Thanks God for Giving us Kikwete

Rev Kishoka,

Kuna mengi sana umeandika na kwa kuwa kwa busara zako na cheo chako umeandika ukiwa na mantiki nzuri ILA BILA SHAKA ULISAHAU NENO ZAMA. KWANI SOTE TUNAAMINI KILA MTU NA ZAMA ZaKE.

Ni msingi mkuu kwenu sasa KUCHAGUA VIONGOZI SAHIHI NA SIO VIONGOZI BORA ILI WAFANYE MAAMUZI SAHIHI kwa mustakabali wa kukuza uchumi wenu.

Shukran



Siku zote, nia ya mtoa hoja ni kuleta mahojiano na ubadilishano wa fikra na mawazo. Kama wengi tungelipokea hili kwa chachu na kwa niliyoyanukuu hapo, basi ni wazi ingekuwa ni rahisi sana kwa dhamira yangu kueleweka pamoja na hoja nyingi nilizojengwa kwa umahiri kumkosoa Kikwete.

Ukweli ni kwamba leo tunapoangalia watangaza nia, kampeni chafu ndani ya chama tawala, lundo la tuhuma na uchafu wa kila namna, kwa nini basi tusishukuru "madhaifu" ya Kikwete kutufunulia Watanzania aina ya watu wanaotaka tunu na dhamana ya kuongoza Taifa ilhali si watu wanaofaa?

Ni moaka lini au kwa ishara gani Watanzania tuendelee kuwa wanyonge na wadanganyika wa kauli tamu huku utendaji hakuna na ukweli hawa wote wanataka kutumikia na kuneemesha matumbo yao na whya wafuasi wao?
 
Siku zote, nia ya mtoa hoja ni kuleta mahojiano na ubadilishano wa fikra na mawazo. Kama wengi tungelipokea hili kwa chachu na kwa niliyoyanukuu hapo, basi ni wazi ingekuwa ni rahisi sana kwa dhamira yangu kueleweka pamoja na hoja nyingi nilizojengwa kwa umahiri kumkosoa Kikwete.

Ukweli ni kwamba leo tunapoangalia watangaza nia, kampeni chafu ndani ya chama tawala, lundo la tuhuma na uchafu wa kila namna, kwa nini basi tusishukuru "madhaifu" ya Kikwete kutufunulia Watanzania aina ya watu wanaotaka tunu na dhamana ya kuongoza Taifa ilhali si watu wanaofaa?

Ni moaka lini au kwa ishara gani Watanzania tuendelee kuwa wanyonge na wadanganyika wa kauli tamu huku utendaji hakuna na ukweli hawa wote wanataka kutumikia na kuneemesha matumbo yao na whya wafuasi ?

Rev Kishoka.

Rev unajua mimi na wewe tumetoka mbaaali sana na kwa kuwa humu bado kupata watu makini katika discussion kama ilivyokuwa kule tulikotoka ambako walikuwepo akina Mdosi Mzalendo. Mtukwao etc.

Binafsi naamini wewe ni mtu mzima yaani upo above 40 yrs na angalau uliuona utawala wa Nyerere ambaye ndio muasisi wa Taifa na kila kitu. Hata hao unaouita utitiri wa viongozi kugombea uraisi zaidi ya 86% ni zao la Nyerere ambaye ndie aliewalea na hata kuwatengeneza kimaadili lakin pia hata kuweka misingi ya CCM. Kwa haraka haraka zao la Kikwete katika hao ni Mwigulu Nchemba na January makamba.

Kwa msingi huo uozo wooote huo ni mbegu zilizopandwa na Nyerere leo ndio mnaingia katika mavuno. Kama ilivyokuwa rushwa au ulanguzi. Nchi ya Tgk kabla uhuru kwa maana wakti wa ukoloni hakukuwa na rushwa wala ulanguzi hivyo vyote aliviasisi Nyerere wakt wa utawala wake na leo vimepevuka na kuweza kuitwa UFISADI.

Sasa mimi nafikiri badala kulilaumu tawi turudi kwenye mzizi ambao ni Nyerere. Kikwete itakuwa ni kumuonea tu.

