The inevitable class struggle between the haves and the have nots...!

The inevitable class struggle between the haves and the have nots...!

Mkuu Masopakyindi sijakataa jumla unachosema. Aidha, kwa kukosoa uongozi wa nchi naweza kuonekana kirahisi nimeingiza siasa za vyama; kama vile nakishambulia chama kilichoko madarakani. Sivyo kabisa. Wasiwasi wangu mkubwa sana kuhusu Tanzania leo hii ni ule utamaduni tulioujenga kwa miaka mingi wa kuchukulia madaraka kama njia ya kuinua uchumi binafsi wa mtu badala ya taifa. Sidhani kama unahitaji kuelezwa kuwa hata biashara kubwa Tanzania zinahusishwa na ukaribu na walioko madarakani. Kwamba usipokuwa na madaraka au kuwa karibu na wenye nayo si rahisi ukafika mbali kibiashara (nikiweka utani: utaishia kunadi juisi na matunda - tena mitaani!).

Mtazamo wangu wa dhati kabisa, si kwa chama kilichoko madarakani tu, hata vikija vingine naona uwezekano wa kujikuta tukiendelea na mfumo wa "kleptocracy" ni mkubwa sana. Leo hii nikiwatizama Watanzania wengi wanaowania nafasi za uongozi (wa vyama vyote) naona wanasukumwa zaidi na mtazamo wa "sasa ni zamu yetu kula". Wapo wanaonishawishi kuwa wanajitoa kwa taifa - kama alivyojanya JKN (pamoja na mapungufu yake ya kimkakati). Lakini ni wachache sana. Na naheshimu sana uwezo mkubwa wa binadamu kulaghai kikamilifu (ultimate deception capacity).

Kwa upande wetu kama jamii, SIJUI kama itakuwa rahisi kufuta mtazamo uliojengeka sana wa kuwaona viongozi kama miungu (wakiwa juu ya sheria na taratibu). Kunahitajika "mapinduzi" makubwa hasa kurejesha uwajibikaji kwa viongozi nchini ukichukulia kwamba kiwango cha unafiki na ubinafsi katika jamii ni kikubwa sana. Atakayefanikiwa kuchukua uongozi wa nchi (chama chochote) akiwa na ajenda ya dhati ya aina hiyo basi naona huyo awe tayari kupoteza umaarufu mapema sana, awe tayari kupoteza marafiki na hata ndugu na kutawala kipindi kimoja tu. Zaidi ya hapo, awe tayari kuwa mtu mpweke sana. Naomba sana niwe NIMEKOSEA katika mtazamo wa aina hii. I really wish to be completely wrong!

Kwa vyovyote vile, nisingependa sana kuchukulia mpambano unaosababishwa na tofauti za kiuchumi zinazotokana na mfumo wa wizi/rushwa katika tabaka la watawala (kleptocracy) kama kielelezo cha genuine class struggle. Kwangu mimi hizo ni vurugu zitokanazo na uongozi mbovu.
Very true !!
Mkuu mtazamo wako kwa yanayoonekana katika uwanda wa uongozi ncini ni huo ulioonyesha kinaga ubaga.
Na nakubaliana na maoni yako kuwa kwa kila atakayeingia madarakani(awe wa chama chochote kile) msukumo mkubwa ni primitive accumulation of wealth , na kama nilivosema huko nyuma hilo linafanyika kwa wizi, rushwa,na hata outright grand fraud.
Haya tunayaona sasa na sitegemei kuwa hata kikiingia chama kingine yatakwisha haya.

Mimi ninayo yaongelea ni matokeo ya kuupanga uchumi wetu kwa kuendekeza hizo sera zinazoendeleza tofauti kubwa za kipato, hivo kuendeleza classes hizo za the haves and the have nots.

Pengine tunapopishana ni position tunazoziona kwamba nini kinaanza na nini kinafuata.
Ni dhahiri kuwa uongozi mbovu, usiotilia maanani matakwa ya wananchi ndio unaolea sera za kupulanila(unchecked and conspicuous theft on a grand scale of resources).

