The inevitable class struggle between the haves and the have nots...!

The inevitable class struggle between the haves and the have nots...!

Hata hapa kwangu napoishi, muda mfupi uliopita tulikuwa tunazungumzia swala hili na mwanamama mmoja na nikamueleza chanzo kimojawapo cha matukio kama haya ni watu kukosa ajira na kukata tama.

Bahati mbaya sana,kama ilivyo kwa wana-CCM wengi,mama huyu alipinga hoja yangu na kutoa sababu zake kama vijana kuvuta bangi n.k.

Huyu mama angekuwa na akili angejiuiliza kwanza ni kwanini vijana hawa wavute bangi n.k.

Najua kuna wengine hata akiwa na maisha mazuri kuvuta bangi na mambo ya aina hiyo ndio hulka yake.Lakini je,wote hawa kwa makumi au mamia wanafanya vitendo kama hivi kutokana na hulka zao tu?

Polisi kama wana akili,vijana waliowakamata wawahoji kistaarabu ili wawape sababu za wao kufanya walioyafanya na taarifa wazipeleke serikalini kwa utatuzi kama tunataka haya yasijirudie tena.Tofauti na hapo ni kujidanganya tu.

In short,civil disobedience in our country is around the corner.
Hili tatizo la Panya Road liko juu ya uwezo wa Polisi peke yao kulitatua.
Kwanza hakuna polisi wa kutosha kuwadhibiti vijana hawa kama wakiamua kuingia barabarani na kuanza kupora kama ilivyoonekana majuzi.
Hili ni swala la kulitatua kimipango zaidi na kimkakati ili kwa muda mrefu sana ujao vijana hawa waajirike au wajiajiri ili nguvu yao itumike kwa manufaa kwao na kwa nchi.
 
Asilimia kubwa ya makundi mengi ya uhalifu duniani kote ni mazao ya unyonyaji na ukandamizaji,hili huwa linafichwa kwa propaganda kali kwenye vyombo vya habari.
Jamii yoyote isiyo na usawa,taifa lolote lisilojali mgawanyiko sahihi na stahiki wa utajiri wake kwa wenye nchi ni dhahiri haya lazima yajitokeze.
Viongozi wetu wanalijua hili lakini wameweka pamba masikioni kwa sababu ya ubinafsi utadhani madhara yake hayatavigusa vizazi vyao vijavyo.
 
Wenye nacho watakwambia Panya Roads ni Wahuni tu,Wazembe wa kutopenda kufanya kazi ila kupora Mali.Hawalioni Tatizo la ajira wao kila kitu ni ktk Mtizamo wa Kisiasa tu.

Wasio nacho kwa upande wa pili wanaliona tatizo la Panya Roads kama kushindwa kwa serikali kuweka mikakati ya kuwawezesha vijana.

Wanaina serikali ya CCM chini ya Rais Jakaya Imewatelekeza vijana na watanzania kwa ujumla, Maisha bora kwa kila Mtanzania waliyoahidiwa yameyeyuka ka barafu na Kuacha simanzi ya Sintofahamu kwa Vijana.

Vijana wanasema Serikali ya CCM imewatapeli na Kilichobaki kwa sasa ni Hasira zao kwa CCM 2015, watakapokuwa wakifanya maamuzi yenye busara,kwa Kuzijaribu sera za UKAWA zenye kulejesha matumaini ya kushiriki kufaidi Keki ya Taifa, ambayo kwa sasa ni Kwa matajiri na Wanasisa Uchwara ( wapiga dili).
 
Very true mkuu!!
Inasikitisha kuwa watu hawaendani na utatuzi wa yanayotukabili kitaalam
In actual fact we are sowing the seeds of our own social disharmony.

Mipango yetu haiwafikirii wanyonge the we expect the best!!!!
mipango yetu ya kisiasa na kiuchumi ina matatizo ambayo sasa ni kama ina fuel social conflicts.
Very good...umeandika maneno mazito sana mkuu....inaonyesha jinsi gani ulivyojawa na shauku ya kuiona TANZANIA MPYA........tutafika tu hata kwa mwendo wa konokono ili tu tunasonga mbele na sio nyuma na mapambano yanaendelea.....ALUTA CONTINUA...........
 
