Teuzi za Rais Samia zinavyoakisi dhamira njema aliyonayo kwa Watanzania

Babuwatanga

Member
Oct 29, 2022
8
5
Teuzi za raisi samia zinavyoakisi dhamira njema aliyonayo kwa Watanzania.

Kassim mpingi

Rufiji -pwani

Duniani kote teuzi za kisiasa huwa na kazi kuu mbili, kazi ya kwanza ni shukran kwa kiongozi kwa waliomsaidia ushindi na kazi ya pili kudhibiti mamlaka ya uongozi hasa kwa kuweka watu makini wanoweza kufanya udhibiti huu.

Mwaka 1832 aliyekuwa seneta wa jiji la new york bw.William marcy alitoa kauli maarufu wakati anatetea teuzi zilizofanywa na raisi wa wakati huo wa marekani bw andrew jackson

Nina nukuu

“to the victor belong the spoil of the enemy “

Wakati huo neno “spoil “ likimaanisha teuzi za kisiasa kama vile ukuu wa mkoa, wilaya, balozi nk.

Hapa seneta wiliam alimaanisha mshindi (victor) ana haki ya kufanya teuzi atakazo kwa kuzingatia kazi zote mbili za teuzi ama shukran kwa kusaidia ushindi au kumsaidia usimamizi na kudhibiti dola

Mara nyingi kazi ya kwanza ya teuzi yenye lengo la shukran na pongezi kusaidia ushindi huwa haizingatii umahiri na uchapakazi wa mteuliwa,bali nafasi ya mteuliwa kwenye kufanikisha ushindi wa kiongozi anayeteua.

Mara nyingi kazi hii ya teuzi haituletei watu makini sana kwenye kuitumikia jamii na siku zote wateule huisi wao ni sehemu ya ushindi na ni ngumu kuwatenganisha wao na mamlaka iliyowateua.

Nadharia ya pili ya kazi ya teuzi ni hii ya kudhibiti mamlaka. Nadharia hii mara nyingi hupelekea teuzi zenye tija kwa jamii husika.

Katika nadharia hii ya pili wateule hupatikana kwa kuangali sifa zao na namna wanavyoweza kuleta mabadiliko yanayohitajika kwenye jamii husika, hapa kiongozi anayeteua hutazama nini jamii inataka na nani mteule yupi anaweza kufanikisha mahitajia hayo ya jamii.


Kiongozi anayeteua kwa kuzingatia kazi ya pili ya teuzi hana haja ya kutazama kama mteule alichangia ushindi wake au la.

Aina hii ya pili ya teuzi mara nyingi hafanikiwa kuleta mabadiliko yanayohitajika katika jamii husika.

Ukitazama teuzi anazofanya raisi samia toka aingie madarakani hatazami nafasi ya mteuliwa kwenye kufanikisha serikali anayoingoza kuingia madarakani,hatazami ni kwa vipi mteule husika alimsaidia yeye na raisi aliyegombea nae kama mgombea mwenza 2020.

Ndio maana huashangai kuona baadhi ya waliokuwa wagombea wa uraisi wa upinzani, watu waliokuwa sekta binafsi wenye uwezo mkubwa wa kutumikia jamii wamekuwa sehemu ya teuzi zake na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuleta mabadiliko yanayohitajika katika jamii.

Taasisi na bodi za mashirika mbalimbali nchini zinaongozwa na watu makini ambao pengine hawakuwa na mchango wa moja kwa moja wa ushindi wa chama chake bali ni watu wenye uwezo usio na shaka hata chembe, huku yeye akisisitiza atamteua yeyote mwenye sifa ili tusaidinae kwa pamoja kuijenga Tanzania tuitakayo.

Hakika teuzi za raisi samia zinaakisi dhamira njema aliyonayo kwa watanzania

Mungu ibariki afrika,mungu ibariki tanzania

#kaziiendelee

safar.png
 
Kuna kipindi mteuzi alikuwa akiangalia kama ni kabila fulani au angalau umetoka katika kanda fulani basi ndio ilikuwa sifa muhimu.
 