Ni wazi kuwa matokeo ya sera kama hizo ndio zinazaa class struggle.
Najua kuwa kuna wasomi wazuri tu juu ya somo kama hili, lakini tatizo si tu la uongozi mbaya hadi tupate makundi kinzani kijamii, bali vile vile lazima tuwe na analysis nzuri tu ya ownership ya means of production.

Zamani hili lilikuwa rahisi kulicontrol maana serikali ilijizatiti na kuweka ownership ya means of production chini yake.
Mambo yamebadilika sasa maana with private ownership of means of production ndio nasema wanyonge sana sana wanakuwa a tool of production, yaani sana sana wanaweza kuuza nguvu ya(labour) inayoweza kuwa manipulated at will na owners of meands of production.
Na hapo ndio tunaziendeleza classes.
 
Nimesoma kwenye gazeti wamekamatwa vijana zaidi ya 300! Sijui ni Magereza gani watawaweka. Suluhisho si kukamata, suluhisho ni mfumo. Ukosefu wa ajira ni moja, lakini pia mfumo unaowapendelea walioko kwenye madaraka na matajiri unazidisha tatizo. Vijana wa kosa matumaini. Nimesikia na kusikitika maoni ya mtu mmoja katika radio akidai hawa panya rodi wanatengenezwa na chama cha siasa kuleta vurugu!
 
Nimesoma kwenye gazeti wamekamatwa vijana zaidi ya 300! Sijui ni Magereza gani watawaweka. Suluhisho si kukamata, suluhisho ni mfumo. Ukosefu wa ajira ni moja, lakini pia mfumo unaowapendelea walioko kwenye madaraka na matajiri unazidisha tatizo. Vijana wa kosa matumaini. Nimesikia na kusikitika maoni ya mtu mmoja katika radio akidai hawa panya rodi wanatengenezwa na chama cha siasa kuleta vurugu!
Hao wanaosema Panya Road wametengenezwa na wanasiasa wanasema kweli, lakini wametengenezwa kwa kubaguliwa kutoka katika njia kuu za uchumi.
Na serikali iwapandisje vyeo kina Kova , wawe wengi sana , lakini hawatweza kulitatua tatizo hili hadi watakapoelewa chanzo cha tatizo.
Leo wamekamata 300, kesho watakuja 1,000 kazi kwao.
 
Mkuu Masopyokindi umewaza nje ya 'box' nimechelewa uzii huu for being do busy.Revolution is coming as a quick solution for have not class.
 
Mimi nije kwa upande mwingine ni dhahiri kabisa nchi imeonekana usalama wa wanachi ni mdogo ama hakuna ulinzi wa raia na mali zake, nikawaza juu ya police wa Tanzania hawana siraha wanatembea na vifimbo mkononi.Dunia imebadilika uharifu umeongezeka bado police ya Tanzania wanafikiri watu wanaogopa mavazi yao ni aibu kubwa kwa jeshi la police kukosa siraha.Mharifu anaweza kutokea wakati wowote ule police anapaswa kuwa tayari muda wowote ule kupambana na uharifu,iwe traffic police iwe police wa kawaida, popote pale alipo anapaswa kuwa na siraha ya kujihami ama kuzuia uhalifu.Mmebaki na propaganda za kova kuonea wanasiasa pindi wanapotaka kuandamana kwa manufaa ya umma. Kingine hawa panya road ni mtandao wa watu ambao ndio wafadhiri wa hao watoto, siamini kama hao vijana wamejikusanya from no where wakaanza kupora mali za watu na kujeruhi watu lazima wapo wahusika wa hili kundi.
 
Good analysis.

Ni naona hawa vijana ndo itakuwa chachu ya mabadiliko katika jamii zetu kwa kuanzia na Dar then watasambaa hadi mikoani.

Kivipi; Wakiendelea kuwatandika walala hoi wenzao,watawaamusha na kuanza kutafuta chanzo cha tatizo ambalo ni utawala mbovu hivyo basi solution watakayo amua ni kubadili uongozi huu ulioshindwa.

Tena inabidi wapate na silaha za Moto ili muziki uwe chorus mpaka jamii itakapo amuka na kuchukua hatua stahiki.