Social stratification is inevitable in capitalist world! Ila inapokuwa imejijenga katika misingi ya kinyonyaji na kikandamizaji ndipo matatizo yanapoanzia, matabaka yana manufaa in survival of any society lakini tabaka moja likiwa linamiliki na kufaidi mema yote ya nchi migogoro haitoepukika, our country needs intensive reformation unless....
 
Kwanza kundi hili mm nasema kwa risasi ni kama mtu anaumwa kichwa ukampa panadoh. Ukifanya hivyo utakuwa unapunguza maumivu na si kutibu, na ndiyo yanayofanywa na serikali. Kuna kundi kubwa sana tena ni jeshi ambalo liko nyuma ya hii kitu nalo ni ukosefu wa ajira. Vijana wengi wanamaliza darasa la saba,kidato cha nne,cha Sita na wengine wana shahada zao. Jambo lililo wazi ni kwamba elimu yetu haiwaandai vijana wetu kujiajiri zaidi ya kutafuta ajira Maofisini. Tutatumia siraha kuwatuliza hawa vijana lakini tatizo liko pale pale, haiondoi uhalisia wa kwamba vijana wanapokosa namna yoyote wanaanza kujiingiza kwenye biashara za ajabu kama madawa ya kulevya n.k

Tufanye nini?

1. Nashukuru Nacte, na TCU wameanza kupiga hatua kidogo yaani kuviamrisha taasisi za elimu kuanza mara moja kutengeneza mitaala itakayowafanya vijana kujiajiri na si kutegemea kuajiriwa tu.

2. Vyuo vyetu vya kilimo havina nguvu kama zamani,hata wanasoma wanafikiria kukaa ofisi ni wakati wanasomea kilimo...lazima tujaribu kuvirudisha vifanane na uhalisia

3. Vyuo vyetu vya biashara kama C.B.E na vingine lazima vianze kufundisha mambo yenye uhalisia kwa asilimia 50 na nadharia iwe asilimia 59. Maana yangu ni kwamba kwa muhula mmoja wawe wanakaa darasani mwingine waende kufanya vitendo itasaidia sana. Na hili jambo limetuasili kwa sababu tumefungwa na U Max,Lenin, uliberali na Ujamaa bila kuangalia mahitaji yetu ya msingi kama Taifa.

4. Taasisi ziongezwe vijijini zitakazoweza kuhudumia au kupokea wasomi wetu kama kilimo,biashara,ufundi n.k

5. Vyuo vyetu vya ufundi viimarishwe na tusing'ang'anie ufundi aw magari hata uashi, kutengeneza vifanane vidogo vidogo vinavyotumiwa na jamii kwa wingi kama sahani,vyakula kama mikate tufundishane kwa sana

6. Soko holera nalo ni changamoto kubwa ni lazima lizibitiwe.

7. Na cha msingi tuelekee kwenye kupunguza umasikini maana ndiyo changamoto kubwa sana.
 
Hujapatia sana chanzo na hitimisho lako. Kwanza, ubepari haukwepeki kabisa bali unatakiwa kusimamiwa kwa vigezo vilivyo wazi na kukubalika kwa wote. Vigezo hivyo ni pamoja na vile vinavyotoa fursa na haki sawa kwa wote huku maadili na sheria vikisimamiwa kwa uwazi na bila kuyumbishwa na chochote kile (blind justice). Aidha, uchumi wa kibepari unaoendeshwa inavyostahili na kwa uwazi, huwatupi kabisa wasiojiweza; hujitahidi kuimarisha huduma za kijamii kama vile za afya na elimu ya msingi kiasi cha kuweza kuwafikia wote. Cha muhimu zaidi, wananchi wakiona mambo yanaeleweka; fursa zipo na zinatolewa kwa haki; matumizi ya rasilimali yako wazi na jitihada za kuhakikisha kuwa zinachangia vilivyo katika ustawi wao zinafanyika - hawapati taabu na tofauti zilizoko kati ya vipato na tofauti za madaraja ya utajiri binafsi.

