The Legacy of Julius Nyerere

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,212
113,520


Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikijiuliza na kuuliza bila mafanikio kama Nyerere aliwahi kukutana au kama alikuwa na uhusiano wowote ule na Dr. Martin Luther King Jr. Hebu angalia hiki kipande cha tatu kuanzia kwenye dakika ya 5 na sekunde 45 (5:45) hadi dakika ya 5 na sekunde 49 (5:49). Hapo namuona Dr. King akisalimiana na mtu ambaye sura yake haionekani ila ambaye shingo na kichwa chake ni kama vya Nyerere!! Wadau mnasemaje hapo? Huyo ni Nyerere na Dr. King ama?
 
Last edited by a moderator:
Asante sana X-Paster. Ombi kwa mods - kama mnaweza kuziweka vizuri hizo clips kwenye bandiko la kwanza itapendeza sana.
 
Ni kumbukumbu nzuri mkuu, vitu kama hivi vinapaswa kufanywa kwenye kila nyanja, na haswa kwa wanasiasa wetu, ili vizazi vijavyo vipate adidu za rejea zilizo yakinifu.
 
Ni kumbukumbu nzuri mkuu, vitu kama hivi vinapaswa kufanywa kwenye kila nyanja, na haswa kwa wanasiasa wetu, ili vizazi vijavyo vipate adidu za rejea zilizo yakinifu.

Nimeipenda sana hii mini-documentary. Kuna baadhi ya maswali kama lile la "collectivization" kwa mfano, ambayo Nyerere mwenyewe anajibu laivu bila ya chenga.

Oh na kwa wale ambao wanasemaga Nyerere hakuwahi kukubali makosa....hebu na waangalie hiyo clip ya pili.
 
Mkuu, wakati wa kukopi address ya youtube, click kwenye alama ya "insert video", na si kwenye alama ya "link"

Unaweza kurekebisha mkuu.
 
Nimeipenda sana hii mini-documentary. Kuna baadhi ya maswali kama lile la "collectivization" kwa mfano, ambayo Nyerere mwenyewe anajibu laivu bila ya chenga.

Oh na kwa wale ambao wanasemaga Nyerere hakuwahi kukubali makosa....hebu na waangalie hiyo clip ya pili.
Mkuu, wanao mtetea Nyerere wanataka kumfanya kama malaika, Waswahili tuna msemo huu "Hapana kapa isiyokuwa na usubi" yaani hakuna kiumbe ambaye ni mkamilifu.
 
Hata mimi nimeipenda hii documentary japo naamini ingeweza kwenda mbali zaidi. Kuna vitu kadhaa ambavyo nimevipenda.

a. Ukosoaji wake wa IMF na WB ni classic! Sijui kama kuna kiongozi yeyote ambaye alifahamu tatizo la IMF na kukosoa namna hii. Alichokisema Nyerere kimekuja kujionesha katika anti-globalization movement.

b. Hotuba yake ya Bunge la RSA niliwahi kuisoma yote lakini sikuwahi kuona hasa ambavyo wasikilizaji wake walivyokuwa captivated naye. Tukisema Nyerere alikuwa mzungumzaji mzuri, hatumtendei haki. He was a great orator.

c. Nami kama NN sikujua kama Nyerere amewahi kukutana na MLK Jr, lakini ni wazi waliwahi kukutana, I wish we could find a more clearer picture of their meetings, kwani inaonekana kwenye clip ya video hapa ni MLK aliyeonekana kuvutwa sana na JKN - in my so openly biased opinion.

d. Mambo mengine nadhani yako wazi, Nyerere alijua makosa ya uongozi wake, kabla na baada ya kuondoka. Leo hiso Mwinyi, Mkapa wala Kikwete waliowahi kusema makosa yao ya kiongozi ni yapi (Mkapa alisikitika tu kwa mauaji ya Pemba).

Thanks kwa hii.. it'll add to my collection. Sijui kwanini wameweka katika sehemu tatu kwa sababu siku hizi unaweza kutengeneza clip moja ndefu.. nadhani wanafikiria bado kuna limit ya dakika kumi.
 
Hata mimi nimeipenda hii documentary japo naamini ingeweza kwenda mbali zaidi. Kuna vitu kadhaa ambavyo nimevipenda.

a. Ukosoaji wake wa IMF na WB ni classic! Sijui kama kuna kiongozi yeyote ambaye alifahamu tatizo la IMF na kukosoa namna hii. Alichokisema Nyerere kimekuja kujionesha katika anti-globalization movement.
.