Haiwezekani wanasiasa waishi kama wako mbinguni ilhali kuna population kubwa hata milo miwili ni kitendawili.

Panya road ni catalyst itayospid up mabadiliko.

Hivyo waendelee Tu.
 
ningekuwa na research ningetumia case study yako masopakwindi! umejenga hoja mtambukaaa! umeelezea vitu bila unafiki! wanafiki hawawezi Changsha kitu hapa!

The other day nilikuwa namuambia mtu humu, criticism ni kwa ajiri ya kujenga that stupid only won't take it! you ate prudent I salute you kikolo!
 
Kulikuwa na "panyaroad" hata wakati wa siasa za ujamaa za Nyerere. Uchumi wa kiujamaa na wa kibepari wote ulileta "have" na "have not".

Kwa mfano, wafanyabiashara wengi wa asili ya kihindi au kiarabu hawajateseka sana kama Wazawa Wakati wa ujamaa kwenye mahitaji ya kula. Wafanyakazi wengi wa serikali pia waliweza kupata Mlo kutokana na rushwa. Hawa Ndio waliokuwa "have" katika siasa ya ujamaa. Hata Urusi, hamna ofisa wa serikali alilala njaa. Ni wananchi wasiokuwa na connection. Pamoja na njaa kali iliyoikabili Tanzania ya Nyerere, maofisa wake wote walitumia connection zao kupata unga na Sukari Ugawaji. Mali za wananchi, hasa wenye asili ya kihindi au kiarabu, walipewa "wakubwa" sio Wananchi ,kama alipotaifisha Raisi wa Zimbabwe. Hawa ndio "have" wa Tanzania ya ujamaa wa Nyerere.

Karl Max aliandika vizuri kuhusu hili swala la class struggle lakini hali halisi ya binadamu na theories ni vitu viwili tofauti . Binadamu amezaliwa kujitafutia rizki Yake kwanza Kabla hajamsaidia mwenzake. Kama hajashiba haweza kumshibisha mwenzake. Hii ndio sababu muhimu siasa ya kiujamaa ilifeli.

Kuna umasikini mkali katika nchi za kibepari pia. Lakini serikali inasaidia kwa kuwapa chakula, nyumba za bei nafuu, masomo na tiba bure. Pia nchi za Scandinavia zinajaribu kupunguza masikini (have not) kwa kutoza ushuru mkubwa kwa wafanyabiashara wake iwasaidie wananchi wa Hali ya chini. Norway au Finland biashara hulipa Mpaka asilimia 60 au 70 ya fedha zao serikali ni lakini wanapata matibabu mazuri na wanaangaliwa vizuri na serikali zao. Pengine no rahisi kufanya hivyo kwa kuwa ni nchi Tajiri yenye watu wachache. Kanada pia huwapa wananchi tiba bure lakini wanalipa income tax kubwa kuliko Marekani ambapo tiba bure ni kwa ajili ya watu wachache tu.

Kwa kuwa Tanzania ni nchi masikini, itachukua mda mpaka masikini wapate nafuu kimaisha hata kama hongo ikipungua. Uzalishaji ni mdogo mno kuleta maendeleo haraka haraka. Mpaka pale ambapo tutakuwa na viwanda vya kuzalisha Mali kama magari, kompyuta, na kadhalika, masikini hawatapungua. Elimu yetu pia ni hafifu. Barabara, maji na umeme pamoja na rushwa ni janga la maendeleo. Elimu Kwanza ni Nzuri kwa kulisha mwananchi sio kutajirisha nchi. Hamna hata nchi Moja duniani iliyotajirika kwa kuuza mazao tu.

Utajiri hauhitaji nchi kuwa na Mali ardhini. Singapore , Korea ,Hong Kong, Japan na Taiwan Hawana Mafuta wala gesi. Wana elimu . Wana wananchi wanaochapa kazi masaa 24. Wananumua chuma nchi masikini na wanawauzia chuma zao wenyewe katika magari yao kwa faida kubwa.