Kilichopo Tanzania leo hii sio mfumo wa ubepari bali ni kleptocracy (sijui neno sahihi kiswahili). kwa kifupi, ni kuwa uchumi wetu unaendeshwa kwa kutegemea matakwa ya walioko madarakani. Hao ndio wenye kauli ya mwisho. Wanaweza kujitahidi kuonyesha kuwa wanafuata sheria na taratibu (ambavyo navyo vinapindishwa kirahisi) lakini wanachotaka ndicho hatimaye huwa. Wizi wa mali ya umma na rushwa ni mambo ya kawaida. Katika mazingira hayo, uwazi haupo, fursa, haki vinategemeana na ukaribu wako na watawala, ukubwa wa mfuko wako na utayari wa kugawa vijisenti. Falsafa maarufu ni za "mtu kula mezani kwake", "mtu kula kulingana na urefu wa kamba yake", n.k.

Hakuna class struggle ya ukweli hapo. Kinachotutokea ni vurugu zinazotokana na kukosekana kwa uongozi kukiambatana na mfumo uliokithiri wizi na rushwa vikichochewa na unafiki na ubinafsi uliopitiliza (blind greed) wa wengi wetu. Nadhani wanaojali kwa dhati mustakabali wa Taifa hili wamepungua sana. Panya road ni viashiria tu vya kupotea kwa mwelekeo katika jamii hii.
 
Huu uzi ungetakiwa uwe na page zaidi ya arobaini....kutokana na hali halisi ya hapa nchini mwetu...Watanzania ni kama tuna mitindio wa ubongo.....bado watu wanajionea sawa tu kwa namna mambo yanavyoendeshwa nchini...wanajionea kuwa umaskini na dhiki zinazotukabili ni mipango ya Mungu..na wameamua kumuachia mungu....wakati Mungu kawapa ufahamu wa kuyatafakali mambo kwa kina.....
Watanzania wengi vichwa vyetu tumevielekeza kwenye mahaba na umbea pekee....huu uzi kama ungekuwa wa mapenzi au unamzungumzia mtu flani sasa hivi ungekuwa kwenye page ya mia na......
Bado tuna safari ndefu sana kuelekea ukombozi wa mtanzania...kibaya zaidi hata mfumo mzima wa elimu yetu inatufanya tuzidi kuwa kama mazezeta kwa kuwa hautupi tafakuli na maarifa ya kujiuliza maswali ya msingi yanayotugusa...zaidi kukariri vya kujibia mtihani na kukabidhiwa vyeti vizuri huku kichwani kukiwa hakuna maarifa.....
MABADILIKO YA NCHI YETU YANAANZA NA MIMI NA WEWE.....

Unachosema mkuu ni kweli kabisa, watanzania wengi ni kama wana mtindio wa ubongo, wabongo wengi wanafatilia mambo ya kijinga tu, mahaba, umbea, vitu visivyowahusu na mambo ya kijinga kijinga tu, na kundi hili ni kubwa sana ambalo linameza mpaka wasomi ambao nao elimu yao imeshindwa kuwasaidia mpaka nao wakajikuta wanaingia kwenye mkumbo huo, yaani hawa wasomi ndio ovyo kabisa sasa hivi huwezi kuona tofauti ya form 4 na graduate, nafikiriaga sana nashindwa kupata jibu, mpaka nafikiria ingekuwa km unaweza kupata kazi bila ya vyeti mi nisingesoma, pia hii mpaka inasababisha watu wengi kufoji vyeti vya degree kwa sababu uki-interview mwenye degree ya ukweli na mwenye ya kufoji hamna tofauti.
Kutokana na hayo wabongo kila jambo tunafanya masihara na kulifanya rahisi hata km ni jambo muhimu (mfano suala la ufisadi tumelichukulia masihara sana mpaka limekuwa rahisi kiasi kwamba mtu anayefanya ufisadi anaondoa uwoga), wanasiasa na mabepari kwa makusudi wanatufanya tuwe hivyo na tuendelee kuwa hivyo ili waendelee kutuburuza.
Unajua inakera sana basi tu.
 
