The inevitable class struggle between the haves and the have nots...!

The inevitable class struggle between the haves and the have nots...!

Wallet
Mkuu ni vigumu sana ukiwa kundi jingine kuweza kuona ya upande wa pili na yamkiniki wewe hukutoka kt kundi la walalahoi hivyo huwezi kutambua hawa Pnya road wametokana na nini? Ufahamu tu kwamba hawa vijana ni kati ya umri wa miaka 16 hadi 20 ambao wanatakiwa kuwa shule kama ulivyodai lakini wameshindwa vipi kuwa shuleni? sidhani kama umefanya utafiti huo kwanza!

Na hata tukichukulia juu juu tu ya kwamba shule zetu ni za kulipia na zaidi ya hapo hawa ni failure wa mitihani ama mfumo wa Elimu nchini ambao umewaweka katika nafasi hiyo. Hata wale walioko vitani leo kule Syria na wameshika bunduki sio kwamba wao ni majambazi na terrorist isipokuwa kuwepo kwa vita kumewalazimu kuwa wauaji aidha baada ya kushindwa kukimbia nchi yao ama ile ari ya kuitaka amani.

Swala la class struggle nchini sii la kulifanyia mzaha hata kidogo, ni jinamizi linalokua kwa haraka sana na litakuja kutuangamiza sote maana kesho haitakuwa Panya road tena bali jirani yako ambaye kashindwa kujikimu mahitaji yake wakati wewe jirani yake unatanua. na hii imeanza pia kujitokeza maana kwa kila mwenye nacho leo hii hutafuta makazi mapya sehemu ambazo ataipata amani, hivyo amani inaaza kupotea baadhi ya sehemu za makazi yetu hapa hapa mjini.

haya makuzi ya Dar kuwa na maghorofa ni makuzi ya mwili tu, kama vile wewe huwezi kuwa sawa na ulivyokuwa miaka 12, leo umerefuka una ndevu, sharubu, unavaa suruali badala ya kaptula haya sio maendeleo bali makuzi ya mwili na vitu vinavyoendana na makuzi hayo kwa sababu afya yako bado inaweza kuwa dhoofu zaidi, maisha yako ya taabu zaidi ya utoto. Hata ukienda New York leo utaona mabadiliko makubwa zaidi ktk majengo, New York ya mwaka 1990 sio hii ya leo! wala maendeleo sio kuwa na Kentacky fried Chicken au maduka ya bidhaa kutoka nje, sisi ni mateja tu ktk soko la ubepari! Maendeleo ya nchi yetu, ukitazama miundombinu leo ni mibovu kuliko wakati wowote, mirefeji, barabara, reli, ukulima na hata vyanzo vya ajira. Tuna watu wengi wasokuwa na kazi leo kuliko wakati wowote ule na hii ndio alama kubwa ya maendeleo. Panya road ni sehemu kubwa ya kizazi cha wazazi wasiokuwa na ajira na hivyo kilema hicho kinaendelea chini na kuwa mnyororo wa walalahoi ambao kesho na kesho kutwa ndio watakuwa maadui zako!
Panya road ni tahadhali kubwa ya jamii tunayoijenga leo!
 
Wallet
Mkuu ni vigumu sana ukiwa kundi jingine kuweza kuona ya upande wa pili na yamkiniki wewe hukutoka kt kundi la walalahoi hivyo huwezi kutambua hawa Pnya road wametokana na nini? Ufahamu tu kwamba hawa vijana ni kati ya umri wa miaka 16 hadi 20 ambao wanatakiwa kuwa shule kama ulivyodai lakini wameshindwa vipi kuwa shuleni? sidhani kama umefanya utafiti huo kwanza!

Na hata tukichukulia juu juu tu ya kwamba shule zetu ni za kulipia na zaidi ya hapo hawa ni failure wa mitihani ama mfumo wa Elimu nchini ambao umewaweka katika nafasi hiyo. Hata wale walioko vitani leo kule Syria na wameshika bunduki sio kwamba wao ni majambazi na terrorist isipokuwa kuwepo kwa vita kumewalazimu kuwa wauaji aidha baada ya kushindwa kukimbia nchi yao ama ile ari ya kuitaka amani.

Swala la class struggle nchini sii la kulifanyia mzaha hata kidogo, ni jinamizi linalokua kwa haraka sana na litakuja kutuangamiza sote maana kesho haitakuwa Panya road tena bali jirani yako ambaye kashindwa kujikimu mahitaji yake wakati wewe jirani yake unatanua. na hii imeanza pia kujitokeza maana kwa kila mwenye nacho leo hii hutafuta makazi mapya sehemu ambazo ataipata amani, hivyo amani inaaza kupotea baadhi ya sehemu za makazi yetu hapa hapa mjini.

haya makuzi ya Dar kuwa na maghorofa ni makuzi ya mwili tu, kama vile wewe huwezi kuwa sawa na ulivyokuwa miaka 12, leo umerefuka una ndevu, sharubu, unavaa suruali badala ya kaptula haya sio maendeleo bali makuzi ya mwili na vitu vinavyoendana na makuzi hayo kwa sababu afya yako bado inaweza kuwa dhoofu zaidi, maisha yako ya taabu zaidi ya utoto. Hata ukienda New York leo utaona mabadiliko makubwa zaidi ktk majengo, New York ya mwaka 1990 sio hii ya leo! wala maendeleo sio kuwa na Kentacky fried Chicken au maduka ya bidhaa kutoka nje, sisi ni mateja tu ktk soko la ubepari! Maendeleo ya nchi yetu, ukitazama miundombinu leo ni mibovu kuliko wakati wowote, mirefeji, barabara, reli, ukulima na hata vyanzo vya ajira. Tuna watu wengi wasokuwa na kazi leo kuliko wakati wowote ule na hii ndio alama kubwa ya maendeleo. Panya road ni sehemu kubwa ya kizazi cha wazazi wasiokuwa na ajira na hivyo kilema hicho kinaendelea chini na kuwa mnyororo wa walalahoi ambao kesho na kesho kutwa ndio watakuwa maadui zako!
Panya road ni tahadhali kubwa ya jamii tunayoijenga leo!
Mkuu Mkandara nashukuru kwa wewe kuchukua muda wako kujaribu kuelimisha on the catostrophe inayoikabili jamii ya kitanzania.

Kwa wananchi wenzetu wa kitanzania kama Wallet waliokua katika mazingira ambayo tungeita spoon fed, hawaelewi kabisa majuto yanayowakabili wananchi walio upande wa wale ma proletariats.

Na tatizo kubwa ni kwamba si tu hawaelewi, lakini ukweli ni keamba hawataki kuelewa kwa kuridhika kuwa watawala walio katika payroll ya the bourgeuoeise watawatetea mpaka mwisho wa uhai wao.

Nina sisitiza kuwa ni vema waliokatika utawala kutambua nguvu kubwa ya wananchi wanaolifanya kundi la walala hoi kuwa kubwa , kuwa , kundi hili ni jeshi kubwa sana la mabadiliko ya kijamii.
Na jeshi hili bado ni nguvu kazi inayoweza kutumiwa vizuri sana kwa manufaa ya jamii yote ua kitanzania, kama mipango ya maendeleo ikiwatumia vizuri.
 
Last edited by a moderator:
Wallet
Mkuu ni vigumu sana ukiwa kundi jingine kuweza kuona ya upande wa pili na yamkiniki wewe hukutoka kt kundi la walalahoi hivyo huwezi kutambua hawa Pnya road wametokana na nini? Ufahamu tu kwamba hawa vijana ni kati ya umri wa miaka 16 hadi 20 ambao wanatakiwa kuwa shule kama ulivyodai lakini wameshindwa vipi kuwa shuleni? sidhani kama umefanya utafiti huo kwanza!

