Tembo aua Majangili wawili Mikumi

Tembo aua Majangili wawili Mikumi

Self defence kisheria tembo hana kesi ya kujibu.Kijeshi tuna mtunuku cheo cha hali ya juu kwa kutumia mbinu kali za kuangamiza adui.Big up Mr Tembo.Get well soon
 
Sasa tembo wameamua kujilinda. Juzi, tembo mmoja amewaua majangili wawili waliotaka kumuua. Tukio hilo limetokea katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi-upande wa Kilosa. Mashuhuda wa tukio hilo wamedai kuwa Mjangili hayo yalipita kijijini kwao yakielekea hifadhini kwa ajili ya kuua tembo yakiwa na silaha nzito.

Inadaiwa kuwa tembo aliyewaua majangili alijeruhiwa kwa risasi na kujifanya amekufa.Majangili waliposogea kwa ajili ya kutimiza lengo lao la kuchukua nyara,tembo husika alikurupuka na kuanza kuwashambulia majangili hao hadi kuwaua wote wawili.Halafu, akaziponda maiti na kurundika miti katika maiti hizokiasi cha kuzifanya zisionekane.

Mashuhuda waliofika katika eneo la tukio walikuta maiti hizo pamoja na silaha walizokuwa nazo majangili hao. Natoa pongezi kwa tembo wa Mikumi kwa kujilinda. Tembo wote nchini nao waige mfano huo.

Chanzo: Wananchi wanaoishi kandokando ya Mikumi,upande wa Kilosa na Askari Wanyamapori

Huyo tembo ametibiwa jeraha la risasi?
Amefanya vema huyo tembo.
 
Mwaka umeanza vibaya huu kwa mzee wa vipusa... mizigo imeshinda, hajakaa sawa vijana wa kazi wanauwa tembo..mbona majanga
 
Nadhani mm ni mmoja kati ya watu wachache walioona operesheni tokomeza ilikuwa sawa tu.

Unajua watu wanaokaa kando na hifadhi ndio wanatunza majangili ukiwabana watasema tu ila nchi hii cku hizi mnajifanya utawala wa haki na sheria mtu akipigwa kirungu kwa manufaa ya taifa mnakuja juu....wamewaona majangili wakipita hawakutoa taarifa wakamatwe au wao kuwakamata...------- kbs.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom