Kuna msemo wa KIHAYA usemao, "Eibala lita nyinalyo" yaani jina humuua mwenyewe i.e mwenyejina hilo. Msajili wa vyama vya siasa anaitwa TENDWA. Neno Tendwa ni kitenzi kinachoonesha kuwa kitu au mtu kafanyiwa kitu fulani (hasa kibaya). Utasikia mtu anamwambia mwenzie wamenitenda, moja kwa moja msikiaji hawezi kufikiria kutendwa kuliko chanya bali kuliko asi, yaani kwamba amelogwa, amepigwa au amerubuniwa na watu wabaya.
Sasa tujiulize, hivi kwa matamshi ya jana aliyoyatoa kwenye vyombo vya habari juu ya kufuta vyama vya siasa hasa ndani yake akiwa na CHADEMA kama chama atakachoanza nacho, alikuwa salama, mwenye akili zake timamu,au alikuwa amelogwa yaani ameTendwa?
Mimi naamini alikuwa ametendwa! Na kwa sababu hiyo, si yeye katika u-yeye wake aliyekuwa anatamka matamshi hayo, maana hata mtoto mdogo kwa akili zake za kawaida asingeweza kutamka hivyo.
Inasikitisha na kushangaza kuona kwamba inchi yetu inawekwa katika mazingira ya hatari na watu kwa sababu ya uchu tu wa madaraka. Watu hawa wanapuuza hata evidence zilizo wazi kabisa, na kuanza kuwaada watanzania kwa maneno yao yasiyo na mashiko.
Huyu mzee ametendwa na system, wazee wake walikuwa ni manabii maana waliona tokea mbali kuwa atatendwa, lakini aangalie jinsi anavyotendwa maana lengo kuu la kutendwa ni mauti.
Kwanini asifute chama kilichojaa mafisadi? Kwanini asifute Polisiccm kinachoua raia wasio na hatia? Kama anamachungu ya kufuta kwa nini asifute chama ambacho serikali yake inasaini mikataba ya kinyonyaji? Kwa nini asifute chama chenye wala rushwa waliokubuhu?
Kama anapenda kufuta kwa nini asifute chama ambacho kimetawala kwa miaka hamsini na kwa kipindi hicho watu wake hali zao ni mbaya kuliko zilivyokuwa nyuma?
Pasi na shaka...
TENDWA AMETENDWA!