Tendwa sasa atishia kukifuta CHADEMA

Tendwa sasa atishia kukifuta CHADEMA

Huyu uzee wake unampeleka pabaya, ni bora angepumzika tu, kuliko kuongea pumba kama hizi zinaleta kichefuchefu, asirudie tena kichefuchefu hiki kinanikera sana
 
Much respect mkuu wangu.Katika mkutano wake wa jana muda wote alikuwa anazungumzia CDM mpaka akafikia mahali bila aibu kusema operesheni ya CDM inayoitwa M4C inaleta uchochezi na mauaji.

Msipoteze muda wa kumjadili Tendwa kwakuwa anaropoka tu bila kujijua. Angekuwa Tenda hapo kidogo tungepaswa kutafakari mara mbilimbili kauli yake.

Msajili gani anayejikanyaga kanyaga hata kwa mambo madogo tu ambayo hayahitaji mtu kuwa mwanasheria kujua tafsiri sahihi ya sheria ya vyama vya siasa na namna vinavyofanya kazi. Dakika moja anasema vyama vya siasa vitulie huu si muda wa kampeni lakini dakika ya pili anasema vyama vya siasa vinaruhusiwa kisheria kufanya shughuli zake za kisiasa i.e mikutano na maandamano wakati wowote.

Narudia kusema hivi, msimuogope mtu anayeitwa Tendwa, muogopeni mtu anayeitwa Tenda!!!
 
RPC kwenye shughuli ya CDM kijijini palipo tokea tukio-sikawaida-walikwisha amua liwalo na liwe

Ukisikiliza majibu ya RPC Kamuhanda wa Iringa kabla ya kuondoka mahali pa tukio Kwamba hawezi haribu kazi yake kwani anategemea kustaafu soon halafu ukisikia kwamba kuna Polisi mmoja aliyekuwa akimtetea marehemu kuwa wamwache RIP mwangosi kwani ni mwandishi wa habari anayemfahamu, na mwisho tumethibitishiwa leo kuwa kulikuwa na Askari mamluki (ni ile type ya akina Msangi) kutoka mikoa mingine basi moja kwa moja utagundua kuwa askari mamluki ndio waliokadhibiwa jukumu la kuua (then waishie kwenye vituo vyao ) na walikuwa hawamfahamu kuwa ni mwandishi wa habari au walitaka kutimiza tu ahadi yao kwani hawakupewa qualities za mtu atakayeuawa, kwa vile kulikuwa na utulivu na yeye marehemu akawa anawafuata kuulizia kulikoni basi wakaona kazi tuliyotumwa tumalizie kwa huyuhuyu tusije rudi bila kutimiza lengo tulilopewa na wakuu, lakini...KAMWE DAMU YA MTU HAIPOTEI HIVIHIVI
 
Labda uombewe ufahamu kwani, kila mwenda mbio sana sio mshindi, na kiburi cha CDM kitawangamiza , Hta sensa hawajui maana yake, wana uungwana gani? Dears, KIPYA KINYEMI!
 
Ndugu WanaJF mtiririko wa matukio tangu ADC kuonekana kwenye anga za kusajiriwa. Kupata orodha ya wanachama kila mkoa bila kucehelewa na bendera yao kuwa na rangi za CDM inanitia shaka. Lakini pia matamko ya baadhi ya waandamizi wa CDM kuwa chama hiki nimekitumikia kwa muda mrefu lakini ni kama hayuko CDM kwa sasa inatia shaka sana. Matamko ya Nape na WAsira kuwa CDM inasambaratika soon nayo inatia shaka sana. Mauaji ya wananchi kwenye mikutano ya CDM pekee hata bila sababu inaonyesha dhahiri kuwa CCM wametumia mbinu zote za kawaida imeshindikana na lililopo ni kuwapa chama danganyatoto ADC wananchi wa Tanganyika. WanaJF nina mashaka makubwa!!
 
Labda uombewe ufahamu kwani, kila mwenda mbio sana sio mshindi, na kiburi cha CDM kitawangamiza , Hta sensa hawajui maana yake, wana uungwana gani? Dears, KIPYA KINYEMI!

Sensa ilikuwa Iringa - Nyololo pekee!!?? Zanzibar - Bububu hakukuwa na sensa. But, Mtenda hutendwa. take my word.
 
Hivi hiki kibabu familia yake inaishi Tanzania?

Huyu Tendwa analipa fadhila coz aliokotwa akiwa amelost vibaya akapewa ulaji na serikali ya CHAMA CHA MAJAMBAZI (CCM). usishangae ukasikia anataka kugombea ubunge kwa ticket ya CHAMA CHA MAJAMBAZI CCM !! Shame on him and his entire family!
 
Uzee umemkataa, ameanza mapema kurudia enzi za uchanga maskini sijui nani amwokoe manake hajui atamkalo wala atendalo, lol nchi inaelekea kuishiwa wazee wa hekma
 
Hawezi futa spirit ya mabadiliko ya watanzania M4C imekuwa 100 times sasa.
 
..Akiifuta CDM, nitaomba muungwana mmoja achukue shoka na kunikata moja ya vidole vya kati na akipeleke kwa Tendwa!
 
Leo Tendwa ameumbuka vibaya.Hakika Jaji Amir Manento amemvua nguo sijui ataficha wapi sura yake.
 
"Tendwa amewaambia waandishi wa habari hatishiki na chama chochote kuwa na wabunge kwani SHERIA inamruhusu kufuta chama hata kama kina wabunge 100."

"Hata hivyo amekiri SHERIA inaruhusu vyama kufanya mikutano na maandamano wakati wowote."

Apumzike kwa amani alikuwa anafuata sheria.
 
Back
Top Bottom