Wenye nacho watakwambia Panya Roads ni Wahuni tu,Wazembe wa kutopenda kufanya kazi ila kupora Mali.Hawalioni Tatizo la ajira wao kila kitu ni ktk Mtizamo wa Kisiasa tu.

Wasio nacho kwa upande wa pili wanaliona tatizo la Panya Roads kama kushindwa kwa serikali kuweka mikakati ya kuwawezesha vijana.

Wanaina serikali ya CCM chini ya Rais Jakaya Imewatelekeza vijana na watanzania kwa ujumla, Maisha bora kwa kila Mtanzania waliyoahidiwa yameyeyuka ka barafu na Kuacha simanzi ya Sintofahamu kwa Vijana.

Vijana wanasema Serikali ya CCM imewatapeli na Kilichobaki kwa sasa ni Hasira zao kwa CCM 2015, watakapokuwa wakifanya maamuzi yenye busara,kwa Kuzijaribu sera za UKAWA zenye kulejesha matumaini ya kushiriki kufaidi Keki ya Taifa, ambayo kwa sasa ni Kwa matajiri na Wanasisa Uchwara ( wapiga dili).
Ni kweli hili jambo la Panya Rd lazima litazamwe kwa nia ya kutatua matatizo yanayojitokeza katika jamii.
Haiwezekani kuna watu wachache wenye kugawana mabilioni wakijidiai ETI hela si ya umma , na wengine wanakufa kwa njaa na magonjwa ya kutibika kwa vidonge ambavyo havipatikani hospitalini.

Somebody, somewhere is NOT working.
Na hao Panya Road lazima waelekezwe kwenda huko.
 
Very good...umeandika maneno mazito sana mkuu....inaonyesha jinsi gani ulivyojawa na shauku ya kuiona TANZANIA MPYA........tutafika tu hata kwa mwendo wa konokono ili tu tunasonga mbele na sio nyuma na mapambano yanaendelea.....ALUTA CONTINUA...........
Mkuu kwa kweli lazima tuione Tanzania YOTE kama watanzania.
Haipendezi kuona kuna wananchi wanashindwa kupata huduma za lazima kutokana na muundo wa uchumi ulivyo, tukiendelea na muundo uliopo tunajitengenezea an underclass inayoweza kuleta mapinduzi ya kudai hako zao tupende tusipende.
 
Hujapatia sana chanzo na hitimisho lako. Kwanza, ubepari haukwepeki kabisa bali unatakiwa kusimamiwa kwa vigezo vilivyo wazi na kukubalika kwa wote. Vigezo hivyo ni pamoja na vile vinavyotoa fursa na haki sawa kwa wote huku maadili na sheria vikisimamiwa kwa uwazi na bila kuyumbishwa na chochote kile (blind justice). Aidha, uchumi wa kibepari unaoendeshwa inavyostahili na kwa uwazi, huwatupi kabisa wasiojiweza; hujitahidi kuimarisha huduma za kijamii kama vile za afya na elimu ya msingi kiasi cha kuweza kuwafikia wote. Cha muhimu zaidi, wananchi wakiona mambo yanaeleweka; fursa zipo na zinatolewa kwa haki; matumizi ya rasilimali yako wazi na jitihada za kuhakikisha kuwa zinachangia vilivyo katika ustawi wao zinafanyika - hawapati taabu na tofauti zilizoko kati ya vipato na tofauti za madaraja ya utajiri binafsi.

Kilichopo Tanzania leo hii sio mfumo wa ubepari bali ni kleptocracy (sijui neno sahihi kiswahili). kwa kifupi, ni kuwa uchumi wetu unaendeshwa kwa kutegemea matakwa ya walioko madarakani. Hao ndio wenye kauli ya mwisho. Wanaweza kujitahidi kuonyesha kuwa wanafuata sheria na taratibu (ambavyo navyo vinapindishwa kirahisi) lakini wanachotaka ndicho hatimaye huwa. Wizi wa mali ya umma na rushwa ni mambo ya kawaida. Katika mazingira hayo, uwazi haupo, fursa, haki vinategemeana na ukaribu wako na watawala, ukubwa wa mfuko wako na utayari wa kugawa vijisenti. Falsafa maarufu ni za "mtu kula mezani kwake", "mtu kula kulingana na urefu wa kamba yake", n.k.