Na hata tukichukulia juu juu tu ya kwamba shule zetu ni za kulipia na zaidi ya hapo hawa ni failure wa mitihani ama mfumo wa Elimu nchini ambao umewaweka katika nafasi hiyo. Hata wale walioko vitani leo kule Syria na wameshika bunduki sio kwamba wao ni majambazi na terrorist isipokuwa kuwepo kwa vita kumewalazimu kuwa wauaji aidha baada ya kushindwa kukimbia nchi yao ama ile ari ya kuitaka amani.

Swala la class struggle nchini sii la kulifanyia mzaha hata kidogo, ni jinamizi linalokua kwa haraka sana na litakuja kutuangamiza sote maana kesho haitakuwa Panya road tena bali jirani yako ambaye kashindwa kujikimu mahitaji yake wakati wewe jirani yake unatanua. na hii imeanza pia kujitokeza maana kwa kila mwenye nacho leo hii hutafuta makazi mapya sehemu ambazo ataipata amani, hivyo amani inaaza kupotea baadhi ya sehemu za makazi yetu hapa hapa mjini.

haya makuzi ya Dar kuwa na maghorofa ni makuzi ya mwili tu, kama vile wewe huwezi kuwa sawa na ulivyokuwa miaka 12, leo umerefuka una ndevu, sharubu, unavaa suruali badala ya kaptula haya sio maendeleo bali makuzi ya mwili na vitu vinavyoendana na makuzi hayo kwa sababu afya yako bado inaweza kuwa dhoofu zaidi, maisha yako ya taabu zaidi ya utoto. Hata ukienda New York leo utaona mabadiliko makubwa zaidi ktk majengo, New York ya mwaka 1990 sio hii ya leo! wala maendeleo sio kuwa na Kentacky fried Chicken au maduka ya bidhaa kutoka nje, sisi ni mateja tu ktk soko la ubepari! Maendeleo ya nchi yetu, ukitazama miundombinu leo ni mibovu kuliko wakati wowote, mirefeji, barabara, reli, ukulima na hata vyanzo vya ajira. Tuna watu wengi wasokuwa na kazi leo kuliko wakati wowote ule na hii ndio alama kubwa ya maendeleo. Panya road ni sehemu kubwa ya kizazi cha wazazi wasiokuwa na ajira na hivyo kilema hicho kinaendelea chini na kuwa mnyororo wa walalahoi ambao kesho na kesho kutwa ndio watakuwa maadui zako!
Panya road ni tahadhali kubwa ya jamii tunayoijenga leo!

Mkuu Mkandara.
Kama kuna changamoto inayo tukabili Waafrika ni kuupuza changamoto kama hii! Si Watawala tu hata wengi wa wananchi wetu wanaona hawahusiki kutafuta ufumbuzi so long as hawa siyo watoto wao,ndugu zao na hawana ujirani nao!

Hata kitisho kilicho kuwa kinasikika ktk mitaa ya masikini kinapoanza kuingia hadi mitaa ya Tabata na Sinza bado wao wanaona hayawahusu! Siku wakivamia mitaa ya Watawala na Matajiri,wanaanza kujiuliza na kufanya operesheni za zimamoto kama kwamba kuna jambo la ghafla ambalo halikujulikana! Akili za baadhi yetu hazina tofauti na akili za nyumbu kule Serengeti!
 
Mkuu Mkandara nashukuru kwa wewe kuchukua muda wako kujaribu kuelimisha on the catostrophe inayoikabili jamii ya kitanzania.

Kwa wananchi wenzetu wa kitanzania kama Wallet waliokua katika mazingira ambayo tungeita spoon fed, hawaelewi kabisa majuto yanayowakabili wananchi walio upande wa wale ma proletariats.

Na tatizo kubwa ni kwamba si tu hawaelewi, lakini ukweli ni keamba hawataki kuelewa kwa kuridhika kuwa watawala walio katika payroll ya the bourgeuoeise watawatetea mpaka mwisho wa uhai wao.

Nina sisitiza kuwa ni vema waliokatika utawala kutambua nguvu kubwa ya wananchi wanaolifanya kundi la walala hoi kuwa kubwa , kuwa , kundi hili ni jeshi kubwa sana la mabadiliko ya kijamii.
Na jeshi hili bado ni nguvu kazi inayoweza kutumiwa vizuri sana kwa manufaa ya jamii yote ua kitanzania, kama mipango ya maendeleo ikiwatumia vizuri.
Nami nasikitika bado hutaki kunielewa. Post yangu pamoja na kunipa like lakini bado tu unazunguka? Nikijibu pamoja na hoja ya @Mkandara ni kwamba hao panya road ni tone tu la mnayoyaona na kuyasikia ndani ya nchi hii. Panya road tumeanza kuwasikia juzi tu, tena wapo dar tu. Kumekuwa na matukio mengi sana yanaoashiria kuwepo kwa hali ya kujichokea kimaisha kwa wananchi. Mauaji ya vikongwe na albino, uchunaji wa ngozi, madawa ya kulevya, vurugu za maandamano ya kisiasa, na mauaji, umalaya na ushoga, ufisadi, na mengine kama hayo. Sasa tukizungumzia kwa hawa panya kama base yetu tunakosea. Hapo ndio ugomvi wangu.

Nimeorodhesha katika post yang ya mwisho jinsi mikakati mbalimbali ilivyoshindwa kufanya kazi, tatizo likiwa ni kuamini katika nadharia za wazungu ambazo zimeshindikana kutekelezeka. Kusema tu kwamba kundi hili inapaswa kutumiwa kwa manufaa ya jamii bado haujaleta suluhu. Ni sawa na kumwambia mwenye njaa, katafute chakula ule ushibe. Unajua chanzo cha njaa yake? Pengine ni pesa.

Panya road wanadhibitika na wanajulikana. MAdawa ya kulevya je? ushoga, ufisadi je? Ukiniambia ni solusheni gani kwa haya matatizo ya sasa nitakuambia tubadili mfumo wa uongozi wa sasa. Hakuna kitakachofanyika kamwe kama hawa ndio wataendelea kuongoza Taifa hili. Panya road na kadhia zingine ni zao la ubovu wa uongozi uliopo. Halafu inasikitisha kuona na kusikia kuwa mji mzima ulitikisika kutokana na 'hasira' za hao vijana.

NB: Mimi ni mtu wa maisha ya kawaida sana ninayefukuzana na tonge la siku kama wengine.
 
Nami nasikitika bado hutaki kunielewa. Post yangu pamoja na kunipa like lakini bado tu unazunguka? Nikijibu pamoja na hoja ya @Mkandara ni kwamba hao panya road ni tone tu la mnayoyaona na kuyasikia ndani ya nchi hii. Panya road tumeanza kuwasikia juzi tu, tena wapo dar tu. Kumekuwa na matukio mengi sana yanaoashiria kuwepo kwa hali ya kujichokea kimaisha kwa wananchi. Mauaji ya vikongwe na albino, uchunaji wa ngozi, madawa ya kulevya, vurugu za maandamano ya kisiasa, na mauaji, umalaya na ushoga, ufisadi, na mengine kama hayo. Sasa tukizungumzia kwa hawa panya kama base yetu tunakosea. Hapo ndio ugomvi wangu.

