Tendwa Unasubiri nini kukifuta Chama Cha CUF?

Tendwa Unasubiri nini kukifuta Chama Cha CUF?

Angeanza kukifuta chadema ambacho kampeni za 2010 zilihamishiwa kanisani.

Tendwa akifute CUF kwani ni chama TISHIO tena kwa CCM?

Chama ambacho Tendwa anatakiwa kukifuta ni CDM kwasababu ndiyo TISHIO LA UHAI wa CCM.

Next time uwe unajaribu kutumia AKILI hata kama ni hizo KIDOGO ulizojaliwa na Maulana za kuendea CHOONI.
 
Lipumba akiwa kwenye nyumba ya ibada alidhibitisha kuwa mwaka 1995 aliombwa agombee Urais ili kuwakilisha watu wa Imani yake. Pia Mwaka 2010 Yeye na viongozi wa dini yake walizunguka nchi nzima ili kumuokoa Kikwete dhidi ya mziki mzito wa CHADEMA. Pia Amewataka watu wa dini yake wajipange mwaka 2015 ili waokoe jahazi kupitia CUF.

Sasa kwa MANENO KAMA HAYO YA LIPUMBA ni wazi kwamba CUF ilianzishwa maksudi kwa ajili ya watu wa imani fulani. CUF ni sawa na Chui alievaa ngozi ya Kondoo. Mimi niliwahi kuvutiwa na Sera za LIPUMBA wakati fulani.

Kwa ushahidi wa wazi kama huo, TENDWA UNASUBIRI NINI KUFUTA CHAMA HIKI HATARI AMBACHO HAKIWAKILISHI WATANZANIA WA IMANI ZOTE?

Kuna safari ndefu katika hili.
 
Kunahitajika utashi wa haja kuinusuru Tanzania na siasa za udini kwani hamna dhambi itakayo tutafuna vibaya kama kuifanya dini silaha dhidi ya mamlaka.
 
Hata mimi pia ninajiuliza Zitto Kabwe anasubiri nini Chadema?.
...Yaani Zitto mnapenda sana kumtumia. Bahati nzuri naona naye siku hizi kawashtukia - siku hizi amesimama imara kukijenga chama na kukemea udini. Keep it up Zitto!
 
chama cha kupanga mauaji hakiwezi kuwa chama pendwa, mind you!!!!!!!!

Wewe uenda ukawa ni mmoja wao ya Watanzania wapumbavu wanaoamini kila kitu wakisikia "serikali imesema". Inamaana wewe ujui nani anaratibu mauaji na mateso nchini?. Kwani cdm ndiyo walimuua Mwangosi?
 
Mkuu TOR ya Tendwa haijaandikwa CUF imeandikwa CDM mbona ungeshamuona akitokwa povu mbaya hivi hapo anajipanga atoke vipi ili kupotezea.
 
Tendwa anacho fanya ni kukenua na kutuonesha mwanya wake, na kula pesa ya wananchi, sioni umaana wowte wa yey kuwa hapo...kuna siku alikuwa anahojiwa, yeye akajibu "unajua tatizo la hivi vyama vya wenzetu shida yao wana taka chama tawala kitoke madarakani..." hopeless!

Hahahahahaaaah! Kama kweli hii ni kiboko
 
Lazima Prof. Awe mstaarabu maana inabidi ajiuzulu U-Wenyekiti wa CUF na ajiunge rasmi na CCM maana ametuambia kuwa alijua kuwa Kikwete hajashinda ila Alikwenda kwa Lengo Fulani ili akitaraji matunda. Sasa hiyo haki sawa iko wapi? Kuhalalisha haramu na kufanya halali ili utarajie upate matunda japo ya haramu
 
Lipumba akiwa kwenye nyumba ya ibada alidhibitisha kuwa mwaka 1995 aliombwa agombee Urais ili kuwakilisha watu wa Imani yake. Pia Mwaka 2010 Yeye na viongozi wa dini yake walizunguka nchi nzima ili kumuokoa Kikwete dhidi ya mziki mzito wa CHADEMA. Pia Amewataka watu wa dini yake wajipange mwaka 2015 ili waokoe jahazi kupitia CUF.

