Test Your Earliest Memory: How Long Can You Remember?!.

Nilikuwa na miaka mitatu kuelekea minne hivi, nilikuwa nalia nataka nimuogeshe mdogo wangu na mimi. Binamu aliyekuwepo nyumbani alikuwa ananiambia njoo nikuoshe mdogo wangu kwa hiyo nilipopata mdogo na mimi nkataka nimuoshe.
 
Mnavyohadithia stori za chekechea mnanikumbusha huzuni yangu kuu kipindi hicho nina miaka 4mpaka 5 sijui niite bahati mbaya au nzuri
mimi sikusoma elimu ya awali mama yangu alikuwa ananifundisha mwenyewe nyumbani kusoma na kuandika kipindi hicho nina miaka 4 mpaka 5
nilikuwa natamani mnooo shule lakini mama alipinga akisema yeye ni mwalimu tosha atanifundisha mwenyewe nyumbani na
ilikuwa kila siku asubuhi lazima niwahi kuamka kuangalia watoto wanaokwenda shule hasa wale wa chekechea baada ya hapo nalia kutaka niende shule msimamo wa mama haukubadilika baada ya chai anaanza kunifundisha
nilipokuja kuanza la kwanza pindi nina miaka 7 hakuna siku niliyofurahi kama hiyo
 

Dah, umenipa changamoto hapo mkuu, hivi kila mtu anaweza kufikiri ameshatumia % ngapi kufanya cha maana katika maisha yake tangu azaliwe? Kuna mmoja amelinganisha huu uwezo sawa na MB,GB,TB- Hivi tunaweza kuwachambua viongozi wetu kwa kutumia hivi vigezo?
 
Kila mtu anaweza kukumbuka cd yake ilipokuwa empty
Mimi nakumbuka mwaka 1964 nikiwa mdogo sana naenda chekechea na sister
Nikichoka kutembea alikuwa ananibeba alikuwa mkubwa kwangu kwa miaka miwili
Mpaka mwalimu wangu namkumbuka sana
Ila sasa kumbuka uliofanya nao kazi miaka 10 iliyopita kama ulibadili kazi
Hapo ndio utajua kumbukumbu ni utotoni tu

Saa hizi ukiniambia jina lako leo
Kesho nimelisahau
 
Nakumbuka nkiwa mdogo sana na miaka 3, nilimng'ania kaka yangu niende nae Shamba, nikiwa shamba nkabanwa na Haja akanichimbia shimo karibu na shina la maindi nkakata gogo pale akafukia akaniambia ile ni mbolea hivyo indi litastawi sana basi ikawa kila safari ya shamba nataka niende kuliangalia indi langu, kabla Ya mavuno nikatenganishwa nae kwa Miaka minne ila lile indi lilinikaa sana kichwan na nilipoonana nae nikamkumbusha....
 
Ahhaaaahahahahaha
 
Ahsante kwa mada nzuri mzee pasco @@pascal mayala mayala japo ni ya kitambo kiasi.
Naweza recall kumbukumbu za muda mrefu kupitia MUZIKI.
Kwa mfano enzi za utoto wetu, familia yetu ilikuwa ni ya kidini sana. Baba alikuwa na cassette aliinunua 1992 so me nimezaliwa nimeikuta. So alikuwa ananunua kanda za wanamuziki mbalimbali hasa kwaya za kikatoliki, kilutherani, na nyimbo za dansi kama za kina mzee rojer, mwinjuma muumini nk katapila, na za kusifia juhudi za Nyerere.
So kila nikisikia hata leo baadhi ya hizo nyimbo basi hunikumbusha Family memories kibao.

Kuna kanda fulani hivi imeitwa na mateeneger wa south africa alinunua mzee dah ilikuwa kwa kizulu mixer kiingereza basi nilikuwa naipenda mpka leo. Niihangaika mtandaoni nipate nyimbo zake in digital format nikafanikiwa kupata chache lkn hunipeleka so far kimawazo.
 
Nakumbuka nikiwa na 4yrs, nilitumia mabox na takataka nyingine nikajenga kitu nilichoita nyumba!
, Cha ajabu nikaingiza kiwili wili huku miguu ikiwa nje nikauchapa usingizi wa kutosha! Mama na ndg wengine walihangaika kunitafuta lkn walikuja kuniona baada ya masaa mengi kupita nikiwa bado nauchapa usingizi!
 
Mkuu nazitafuta sana hizo nyimbo za hao Wasouth,kama utaweza naomba uorodheshe majina ya hizo nyimbo hapa nizitafute

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa upande wangu, nilikuwa mkutubi nilipokuwa shule ya msingi na wanafunzi wenzangu wakija kuazima vitabu maktaba nilikuwa siandiki majina yao, lakini nilijua nani kaazima kitabu gani na anatakiwa arudishe lini. Pia darasani mwalimu akifundisha nilikuwa nasoma biblia chini ya dawati (maana yalikuwa yale yenye nafasi ya kuweka madaftari au vitabu chini) au rozari, lakini tukifanya mtihani nilikuwa nakuwa wa pili. Kwa uzoefu wangu, kadiri muda unavyoenda ndivyo ninavyokumbuka vizuri mambo ya zamani na kwa kawaida nikifahamu jambo huwa nakuwa na kumbukumbu nzuri almost ku'reproduce' kilichoandikwa. Enzi hizo kulikuwa na kitabu cha Kiingereza chenye simulizi la 'Mkisi crosses lake Nyasa' hii hadithi niliijua yote 'verbatim' pamoja na ile ya Ziwa Victoria 'Omusoke twahwelela'. Ni ajabu sana!
 
Wa shule ya msingi niliowasahau majina yao watu kumi tu kwenye darasa lililoķuwa na wanafunzi sabini na tisa ila sec wa O na A level niwakumbukao hawazidi watu kumi!
Nalog off
 
Ilikuwa na miaka 3.nilimuona bibi jirani yangu ana mguu wa mtu chumbani kwake... ... Mpaka leo sisahau hiyo kitu...
 
Kumbukumbu ninazo nyingi kiasi nadhani toka nikiwa na miaka 2 hadi mi 3 hivi...siku moja tunacheza na mwenzangu kwenye sebule hivi,ni kama tulitaka kuchukua kitu fulani kwenye gunia lililojaa mkaa kama nusu hivi,kabla ya kulifikia tukamuona nyoka mkubwa kama mweusi hivi,akainua kichwa,tukakimbia kumuita mama mdogo,akamtoa kumvutia nje na akamuua.Yule mama mdogo alikuwa haogopagi nyoka kabisa,mazingira yale yalikuwa na nyoka wengi na matukio machache ninayokumbuka kuhusu nyoka yeye ndo alikua akiwashughulikia.Nadhani matukio yale yalinijengea kuwaogopa nyoka sana mpaka karibuni woga umepungua kiasi kikubwa.
 


Kweli disc imejaa; hivi ni Anna Kilala au Jane Kilala 🤣
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…