Nimeorodhesha katika post yang ya mwisho jinsi mikakati mbalimbali ilivyoshindwa kufanya kazi, tatizo likiwa ni kuamini katika nadharia za wazungu ambazo zimeshindikana kutekelezeka. Kusema tu kwamba kundi hili inapaswa kutumiwa kwa manufaa ya jamii bado haujaleta suluhu. Ni sawa na kumwambia mwenye njaa, katafute chakula ule ushibe. Unajua chanzo cha njaa yake? Pengine ni pesa.

Panya road wanadhibitika na wanajulikana. MAdawa ya kulevya je? ushoga, ufisadi je? Ukiniambia ni solusheni gani kwa haya matatizo ya sasa nitakuambia tubadili mfumo wa uongozi wa sasa. Hakuna kitakachofanyika kamwe kama hawa ndio wataendelea kuongoza Taifa hili. Panya road na kadhia zingine ni zao la ubovu wa uongozi uliopo. Halafu inasikitisha kuona na kusikia kuwa mji mzima ulitikisika kutokana na 'hasira' za hao vijana.

NB: Mimi ni mtu wa maisha ya kawaida sana ninayefukuzana na tonge la siku kama wengine.
Mkuu hujajibu swala kwa sababu unatazama mambo yote kwa mpigo Generalize wakati kila kero ina sababu zake japo yote yanaweza kutokana na ugumu wa maisha. hayo mengine yote uloyataja yapo hata nchi zilizoendelea na zenye unemployment ndogo ukiacha hayo maswala ya imani za kichawi maana hili halihusiani na vijana kukosa ajira.

Swala la panya road halikuanza jana, lipo siku nyingi na cheche zake zimeshaanza kuwa moto japo umeshika nyumba moja (Dar) lakini itafika wakati hawa panya road wataingia mikoani. Kwani hata maradhi iwe kipindupindu huanza mahala fulani (epidemic) ukasambaa nchi nzima na kuwa (pandemic) hapo tena ndio nchi haitatawalika kama tutachukulia mambo jinsi unavyoyatazama. Panya road wanaathiri jamii moja kwa moja kwa kutaka mapanga watu huwezi kuifananisha na Umalaya ama ufisadi!

hatutaki kufika huko ikiwa tunaelewa tatizo hili llinatokana na nini kwani ile vita yetu dhidi ya maradhi, umaskini na ujinga imeishia wapi? kweli imefikia watu tunasema hao watoto hawataki kwenda shule kwa sababu tu sisi wanetu wanaenda shule kutokana na uwezo wetu mzuri? Hivi kweli wewe kama huna uwezo huyo mwanano ataweza vipi kujisomesha! au hujatazama huko!

Imekuwa wao ni kundi fulani tena tunasema dogo wakati leo dunia nzima iunapiga kelele na kundi dogo sana la ma terrorist kwa sanbabu linatishia amani ya watu. Panya road sii swala dogo ukadhania ni vijana walokosa kazi wameamua kutishia amani ya watu, inabidi kwanza ujiulize hawa vijana wasokuwa na kazi wako asilimia ngapi ya jamii hii hasa hawa wa umri wa miaka 18 hadi 30 ukilipata jibu rudi tujadili...
 
Mkandara
si kwamba nataka kujumlisha mambo. waungwana wanasema bora mchawi kuliko mnafiki. hawa watoto ni wachawi tu. hivi ufisadi haufui dafu kwa hawa vijana? vijana waliosoma na wakakosa ajira hawawezi kuwekwa kundi la panya road. machinga watabaki kuitwa machinga. kila kundi lina sababu zake na namna yake ya kukabiliana nalo. suluhu ya educated jobless huwezi kuiapply kwa panya road. halafu umesema nagemeralize wakati umefamya the same, kutaka tuamini kuwa hata machinga ni pamya road.

so what is the way forward?
 
Nakubaliana na hoja zako ikiwa pamoja na suluhisho ulilopendekeza.Lakini ingependeza zaidi serikali kama ingechukua hatua za haraka, kati na za muda mrefu kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili.Tusijisifu kwa kukamata na kuripoti idadi ya waliokamatwa kama tulivyoona jana Polisi wakisema wamefikisha 900 za zaidi.Idadi ya watuhumiwa(Panya Road) haiwezi wanavyojiita,haiwezi kusifiwa kwa utendaji hata kidogoJe hao wote ni wahusika wa mtandao wa Panya Road?Jibu ni hapana.Wamo wasamaria ambao hawakushiriki kwa namna yoyote ile,ila kwa sababu hawana kazi lazima waende vijiweni.
Lakini lazima tuheshimu uhuru wa mtu kwenda popote anapotaka (freedom of movement).Hii ni haki KIKATIBA.Jana niliandika kwenye thread yangu "hili ni bomu lililosemwa na baadhi ya wana siasa wengi lakini walipuuzwa na mawaziri wanaohusika na ajira hivi karibuni"Kukamata siyo suruhu ya matatizo,bali serikali itafute njia ya kutatua suala hili kwani vijana hao wametumia jina la Panya Road ili wasikilzwe haraka.Aidha serikali igawanye rasimali (keki) za taifa kwa uwiano sawa,kwa maana ya kwamba vijana hao wasikae bure kusubiri maisha bora kwa kila mtanzania wakati wao hawayaoni.Serikali imetuweka kwenye vicious cycle of poverty, bomu limeanza kulipuka,tuchukue hatua za haraka kukabiliana nao.Tusitafute populality kwa kutangaza idadi waliokamatwa,ukizingatia magereza yamejaa,lakini pia kodi zetu zitatumika kuhudumia idadi hiyo badala ya kupelekwa kwenye mambo ya msingi kuleta maendeleo tunayoyatarajia.

 
Mkandara
si kwamba nataka kujumlisha mambo. waungwana wanasema bora mchawi kuliko mnafiki. hawa watoto ni wachawi tu. hivi ufisadi haufui dafu kwa hawa vijana? vijana waliosoma na wakakosa ajira hawawezi kuwekwa kundi la panya road. machinga watabaki kuitwa machinga. kila kundi lina sababu zake na namna yake ya kukabiliana nalo. suluhu ya educated jobless huwezi kuiapply kwa panya road. halafu umesema nagemeralize wakati umefamya the same, kutaka tuamini kuwa hata machinga ni pamya road.

so what is the way forward?

I think i get where you are coming from. Panya road isiwe basis ya kuelezea matatizo ya Taifa hili sio? Kwani mbali yao tumeona tatizo hili likipata expression kuanzia hata hizo ngazi za juu. Mfano ufisadi, ukosefu wa uwajibikaji, vitendo vya rushwa iliyokithiri, ukiukwaji wa haki za binadamu na mengineyo.
Kwahiyo in a sense hii lawlessness ipo katika level zote, ni kuwa tu inatisha ikijidhihirisha kwa vijana wadogo walioshika mapanga na kudhuru lakini uhalifu huo huo unafanywa na walio juu na madhara yanachukua expression kwenye vifo vya wagonjwa wanaokosa huduma mahospitalini, elimu duni, miundo mbinu mibovu n.k
Hakuna class struggle kwakweli. The only struggle tunayoiona ni dhidi ya vivuli vyetu wenyewe. Theories za akina Karl Max hazitasaidia Taifa letu kwakweli.
 