Uswisi wanategemea fedha za wageni kuendesha uchumi wao. Matajiri wanaamini Sheria zao na serikali yao inalinda fedha zao makini. Wanakopesha fedha za matajiri na kuwapeleka watoto wao chooni. Hawana asilimali yoyote zaidi ya milima, siasa bora na tulivu na bila kusahau fedha za wizi za akina Mobutu.

Wazungu wananunua kahawa yetu gunia la Kilo 60 sio zaidi ya dola 100. Wanatuuzia kikombe Kimoja cha kahawa yetu dola 3 Starbucks.

Nionavyo mimi, maendeleo yapo sasa kuliko Wakati wa Nyerere .Wazawa wana viwanda sasa. Wazawa wanatajirika. Wazawa wanasafiri na kusoma zaidi. Wazawa wanaishi nje kwa wingi. Umasikini hautaisha leo wala kesho lakini kila nchi ikitajirika, serikali itaweza kuwasaidia wananchi wake wa Hali ya chini. Kinachotakiwa ni serikali ya busara na Nguvu mpya ya wananchi kujisomesha Masomo ya kileo, kufanya kazi kwa bidii na kuzalisha Mali wanazoweza kuuza kwa wingi kwa faida kubwa.

Gari jipya la kawaida la Kijapani kama Toyota Corolla Lina faida kama dola 3000 kwa Toyota. Itachukua magunia mangapi ya kahawa au karafuu kwa mkulima kupata faida ya $3000. Ukijua jibu, utajua muda utakaochukua kuleta maendeleo kwa wote Tanzania.

My 2 cents .
 
I wish kungekuwa na jukwaa kwa watu wenye macho matatu ambao huwaza kwa niaba ya Taifa kama ilivyokuwa kwenye hii thread JF lingekuwa jamvi la kujenga mno sio matusi,leo siyaoni eti.
 
Mkuu wazo zuri tatizo ulitambulisha kwa ubaguzi wa kielimu,ilitosha pia ingenoga ungejenga hoja bila harufu ya udegree ili kuunganisha wachangiaji. Nakushauri fanya siku zijazo. Ila hoja yako ina mashiko makubwa. Wasomi wakat mwingine tunakosea tunapopambanua hoja kwa kuisi utaeleweka kwa kuchanganya lugha ya kigeni. Vijana wanaotaka kukomboa nchi hii hawaelewi lugha hizo. Wategenezee lugha rahisi na wanaoijua vizuri ili wakae mstari wa mbele wa mapambano kawa waliotembea toka geita.mle nina huakika wa degree hayupo ila wameamasika kiuzalendo baada ya kujitambua.watie moyo tanzania nzuri ya asali na maziwa itapitia kwa aina ya watu hao
 
Moja ya wasiwasi wangu mkubwa ni kuibuka makundi ya uhalifu ambao itafika wakati vyombo vya usalama vinaogopa kwenda ktk baadhi ya maeneo. Panya road wataungana na wasomi wasio kuwa na ajira kuunda Gangs za hatari. Hatuko mbali kufikia hapo. Na wale wanaodhani kuta ndefu zinazo zunguka nyumba zao na mbwembwe za walinzi zitawasaidia watakuwa wamekosea sana!

Inasikitisha kwamba hata fursa muhimu za kuonyesha wananchi wetu kwamba bado kuna utawala unaojali zinapo jitokeza watawala wetu wanavurunda na kubaki kulinda tabaka lao. Angalia walivyo dhalilisha Maoni ya Wananchi ktk kuandika Katiba pendekezwa. Angalia danadana zinaendelea kuwalinda akina Muhongo na wezi walio kwapua pesa za Escrow Stanbic bank!
I dont know kuhusu katiba mpya au maoni yake ya awali na hitimisho la warioba hilo swala linataka mjadala wake.