Mkjj, Mwalimu alikuwa na vision ya mbali sana ndio maana hotuba zake nyingi pamoja na kuwa zina miaka mingi sana lakini bado ziko relevant siyo tu katika yanayojiri Tanzania bali duniani kote. Mwalimu alizipinga sana sera za IMF na WB ambazo ukizifuatilia kwa makini utaona kwamba nchi nyingi zilizoamua kuzitekeleza sera zile ikiwemo Tanzania hazikupata mafaniko yoyote yale ya kiuchumi, lakini wale wenye chuki za kutisha dhidi ya Mwalimu hawalioni hili wao yote aliyoyafanya Mwalimu yalikuwa na kasoro tena kubwa sana. Mwalimu hakuona aibu wala woga kusema makosa yake mbali mbali aliyoyafanya akiwa madarakani. Bado tunasubiri kuwasikia akina Mwinyi, Mkapa na huyu wa sasa kama na wao watakuwa tayari kusema makosa waliyoyafanya wakiwa madarakani.

Naamini kabisa kwamba kama watafanya hivyo hawatakuwa wakweli kama alivyokuwa Mwalimu pale alipoamua kuyasema makosa yake hadharani kwa sababu baadhi ya makosa hayo ni kashfa kubwa sana
 
nimesoma tena nimejicheka.. maana kuna wakati mtu unaweza kuficha ur biases, in this case I didn't even attempt to.
Hamuwezi kuifanya MNF ikaifanya kazi hii kwa WATANZANIA walio wengi zaidi? MNF hawawezi kuwa na vipindi hata vya kulipia kwenye TV zetu wengi tukafaidika na busara hizi za Mwalimu. TBC1 wanaonyesha matukio mbalimbali ya ziara za Mwalimu kwa picha mbovu mno zisizo na sauti yake. Naona kama hawatutendei haki WATANZANIA na hata MWALIMU mwenyewe huko aliko. Wangeacha tu.
 
How many African presidents of the independence era willingly gave up power?
How many presidents can say they actively participated in menial labor with their people?
How many presidents can say they went to the front line during an active war?
How many presidents have traveled abroad more times after their retirement than when they were in office?
How many presidents can openly and publicly admit their mistakes?
How many African presidents today can be given numerous honorary doctorates and still prefer a simpler title of "mwalimu" over "Dr."
When our living presidents die will Tanzanians cry for them like we did for Nyerere?

So why are there some Tanzanian leaders today who want to tarnish everything he stood for?
It's because they are opposite of Nyerere. They are greedy and corrupt. They lack vision and leadership skills. Most of them can't even talk like leaders. They want to tarnish the legacy of Nyerere because it is a big shadow they fear.
 
Hakuna mtu anayemtetea Nyerere anayetaka kumfanya malaika (kwa wale ninaowajua mimi); wanaomtetea Nyerere wanawapinga wale wanaotaka kumfamya kama shetani!
Kaka kutokuwa malaika hakukufanyi wewe kuwa shetani, hayo ni mawazo yako hasi kaka. Nyerere atabakia kuwa binadamu, aliyewahi kuitawala Tanzania Kidikteta, na hiyo haimaanishi kuwa yeye alikuwa shetani, labda hiyo ni sifa unayotaka kumpa wewe leo.

Hotuba yake ya Bunge la RSA niliwahi kuisoma yote lakini sikuwahi kuona hasa ambavyo wasikilizaji wake walivyokuwa captivated naye. Tukisema Nyerere alikuwa mzungumzaji mzuri, hatumtendei haki. He was a great orator.

Ni kweli Nyerere was a great orator, kwa maana hakuwa na haya kuutetea uongo ufanane na kweli. Alijionyesha kuwa nimpigania haki, lakini ndani ya Tanzania alifanya kinyume chake. Watanznia tulinjimwa haki ya kuyatoa mawazo yetu na waliojaribu aliwaweka kizuizini.

_______________
Nyerere hakuwahi kukiri kushindwa
by mkjj
 
How many African presidents of the independence era willingly gave up power?
How many presidents can say they actively participated in menial labor with their people?
How many presidents can say they went to the front line during an active war?
How many presidents have traveled abroad more times after their retirement than when they were in office?
How many presidents can openly and publicly admit their mistakes?
How many African presidents today can be given numerous honorary doctorates and still prefer a simpler title of "mwalimu" over "Dr."
When our living presidents die will Tanzanians cry for them like we did for Nyerere?

So why are there some Tanzanian leaders today who want to tarnish everything he stood for?
It's because they are opposite of Nyerere. They are greedy and corrupt. They lack vision and leadership skills. Most of them can't even talk like leaders. They want to tarnish the legacy of Nyerere because it is a big shadow they fear.
mkuu hili jina la mwanafalsafa ulijiita au ulipewa na mtu?kama ulijiita basi hukukosea yani ulijistukia kuwa una mawazo mazito,kama mtu alikuita hakukosea,..post zimetulia especiaaly this masterpiece,...what a comment!!!
 
Back
Top Bottom