Sasa kwa MANENO KAMA HAYO YA LIPUMBA ni wazi kwamba CUF ilianzishwa maksudi kwa ajili ya watu wa imani fulani. CUF ni sawa na Chui alievaa ngozi ya Kondoo. Mimi niliwahi kuvutiwa na Sera za LIPUMBA wakati fulani.

Kwa ushahidi wa wazi kama huo, TENDWA UNASUBIRI NINI KUFUTA CHAMA HIKI HATARI AMBACHO HAKIWAKILISHI WATANZANIA WA IMANI ZOTE?
[TABLE="width: 1"]
[TR]
[TD][/TD]
[TD="align: left"][TABLE="width: 500"]
[TR]
[TD]Ndele Abdande[/TD]
[TD="align: right"]11:57pm May 27[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
LIPUMBA kaonekana mckitni tu mnaxma ni MDINI....huyu MCHUNGAJI,MZINIFU NA MBADHILIFU nae tumwitaje...????



[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Chadema mnakishambulia Cuf kuficha uovu wenu hapa kifutwe cdm na Cuf itakuwa sawa. Slaa kampeni zake kanisani na Lipumba msikitini.
 
Hivi mnafikiri Chadema ikipiga kampeni Makanisani mziki wake mtauweza! Kama Mapadre, Maaskofu na wachungaji wote wakiamua kuubili uzuri wa Chadema makanisani nani atasimama? Kwa taarifa yako kuna sehemu hapa nchini serikali ikisema fanya hivi na padre akasema msifanye, watamsikiliza padre kuliko serikali.
mwaka 2010,kanisa lilitoa waraka wake wa kuwataka waumini wao wamchague kiongozi na wakatoa sifa,kwa mujibu wa maneno yako ina maana waraka ulikua unawambia wamchague nani?na Je walimchagua?
 
Sasa nimejua ni kwa vipi CUF ina uwezo wa kumiliki MIGODI, kumbe inawezeshwa na CCM
 
Leta ushahidi wa video kama tulivyoleta wa Lipumba!

Kuna watu wamefukuzwa dini kwa sbb ya kukiunga mkono ccm, dini nyingine bwana unafukuzwa na binadamu mwenzako.
 
[h=5]CUF YALAANI BAADHI YA VYOMBO VYA HABARI KUTUMIKA KISIASA KUENEZA UDINI.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

CUF TUNALAANI BAADHI YA MAGAZETI KUENEZA UCHOCHEZI WA KIDINI

Imetolewa na Abdul Kambaya

Naibu Mkurugenzi Habari, Uenezi na Haki za Binadamu

Mei 26, 2013

CUF – Chama cha Wananchi tumesikitishwa na baadhi ya magazeti (hususani Tanzania Daima) kuchochea hasama za kidini, na kuwabagua wananchi kwa mujibu wa imani zao huku wakihusisha chochezi hizo na baadhi ya Vyama vya kisiasa na viongozi wao, katika toleo Namba 3096 la Jumapili, Mei 26, 2013.

Kwa mujibu wa waandishi wa gazeti hilo George Maziku na Josephat Isango, ambalo linanalochapishwa kila siku na linamililokiwa na kampuni ya Freemedia ambapo umiliki wake unahusishwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Mandeleo (CHADEMA) Freeman Mboe, muhusika mkuu aliehusishwa na tuhuma hizo za udini ni Prof. Ibrahim Haruna Lipumba Mwenyekiti wa CUF – Chama cha Wananchi.

Gazeti hilo pamoja na mambo mengi waliyoandika ambapo undani wake na tafsiri ni kutaka kuwaonyesha wananchi kuwa Prof. Ibrahim Lipumba na Dk. Jakaya Mrisho Kikwete wakiwa ni wenyeviti wa vyama vyao na walikokuwa wagombea urais mwaka 2010 waligubikwa na imani za udini na waliendesha kampeni zao kwa kutegemea kura za waislam, na Prof. Lipumba amekuwa akitumia misikiti na viongozi wa dini hiyo ili waislam nchini waandelee kukiunga mkono chama chake, na hasa katika uchaguzi ujao wa mwaka 2015.