As for the poverty and exploitation akujatokea tu wanasiasa wenye nia ya kuingia msituni au sophisticated gang leaders lakini viashirio vya uwepo wa nguvu kazi viko wazi, kwa sasa watanzania wengi wameanza kuamini viongozi wao wa nyumba za ibada kuliko wanasiasa, makundi yao wanaoshirikiana katika kutafuta mkate kuliko sera za siasa, na viashiria vingine vya kuweza kujisaidia kimaisha kwenye miji mikubwa (sijajua jua bado kuhusu vijijini) hila kwenye miji watu wanaanza kuona serikari ni disciplinary tu lakini aina wajibu kwa raia maana ata amani sasa ni jukulu la raia kujilinda na uona walinzi na bastola nje nje. Nchi zingine hiyo ni alarming sana kama sio kuja na sera za kusaidia walio chini basi propaganda za utaifa kwa sababu serikari lazima iaminiwe sio lazima chama lakini mfumo wake wote.

Jamaa wa usalama wanadhani uchumi usiowafikia watu sio threat to national security, yote kwa sababu kwa sasa madhara yanatupata sie walalahoi tunaovamiwa mabar iwe majambazi kushirikiana na polisi au mipango yao wenyewe, kuporwa kwa watu mchana kweupe, wezi kupewa dili na watu wa ndani kwenye taasisi za fedha, utapeli, uongo, baadhi ya wafanyakazi wa taasisi za ulinzi kushiriki kwenye vitendo vya kihalifu.

Bado wahusika wanataka kutupia lawana uhuni, sijui kuvuta bangi whilst ignoring the main factors za umaskini, malezi wanayopata vijana wa mtaani na socialization process wanayopitia. Kijana wa mtaani uzalendo kajifunzia wapi au anasababu gani ya kuwa mzalendo kwanza una nafasi gani kwakwe, atakuwa vipi na empathy na mtu mwengine wakati anachojua yeye ni kujilinda yeye kwanza na kuwa loyal kwa watu wanaoshirikiana and how difficult kumshauri kuwa rebel mtu huyu one day na kuingia msituni.

Watu hawana matatizo huko brunei au saudi arabia ya kutaka kupindua nchi kwa sababu mahitaji yao yanatimizwa, ni nchi ambazo raia wanamatatizo ndio watu wanasababu za kupindua serikari just as the reasons that fueled french or soviet revolutions to occur ndio sababu most places where there are civil wars ni kwa sababu ya umaskini, angola leo nani anataka kuwa rebel.

Kwa kweli hali ya walio nacho na wasio nacho inatisha badala ya kuona ni tatizo viongozi wako happy kunyenyekewa kwa kujua wenye shida inabidi wawaombe kwa kujipendekeza sijui ni nani aliewaambia keki ya taifa ni yao by birth merit.
 
Mkuu wazo zuri tatizo ulitambulisha kwa ubaguzi wa kielimu,ilitosha pia ingenoga ungejenga hoja bila harufu ya udegree ili kuunganisha wachangiaji. Nakushauri fanya siku zijazo. Ila hoja yako ina mashiko makubwa. Wasomi wakat mwingine tunakosea tunapopambanua hoja kwa kuisi utaeleweka kwa kuchanganya lugha ya kigeni. Vijana wanaotaka kukomboa nchi hii hawaelewi lugha hizo. Wategenezee lugha rahisi na wanaoijua vizuri ili wakae mstari wa mbele wa mapambano kawa waliotembea toka geita.mle nina huakika wa degree hayupo ila wameamasika kiuzalendo baada ya kujitambua.watie moyo tanzania nzuri ya asali na maziwa itapitia kwa aina ya watu hao

Nakubaliana nawe kwamba wakati wa uongozi wa Mwl. Nyerere walikuepo walio pigika lakini walikuwa na matumaini! Matumaini juu ya maisha yao na watoto wao. Ajira zikiwatafuta watu badala ya wao kuzitafuta! Watoto wao waliweza kusoma bila kuangalia kigezo cha utajiri na umasikini wa mzazi! Akili ya mtoto na juhudi zilimfikisha ktkt kilele cha ndoto zake!

Ni kweli kuna maendeleo ya vitu na baadhi ya watu wachache yamepatikana lakini umasikini umeongozeka kwa wananchi wetu wengi kuliko wakati wa Nyerere mpaka Mwinyi. Viashiria vya uvunjifu wa amani na usalama si kipaumbele cha watawala wa sasa. Kipaumbele chao kikubwa ni kulinda madaraka kwa njia yoyote na kupora kutoka hazina ya nchi.
 