Mkandara
si kwamba nataka kujumlisha mambo. waungwana wanasema bora mchawi kuliko mnafiki. hawa watoto ni wachawi tu. hivi ufisadi haufui dafu kwa hawa vijana? vijana waliosoma na wakakosa ajira hawawezi kuwekwa kundi la panya road. machinga watabaki kuitwa machinga. kila kundi lina sababu zake na namna yake ya kukabiliana nalo. suluhu ya educated jobless huwezi kuiapply kwa panya road. halafu umesema nagemeralize wakati umefamya the same, kutaka tuamini kuwa hata machinga ni Pamya road.

so what is the way forward?
Kuna mahala nimeandika Machinga ni panya road?..mkuu tunazungumzia swala la panya road na nini sababu za vijana hawa kuchukua hatua kama hizi? na ndipo tunasema pasipo sisi kuwahukumu wao kwanza ni muhimu tutazame sababu na hakika unemployment ndio chanzo cha yote haya. Hujaniuliza chanzo ama sababu za Mafisadi, Malaya au wauza unga nikapinga, ila wewe unachukulia imani yako kuwa sin is the sin haijalishi upo katika mazingira gani.

Kumbuka tu kuharibika kwa vijana huaanzia nyumbani, na hata hao mafisadi na malaya kuna mazingira yalokuwepo ndio chanzo!hakuna mtu alozaliwa fisadi, malaya au muuza unga ni kutokana na maisha na mazingira aliyopo mtu huyo. panya road sii swala la malezi mabaya ama wahalifu tu, bali ugumu wa maisha toka nyumbani kwao husababisha kizazi cha aina hii na tusipoangalia tutakuwa na Panya road kila mkoa kila wilaya na kadhalika.

Sasa sikuelewi wewe unaona vigumu vipi kuamini kwamba hawa watoto wameshindwa kwenda shule kutokana na mfumo wa elimu uliopo. Wameshindwa kwenda shule kutokana na uwezo mdogo wa wazazi wao na hivyo wao kuwa kizazi cha fukara wa kutupwa ktk mji wenye matunda kama Dar. Nina hakika ukiwakusanya nna kuwapeleka camp ya shule ya kijeshi basi hawa hawa watatokea kuwa wawajibikaji na waadilifu.

Hawa vijana wanayaona maedeleo ya watu wengine, wanaona jinsi mnavyojirusha na ufahari wa kubebana, kwao inawaingia hasira ambayo wewe na mimi hatuwezi kuitambua kama hatupo ktk viatu walivyovaa na rahisi kuwanyooshea kidole na kusema uloyasema lakini mkuu wangu hujafa hujaumbika! criminals mara zote hufanya mambo kwa kupanga dhidi ya sheria aidha peke yao ama na washirika lakini genge la watu wanapoingia mjini na kufanyiza pasipo kuchagua jua hizo ni hasira, hawa hawafikiri wala hawaogopi sheria!

Hawa watoto wanatakiwa kuangaliwa na sio kuadhibiwa kwa sababu wapo wengi mfano wao, kama alianza wazo hili mmoja wao leo tuna kundi zima na kesho watakuwa maelfu. Wazo huanza na mtu mmoja tu likawagusa wengi na ndio haya ya Panya road. Hiki sio kizazi tofauti na wewe bali ni baina yako isipokuwa are less fortune kutokana na mfumo uliotugawa kwa wenye nacho na wasionacho. Na kwa bahati mbaya sana kuna kundi kubwa la wasionacho ambao hawapati hata mlo mmoja kwa siku hawatazamwi kabisa kama sehemu ya jami hii!..
 
Kuna mahala nimeandika Machinga ni panya road?..mkuu tunazungumzia swala la panya road na nini sababu za vijana hawa kuchukua hatua kama hizi? na ndipo tunasema pasipo sisi kuwahukumu wao kwanza ni muhimu tutazame sababu na hakika unemployment ndio chanzo cha yote haya. Hujaniuliza chanzo ama sababu za Mafisadi, Malaya au wauza unga nikapinga, ila wewe unachukulia imani yako kuwa sin is the sin haijalishi upo katika mazingira gani.

Kumbuka tu kuharibika kwa vijana huaanzia nyumbani, na hata hao mafisadi na malaya kuna mazingira yalokuwepo ndio chanzo!hakuna mtu alozaliwa fisadi, malaya au muuza unga ni kutokana na maisha na mazingira aliyopo mtu huyo. panya road sii swala la malezi mabaya ama wahalifu tu, bali ugumu wa maisha toka nyumbani kwao husababisha kizazi cha aina hii na tusipoangalia tutakuwa na Panya road kila mkoa kila wilaya na kadhalika.

Sasa sikuelewi wewe unaona vigumu vipi kuamini kwamba hawa watoto wameshindwa kwenda shule kutokana na mfumo wa elimu uliopo. Wameshindwa kwenda shule kutokana na uwezo mdogo wa wazazi wao na hivyo wao kuwa kizazi cha fukara wa kutupwa ktk mji wenye matunda kama Dar. Nina hakika ukiwakusanya nna kuwapeleka camp ya shule ya kijeshi basi hawa hawa watatokea kuwa wawajibikaji na waadilifu.

Hawa vijana wanayaona maedeleo ya watu wengine, wanaona jinsi mnavyojirusha na ufahari wa kubebana, kwao inawaingia hasira ambayo wewe na mimi hatuwezi kuitambua kama hatupo ktk viatu walivyovaa na rahisi kuwanyooshea kidole na kusema uloyasema lakini mkuu wangu hujafa hujaumbika! criminals mara zote hufanya mambo kwa kupanga dhidi ya sheria aidha peke yao ama na washirika lakini genge la watu wanapoingia mjini na kufanyiza pasipo kuchagua jua hizo ni hasira, hawa hawafikiri wala hawaogopi sheria!

Hawa watoto wanatakiwa kuangaliwa na sio kuadhibiwa kwa sababu wapo wengi mfano wao, kama alianza wazo hili mmoja wao leo tuna kundi zima na kesho watakuwa maelfu. Wazo huanza na mtu mmoja tu likawagusa wengi na ndio haya ya Panya road. Hiki sio kizazi tofauti na wewe bali ni baina yako isipokuwa are less fortune kutokana na mfumo uliotugawa kwa wenye nacho na wasionacho. Na kwa bahati mbaya sana kuna kundi kubwa la wasionacho ambao hawapati hata mlo mmoja kwa siku hawatazamwi kabisa kama sehemu ya jami hii!..
Kumbe tunajua kuwa tatizo ni mfumo? Haya, juzi kuna (nadhani) vijana waliandamana kwenda ikulu ( si wale wa magunia) kumwona Rais. Hawa walipelekwa kambi na kufundushwa mbinu kadha wa kadha na stadi za kazi na mwisho wa siku wakatoswa, sasa wakawa wanaenda kwa Rais kuhoji kulikoni. Hakuna mikakati yakini ya kuweza kukabiliana na haya yote. Tutabaki kuwaonea huruma tu hawa vijana na mwisho wa siku ni hatua gani zitachukuliwa? Pia kubaki kuamini tu kuwa hawa waoto hawakupata fursa tutakuwa hatujitendeai haki. Hivi ukishaona hali imekuwa taiti ndio uchukue mapanga na bisi bisi kwenda kukata wenzio kisa yeye anacho na mimi sina? Hivi kijana anayeosha magari na kuuza mitumba na kuendesha bodaboda wana tofatti kubwa na hao panya road kwa maana ya kukosa fursa wakati fulani? Kwa nini hawa wawe wahalifu na hawa wengine wajiajiri kwenye biashara ndogo ndogo? Hapo hakuna sababu ya kumtetea mhalifu. Tusisahau pia kuna Mungu. Wanayotenda ni haki? Kwa nini basi tuwatetee?