Hakuna class struggle ya ukweli hapo. Kinachotutokea ni vurugu zinazotokana na kukosekana kwa uongozi kukiambatana na mfumo uliokithiri wizi na rushwa vikichochewa na unafiki na ubinafsi uliopitiliza (blind greed) wa wengi wetu. Nadhani wanaojali kwa dhati mustakabali wa Taifa hili wamepungua sana. Panya road ni viashiria tu vya kupotea kwa mwelekeo katika jamii hii.
Asante kwa kuchangia mada hii na kuitazama from an abstract point of view.
Haya ndo mawazo mbadala ambayo ningependa kujadiliana nayo mtandaoni.

Hiyo ni licha ya kwamba sikubaliani moja kwa moja na mawazo haya.

Tukubali kuwa sasa hivi kuna matabaka yanayojitokeza kutaokana na uwezo wa kipato na hata kiuongozi.
Na hapa siongelei chama wala itikadi, hizi zinazoanza kujitokeza ni social dynamics.

Kutokana na tofauti zilizopo katika classes za kipato (socioeconomic interests), makundi haya ni lazima yatakinzana.
Na yatakinzana kwa sababu mwenye kipato cha juu, kwake mtu wa kipato cha chini ni just an expendable labour resource.
The driving force kwa mfano sasa hivi kwa the ruling class, economic driving force ni pripitive accumultaion of wealth.
Primitive in the sense kuwa kuna wafanya biashara/viongozi wanaiba, wanapata faida kwa rushwa, wanauza rasilmali isivohhalali(wanyama mbugani), wanafilisi mali za umma-EPA etc.

wakati huo huo mtu masikini na wa kipato cha chini struggle zake zinasukumwa na magonjwa, mishahara midogo isiyokidhi , ukosefu wa makazi, kukosa kazi,vifo vinavyoweza kuzuilika n. k.

Hivyo basi ukisema hakuna class struggle wakati tunaona low level conflicts ambazo hatukuwahi kuziona nchini zinajitokeza kwa kasi, ni kuto appreciate kuwa class struggle ipo na inaendelea kwa kasi.
Mifano ni mingi
Tuna Panya Road, tuna mapigano ya wafugaji na wakulima, wafanya biashara ya mabasi wanaua wananchi kila kukicha-to maximise profits,proloiferation of squatters etc

This class conflict is seen to occur primarily between the bourgeoisie and the proletariat, and takes the form of conflict over hours of work, value of wages, division of profits, cost of consumer goods, the culture at work, control over parliament or bureaucracy, and economic inequality.
(Wiki)

Hizi ndo dalili zenyewe kuwa tunakoenda ni bomu, tena kubwa tu.
 
Mkuu kwa kweli lazima tuione Tanzania YOTE kama watanzania.
Haipendezi kuona kuna wananchi wanashindwa kupata huduma za lazima kutokana na muundo wa uchumi ulivyo, tukiendelea na muundo uliopo tunajitengenezea an underclass inayoweza kuleta mapinduzi ya kudai hako zao tupende tusipende.

Yaani viongozi wa Bongo ni hopeless kabisa, wanapenda kutafuta "kindergarten answers to intercontinental questions" na sio kuwa wanafanya hivyo wakiwa hawajui, wanajua fika ila ni kwa makusudi/maslahi binafsi

Na sasa hivi hao panya road wataanza kushika na silaha za moto na kuanza kupambana na watu wenye vinyumba vyao vya kudunduliza huko mbezi, tabata, tegeta. Ukionekana una kigari chako cha mkopo na wewe unawekwa kwenye target, wafanye nini sasa wakati wao kesho yao hawaijui???