Very true !!
Mkuu mtazamo wako kwa yanayoonekana katika uwanda wa uongozi ncini ni huo ulioonyesha kinaga ubaga.
Na nakubaliana na maoni yako kuwa kwa kila atakayeingia madarakani(awe wa chama chochote kile) msukumo mkubwa ni primitive accumulation of wealth , na kama nilivosema huko nyuma hilo linafanyika kwa wizi, rushwa,na hata outright grand fraud.
Haya tunayaona sasa na sitegemei kuwa hata kikiingia chama kingine yatakwisha haya.

Mimi ninayo yaongelea ni matokeo ya kuupanga uchumi wetu kwa kuendekeza hizo sera zinazoendeleza tofauti kubwa za kipato, hivo kuendeleza classes hizo za the haves and the have nots.

Pengine tunapopishana ni position tunazoziona kwamba nini kinaanza na nini kinafuata.
Ni dhahiri kuwa uongozi mbovu, usiotilia maanani matakwa ya wananchi ndio unaolea sera za kupulanila(unchecked and conspicuous theft on a grand scale of resources).

Ni wazi kuwa matokeo ya sera kama hizo ndio zinazaa class struggle.
Najua kuwa kuna wasomi wazuri tu juu ya somo kama hili, lakini tatizo si tu la uongozi mbaya hadi tupate makundi kinzani kijamii, bali vile vile lazima tuwe na analysis nzuri tu ya ownership ya means of production.

Zamani hili lilikuwa rahisi kulicontrol maana serikali ilijizatiti na kuweka ownership ya means of production chini yake.
Mambo yamebadilika sasa maana with private ownership of means of production ndio nasema wanyonge sana sana wanakuwa a tool of production, yaani sana sana wanaweza kuuza nguvu ya(labour) inayoweza kuwa manipulated at will na owners of meands of production.
Na hapo ndio tunaziendeleza classes.

Maso. inawezekana baadhi yetu tukaamini kwamba mabadiliko ya kuondoka CCM yanaweza yakawa siyo jibu la matatizo ya uongozi ktk nchi yetu lakini mimi ni tofauti na mawazo ya aina hii.

Baada ya watu karibu wale wale kuzitawala siasa za nchi yetu kuanzia baba,watoto na sasa kizazi cha wajukuu huwezi badili watu wa aina hii bado ukabakia kwamba hakuna tumaini ndani yake. Nguvu itakayo fanya mageuzi haya ndiyo itakayo yaongoza na wakishindwa na wao wataondolewa!

Kwa mara ya kwanza Watanzania wataweza tambua wanao uwezo wa kuchagua na kuondoa chama cha siasa kisicho kidhi matumaini yao. Kwa mara ya kwanza Watumishi wa Umma na Vyombo vya Dola watafahamu kazi yao siyo kulinda chama tawala bali ni kuwatumikia Watanzania. Kwa mara ya kwanza Wanasiasa wa CCM watatambua kwamba kazi ya siasa siyo ajira wala biashara ya kutajirika kwa njia ya mkato! Watarudi mitaani na kuanza maisha mapya ya kujitegemea na kulipa kodi kama ni wafanyabiashara!
 
Maso. inawezekana baadhi yetu tukaamini kwamba mabadiliko ya kuondoka CCM yanaweza yakawa siyo jibu la matatizo ya uongozi ktk nchi yetu lakini mimi ni tofauti na mawazo ya aina hii.

Baada ya watu karibu wale wale kuzitawala siasa za nchi yetu kuanzia baba,watoto na sasa kizazi cha wajukuu huwezi badili watu wa aina hii bado ukabakia kwamba hakuna tumaini ndani yake. Nguvu itakayo fanya mageuzi haya ndiyo itakayo yaongoza na wakishindwa na wao wataondolewa!