Umegusia malezi. Bila shaka utakubaliana nami kuwa hata kama kulikuwa na ugumu wa maisha, wazazi walipaswa kuwalea vyema. Kama wazazi walikosea kuwalea tuwalaumu vipi tena wenye nacho? Wenye shida zao ni wengi kuliko hilo kundi la panya lakini wanahangaika mchana na usiku kujipatia riziki halali. Hao panya ni kundi fulani lililoamua kujipatia riziki zao kwa njia hizo na ni njia si halali. Bahati mbaya hata huko jela wanakopelekwa hawatajifunza chochote kulingana na hali halisi. Hebu tubadili mfumo uliopo kwanza ndipo tuone kama kweli panya road wataendelea ama la.
 
Kulikuwa na "panyaroad" hata wakati wa siasa za ujamaa za Nyerere. Uchumi wa kiujamaa na wa kibepari wote ulileta "have" na "have not".

Kwa mfano, wafanyabiashara wengi wa asili ya kihindi au kiarabu hawajateseka sana kama Wazawa Wakati wa ujamaa kwenye mahitaji ya kula. Wafanyakazi wengi wa serikali pia waliweza kupata Mlo kutokana na rushwa. Hawa Ndio waliokuwa "have" katika siasa ya ujamaa. Hata Urusi, hamna ofisa wa serikali alilala njaa. Ni wananchi wasiokuwa na connection. Pamoja na njaa kali iliyoikabili Tanzania ya Nyerere, maofisa wake wote walitumia connection zao kupata unga na Sukari Ugawaji. Mali za wananchi, hasa wenye asili ya kihindi au kiarabu, walipewa "wakubwa" sio Wananchi ,kama alipotaifisha Raisi wa Zimbabwe. Hawa ndio "have" wa Tanzania ya ujamaa wa Nyerere.

Karl Max aliandika vizuri kuhusu hili swala la class struggle lakini hali halisi ya binadamu na theories ni vitu viwili tofauti . Binadamu amezaliwa kujitafutia rizki Yake kwanza Kabla hajamsaidia mwenzake. Kama hajashiba haweza kumshibisha mwenzake. Hii ndio sababu muhimu siasa ya kiujamaa ilifeli.

Kuna umasikini mkali katika nchi za kibepari pia. Lakini serikali inasaidia kwa kuwapa chakula, nyumba za bei nafuu, masomo na tiba bure. Pia nchi za Scandinavia zinajaribu kupunguza masikini (have not) kwa kutoza ushuru mkubwa kwa wafanyabiashara wake iwasaidie wananchi wa Hali ya chini. Norway au Finland biashara hulipa Mpaka asilimia 60 au 70 ya fedha zao serikali ni lakini wanapata matibabu mazuri na wanaangaliwa vizuri na serikali zao. Pengine no rahisi kufanya hivyo kwa kuwa ni nchi Tajiri yenye watu wachache. Kanada pia huwapa wananchi tiba bure lakini wanalipa income tax kubwa kuliko Marekani ambapo tiba bure ni kwa ajili ya watu wachache tu.

Kwa kuwa Tanzania ni nchi masikini, itachukua mda mpaka masikini wapate nafuu kimaisha hata kama hongo ikipungua. Uzalishaji ni mdogo mno kuleta maendeleo haraka haraka. Mpaka pale ambapo tutakuwa na viwanda vya kuzalisha Mali kama magari, kompyuta, na kadhalika, masikini hawatapungua. Elimu yetu pia ni hafifu. Barabara, maji na umeme pamoja na rushwa ni janga la maendeleo. Elimu Kwanza ni Nzuri kwa kulisha mwananchi sio kutajirisha nchi. Hamna hata nchi Moja duniani iliyotajirika kwa kuuza mazao tu.

Utajiri hauhitaji nchi kuwa na Mali ardhini. Singapore , Korea ,Hong Kong, Japan na Taiwan Hawana Mafuta wala gesi. Wana elimu . Wana wananchi wanaochapa kazi masaa 24. Wananumua chuma nchi masikini na wanawauzia chuma zao wenyewe katika magari yao kwa faida kubwa.

Uswisi wanategemea fedha za wageni kuendesha uchumi wao. Matajiri wanaamini Sheria zao na serikali yao inalinda fedha zao makini. Wanakopesha fedha za matajiri na kuwapeleka watoto wao chooni. Hawana asilimali yoyote zaidi ya milima, siasa bora na tulivu na bila kusahau fedha za wizi za akina Mobutu.

Wazungu wananunua kahawa yetu gunia la Kilo 60 sio zaidi ya dola 100. Wanatuuzia kikombe Kimoja cha kahawa yetu dola 3 Starbucks.

Nionavyo mimi, maendeleo yapo sasa kuliko Wakati wa Nyerere .Wazawa wana viwanda sasa. Wazawa wanatajirika. Wazawa wanasafiri na kusoma zaidi. Wazawa wanaishi nje kwa wingi. Umasikini hautaisha leo wala kesho lakini kila nchi ikitajirika, serikali itaweza kuwasaidia wananchi wake wa Hali ya chini. Kinachotakiwa ni serikali ya busara na Nguvu mpya ya wananchi kujisomesha Masomo ya kileo, kufanya kazi kwa bidii na kuzalisha Mali wanazoweza kuuza kwa wingi kwa faida kubwa.

Gari jipya la kawaida la Kijapani kama Toyota Corolla Lina faida kama dola 3000 kwa Toyota. Itachukua magunia mangapi ya kahawa au karafuu kwa mkulima kupata faida ya $3000. Ukijua jibu, utajua muda utakaochukua kuleta maendeleo kwa wote Tanzania.

My 2 cents .
Mkuu, nimeipitia kwa karibu maoni yako ambayo kiujumla yapo sahihi.
Tutakapotofautiana ni mtazamo wa suala la umasikini na jinsi ya kuutatua.
Mtazamo wako kwa Utawala wa Mwalimu si sahihi, kwa vile unazungumzia wakati ule wa "kufunga mikanda" baada ya vita ya Kagera.
Ule ulikuwa wakati wa matatizo maalum yaliyogusa kila sekta ya nchi, kuanzia viwanda, utawala hadi huduma mashuleni ,mahospitalini na hata kwenye ajira na sekta ya fedha.
Ni wakati ule ambapo wengi hawakumbuki, lakini inflation ilikuwa zaidi ya 30%!!
Inabidi turudi nyuma kuona kuwa sera za Mwalimu bado zilikuwa na relevance.
Kimsingi sera za Mwalimu zilikuwa pro masikini, sera zilizomjali mtu wa hali ya chini kuliko wale waliotangulia kiuchumi na kimaendeleo kiujumla.
Hivyo basi pamoja na kwamba sera za Mwalimu haziko sawa na za Karl Marx, zina shabihiana katika namna ya kutatua tatizo kati ya masikini na matajiri.

Tukikumbuka Siasa ya Ujamaa na kujitegemea, Mwalimu ali anza na mtazamo kuwa ili maendeleo yapatikane, tunahitaji kuzingatia yafuatayo,
  • Maendeleo ya watu, kama resource
  • siasa lazima iwe inclusive kwa watu wote, na iwe safi
  • ardhi na umiliki wake lazima uwe wa umma
  • Uongozi lazima uwe bora na utokane na watu wenyewe
Mkuu na hapo ndo mambo yalianza, aidha kwa kukanganyika au kama yangeendelezwa vizuri, Tanzania ya leo ingekuwa tofauti kabisa.
Kwa kuendeleza rasilmali watu, elimu ilipewa kipaumbele sana kuliko kitu kingine chochote.
Na huo ulikuwa mkakati vile vile wa kuondoa umasikini.