Kumbuka utawala wa Tgk wakt wa Nyerere ulitukuza sana kuogopwa na kila alilotamka Nyrere haikuruhusiwa na chombo chochote kuhojiwa au hata kukijadili alilotaka lilifanyika jambo ambalo leo hii kila anachofanya au kusemwa na Raisi wananchi wanapata fursa kuhoji na hata kuki[inga hadhwarani sababu ku ni UTANDAWAZI.

Ndio maana nikakwambia KILA MTU NA ZAMA ZAKE.Yaani kila kiongozi na wakt wake. Tuyaache hayo tusifukue mengi buree ni bora tu mupeane moyo KUCHAGUA KIONGOZI SAHIHI na wala msianze kulaumiana na kuangalia mapungufu ya viongozi wenu wakuu waliopita. Kwani waislam tunaamini kila mtu ni mkosefu, lakin m'bora wa mkosefu ni yue anayetubia kwa mola wake.

Maaa salaam
 
Rev Kishoka.

Rev unajua mimi na wewe tumetoka mbaaali sana na kwa kuwa humu bado kupata watu makini katika discussion kama ilivyokuwa kule tulikotoka ambako walikuwepo akina Mdosi Mzalendo. Mtukwao etc.

Binafsi naamini wewe ni mtu mzima yaani upo above 40 yrs na angalau uliuona utawala wa Nyerere ambaye ndio muasisi wa Taifa na kila kitu. Hata hao unaouita utitiri wa viongozi kugombea uraisi zaidi ya 86% ni zao la Nyerere ambaye ndie aliewalea na hata kuwatengeneza kimaadili lakin pia hata kuweka misingi ya CCM. Kwa haraka haraka zao la Kikwete katika hao ni Mwigulu Nchemba na January makamba.

Kwa msingi huo uozo wooote huo ni mbegu zilizopandwa na Nyerere leo ndio mnaingia katika mavuno. Kama ilivyokuwa rushwa au ulanguzi. Nchi ya Tgk kabla uhuru kwa maana wakti wa ukoloni hakukuwa na rushwa wala ulanguzi hivyo vyote aliviasisi Nyerere wakt wa utawala wake na leo vimepevuka na kuweza kuitwa UFISADI.

Sasa mimi nafikiri badala kulilaumu tawi turudi kwenye mzizi ambao ni Nyerere. Kikwete itakuwa ni kumuonea tu.

Kumbuka utawala wa Tgk wakt wa Nyerere ulitukuza sana kuogopwa na kila alilotamka Nyrere haikuruhusiwa na chombo chochote kuhojiwa au hata kukijadili alilotaka lilifanyika jambo ambalo leo hii kila anachofanya au kusemwa na Raisi wananchi wanapata fursa kuhoji na hata kuki[inga hadhwarani sababu ku ni UTANDAWAZI.

Ndio maana nikakwambia KILA MTU NA ZAMA ZAKE.Yaani kila kiongozi na wakt wake. Tuyaache hayo tusifukue mengi buree ni bora tu mupeane moyo KUCHAGUA KIONGOZI SAHIHI na wala msianze kulaumiana na kuangalia mapungufu ya viongozi wenu wakuu waliopita. Kwani waislam tunaamini kila mtu ni mkosefu, lakin m'bora wa mkosefu ni yue anayetubia kwa mola wake.

Maaa salaam
Mkuu tafadhali, hulka ya binadamu hutokana na hisia zake mwenywe na hakuna kitu kibaya duniani kama mtu anayeiga jambo ama anayetaka kuwa kama wengine. Halafu kuna wale ambao kwa sababu walinyimwa sana UHURU wanapoupata huufanyia kufuru ndio maana nchi za wenzetu swala la sex hufundishwa watoto wakingali wadogo kuelewa ubaya wa baadhi ya vitendo ambavyo vilisadikiwa kuwa ni siri kama kulawiti watoto na kadhalika.

Zamani maswala kama haya yalifichwa na watoto wengi walifikia kuingia utumwa wa mwili wao kwa kudhani ilikuwa sawa maana hawakufundishwa kuwa lilikuwa jambo baya kushikwa tupu zako na mtu yeyote asokuwa mama yako. Hivyo ndivyo nilivyoitazama Tanzania ya leo na Ujio wa kina Mkapa hadi JK tumeyaona mengi yalotokana na fursa zilizojitokeza. Fursa za ukahaba, ulafi, ufisadi na kila aina ya mabaya yalokuwa wamefichwa chini ya uvungu na wengine waki wish kuwa na maisha haya..