Katika kuonyesha kuwa gazeti hili la Tanzania Daima limekusudia kuvigawa vyama vya siasa kwa falsafa ya udini, ni pale mwandishi anapomshutumua Rais Kikwete kwamba mwaka 2010 pamoja mgombea huyo wa CCM kuwashiwishi viongozi wa dini ya Kiislam kuwakataza waumini wao wasimuunge mkono mgombea wa CHADEMA ambae alishawahi kuwa Padre Dk. Silaa na ametumwa na Kanisa Katoliki lakini pia Propaganda hizo za Rais Kikwete alizielekeza kwa viongozi wa CUF na wafuasi wao kumpigia kura Muislam mwenzao yeye Kikwete huku wakiahidiwa kuwa Waislam wa CCM watampigia mgombea CUF mwaka 2015 kwa hoja kuwa CCM watakuwa wamesimamisha mgombea mkiristo.

CUF – Chama cha Wananchi hatushangazwi na gazeti hili ambalo uandishi wake linatumikia utashi wa mmiliki wake, ambapo mwaka huu wameibuka wakiwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumuhusisha Rais Jakaya Kikwete na tuhuma za udini, hususani uislam, na hivyo wanataka pia tuhuma kama hizo wamuhusishe nazo Mwenyekiti wetu Prof. Ibrahim Haruna Lipumba.

CUF – Tunatambua kuwa Mwenyekiti wetu Prof. Ibrahim Haruna Lipumba ni Muislam, chama hakitoweza kumzuia kuhudhuria ibada katika msikiti wowote atakaotaka kwenda kuabudu na hata kualikwa iwe msikitini, kanisani na hata kwenye mahekalu ya kihindu na kutakiwa kutoa hutoba kwa waumuni wenzie au waliomualika, kama wafanyavyo viongozi wengine wa vyama vya siasa vikiwemo CHADEMA, CCM na vyama vingine, ambapo kumbukumbu zinaonyesha kuwa Rais wa awamu ya nne Benjamin William Mkapa alipokuwa madarakani alitangaza kuwapa Waislam chuo cha Tanesco Morogoro na kuwa Chuo Kikuu cha Kiislam na kutoka kauli kama ya Prof. Ibrahim Lipumba ya kuwataka "Waislam Wajipange" kwenye ibada aliyoalikwa na Waislam.

CUF – Tunasisitiza tunalaani gazeti hili la Tanzania Daima na tutaendelea kulaani chombo chochote kinachotaka kuwagawa Watanzania wawe ni Viongozi au wananchi kwa misingi ya dini zao, na tunaitaka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo kutovifumbia macho vyombo ambavyo vinataka kutupeleka kusiko na hasa ukizingatia nchi yetu kwa sasa umegubikwa na matukio mengi yahusuyo migongano katika dini zetu na uharibifu wa nyumba za ibada.

Kwa mawasiliano zaidi 0719 566567
[/h]
 
Angekifuta kwanza chadema kwa kusigina katiba yake,kumlazimisha zitto kabwe kujitoa kwenye kinyan'ganyiro cha uwenyekiti.live watanzania wote waliona.maana ya cdm ni chama demokrasia na maendeleo.swala la lipumba si la kweli ni la kuungaunga.

etii kuungwa??
Kitu Live hata Kukimbia hawezi tumeona kwenye Video tena si kama ile ya lwakatale sema proff naye uwezo wake umepungua sana siku hizi hata kamera hakuziona?
 
Kuna watu wamefukuzwa dini kwa sbb ya kukiunga mkono ccm, dini nyingine bwana unafukuzwa na binadamu mwenzako.
Leta ushahidi. Ni nani amefukuzwa kanisani au msikitini kwa kosa la kuiunga mkono CCM?
 
Back
Top Bottom