tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,859
- 18,282
Tulizoea kuona wazaznzibar (maarufu kwa jina la wapemba) wametapakaa kila mahali hapa Tanganyika wakifanya biashara na shughuli nyingine za kiuchumi. Hili kama watanganyika hatuna shida nalo. Hawa ni wajasiriamali na watafutaji kama walivyo watu wa mataifa mengine waliomo hapa nchini. Tunao wachina, wahindi, wakenya, n.k, na haijawahi kuwa shida.
Kinachoudhi na kusikitisha zaidi ni kitendo cha Rais Dr Samia kuwachukua wazanzibar (hata wasiokuwa na vigezo) na kuwapa vyeo hapa Tanganyika wakati watanganyika hawana kazi. Ukitembelea kwenye ofisi za umma utashangaa kuona utitiri wa wazanzibar wakiwa wamepewa nyadhfa mbali kama vile wakurugenzi, DAS, RAS, wakuu wa mashirika ya umma, wenyeviti wa bodi mbalimbali, n.k. Rais anafanya haya yote kwa makusudi na kwa lazima huku akiwaacha watanganyika wakipuyanga bila kazi. Huu ni zaidi ya uhujumu uchumi.
Ndugu wanaJF na wananchi kwa ujumla, tuhuma hizi hazijaanza leo. Soma baadhi ya nyuzi zilizowahi kuwekwa humu kulalamikia upendeleo unaofanywa na mamlaka kwenye teuzi mbalimbali:
1. Teuzi za Rais Samia zina upendeleo?
2. Teuzi za Rais Samia kulikoni?
3. Wafahamu Wajumbe wa Bodi ya TCRA iliyovunjwa
Kelele za watanganyika kukosa kazi baada ya kuhitimu zipo dhahiri. Hata humu JF siku za karibuni kumekuwa na nyuzi nyingi zinazoonyesha wasomi wa Tanganyika kuhitimu vyuo vikuu na kuishia kufanya kazi za ovyo ovyo wakati kazi walizostahili kufanya zinagawiwa ovyo kwa wazanzibar. Nyuzi zifuatazo ni sehemu ya ushahidi huo:
1. Nimekutana na Degree Graduate wa HR kutoka Mzumbe anauza Pub
2. Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!
3. Graduates wengi tunapitia wakati mgumu sana, sema jamii inaona kama hatujielewi
MAONI YANGU
Idadi ya watu wa Zanzibar (Pemba, Unguja na visiwa vingine) haipindukii milioni moja. Tanganyika ina idadi ya zaidi ya watu milioni 64. Sasa iweje Zanzibar yenye watu wachache kiasi hiki wananchi wake wapewe kipaumbele huku watanganyika walio wengi wanaendelea kusaga meno?
Ifike mahali katiba itamke bayana idadi ya nafasi wanazostahili wazanzibar (kwa kufuata uwiano wa idadi ya watu) badala ya kufanya teuzi kibubu na kusababisha malalamiko. Na tunapendekeza hili jambo liingizwe kwenye katiba mpya kabisa ili kukata mzizi wa fitna.
Nawasilisha.
Kinachoudhi na kusikitisha zaidi ni kitendo cha Rais Dr Samia kuwachukua wazanzibar (hata wasiokuwa na vigezo) na kuwapa vyeo hapa Tanganyika wakati watanganyika hawana kazi. Ukitembelea kwenye ofisi za umma utashangaa kuona utitiri wa wazanzibar wakiwa wamepewa nyadhfa mbali kama vile wakurugenzi, DAS, RAS, wakuu wa mashirika ya umma, wenyeviti wa bodi mbalimbali, n.k. Rais anafanya haya yote kwa makusudi na kwa lazima huku akiwaacha watanganyika wakipuyanga bila kazi. Huu ni zaidi ya uhujumu uchumi.
Ndugu wanaJF na wananchi kwa ujumla, tuhuma hizi hazijaanza leo. Soma baadhi ya nyuzi zilizowahi kuwekwa humu kulalamikia upendeleo unaofanywa na mamlaka kwenye teuzi mbalimbali:
1. Teuzi za Rais Samia zina upendeleo?
2. Teuzi za Rais Samia kulikoni?
3. Wafahamu Wajumbe wa Bodi ya TCRA iliyovunjwa
Kelele za watanganyika kukosa kazi baada ya kuhitimu zipo dhahiri. Hata humu JF siku za karibuni kumekuwa na nyuzi nyingi zinazoonyesha wasomi wa Tanganyika kuhitimu vyuo vikuu na kuishia kufanya kazi za ovyo ovyo wakati kazi walizostahili kufanya zinagawiwa ovyo kwa wazanzibar. Nyuzi zifuatazo ni sehemu ya ushahidi huo:
1. Nimekutana na Degree Graduate wa HR kutoka Mzumbe anauza Pub
2. Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!
3. Graduates wengi tunapitia wakati mgumu sana, sema jamii inaona kama hatujielewi
MAONI YANGU
Idadi ya watu wa Zanzibar (Pemba, Unguja na visiwa vingine) haipindukii milioni moja. Tanganyika ina idadi ya zaidi ya watu milioni 64. Sasa iweje Zanzibar yenye watu wachache kiasi hiki wananchi wake wapewe kipaumbele huku watanganyika walio wengi wanaendelea kusaga meno?
Ifike mahali katiba itamke bayana idadi ya nafasi wanazostahili wazanzibar (kwa kufuata uwiano wa idadi ya watu) badala ya kufanya teuzi kibubu na kusababisha malalamiko. Na tunapendekeza hili jambo liingizwe kwenye katiba mpya kabisa ili kukata mzizi wa fitna.
Nawasilisha.