Tatizo linakuja ya kwamba pamoja na Uleberali uliopo viongozi wa leo hawawezi kutubia mabaya yao ikiwa wao wenyewe wanaona haya ndio maisha bora zaidi ya yale yenye Miiko na Maadili maana wanaamini katika UHURU wa kila mtu kuamua jambo hata kama linamdhuru mwingine. Maadili imekuwa siasa na sii mwenendo wa Binaadam yaani UTU wetu umekuwa na gharama zake. Unaweza kununua UTU wa watu kwa fedha na ukaonekana KIONGOZI SAHIHI kwa sababu unawatoa njaa ama kiongozi sahihi kwa sababu una uwezo wa kupigana.

Ipo misingi ya UONGOZI BORA ambayo inaambatana na miiko yake, hivyo maadili yanakuwa sehemu ya Uadilifu ambao kiongozi anatakiwa kufuata misingi ya kijamii ilowekwa. Ebu tazama leo Lowassa ambaye baraza la Mawaziri lilipitisha mradi wa Richmond usipitishwe badala yake wapewe shirika jingine, yeye kwa maamuzi yake akasema wapewe Richmond leo anadiriki kusema hakuhusika na KASHFA ile tena kwa madaha kabisa akidai hizi ni TUHUMA..Kwake uliona ni maamuzi magumu na sahihi japo kwa mabavu na kuvunja miiko ya uongozi bora!

Nchi za wenzetu, kiongozi yeyote unapoingia katika KASHFA yoyote ile inakuondoa sii Uwaziri pekee hata Ubunge, ujumbe wa kamati kuu na ndio maana ya KUWAJIBIKA. Hivyo hili neno kiongozi sahihi (The right Leader) inategemea na udhuru uliopo maana ukitaka kupigana unamtafuta bouncer, wakati kiongozi bora ni yule atakayefikiria kwanza kwa nini tuende kupigana?
 
Mkuu tafadhali, hulka ya binadamu hutokana na hisia zake mwenywe na hakuna kitu kibaya duniani kama mtu anayeiga jambo ama anayetaka kuwa kama wengine. Halafu kuna wale ambao kwa sababu walinyimwa sana UHURU wanapoupata huufanyia kufuru ndio maana nchi za wenzetu swala la sex hufundishwa watoto wakingali wadogo kuelewa ubaya wa baadhi ya vitendo ambavyo vilisadikiwa kuwa ni siri kama kulawiti watoto na kadhalika.

Zamani maswala kama haya yalifichwa na watoto wengi walifikia kuingia utumwa wa mwili wao kwa kudhani ilikuwa sawa maana hawakufundishwa kuwa lilikuwa jambo baya kushikwa tupu zako na mtu yeyote asokuwa mama yako. Hivyo ndivyo nilivyoitazama Tanzania ya leo na Ujio wa kina Mkapa hadi JK tumeyaona mengi yalotokana na fursa zilizojitokeza. Fursa za ukahaba, ulafi, ufisadi na kila aina ya mabaya yalokuwa wamefichwa chini ya uvungu na wengine waki wish kuwa na maisha haya..

Tatizo linakuja ya kwamba pamoja na Uleberali uliopo viongozi wa leo hawawezi kutubia mabaya yao ikiwa wao wenyewe wanaona haya ndio maisha bora zaidi ya yale yenye Miiko na Maadili maana wanaamini katika UHURU wa kila mtu kuamua jambo hata kama linamdhuru mwingine. Maadili imekuwa siasa na sii mwenendo wa Binaadam yaani UTU wetu umekuwa na gharama zake. Unaweza kununua UTU wa watu kwa fedha na ukaonekana KIONGOZI SAHIHI kwa sababu unawatoa njaa ama kiongozi sahihi kwa sababu una uwezo wa kupigana.

Ipo misingi ya UONGOZI BORA ambayo inaambatana na miiko yake, hivyo maadili yanakuwa sehemu ya Uadilifu ambao kiongozi anatakiwa kufuata misingi ya kijamii ilowekwa. Ebu tazama leo Lowassa ambaye baraza la Mawaziri lilipitisha mradi wa Richmond usipitishwe badala yake wapewe shirika jingine, yeye kwa maamuzi yake akasema wapewe Richmond leo anadiriki kusema hakuhusika na KASHFA ile tena kwa madaha kabisa akidai hizi ni TUHUMA..Kwake uliona ni maamuzi magumu na sahihi japo kwa mabavu na kuvunja miiko ya uongozi bora!