Mfano mzuri ni South Africa, wanaionja joto ya jiwe kwaajili ya hizi class za jamii
 


Hivi kama hawa huwa wanaishia wapi? au how much does it take to influence to do something evil considering only he know the survival of the fittest. Mtoto keshabakwa, keshatumiwa vya kutosha kwa namna moja ama nyingine, ukute kesha lazimishwa kuiba tayari au kufanya shoplift na hana pa kukimbilia akiwa mdogo, utamwambia nini ukubwani wakati bado fursa hana.

Ingawa serikari inaweza kuwa na majukumu ya asilimia 70% na sisi kama jamii tuna majukumu ya kuwaelimisha marafiki zetu wasio nacho uzazi wa mpango, tuna majukumu ya kuishinikiza serikari kuchukua hatua za kutatua kero, tunamajukumu ya kuchangia taasisi za misaada ili waongeze huduma wanazotoa, tuna majukumu ya kuchagua viongozi wenye muono wa kero za jamii.

It is a matter of time before proper gangs are formed ambapo vijana wanaishi by the code. Si kwamba ni maajabu kwa sababu hali inapofikia pabaya hayo ndio madhara yake.

Kwakweli lazima viongozi wetu wajipime kama kweli changamoto za leo wanaziweza, hata ukiacha hawa watoto wa mtaani hali ya umaskini kwa Tanzania inatisha basi tu wengine utapeli wa hapa na pale kwa ndugu, jamaa na marafiki unapeleka siku.


Moja ya wasiwasi wangu mkubwa ni kuibuka makundi ya uhalifu ambao itafika wakati vyombo vya usalama vinaogopa kwenda ktk baadhi ya maeneo. Panya road wataungana na wasomi wasio kuwa na ajira kuunda Gangs za hatari. Hatuko mbali kufikia hapo. Na wale wanaodhani kuta ndefu zinazo zunguka nyumba zao na mbwembwe za walinzi zitawasaidia watakuwa wamekosea sana!

Inasikitisha kwamba hata fursa muhimu za kuonyesha wananchi wetu kwamba bado kuna utawala unaojali zinapo jitokeza watawala wetu wanavurunda na kubaki kulinda tabaka lao. Angalia walivyo dhalilisha Maoni ya Wananchi ktk kuandika Katiba pendekezwa. Angalia danadana zinaendelea kuwalinda akina Muhongo na wezi walio kwapua pesa za Escrow Stanbic bank!
 
Last edited by a moderator:
Asante kwa kuchangia mada hii na kuitazama froma an abstract point of view.
Haya ndo mawazo mbadala ambayo ningependa kujadiliana nayo mtandaoni.

Hiyo ni licha ya kwamba sikubaliani moja kwa moja na mawazo haya.

Tukubali kuwa sasa hivi kuna matabaka yanayojitokeza kutaokana na uwezo wa kipato na hata kiuongozi.
Na hapa siongelei chama wala itikadi, hizi zinazoanza kujitokeza ni social dynamics.

Kutokana na tofauti zilizopo katika classes za kipato (socioeconomic interests), makundi haya ni lazima yatakinzana.
Na yatakinzana kwa sababu mwenye kipato cha juu, kwake mtu wa kipato cha chini ni just an expendable labour resource.
The driving force kwa mfano sasa hivi kwa the ruling class, economic driving force ni pripitive accumultaion of wealth.
Primitive in the sense kuwa kuna wafanya biashara/viongozi wanaiba, wanapata faida kwa rushwa, wanauza rasilmali isivohhalali(wanyama mbugani), wanafilisi mali za umma-EPA etc.

wakati huo huo mtu masikini na wa kipato cha chini struggle zake zinasukumwa na magonjwa, mishahara midogo isiyokidhi , ukosefu wa makazi, kukosa kazi,vifo vinavyoweza kuzuilika n. k.

Hivyo basi ukisema hakuna class struggle wakati tunaona low level conflicts ambazo hatukuwahi kuziona nchini zinajitokeza kwa kasi, ni kuto appreciate kuwa class struggle ipo na inaendelea kwa kasi.
Mifano ni mingi
Tuna Panya Road, tuna mapigano ya wafugaji na wakulima, wafanya biashara ya mabasi wanaua wananchi kila kukicha-to maximise profits,proloiferation of squatters etc

Hizi ndo dalili zenyewe kuwa tunakoenda ni bomu, tena kubwa tu.