Mwalimu alidiriki kutaifisha shule zote za dini, vyama vya ushirika na kujenga nyingine.
Elimu ikwa bure, I mean BURE KABISA, kwa mtu aliyejitahidi kusoma.
Watu kama kina Kikwete wamesomea shule nyingine za mission, na wamesoma bure kabisa hadi chuo kikuu.
Hili lisingewezekana kama ungekuwepo ubaguzi wa kidini, na rangi milango ilifunguliwa.
Milango ambayo ingekuwa closed , fursa ya elimu ya bure isingekuwepo kwao.
Na viongozi wengi waliopo madarakani sasa ni wale waliofaidika na mfumo huu wa elimu wa Mwalimu.

Kwa kuendana na siasa ya ujamaa na kujitegemea, Mwalimu alitaifisha na kuziweka njia kuu za uchumi chini ya umma.
Hili ni suala litakalobisganiwa kwa miaka mingi sana ijayayo.
Hata hivyo nia iliyokuwapo ilikuwa kujitengenezea an economic base kiinchi.

Tatizo kubwa tulilolipata ni commitment ya huo uongozi na drive ya kuperform.
Viongozi wanapenda na kuridhika sana "kubebwa bebwa na kuendelezwa" kuliko kujiendeleza wenyewe kwa kujitegemea.
Mawaziri wanadiriki kusema sisi watanzania ni wa kujifanyia mambo madogo madogo tu , yale makubwa tuwasubiri wakubwa au mjomba.
Statements kama za kina Muhongo ni hatari kwa maendeleo ya taifa, tunashindwa hata ku copy and adapt kama wezetu wanaoiba kwa nguvu siri za mafanikio ya wengine.

Kuna wanao argue kuwa tatizo ni ownership, lakini mimi nasema mbona China wameshikilia msimamo huo wa state economy kwa miongo sasa na matunda yake ndiyo wanayaona sasa, they are an economic giant.
Tanzania ya miaka ya 1960s haikuwa tofauti sana na China ya miaka hiyo.
Na hata kampuni karibu zote za China zinazokuja kufanya biashara nchini kwetu, iwe za ujenzi, uundaji magari etc, ni za serikali.

Umasikini hata hivyo wakati wa Mwalimu ulikuwepo, lakini si kwa kiwango tunachokiona sasa.
Na tofauti za kipato haikuwa kubwa kama ilovyo sasa.
Mishahara iliratibiwa ili kipato kilingane katika sekta ya umma.

Tatizo kubwa la kwetu watanzania ni uvivu, wa kufikiri na hata wa utendaji.
Tunapenda kupata Big Results bila kufanya kazi, na kwa kumtegemea mjomba atakayeleta mitaji toka nje.

Uwezo wa kujitengenezea mikakati ya maendeleo yatakayoweza kubadilisha uchumi wetu na wa watoto wetu, tunao.
Tatizo hatuna uthubutu wala ujasiri wa kujitegemea , na hili litawezekana ikiwa tu tutakuwa na mipango endelevu ya miaka mingi ijayo.

China wameweza, sisi tunashindwa nini.
 
Kumbe tunajua kuwa tatizo ni mfumo? Haya, juzi kuna (nadhani) vijana waliandamana kwenda ikulu ( si wale wa magunia) kumwona Rais. Hawa walipelekwa kambi na kufundushwa mbinu kadha wa kadha na stadi za kazi na mwisho wa siku wakatoswa, sasa wakawa wanaenda kwa Rais kuhoji kulikoni. Hakuna mikakati yakini ya kuweza kukabiliana na haya yote. Tutabaki kuwaonea huruma tu hawa vijana na mwisho wa siku ni hatua gani zitachukuliwa? Pia kubaki kuamini tu kuwa hawa waoto hawakupata fursa tutakuwa hatujitendeai haki. Hivi ukishaona hali imekuwa taiti ndio uchukue mapanga na bisi bisi kwenda kukata wenzio kisa yeye anacho na mimi sina? Hivi kijana anayeosha magari na kuuza mitumba na kuendesha bodaboda wana tofatti kubwa na hao panya road kwa maana ya kukosa fursa wakati fulani? Kwa nini hawa wawe wahalifu na hawa wengine wajiajiri kwenye biashara ndogo ndogo? Hapo hakuna sababu ya kumtetea mhalifu. Tusisahau pia kuna Mungu. Wanayotenda ni haki? Kwa nini basi tuwatetee?

Umegusia malezi. Bila shaka utakubaliana nami kuwa hata kama kulikuwa na ugumu wa maisha, wazazi walipaswa kuwalea vyema. Kama wazazi walikosea kuwalea tuwalaumu vipi tena wenye nacho? Wenye shida zao ni wengi kuliko hilo kundi la panya lakini wanahangaika mchana na usiku kujipatia riziki halali. Hao panya ni kundi fulani lililoamua kujipatia riziki zao kwa njia hizo na ni njia si halali. Bahati mbaya hata huko jela wanakopelekwa hawatajifunza chochote kulingana na hali halisi. Hebu tubadili mfumo uliopo kwanza ndipo tuone kama kweli panya road wataendelea ama la.
Mkuu wangu hakuna mtu anayewatetea Panya road kwa uhalifu wanaoufanya isipokuwa tunazungumzia njia ama mbinu za kuokoa Taifa hili lisijeangamia maaa hawa ndio taifa la kesho! Mkuu Somalia ilianza hivi hivi na vijana wadogo kuanza kuchukua silaha against serikali yao, yametokea Uganda pia na yule muuaji kuwatumia vijana kama hawa kujiunga dhidi ya serikali. Mifano ni mingi na kuwasweka ndani haiwezi kuondoa FIKRA zao. mandela aliswekwa ndani kwa miaka 20, wakaitwa magaidi na kweli ANC walifanya Uhalifu kwa jicho la kaburu lakini makaburu hawakutazama chanzo.

Nachojaribu kukwambia nasi tusiwe kama kaburu, tutazame chanzo na kisha tutafute suluhisho ndio sababu ya kusema AJIRA ndio chanzo. Mkuu tumekuwa hapa JF miaka tukizungumzia mbinu za kupambanan a Ufisadi, madawa ya kulevya, Ubwanyenye na kadhalika na binafsi siamini kama kuwasweka ndani wahalifu ndio solution isipokuwa tutazame kiini chake. Wahalifu sio virus ama bacteria ni WATU.

Hivyo, Ufisadi una chanzo na dawa yake sio jela maana Jela ni hukumu baada ya Uhalifu kutendeka, Madawa ya kulevya yana chanzo na njia za kuzuia zipo, jela haijakomesha na wala haitakomesha kwa sababu utakuwa una deal na baada ya kitendo. Vivyo hivyo uhalifu mwingineo lakini katika swala hili na Panya road lazima tukubali kwamba ukosefu wa ajira ni chanzo cha kuwasha cheche hizi za uhalifu. Ukiweza kuzalisha ajira uhalifu utapungua na sheria inakuwa na nafasi yake pande zote.

Labda nikwambie tu ya kwamba wapo watu wanaweza kukata mapanga mgoni alomfumania lakini sio mimi wala wewe cha kujiuliza sisi ni kwa nini uhalifu huo umetokea? tunakuta kumbe kuna uhalifu ulotangulia wa mtu katembea na mkewe/mumewe hivyo kuhalamisha mtu kutembea na mke/mume wa mtu ktk ndoa zao inaweza kupunguza ghadhabu za watu na kuipa nafasi sheria. na hao vijanna walokwenda kumuona rais kesho watakuwa Panya road tusipolifanya swala hili kuwa muhimu maana hawa ndio taifa la kesho!

