Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 57,242
- 90,300
Kuna watu wanateseka sana kwenye hii dunia, wengine wanateseka tangu wanazaliwa mpaka wanakufa, wengine wanateseka nusu ya maisha yao yote n.k
Fikiria watu wanaugua kansa za kila aina, watu wanapata ajali wanabaki vilema wasiojiweza maisha yao yote, watu wanafungwa maisha au miaka mingi pasipo kuwa wametenda kosa lolote, watu masikini wanaoishi maisha yao yote wakiwa hawajui hata mlo unaofuata utatoka wapi n.k
Hawa na wengine wote wa aina hii uwaambie hakuna Mungu na dini ni kitu cha kutunga tu kisicho na uhalisia wowote watakuelewa kweli?
Yani baada ya haya mateso yao yote hata kama waliishi maisha mema kiasi gani wakifa ndio imeisha tu hivyo hakuna kitakachoendelea huko mbele, hakika sio rahisi kwa jambo hilo kueleweka au kukubalika. Linapoteza maana na matumaini ya kuishi kabisa.
Dini inawapa binadamu wengi tumaini kwamba mateso yao wanayopitoa angalau sio bure tu.
Fikiria watu wanaugua kansa za kila aina, watu wanapata ajali wanabaki vilema wasiojiweza maisha yao yote, watu wanafungwa maisha au miaka mingi pasipo kuwa wametenda kosa lolote, watu masikini wanaoishi maisha yao yote wakiwa hawajui hata mlo unaofuata utatoka wapi n.k
Hawa na wengine wote wa aina hii uwaambie hakuna Mungu na dini ni kitu cha kutunga tu kisicho na uhalisia wowote watakuelewa kweli?
Yani baada ya haya mateso yao yote hata kama waliishi maisha mema kiasi gani wakifa ndio imeisha tu hivyo hakuna kitakachoendelea huko mbele, hakika sio rahisi kwa jambo hilo kueleweka au kukubalika. Linapoteza maana na matumaini ya kuishi kabisa.
Dini inawapa binadamu wengi tumaini kwamba mateso yao wanayopitoa angalau sio bure tu.