Safari Moja na Mama 2025-2030
Slogan tam sana....Kila la kheri.
Sisi wa mei Mosi mwezi Mei umepita salama kabisa, shukrani kwake Muumba mwenye sifa zote!

Tumaini kubwa tunalo mwezi Julai
 
Teuzi za raisi samia zinavyoakisi dhamira njema aliyonayo kwa Watanzania.

Kassim mpingi

Rufiji -pwani

Duniani kote teuzi za kisiasa huwa na kazi kuu mbili, kazi ya kwanza ni shukran kwa kiongozi kwa waliomsaidia ushindi na kazi ya pili kudhibiti mamlaka ya uongozi hasa kwa kuweka watu makini wanoweza kufanya udhibiti huu.

Mwaka 1832 aliyekuwa seneta wa jiji la new york bw.William marcy alitoa kauli maarufu wakati anatetea teuzi zilizofanywa na raisi wa wakati huo wa marekani bw andrew jackson

Nina nukuu

“to the victor belong the spoil of the enemy “

Wakati huo neno “spoil “ likimaanisha teuzi za kisiasa kama vile ukuu wa mkoa, wilaya, balozi nk.

Hapa seneta wiliam alimaanisha mshindi (victor) ana haki ya kufanya teuzi atakazo kwa kuzingatia kazi zote mbili za teuzi ama shukran kwa kusaidia ushindi au kumsaidia usimamizi na kudhibiti dola

Mara nyingi kazi ya kwanza ya teuzi yenye lengo la shukran na pongezi kusaidia ushindi huwa haizingatii umahiri na uchapakazi wa mteuliwa,bali nafasi ya mteuliwa kwenye kufanikisha ushindi wa kiongozi anayeteua.

Mara nyingi kazi hii ya teuzi haituletei watu makini sana kwenye kuitumikia jamii na siku zote wateule huisi wao ni sehemu ya ushindi na ni ngumu kuwatenganisha wao na mamlaka iliyowateua.

Nadharia ya pili ya kazi ya teuzi ni hii ya kudhibiti mamlaka. Nadharia hii mara nyingi hupelekea teuzi zenye tija kwa jamii husika.

Katika nadharia hii ya pili wateule hupatikana kwa kuangali sifa zao na namna wanavyoweza kuleta mabadiliko yanayohitajika kwenye jamii husika, hapa kiongozi anayeteua hutazama nini jamii inataka na nani mteule yupi anaweza kufanikisha mahitajia hayo ya jamii.


Kiongozi anayeteua kwa kuzingatia kazi ya pili ya teuzi hana haja ya kutazama kama mteule alichangia ushindi wake au la.

Aina hii ya pili ya teuzi mara nyingi hafanikiwa kuleta mabadiliko yanayohitajika katika jamii husika.

Ukitazama teuzi anazofanya raisi samia toka aingie madarakani hatazami nafasi ya mteuliwa kwenye kufanikisha serikali anayoingoza kuingia madarakani,hatazami ni kwa vipi mteule husika alimsaidia yeye na raisi aliyegombea nae kama mgombea mwenza 2020.

Ndio maana huashangai kuona baadhi ya waliokuwa wagombea wa uraisi wa upinzani, watu waliokuwa sekta binafsi wenye uwezo mkubwa wa kutumikia jamii wamekuwa sehemu ya teuzi zake na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuleta mabadiliko yanayohitajika katika jamii.

Taasisi na bodi za mashirika mbalimbali nchini zinaongozwa na watu makini ambao pengine hawakuwa na mchango wa moja kwa moja wa ushindi wa chama chake bali ni watu wenye uwezo usio na shaka hata chembe, huku yeye akisisitiza atamteua yeyote mwenye sifa ili tusaidinae kwa pamoja kuijenga Tanzania tuitakayo.

Hakika teuzi za raisi samia zinaakisi dhamira njema aliyonayo kwa watanzania

Mungu ibariki afrika,mungu ibariki tanzania

#kaziiendelee

View attachment 2633536
Huyo ni Rais wa Pwani na Tanga we sympathize with you for projecting unrealistic ambitions
 
Back
Top Bottom