The Bold: Shukrani Wakuu

The Bold: Shukrani Wakuu

The bold
Anayejituma na kuishi vema au kutimiza wajibu wake hupata heshima na ushirikiano toka kwa wengine,
Hii si bahati mbaya au muujiza ni jitihada zako kutimiza kile unachoamini kuwa kitawapendeza wengine basi nasi bila nongwa wewe kama Fanani unastahiki heshima kwa nawe umetenda pasi na majivuno kwa hadhira.
Basi nami bila fulusi nakupa kongole
Pamoja sana Mkuu wambura marwa! Shukrani..
 
The bold heshima / hakima na maarifa uliyojaliwa hakika yamekuwa sehemu ya maisha yetu ya hapa JF ..

Asante kwa elimu / maarifa bora uliyonipatia na shukrani kwa kujitolea muda wako.
 
tetesi zilizonifikia mezani kwangu kumbe na wewe ni " mwanaidara ". najua idara itakuwa inajivunia uwepo wa vijana " imara " kama wewe. hongera mdogo wangu.
 
Neno wakati mwingine si kwa chuki bali challenge kama umerudi kutetea hoja kwa nguvu ya hoja badala ya hoja ya nguvu maana kipindi kile ukiwa na vita baridi na yule bi. Dada mange ulikuwa umetumbukiwa nyongo hukuwa na simile na wala hukuzikwepa fatiki basi nawe makofi kwako maana kupata heshima si kazi bali kazi kulinda heshima yako
Shukraan mkuu
 
Allah awabariki katika safari yenu mlioianzisha isiishie hum tukaona mmeishia kupotezeana niffah The bold
We don't want to have an amazing couple of months and then it be all over in a flash.
We don't want to experience the feelings of hurt,confusion and disappointment.
No matter what we'll run into and no matter how hard things get...we want us to stick together.. FOREVER!

Amen
Thank you Dearest
Insha allah..
Mwenyezi Mungu atuwezeshe tufikie goals!

Shukrani
Amen
 
We don't want to have an amazing couple of months and then it be all over in a flash.
We don't want to experience the feelings of hurt,confusion and disappointment.
No matter what we'll run into and no matter how hard things get...we want us to stick together.. FOREVER!

Amen
Thank you Dearest

Amen
Awwwwwww my best couple on jf
 
Mungu wangu! Am speechless.
Sikuwahi kufikiri kama ipo siku nami nitakuwepo katika list yako ya kukumbukwa!
What a honour?
Asante sana The bold.

Ni kweli kabisa, nakiri tulikuwa maadui wakubwa sana.
Kila tulipokutana ktk threads tuliumana kwelikweli, namshukuru Mungu kwa busara alizokujaalia maana siku zote ulijishusha wewe.

Nakupongeza kwa aina ya makala ulizoamua kuja nazo ndizo zilizonifanya niweke silaha chini na kuomba kuimaliza vita.

Kupitia kwako nimejifunza mengi kubwa zaidi ya yote ni kumheshimu kila mtu.
Nilikuchukia kipindi kile,sikuwahi kufikiri kama una akili kubwa kiasi cha kunifanya nianze kuvutiwa nawe.
Hivi sasa nimebadilika sana,namheshimu kila mtu humu JF,nimeamua kwa nia ya dhati kuachana na vita vya maneno na members humu.

Never say never,nobody knows tomorrow...
Leo hii wewe niliyekuchukia ndiye kitu cha kwanza kunijea ktk akili yangu kila niamkapo.
Lazima nikutafute nikutakie asubuhi njema ndipo mambo mengine yaendelee.

Nakutakia kila la kheri katika makala zako za kusimumua,daima nitakuwa nawe bega kwa bega.
You got my full support my love...
#TheBoldIsMine#
Kwanza una heshima ya kinywa, utapiki takataka ingawa unajua upo nyuma ya keyboard pili booooooonge la mstaarabu nimekupendaje
 
The Bold: hongera kwa kuiwakilisha na kuitendea haki ID yako siyo tu kwa michango ila pia kuthubutu (being bold) kuleta uzi huu.

Baadhi ya mada na michango yako sikuunga mkono lakini hakika umeifahamisha, bila woga, wanaJF unachoamini.

KEEP IT UP in the coming year. Some more contributions are expected of you.
 
Back
Top Bottom