendekezwa kugombea awamu ya pili...
Mkuu wangu mjadala huu ni mfano mzuri sana wa fikra zetu sisi wenyewe, dhahiri inaonyesha wazi jinsi tulivyojipanga nyuma ya CCM hata kama tunapinga uongozi wa chama hicho na madudu yake yote..
Moja ya miiko ya chama hicho ni KUTUPANA.. nikiwa na maana KULINDANA ni moja ya maadili ya chama nje ya maandishi..na Kikwete anafanya kama chama kinavyotaka KUKILINDAchama na KULINDA viongozi wake waliobarikiwa kama tulivyomuomba Mungu ktk wimbo wa Taifa..
Sasa mimi nitapenda sana kujua mtu huyo ambaye yuko tayari kukiuka haya maadili ya chama ya kulindana ambaye yuko tayari kuwafikisha Mafisadi wote mahakamani kama atapewa nafasi ya Urais mwaka 2010..navyofahamu mimi viongozi wote wa CCM wamekubaliana swala la kumfikisha Mkapa, Lowassa, au Rostam mahakamani ni kuliweka taifa ktk hatari ya kudhoofisha usalama wa taifa... sasa wewe nambie nani ambaye anaamini tofauti na wazo hilo kwani kinacvhogomba hapa ni sisi wote kuamini kwamba JK ameshindwa kuwafikisha mahakamani Mafisadi kwa sababu anakilinda chama badala ya maslahi ya Taifa..
Mkuu there is a thin line between LOVE and HATE, unapoona wewe na kuchukia kwamba JK ameshindwa, hafai na kadhalika, wanachama wanaona JK ameweza kukilinda na kuinusuru nchi toka machafuko ya kisiasa..tena kuna baadhi wanamwona amekuwa soft kuwafikisha mahakamani baadhi ya viongozi au kuachia magazeti kuwazungumzia viongozi waliobarikiwa..Kwa mtazamo wao watu kama wewe are Hater!...na Kikwete hakutakiwa kuwasikiliza, wakati wewe unafikiria kufanya hivyo na zaidi ni kutokana na mapenzi ya nchi yako..
Kwa nini nguvu zako usiziweke kwa Wapinzani!.. hata kamaKikwete atasimama against watu kama Mwakyembe au Lau Masha..nadhani muhimu pia utazame uwezekano wa watu hawa kutuongoza vizuri kwa sababu sio swala la katiba ya chama kutazama maslahi ya Taifa isipokuwa chaguo lako ndilo litatazama maslahi ya taifa. Huyo Mwakyembe , Masha na wengine wote wamesimama upande wa Mafisadi,sasa wanapoweka ushindani ndani ya chama itakusaidia nini wewe zaidi ya kuona utaratibu unaopendekeza wewe umefanyika..Utaratibu ambao won't change maisha ya mwananchi..