Kwa mara ya kwanza Watanzania wataweza tambua wanao uwezo wa kuchagua na kuondoa chama cha siasa kisicho kidhi matumaini yao. Kwa mara ya kwanza Watumishi wa Umma na Vyombo vya Dola watafahamu kazi yao siyo kulinda chama tawala bali ni kuwatumikia Watanzania. Kwa mara ya kwanza Wanasiasa wa CCM watatambua kwamba kazi ya siasa siyo ajira wala biashara ya kutajirika kwa njia ya mkato! Watarudi mitaani na kuanza maisha mapya ya kujitegemea na kulipa kodi kama ni wafanyabiashara!
Ni kweli mkuu!!
Siasa si ajira, bali uanaharakati uliopevuka, na kwa minajili ya kutekeleza yale wanayoyataka wananchi.
Hivyobasi kuna wale wanaoichukua siasa kuwa ajira, ndio mwisho wa siku inakuwa rahisi kupeperushwa kama bendera kutimiza yale washawishiwayo na kwa ahadi ya utajirisho binafsi.

Hao hatuna haja ya kuwajadili sasa kwani watu wa aina hiyo nao ni sehemu ya tools of production, sawa na the have nots.

Ukiwafuatilia sana utagundus kuwa baada ya kutoka uongozini na wao ni hohehahe kama the have nots.
Afadhali yao ingalau ni kuwa na nyumba na gari.
Laiti wangejua kuwa usomi wao ni uwakilishi wa sehemu kubwa ya wanyonge, wangekuwa na mtazamo tofauti.
 
Kulikuwa na "panyaroad" hata wakati wa siasa za ujamaa za Nyerere. Uchumi wa kiujamaa na wa kibepari wote ulileta "have" na "have not".

Kwa mfano, wafanyabiashara wengi wa asili ya kihindi au kiarabu hawajateseka sana kama Wazawa Wakati wa ujamaa kwenye mahitaji ya kula. Wafanyakazi wengi wa serikali pia waliweza kupata Mlo kutokana na rushwa. Hawa Ndio waliokuwa "have" katika siasa ya ujamaa. Hata Urusi, hamna ofisa wa serikali alilala njaa. Ni wananchi wasiokuwa na connection. Pamoja na njaa kali iliyoikabili Tanzania ya Nyerere, maofisa wake wote walitumia connection zao kupata unga na Sukari Ugawaji. Mali za wananchi, hasa wenye asili ya kihindi au kiarabu, walipewa "wakubwa" sio Wananchi ,kama alipotaifisha Raisi wa Zimbabwe. Hawa ndio "have" wa Tanzania ya ujamaa wa Nyerere.

Karl Max aliandika vizuri kuhusu hili swala la class struggle lakini hali halisi ya binadamu na theories ni vitu viwili tofauti . Binadamu amezaliwa kujitafutia rizki Yake kwanza Kabla hajamsaidia mwenzake. Kama hajashiba haweza kumshibisha mwenzake. Hii ndio sababu muhimu siasa ya kiujamaa ilifeli.

Kuna umasikini mkali katika nchi za kibepari pia. Lakini serikali inasaidia kwa kuwapa chakula, nyumba za bei nafuu, masomo na tiba bure. Pia nchi za Scandinavia zinajaribu kupunguza masikini (have not) kwa kutoza ushuru mkubwa kwa wafanyabiashara wake iwasaidie wananchi wa Hali ya chini. Norway au Finland biashara hulipa Mpaka asilimia 60 au 70 ya fedha zao serikali ni lakini wanapata matibabu mazuri na wanaangaliwa vizuri na serikali zao. Pengine no rahisi kufanya hivyo kwa kuwa ni nchi Tajiri yenye watu wachache. Kanada pia huwapa wananchi tiba bure lakini wanalipa income tax kubwa kuliko Marekani ambapo tiba bure ni kwa ajili ya watu wachache tu.

Kwa kuwa Tanzania ni nchi masikini, itachukua mda mpaka masikini wapate nafuu kimaisha hata kama hongo ikipungua. Uzalishaji ni mdogo mno kuleta maendeleo haraka haraka. Mpaka pale ambapo tutakuwa na viwanda vya kuzalisha Mali kama magari, kompyuta, na kadhalika, masikini hawatapungua. Elimu yetu pia ni hafifu. Barabara, maji na umeme pamoja na rushwa ni janga la maendeleo. Elimu Kwanza ni Nzuri kwa kulisha mwananchi sio kutajirisha nchi. Hamna hata nchi Moja duniani iliyotajirika kwa kuuza mazao tu.

