Telekinesis

Telekinesis

Hili chaweza kuwa kitu kigeni mno masikioni mwa wengi lakini ni kitu kilichopo Katika Ulimwengu huu
Telekinesis ni hali ya kuwa na uwezo na nguvu za kiasili za kuweza kunyanyua na kusogeza vitu kwa viungo vya mwili hasa mikono bila kuvigusaView attachment 299478
Telekinesis ni tendo la psychic ambalo ambalo uwezo wake ni uleule wa kusogeza vitu na kuvihamisha bila kuvigusa-psychokinesis

Sasa hiajalishi kama ni telekinesis au psychokinesis lakini matendo yote haya mawili ni sehemu mojawapo ambayo kisayansi bado yanaacha maswali mengi huku baadhi ya watu Katika tafiti na mabandiko yao wakizihusisha a nguvu za giza
Lakini ukweli ni kwamba mind/ufahamu wa binadamu ni kitu chenye nguvu mno na kwakweli tunachotumia ni sehemu ndogo tu ya nguvu ya ufahamu wote tukio nao... Kidini hasa katika Biblia takatifu hii nguvu inaitwa imani, na tunaambiwa ukiwa na imani ndogo tu isiyozidi ukubwa wa chembe ya haradali utakuwa na uwezo hata wa kuhamisha milima... Hii imani katika Bible ndio telekinesis kwa upande mwingine

Sasa watu hujaribu kumiliki hizi nguvu kwa njia ya mkato au ya kujituma na kupractice, tunapoongelea mambo ya meditation, psychic powers n abilities yoga astral practice nk kimsingi Tunaongelea telekinesis katika secondary stage, baada ya kuchanganya na maarifa mengine Kama hayo
Lakini pia kuna wale ambao hupenda kumiliki nguvu za telekinesis kwa njia za mkato na hapa ndipo watu huingia mikataba na kuzimu na kufanya makafara huku wengi wakiingizwa kwenye dini ya mashetani ili tu aweze kufanya mambo kama hayo

Siku hizi tuna manabii na mitume wengi wanaofanya miujiza mingi hasa ile ya kuwapuliza tu watu na watu hao kuanguka au kunyoosha tu mkono au kidole na nguvu yake kuwaangusha watu.... Msidanganyike ile si nguvu ya kiMungu bali ni aina fulani ya nguvu za kitelekinesis na ki psychokinesis zilizochakachuliwa na mwishowe kuchomekea jina la Yesu kristo kupumbaza watu

Tuna waganga wa kienyeji pia wenye hizi nguvu, lakini huchanganya na mambo mengine ya giza na kuweza kuwapumbaza na kuwarubuni maelfu kwa maelfu

Telekinesis ya kiasili na isiyochakachuliwa haina madhara zaidi ya mtu mwenye hizi nguvu kuweza kufanya maajabu ya kusogeza vitu bila kuvigusa.... Dunia bado ina mengi na mengi bado hatuyajui... Usiunyime ufahamu wako maarifa bado kuna mengi huyajui
Mshana Jr.umenifurahisha si kwa bandiko hili kwa ukweli uliousema kuhusu nguvu alizoumbwa nazo mwanadamu.Kwa wale Wakristu tunasoma katika kitabu cha Mwanzo: "...Na tumfanye mtu kwa mfano wetu..."Hii sentensi inaelezea kwa ufupi sana ukuu na uweza na nguvu alizorithishwa mwanadamu kutoka kwa Mungu.Na tumepewa uweza huo ili tushirikiane na Mungu katika kazi ya Uumbaji.Ulimwengu (the Universe) bado unaendelea kuumbwa.Na pengine alifanya hivi ili Mungu apate nafasi ya kutosha kujenga makazi yetu huko aliko."...Nyumbani mwa Baba Yangu kuna makao mengi...la sivyo ningeliwaambia...naenda kuwaandalia makao kisha nije kuwachukueni". Hayo ni maneno ya Yesu na ndio ushahidi wa kwa nini aliturithisha nguvu na uweza wake.Ni ili yeye apate muda na nafasi ya kufanya mengine.Ni sawa tu na wewe unamuachia binti wa kazi nyumbani kazi fulani fulani ili wewe upate nafasi ya ku-handle mambo makubwa na muhimu zaidi.
Kwa hiyo, binadamu laiti tungetambua huo uwezo tulio nao wala tusingekuwa tunalialia juu ya changamoto zinazotukabili maishani.
 
Back
Top Bottom