Mkuu Masopakyindi sijakataa jumla unachosema. Aidha, kwa kukosoa uongozi wa nchi naweza kuonekana kirahisi nimeingiza siasa za vyama; kama vile nakishambulia chama kilichoko madarakani. Sivyo kabisa. Wasiwasi wangu mkubwa sana kuhusu Tanzania leo hii ni ule utamaduni tulioujenga kwa miaka mingi wa kuchukulia madaraka kama njia ya kuinua uchumi binafsi wa mtu badala ya taifa. Sidhani kama unahitaji kuelezwa kuwa hata biashara kubwa Tanzania zinahusishwa na ukaribu na walioko madarakani. Kwamba usipokuwa na madaraka au kuwa karibu na wenye nayo si rahisi ukafika mbali kibiashara (nikiweka utani: utaishia kunadi juisi na matunda - tena mitaani!).

Mtazamo wangu wa dhati kabisa, si kwa chama kilichoko madarakani tu, hata vikija vingine naona uwezekano wa kujikuta tukiendelea na mfumo wa "kleptocracy" ni mkubwa sana. Leo hii nikiwatizama Watanzania wengi wanaowania nafasi za uongozi (wa vyama vyote) naona wanasukumwa zaidi na mtazamo wa "sasa ni zamu yetu kula". Wapo wanaonishawishi kuwa wanajitoa kwa taifa - kama alivyojanya JKN (pamoja na mapungufu yake ya kimkakati). Lakini ni wachache sana. Na naheshimu sana uwezo mkubwa wa binadamu kulaghai kikamilifu (ultimate deception capacity).

Kwa upande wetu kama jamii, SIJUI kama itakuwa rahisi kufuta mtazamo uliojengeka sana wa kuwaona viongozi kama miungu (wakiwa juu ya sheria na taratibu). Kunahitajika "mapinduzi" makubwa hasa kurejesha uwajibikaji kwa viongozi nchini ukichukulia kwamba kiwango cha unafiki na ubinafsi katika jamii ni kikubwa sana. Atakayefanikiwa kuchukua uongozi wa nchi (chama chochote) akiwa na ajenda ya dhati ya aina hiyo basi naona huyo awe tayari kupoteza umaarufu mapema sana, awe tayari kupoteza marafiki na hata ndugu na kutawala kipindi kimoja tu. Zaidi ya hapo, awe tayari kuwa mtu mpweke sana. Naomba sana niwe NIMEKOSEA katika mtazamo wa aina hii. I really wish to be completely wrong!

Kwa vyovyote vile, nisingependa sana kuchukulia mpambano unaosababishwa na tofauti za kiuchumi zinazotokana na mfumo wa wizi/rushwa katika tabaka la watawala (kleptocracy) kama kielelezo cha genuine class struggle. Kwangu mimi hizo ni vurugu zitokanazo na uongozi mbovu.
 
Asante kwa kuchangia mada hii na kuitazama from an abstract point of view.
Haya ndo mawazo mbadala ambayo ningependa kujadiliana nayo mtandaoni.

Hiyo ni licha ya kwamba sikubaliani moja kwa moja na mawazo haya.

Tukubali kuwa sasa hivi kuna matabaka yanayojitokeza kutaokana na uwezo wa kipato na hata kiuongozi.
Na hapa siongelei chama wala itikadi, hizi zinazoanza kujitokeza ni social dynamics.

Kutokana na tofauti zilizopo katika classes za kipato (socioeconomic interests), makundi haya ni lazima yatakinzana.
Na yatakinzana kwa sababu mwenye kipato cha juu, kwake mtu wa kipato cha chini ni just an expendable labour resource.
The driving force kwa mfano sasa hivi kwa the ruling class, economic driving force ni pripitive accumultaion of wealth.
Primitive in the sense kuwa kuna wafanya biashara/viongozi wanaiba, wanapata faida kwa rushwa, wanauza rasilmali isivohhalali(wanyama mbugani), wanafilisi mali za umma-EPA etc.

wakati huo huo mtu masikini na wa kipato cha chini struggle zake zinasukumwa na magonjwa, mishahara midogo isiyokidhi , ukosefu wa makazi, kukosa kazi,vifo vinavyoweza kuzuilika n. k.