Utajiri hauhitaji nchi kuwa na Mali ardhini. Singapore , Korea ,Hong Kong, Japan na Taiwan Hawana Mafuta wala gesi. Wana elimu . Wana wananchi wanaochapa kazi masaa 24. Wananumua chuma nchi masikini na wanawauzia chuma zao wenyewe katika magari yao kwa faida kubwa.

Uswisi wanategemea fedha za wageni kuendesha uchumi wao. Matajiri wanaamini Sheria zao na serikali yao inalinda fedha zao makini. Wanakopesha fedha za matajiri na kuwapeleka watoto wao chooni. Hawana asilimali yoyote zaidi ya milima, siasa bora na tulivu na bila kusahau fedha za wizi za akina Mobutu.

Wazungu wananunua kahawa yetu gunia la Kilo 60 sio zaidi ya dola 100. Wanatuuzia kikombe Kimoja cha kahawa yetu dola 3 Starbucks.

Nionavyo mimi, maendeleo yapo sasa kuliko Wakati wa Nyerere .Wazawa wana viwanda sasa. Wazawa wanatajirika. Wazawa wanasafiri na kusoma zaidi. Wazawa wanaishi nje kwa wingi. Umasikini hautaisha leo wala kesho lakini kila nchi ikitajirika, serikali itaweza kuwasaidia wananchi wake wa Hali ya chini. Kinachotakiwa ni serikali ya busara na Nguvu mpya ya wananchi kujisomesha Masomo ya kileo, kufanya kazi kwa bidii na kuzalisha Mali wanazoweza kuuza kwa wingi kwa faida kubwa.

Gari jipya la kawaida la Kijapani kama Toyota Corolla Lina faida kama dola 3000 kwa Toyota. Itachukua magunia mangapi ya kahawa au karafuu kwa mkulima kupata faida ya $3000. Ukijua jibu, utajua muda utakaochukua kuleta maendeleo kwa wote Tanzania.

My 2 cents .
Mkuu nitarudi kuichambua hii post baada ya kuisoma kwa makini.
 
ningekuwa na research ningetumia case study yako masopakwindi! umejenga hoja mtambukaaa! umeelezea vitu bila unafiki! wanafiki hawawezi Changsha kitu hapa!

The other day nilikuwa namuambia mtu humu, criticism ni kwa ajiri ya kujenga that stupid only won't take it! you ate prudent I salute you kikolo!
Asante malafyale!
Elimu inatskiwa itumike kuikomboa jamii ya kiTanzania.
Kwa wale waliopitia UDSM miaka hiyo, kulikuwepo na bango pale Main Library.

Na lilikuwa linasema....Katika kijiji kilichokumbwa na njaa, mtu mmoja mwenye nguvu, kijana, alitumwa vijiji vya jirani ili akatafute chakula kwa ajili ya wanakijiji wenziwe waliokuwa na njaa na wzmedhoofu.
Mtu huyo anapaswa baada ya kula na kushiba. Kurudisha neema ile kijijini kwao ili wengine wapate chakula na nguvu na wao waisaidie jamii yao.

Mkuu ndivyo ninavyoichukylia mada hii.
 
tunaambiwa kuwa hao panya road ni kuanzia miaka 14 - 23. si walipaswa kuwa shule hao? wanastrago kwa lipi? wako wazazi masikini na wamemudu kujikongoja kusomesha watoto wao hadi wakafanikiwa. mitoto mingine minunda tu. peer pressure imewafikisha huko. na bahati mbaya biblia imethibitisha kuwa the have nots are here to stay. epa na richmond na escrow Visiwe vigezo vya kuendekeza hilo gepu. panya rod si kgezo sahihi cha kufanyia analysis yako ndugu mleta mada
 
Back
Top Bottom