Siwapongezi watu wanaofanya uamuzi wa kuua kwa hasira zao bali nachosema mimi tusikurupuke kwanza tutazame chanzo chake na kama mfumo uliopo unahalalisha kuwatupa vijana kama hawa kama masalia basi hizi ndizo athari zake.. Sijui kama umenielewa...
 
quote_icon.png
By SoNotorious

Tatizo wewe binafsi ndio umekuwa meza ya hiari ambayo hawa ma-architect wa huu mfumo wameweka drawing board yao. Hiki unachokiandika ni unafiki na machozi ya mamba kwa panya road.

Matatizo kama tunayoyaona ni lazima yashughilikiwe kisomi.
They must be viewed from the abstract, drawing board ni muhimu maana all the facts na matrix za solutions zinawekwa mezani.
Na ndio maana ya usomi.

SoNotorious alikuwa na maana kwamba misimamo yako ya kuunga mkono utawala wa sasa hivi imemaanisha kwamba unakubaliana na matokeo ya sera za utawala huu, ambayo ndio hayo unayoyajadili. Contradiction?

Mimi nadhani inabidi turudi mwanzo kabisa, kujiuliza ajira kuu ya watanzania ni ipi, na tuanzie wapi. siyo rahisi kutekeleza hayo kwa sababu watu wameonja asali na wamejipanga katika kushika nchi hii. watatumia kila aina ya mbinu kuhakikisha kwamba wanabaki madarakani.
 
Matatizo kama tunayoyaona ni lazima yashughilikiwe kisomi.
They must be viewed from the abstract, drawing board ni muhimu maana all the facts na matrix za solutions zinawekwa mezani.
Na ndio maana ya usomi.

Kulikuwa na "panyaroad" hata wakati wa siasa za ujamaa za Nyerere. Uchumi wa kiujamaa na wa kibepari wote ulileta "have" na "have not".

..........................

Nionavyo mimi, maendeleo yapo sasa kuliko Wakati wa Nyerere .Wazawa wana viwanda sasa. Wazawa wanatajirika. Wazawa wanasafiri na kusoma zaidi. Wazawa wanaishi nje kwa wingi. Umasikini hautaisha leo wala kesho lakini kila nchi ikitajirika, serikali itaweza kuwasaidia wananchi wake wa Hali ya chini. Kinachotakiwa ni serikali ya busara na Nguvu mpya ya wananchi kujisomesha Masomo ya kileo, kufanya kazi kwa bidii na kuzalisha Mali wanazoweza kuuza kwa wingi kwa faida kubwa .

Sidhani kama umefanya utafiti vizuri. kwamba Tanzania iliyokuwa na viwanda vingi enzi hizo, ajira nyingi, nyumba za wafanyakazi, mabasi ya kupeleka na kurudisha wafanyakazi, klabu za michezo kazini, viwanda vilivyotegemeana - linganisha na sasa hivi ambapo kila kitu kinatoka nje, viwanda vilivyobinafsishwa vinatumia inputs nyingi zaidi kutoka nje - halafu unaniambia kwamba hali ni nzuri zaidi?? kuna maendeleo ya "vitu" ambayo kwangu mimi hayo siyo maendeleo.

Ukiongelea upande wa vijijini ndio kabisa. mkulima alikuwa anamdharau mfanyakazi anayetegemea mshahara. mkulima alikuwa strong. siyo sasa hivi ambapo hali imeharibika kabisa huko vijijini ambapo asilimia kubwa ya watanzania ndio wapo huko.
 
good analysis masopakyindi. huu ndio ukweli ambao maCCM hawapendi kuusikia.
Mkuu pamoja na pongezi zako, sijawahi kusikia sera shirikishi za vyama vingine. Sera zinazoweza kumkomboa mTanzania kutokana na lindi la umasikini na hasa kuwashikisha vijana katika uchumi endelevu.
 
Sidhani kama umefanya utafiti vizuri. kwamba Tanzania iliyokuwa na viwanda vingi enzi hizo, ajira nyingi, nyumba za wafanyakazi, mabasi ya kupeleka na kurudisha wafanyakazi, klabu za michezo kazini, viwanda vilivyotegemeana - linganisha na sasa hivi ambapo kila kitu kinatoka nje, viwanda vilivyobinafsishwa vinatumia inputs nyingi zaidi kutoka nje - halafu unaniambia kwamba hali ni nzuri zaidi?? kuna maendeleo ya "vitu" ambayo kwangu mimi hayo siyo maendeleo.

Ukiongelea upande wa vijijini ndio kabisa. mkulima alikuwa anamdharau mfanyakazi anayetegemea mshahara. mkulima alikuwa strong. siyo sasa hivi ambapo hali imeharibika kabisa huko vijijini ambapo asilimia kubwa ya watanzania ndio wapo huko.

Mkuu. Katika sera ya Ujamaa ajira ni muhimu kuliko faida. Ndio maana ukakuta watu watatu wanafanya kazi ya Mtu mmoja, thus, ajira nyingi.

Pili, hivyo viwanda kama vilikuwa na faida na kuzalisha kwa wingi, kwa nini vitu vilikuwa adimu? Si unakumbuka resheni?

Kama mkulima alikuwa "Strong" kwa nini mchele na unga ilikuwa adimu?

Hamna kiwanda kinachotumia input ya nyumbani tu. Viwanda vya Ujamaa vilitumia mashine za kirusi na kichina. Wafanyakazi wake pia walitumia ujuzi waliofundishwa huko. Hizi sio input za nje? Tulitengeneza matrekta wenyewe kusaidia wakulima?

Kama leo hukai mstari kusuburi resheni yako ya chakula, unasema leo tuko nyuma zaidi? Je, Uhuru wa fikra? Uhuru wa kusoma, Haki za binadamu tulipata pia?

Uzalishaji wa Tanzania leo ni dola bilioni 40. Tanzania ya Ujamaa pamoja na viwanda vingi unavyovidai vilizalisha kiasi gani?
 
Mkuu, nimeipitia kwa karibu maoni yako ambayo kiujumla yapo sahihi.
Tutakapotofautiana ni mtazamo wa suala la umasikini na jinsi ya kuutatua.
Mtazamo wako kwa Utawala wa Mwalimu si sahihi, kwa vile unazungumzia wakati ule wa "kufunga mikanda" baada ya vita ya Kagera.
Ule ulikuwa wakati wa matatizo maalum yaliyogusa kila sekta ya nchi, kuanzia viwanda, utawala hadi huduma mashuleni ,mahospitalini na hata kwenye ajira na sekta ya fedha.
Ni wakati ule ambapo wengi hawakumbuki, lakini inflation ilikuwa zaidi ya 30%!!
Inabidi turudi nyuma kuona kuwa sera za Mwalimu bado zilikuwa na relevance.
Kimsingi sera za Mwalimu zilikuwa pro masikini, sera zilizomjali mtu wa hali ya chini kuliko wale waliotangulia kiuchumi na kimaendeleo kiujumla.
Hivyo basi pamoja na kwamba sera za Mwalimu haziko sawa na za Karl Marx, zina shabihiana katika namna ya kutatua tatizo kati ya masikini na matajiri.