Hivyo basi ukisema hakuna class struggle wakati tunaona low level conflicts ambazo hatukuwahi kuziona nchini zinajitokeza kwa kasi, ni kuto appreciate kuwa class struggle ipo na inaendelea kwa kasi.
Mifano ni mingi
Tuna Panya Road, tuna mapigano ya wafugaji na wakulima, wafanya biashara ya mabasi wanaua wananchi kila kukicha-to maximise profits,proloiferation of squatters etc

This class conflict is seen to occur primarily between the bourgeoisie and the proletariat, and takes the form of conflict over hours of work, value of wages, division of profits, cost of consumer goods, the culture at work, control over parliament or bureaucracy, and economic inequality.
(Wiki)

Hizi ndo dalili zenyewe kuwa tunakoenda ni bomu, tena kubwa tu.

Mkuu Masopakyindi sijakataa jumla unachosema. Aidha, kwa kukosoa uongozi wa nchi naweza kuonekana kirahisi nimeingiza siasa za vyama; kama vile nakishambulia chama kilichoko madarakani. Sivyo kabisa. Wasiwasi wangu mkubwa sana kuhusu Tanzania leo hii ni ule utamaduni tulioujenga kwa miaka mingi wa kuchukulia madaraka kama njia ya kuinua uchumi binafsi wa mtu badala ya taifa. Sidhani kama unahitaji kuelezwa kuwa hata biashara kubwa Tanzania zinahusishwa na ukaribu na walioko madarakani. Kwamba usipokuwa na madaraka au kuwa karibu na wenye nayo si rahisi ukafika mbali kibiashara (nikiweka utani: utaishia kunadi juisi na matunda - tena mitaani!).

Mtazamo wangu wa dhati kabisa, si kwa chama kilichoko madarakani tu, hata vikija vingine naona uwezekano wa kujikuta tukiendelea na mfumo wa "kleptocracy" ni mkubwa sana. Leo hii nikiwatizama Watanzania wengi wanaowania nafasi za uongozi (wa vyama vyote) naona wanasukumwa zaidi na mtazamo wa "sasa ni zamu yetu kula". Wapo wanaonishawishi kuwa wanajitoa kwa taifa - kama alivyojanya JKN (pamoja na mapungufu yake ya kimkakati). Lakini ni wachache sana. Na naheshimu sana uwezo mkubwa wa binadamu kulaghai kikamilifu (ultimate deception capacity).

Kwa upande wetu kama jamii, SIJUI kama itakuwa rahisi kufuta mtazamo uliojengeka sana wa kuwaona viongozi kama miungu (wakiwa juu ya sheria na taratibu). Kunahitajika "mapinduzi" makubwa hasa kurejesha uwajibikaji kwa viongozi nchini ukichukulia kwamba kiwango cha unafiki na ubinafsi katika jamii ni kikubwa sana. Atakayefanikiwa kuchukua uongozi wa nchi (chama chochote) akiwa na ajenda ya dhati ya aina hiyo basi naona huyo awe tayari kupoteza umaarufu mapema sana, awe tayari kupoteza marafiki na hata ndugu na kutawala kipindi kimoja tu. Zaidi ya hapo, awe tayari kuwa mtu mpweke sana. Naomba sana niwe NIMEKOSEA katika mtazamo wa aina hii. I really wish to be completely wrong!

Kwa vyovyote vile, nisingependa sana kuchukulia mpambano unaosababishwa na tofauti za kiuchumi zinazotokana na mfumo wa wizi/rushwa katika tabaka la watawala (kleptocracy) kama kielelezo cha genuine class struggle. Kwangu mimi hizo ni vurugu zitokanazo na uongozi mbovu.
 
Back
Top Bottom