Nchi za wenzetu, kiongozi yeyote unapoingia katika KASHFA yoyote ile inakuondoa sii Uwaziri pekee hata Ubunge, ujumbe wa kamati kuu na ndio maana ya KUWAJIBIKA. Hivyo hili neno kiongozi sahihi (The right Leader) inategemea na udhuru uliopo maana ukitaka kupigana unamtafuta bouncer, wakati kiongozi bora ni yule atakayefikiria kwanza kwa nini tuende kupigana?

Mkandara.

Nimependa sana maelezo na ufafanuzi wako.

Lakin kiongozi SAHIHI ni yule anayeweza kufanya maamuzi sahihi kwa maslahi ya jamii yake japo yanaweza kuumiza baadhwi ya watu. Mfano wewe mshahara wako ni Riyal 200 kwa mwezi na unachukua Riyal 150 ukatoa rushwa ili uchaguliwe uwe kiongozi. Utagundua kutoa hizo Riyal 150 ni uamuzi bora sana kwani ukipata uongozi utapata zaidi ya hizo. LAKIN kwa upande mwingine kutoa hiyo Riyal 150 SI UAMUZI SAHIHI kutokana na kipato chako cha mwezi kutoa rushwa.

Ahsantum
 
Barubaru, Mkandara,


TUtamlaumu sana Nyerere kwa sababu milioni tutakazozitoa, lakini kwani ni Nyerere aliyewalazimisha hawa mabwana wakawa wahujumu?

Kama wakati wa Nyerere na utawala wake wa mabavu hawa jamaa walijificha uvunguni, kuficha tupu zao zisionekane, si sasa wanaendelea kwa kiburi na jeuri kutuonyehsa hawajali na hawana uoga?

Hata misahafu si ina amri na misingi ambayo sisi binaadamu kila siku tunaivunja na kuikiuka, na Mwenyezi Mungu si yupo akituona na uhayawani tunaoufanya kwa kutumia utashi wa binafsi (free will), je tuigeukie mbingu na kumnyooshea Mungu vidole kuwa analelea uhalifu na dhuluma kwa kukaa kimya vizazi hadi vizazi?

Mzizi ama Shina iwe ni NYerere, Mwinyi, MKapa au Kikwete, ni vipi leo tuendelee na upofu na kuwakabidhi dhamana watu ambao tunajua wazi sasa kwa uwazi wana walakini?

Leo unajua mjumbe wako wa shina ni mzinifu mzengea wasichana wabichi, lakini unampa dhamana ya kuwa mjumbe wa kuzunguka hizo nyumba, na humo haeshi kuwa "mjomba" kwa hawa watoto, je wa kulaumiwa ni nani?

hivyo udhaifu wa Kikwete ambao ni baraka kwetu ni lazima tukubali kuwajibika sasa kwamba hakuna ya uvunguni au tetezi kama enzi za Nyerere, leo hii tunaviona kwa macho yetu, tunavisikia wazi, na hawa mafidhuli hawana woga tena wa Mchonga Meno au Kifimbo, wanakosa utii kwa Rais aliyewapa madaraka kumsaidia yeye dhamana tuliyompa sisi kwa kura zetu kuiongoza nchi.

Kama ni kuuchoma mmea mzima, basi na kura zetu ziinyime CCM dhamana na mamlaka kila kona ya nchi ili iweze kuzaliwa upya na yale mabaki ya mfumo mbovu yateketezwe.

Bwana Yesu alisema, Mimi ni mzabibu wa kweli, tawi langu lisilozaa, nitaliondoa na kulitupa. Sasa na sisi wapiga kura ndio mizabibu wa Tanzania, wale wote tunaowajua hawatufai, tuwaondoe na kuwatupilia mbali!

Ndio maana ntaendelea kumshukuru Mungu kwa kupitia Kikwete tumefunuliwa memngi ambayo tulikuwa hatukubali kuyaaamini, na sasa ni kwa utashi wetu tuamue kusuka au kunyoa.
 
Back
Top Bottom