Tukikumbuka Siasa ya Ujamaa na kujitegemea, Mwalimu ali anza na mtazamo kuwa ili maendeleo yapatikane, tunahitaji kuzingatia yafuatayo,
  • Maendeleo ya watu, kama resource
  • siasa lazima iwe inclusive kwa watu wote, na iwe safi
  • ardhi na umiliki wake lazima uwe wa umma
  • Uongozi lazima uwe bora na utokane na watu wenyewe
Mkuu na hapo ndo mambo yalianza, aidha kwa kukanganyika au kama yangeendelezwa vizuri, Tanzania ya leo ingekuwa tofauti kabisa.
Kwa kuendeleza rasilmali watu, elimu ilipewa kipaumbele sana kuliko kitu kingine chochote.
Na huo ulikuwa mkakati vile vile wa kuondoa umasikini.

Mwalimu alidiriki kutaifisha shule zote za dini, vyama vya ushirika na kujenga nyingine.
Elimu ikwa bure, I mean BURE KABISA, kwa mtu aliyejitahidi kusoma.
Watu kama kina Kikwete wamesomea shule nyingine za mission, na wamesoma bure kabisa hadi chuo kikuu.
Hili lisingewezekana kama ungekuwepo ubaguzi wa kidini, na rangi milango ilifunguliwa.
Milango ambayo ingekuwa closed , fursa ya elimu ya bure isingekuwepo kwao.
Na viongozi wengi waliopo madarakani sasa ni wale waliofaidika na mfumo huu wa elimu wa Mwalimu.

Kwa kuendana na siasa ya ujamaa na kujitegemea, Mwalimu alitaifisha na kuziweka njia kuu za uchumi chini ya umma.
Hili ni suala litakalobisganiwa kwa miaka mingi sana ijayayo.
Hata hivyo nia iliyokuwapo ilikuwa kujitengenezea an economic base kiinchi.

Tatizo kubwa tulilolipata ni commitment ya huo uongozi na drive ya kuperform.
Viongozi wanapenda na kuridhika sana "kubebwa bebwa na kuendelezwa" kuliko kujiendeleza wenyewe kwa kujitegemea.
Mawaziri wanadiriki kusema sisi watanzania ni wa kujifanyia mambo madogo madogo tu , yale makubwa tuwasubiri wakubwa au mjomba.
Statements kama za kina Muhongo ni hatari kwa maendeleo ya taifa, tunashindwa hata ku copy and adapt kama wezetu wanaoiba kwa nguvu siri za mafanikio ya wengine.

Kuna wanao argue kuwa tatizo ni ownership, lakini mimi nasema mbona China wameshikilia msimamo huo wa state economy kwa miongo sasa na matunda yake ndiyo wanayaona sasa, they are an economic giant.
Tanzania ya miaka ya 1960s haikuwa tofauti sana na China ya miaka hiyo.
Na hata kampuni karibu zote za China zinazokuja kufanya biashara nchini kwetu, iwe za ujenzi, uundaji magari etc, ni za serikali.

Umasikini hata hivyo wakati wa Mwalimu ulikuwepo, lakini si kwa kiwango tunachokiona sasa.
Na tofauti za kipato haikuwa kubwa kama ilovyo sasa.
Mishahara iliratibiwa ili kipato kilingane katika sekta ya umma.

Tatizo kubwa la kwetu watanzania ni uvivu, wa kufikiri na hata wa utendaji.
Tunapenda kupata Big Results bila kufanya kazi, na kwa kumtegemea mjomba atakayeleta mitaji toka nje.

Uwezo wa kujitengenezea mikakati ya maendeleo yatakayoweza kubadilisha uchumi wetu na wa watoto wetu, tunao.
Tatizo hatuna uthubutu wala ujasiri wa kujitegemea , na hili litawezekana ikiwa tu tutakuwa na mipango endelevu ya miaka mingi ijayo.

China wameweza, sisi tunashindwa nini.

Mkuu nashukuri kwa kutumia muda wako kunipa feedback.

Mimi naamini kuwa lengo la Nyerere lilikuwa zuri sana la kujiendeleza lakini siamini kuwa siasa yake ya Ujamaa na Kujitegemea ingewatoa Watanzania katika umasikini na kuwaletea maendeleo kwa wote. Hapa ndio kuna upingamizi.

Pili, vita vya kagera vilianza miaka kumi baada ya yeye kuishika nchi. Kama Ujamaa ungekuwa na maendeleo, yangejionyesha.

Tatu, kumfuata Nyerere ni kumfuata Dikteta. Siwezi kufuata sera za Kiongozi ambaye hajanipa haki ya kumchagua. Pia, Elimu chini yake haikuwa elimu huru. Hata wananchi kama wamesoma bure, haki ya kufikiri ilikuwa hamna. Maoni ninayoyaandika leo hapa yangenipeleka kifungoni wakati wa Ujamaa.

Nne, sikubaliani kuwa mashirika ya umma ya Ujamaa yana uwezo wa kuzalisha kwa faida zaidi kuliko viwanda binafsi. Siasa ilikuwa mbele kuliko faida. Japokuwa lengo la Nyerere lilikuwa kuleta usawa, binadamu hakuzaliwa na lengo hilo. Hawezi kumshibisha mwenzake kabla yake.

Viwanda vilifilisika sio kutokana na viongozi wabovu ila kutokana na sera za Kijamaa za kutoheshimu faida. Pia, uchumi wa Tanzania ulikuwa mdogo. Hata leo, japokuwa uchumi unakua, tunazalisha $40 bilioni tu, wakati Nigeria pamoja na historia yake ya vita vya Biafra na kuendeshwa kijeshi miaka mingi, wanazalisha $500 bilioni.

Kwa kuwa wananchi walibanwa kuzalisha kibepari, kulikuwa hamba mzunguko wa fedha wa kuzalisha mali zaidi na kuipatia serikali mapato.

Tano, China ni Mjamaa kwa jina tu na waliporuhusiwa kujenga viwanda binafsi na Deng Xioping ( Getting rich is Glorious alisema) walijenga kwa kasi mno. Pia ukumbuke uwezo wao wa kifedha kama raia ni mkubwa kuliko sisi. Wao wana ndugu wengi nchi za kitajiri kukopa kufanya biashara na wamejisomesha vya kutosha na kuona faida ya sera za kibepari kwa ndugu zao Hong Kong, Macau , Singapore na Malaysia.

Sisi uchumi wetu, uwezo wa kifedha wa wananchi wetu na elimu yetu haikuwa sawa. Itakuwa kama unafananisha tufaha na chungwa. Biashara zao hata za umma zinaendeshwa kibepari. Wanafunzi wa Kichina ndio wanafunzu wa kigeni namba Moja vyuoni Marekani.

Naungana na wewe kuwa Watanzania ni wavivu wa kazi na fikra. Tunapenda kulalamika tu. Tunataka bure, spoon fed. Leo Mtanzania ana haki ya kufanya biashara yoyote lakini haifanyi mpaka aje mgeni. Leo ana uwezo wa kumchagua Kiongozi, lakini aidha hapigi kura au anachagua viongozi fisadi kwa kuwa amehongwa pesa na doti moja ya kanga. Wenzetu wanafanya maandamo na kuwatimua viongozi wabovu.

Nawakilisha.
 
Mkuu pamoja na pongezi zako, sijawahi kusikia sera shirikishi za vyama vingine. Sera zinazoweza kumkomboa mTanzania kutokana na lindi la umasikini na hasa kuwashikisha vijana katika uchumi endelevu.

Kwa hiyo unashauri nini kifanyike?
 
Back
Top Bottom