Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Leo asubuhi ktk kipindi cha Nipashe cha Radio 1 Stereo Tendwa alionekana akiwabembeleza CDM wakutane naye, akitoa haja kwamba ule mkutano wa juzi kati yake na vyama hauhusiani kabisa na madai yao, hivyo anawashangaa kwa nini hawakuhudhuria mkutano, na hata vyama vingine vilivyohudhuria viliwashangaa CDM.
Kama kawaida mtangazaji aliyekuwa akimhoji alishindwa kumuuliza swali la msingi kabisa - kwa nini yeye Tendwa, baada ya tukio la kuuwawa kwa Mwangosi alikimbilia kwenda vyombo vya habari na kutoa kauli ya moja kwa moja kuilaumu CDM kuhusiana na tukio hilo na kutishia kukifuta CDM?
Yaani mtangazaji hakumuuliza kwa nini hata kabla ya tume ya uchunguzi kufanya kazi yake yeye aliishaamua kuwa CDM ndiyo wakosaji, hivyo kingefaa kufutwa. Pia mtangazaji hakumuuliza Tendwa kwa nini badala ya kwenda vyombo vya habari asiombe kwanza kukutana na CDM kabya ya kubwabwaja katika vyombo vya habari?
Kwa ujumla Tendwa alionekana kama vile anawabembeleza CDM wakutane.
Ushauri wangu: CDM wakutane na Tendwa lakini kwa sharti moja -- afute na aombe radhi kauli yake kwa vyombo vya habari kwamba CDM ndiyo mhusika wa tukio la mauaji ya Mwangosi hadi kufikia kutishia kukifuta chama.
Kama kawaida mtangazaji aliyekuwa akimhoji alishindwa kumuuliza swali la msingi kabisa - kwa nini yeye Tendwa, baada ya tukio la kuuwawa kwa Mwangosi alikimbilia kwenda vyombo vya habari na kutoa kauli ya moja kwa moja kuilaumu CDM kuhusiana na tukio hilo na kutishia kukifuta CDM?
Yaani mtangazaji hakumuuliza kwa nini hata kabla ya tume ya uchunguzi kufanya kazi yake yeye aliishaamua kuwa CDM ndiyo wakosaji, hivyo kingefaa kufutwa. Pia mtangazaji hakumuuliza Tendwa kwa nini badala ya kwenda vyombo vya habari asiombe kwanza kukutana na CDM kabya ya kubwabwaja katika vyombo vya habari?
Kwa ujumla Tendwa alionekana kama vile anawabembeleza CDM wakutane.
Ushauri wangu: CDM wakutane na Tendwa lakini kwa sharti moja -- afute na aombe radhi kauli yake kwa vyombo vya habari kwamba CDM ndiyo mhusika wa tukio la mauaji ya Mwangosi hadi kufikia kutishia kukifuta chama.